TRA: Kariakoo lazima EFD kwa wote

TRA: Kariakoo lazima EFD kwa wote

Wamegundua kosa lao?

Hata hivyo hangaya si alisema hataki kodi za dhuruma na kwamba anataka watu waachwe walipe kodi kwa hiari yao?
Kutumia mashine ni dhuruma? Unataka zile za kuandikwa kwa mkono sio? Zile za ujajanujanja?
 
Watanzania tunapenda sana janjajanja, ukienda kwa Kagame hadi fundi viatu anatoa receipt ya electronic, Bongo wengi tunapenda kona kona sana
Badilisheni sheria
 
Na elimu kwa wananchi itiliwe nguvu, wahamasishwe kutokukubali risiti ya kubebea mzigo (Kiasi cha risiti kiendane na pesa ya malipo)
Alafu hela ikipatikana akina Mwigulu wakanunue Ma VXR ya mwaka 2022 moja tu thamqni yake ni 560 milioni? Hela ipo waache anasa
 
Alitaka walipe kodi halali na halisi na sio zile za kuchomekewa kwamba sijui anadaiwa kodi za miaka mitano au kumi iliyopita hesabu zake zilipigwa chini ya kile alichotakiwa kulipa hivyo analazimishwa kulipa huku akaunti yake ya benki ikipigwa pin na kutishiwa kufunguliwa kesi ya uhujumu uchumi.
Hizo ndio Rais Samia alikataa.

Samuel Eto mchezaji wa zamani wa Cameroon na timu kadhaa za ulaya majuzi amefunguliwa kesi ya ukwepaji kodi uliofanyika miaka zaidi ya 10 iliyopita.

Tunatamani maendeleo ya wenzetu ilhali bado tunaendekeza na kushabikia fikra za kiumama umama na kiubwete ubwete
 
Kkoo mbona Kuna biashara nyingi tu ambazo ni ndogo sana, na wanastahili kuwepo.
Sheria inasema chini ya mil 12(kabla ya mama ilikua chini ya mil 14) hawatahusika na efd machine,. Sasa Sheria ibadiloshwe Kama mnataka kila biasharaa itoe risiti
Frame 500,000 na kuendelea halafu uuze chini ya 1m Kwa mwezi? Sio Kariakoo.
 
Kama huna biashara yenye mauzo ya 12m kwa mwaka unafanya nini huko Kkoo nenda kwenye maeneo ya biashara za mzunguko mdogo
Sio mauzo ya Mwaka, ni kila mwenye biashara KKOO lazima awe na Mashine sio ombi tena
 
Frame 500,000 na kuendelea halafu uuze chini ya 1m Kwa mwezi? Sio Kariakoo.
Tangazo jipya limesisitiza kuwa kwa walio kariakoo EFD ni ya lazima, sio ombi kama zamani
 
Naunga mkono hoja.
Naunga mkono kila mfanyabiashara kutoa risiti ya efd, lakini tra wanapaswa kupunguza gharama ya mashine hizo wasizifanye kuwa biashara kwakuwa zinatumika kukusanya mapato ya serikali, au wazitoe bure kama wanavyopewa wakandarasi wa kuzoa taka na wale wa parking
 
Back
Top Bottom