Mtu wa Pwani
JF-Expert Member
- Dec 26, 2006
- 4,184
- 671
TRA watibua nyongo za Wanzanzibari
Monday, 25 October 2010 07:52
0diggs
digg
Ally Mkoreha, Zanzibar
IDARA ya Ushuru wa Forodha katika Bandari ya Dar es Salaam, imetajwa kuwa mmoja ya taasisi zinazochafua sura ya Muungano wa Tanzania baada ya baadhi ya maofisa wake kudaiwa kuwanyanyasa Wazanzibari.
Tayari maofisa wa Wizara ya Fedha na Uchumi katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, wamepanga kwenda Dar es Salaam mapema wiki hii kukutana na maofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kuzungumzia suala hilo .
Malalamiko kuhusu watu wa Zanzibar kunyanyaswa na maofisa wa Idara ya Ushuru wa Forodha kwa kutakiwa kulipia ushuru wa vifaa ambavyo si kwa ajili ya biashara, ulitolewa jana katika Mkutano Maalumu wa Baraza la Biashara la Zanzibar.
Hali kadhalika na uamuzi wa maofisa wa Wizara ya Fedha na Uchumi kwenda Dar es Salaam kuonana na maofisa wa TRA.
Mkutano huo, uliokuwa chini ya Mwenyekiti wa Baraza la Biashara la Zanzibar , Rais Amani Abeid Karume ulifanyika katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, ulioko katika eneo la Mnazi Mmoja, mjini Unguja.
Katika mkutano huo, mmoja wa wajumbe wa sekta binafsi Salum Hassan Turky, alisema maofisa wa Idara ya Ushuru wa Forodha katika Bandari ya Dar es Salaam, wanawanyanyasa na kuwadhalilisha Wazanzibari wanapopita katika bandari hiyo wakiwa na vifaa ambavyo ni vya matumizi ya kawaida kwa ndugu zao.
Maofisa wa TRA katika Bandari ya Dar es Salaam, wanaharibu sura ya Muungano wa Tanzania . Wazanzibari wanapopita katika bandari hiyo wakiwa na seti za televisheni kwa ajili ya matumizi ya kawaida, wanasumbuliwa mno utafikiri wanatoka katika nchi nyingine, alisema Turky.
Alisema kero hiyo ni ya muda mrefu na kwamba haijapatiwa ufumbuzi licha ya wakuu wa TRA kuahidi kuishughulikia.
Maelezo hayo yalimlazimisha Waziri wa Utalii, Biashara na Uwekezaji katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Samia Suluhu Hassan kusimama na kujaribu kuitetea TRA.
Suala hili lilishughulikiwa na uongozi wa TRA na kama linaendelea basi halitokani na TRA kama mamlaka na badala yake, linatokana na wafanyakazi wachache watukutu na wala rushwa. Kama mtu anapita pale akiwa na bidhaa lakini hana risiti lazima atasumbuliwa, kinyume chake watu watoe taarifa kuhusu kunyanyaswa, alisema waziri Suluhu.
Hata hivyo maelezo hayo hayakuwaridhisha wajumbe na badala yake, yaliongeza chumvi katika vidonda vya wajumbe ambao walisema tatizo bado ni kubwa na kwamba hatua lazima zichukuliwe ili kuwawezesha Wazanzibari, kupita katika bandari hiyo kwa uhuru kama ilivyo kwa wenzao wa Tanzania bara wanapoingia Zanzibar.
Hatua hiyo, ilimlazimisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,Hamis Mussa, kusimama na kupndekeza kwa Rais Karume, haja ya kuridhia mpango wa maofisa wa wizara yake kwenda Dar es Salaam kukutana na maofisa wa TRA hiyo, kujadili kero hiyo.
Kwa mujibu wa Mussa, safari hiyo itafanyika kati ya leo na kesho.
Monday, 25 October 2010 07:52
0diggs
digg
Ally Mkoreha, Zanzibar
IDARA ya Ushuru wa Forodha katika Bandari ya Dar es Salaam, imetajwa kuwa mmoja ya taasisi zinazochafua sura ya Muungano wa Tanzania baada ya baadhi ya maofisa wake kudaiwa kuwanyanyasa Wazanzibari.
Tayari maofisa wa Wizara ya Fedha na Uchumi katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, wamepanga kwenda Dar es Salaam mapema wiki hii kukutana na maofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kuzungumzia suala hilo .
Malalamiko kuhusu watu wa Zanzibar kunyanyaswa na maofisa wa Idara ya Ushuru wa Forodha kwa kutakiwa kulipia ushuru wa vifaa ambavyo si kwa ajili ya biashara, ulitolewa jana katika Mkutano Maalumu wa Baraza la Biashara la Zanzibar.
Hali kadhalika na uamuzi wa maofisa wa Wizara ya Fedha na Uchumi kwenda Dar es Salaam kuonana na maofisa wa TRA.
Mkutano huo, uliokuwa chini ya Mwenyekiti wa Baraza la Biashara la Zanzibar , Rais Amani Abeid Karume ulifanyika katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar, ulioko katika eneo la Mnazi Mmoja, mjini Unguja.
Katika mkutano huo, mmoja wa wajumbe wa sekta binafsi Salum Hassan Turky, alisema maofisa wa Idara ya Ushuru wa Forodha katika Bandari ya Dar es Salaam, wanawanyanyasa na kuwadhalilisha Wazanzibari wanapopita katika bandari hiyo wakiwa na vifaa ambavyo ni vya matumizi ya kawaida kwa ndugu zao.
Maofisa wa TRA katika Bandari ya Dar es Salaam, wanaharibu sura ya Muungano wa Tanzania . Wazanzibari wanapopita katika bandari hiyo wakiwa na seti za televisheni kwa ajili ya matumizi ya kawaida, wanasumbuliwa mno utafikiri wanatoka katika nchi nyingine, alisema Turky.
Alisema kero hiyo ni ya muda mrefu na kwamba haijapatiwa ufumbuzi licha ya wakuu wa TRA kuahidi kuishughulikia.
Maelezo hayo yalimlazimisha Waziri wa Utalii, Biashara na Uwekezaji katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Samia Suluhu Hassan kusimama na kujaribu kuitetea TRA.
Suala hili lilishughulikiwa na uongozi wa TRA na kama linaendelea basi halitokani na TRA kama mamlaka na badala yake, linatokana na wafanyakazi wachache watukutu na wala rushwa. Kama mtu anapita pale akiwa na bidhaa lakini hana risiti lazima atasumbuliwa, kinyume chake watu watoe taarifa kuhusu kunyanyaswa, alisema waziri Suluhu.
Hata hivyo maelezo hayo hayakuwaridhisha wajumbe na badala yake, yaliongeza chumvi katika vidonda vya wajumbe ambao walisema tatizo bado ni kubwa na kwamba hatua lazima zichukuliwe ili kuwawezesha Wazanzibari, kupita katika bandari hiyo kwa uhuru kama ilivyo kwa wenzao wa Tanzania bara wanapoingia Zanzibar.
Hatua hiyo, ilimlazimisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,Hamis Mussa, kusimama na kupndekeza kwa Rais Karume, haja ya kuridhia mpango wa maofisa wa wizara yake kwenda Dar es Salaam kukutana na maofisa wa TRA hiyo, kujadili kero hiyo.
Kwa mujibu wa Mussa, safari hiyo itafanyika kati ya leo na kesho.