Top CCM leader secretly funding opposition party

Cuf ina wafanya biashara wengi wanaokisaidia chama sio RA.. Lwakatare hoja yake ilikuwa ni nyengine,rudia uzuri.. labda nikusaidie tu,awali wafanya biashara walikuwa wakitoa misaada ilikuwa ni siri ya viongozi na wao,lkn hivi sasa wamebadilisha utaratibu,inaekwa wazi hata kwenye vyanzo vyake.. Lwakatare alikuwa anahoji kwanini isiendelee kuwa siri? lkn viongozi wa juu wameamua kuweka wazi hilo.. rudia barua ya Lwakatare lkn isome kwa uangalifu kipengele hicho utaona,sawa mkuu..?
______________________________

CALLIPSO:

Nadhani hujaielewa kivizuri ile hoja ya Lwakatare hasa katika kifungu husika. Nakinukuu hapa kifungu chenye hiyo hoja -- ambayo nakubali kwanza ukisioma kwa haraka inaonekana ina utata -- yaani inaonyesha maana mbili ingawa maana halisi iko wazi na hasa ukizingatia ile comma baada ya neno 'naye':

"Mhe. Mwenyekiti jana na leo, nilipokuwa nikichangia na kuhoji ndani ya baraza hili kama mjumbe na hasa suala la fedha za mkutano mkuu ambazo hazikupatikana toka kwa mfanyabiashara mmoja tuliyewekeza naye, suala la kutoendelea na utaratibu wa kuifanya SIRI ya viongozi wa juu tu mikataba ya uwekezaji tunayoifanya na baadhi ya wafanyabiashara na hatari iliyopo kwa utaratibu huo, na pia suala la kutoridhishwa na namna Chama kisivyo na utaratibu mzuri wa “Kuwaenzi na kuwaheshimu” viongozi.....

Maana ninayoipata ni kwamba LW anaibua suala la 'kutoendelea na utaratibu' wa kufanya siri ya viongozi wa juu tu iule mikataba ya uwezekaji inayofanywa na chama na baadhi ya wafanyabiashara -- na hatari ya utaratibu huo. Ni dhahiri hapa WL anataka utaratibu uliopo usiwe siri kwa viongozi wa juu tu wa CUF.

Kuna utata kidogo, lakini haiwezekani, katika hali hii ya farakano baina yake na viongozi wengine wa chama LW akahoji vipi usiri uliokuwapo uondolewe? Bila shaka angeohoji vipi usiri uwe unaendelea? -- yaani kama kiongozi anayepigania uwepo wa uwazi katika shughuli za chama hasa kuhusu mapato na matumizi ya fedha.
 
Dots connected.....Ndio maana yule mbunge wa CUF na kiongozi wa upinzani bungeni Hamad Rashid Mohammed alim-bana Pinda kuhusu "baadhi ya wamiliki wa vyombo vya habari wanaotumia vibaya vyombo hivyo kuwatuhumu wenzao" (akimaanisha Mengi alivyoitumia ITV kumuita Rostam papa la ufisadi)!

Kama ni hivi basi CUF kwishney!
 
Zek Malang mkuu..
Nimekupata,lkn naona maelezo yako ni mazuri,si umeona kuwa huyo mfanya biashara pesa zake za kufadhili mkutano mkuu hazikupatikana? kwanini jiulize? kwa sababu ikiwa ndo za RA basi viongozi wamezikataa,hawataki pesa za mafisadi.. Hapo basi ndo inakuja ile dhanna kuwa kile Chama ni kinachofadhiliwa na RA ni CHADEMA!!!!..
Kama unakunywa kahawa vikombe vitano basi sasa punguza kunywa vitatu mzee wangu..
 
Zek malang..
Na suala la alilolielezea Lwakatare la "Usiri" ni sawa hakukosea,ichukue hiyo hiyo tafsiri yake labda mpaka yeye mwenyewe abadilishe,yaani tusimtafsirie kwa mtizamo wetu.. labda kwa kupeana faida tu,Cuf ina wafanyabiashara wengi wanachokisaidia chama kwa kua Cuf ni chama kikubwa,lkn zamani utaratibu ulikuwa ni SIRI na hii ni hao wafanyabiashara wenyewe walikuwa wanataka iwe siri kwa hofu yao ya usalama wao na kuharibiwa biashara zao na CCM kupitia serikali zake,kwani tayari imeshatokea kwa wafanyabiashara ambao ilisemekana wanakisaidia Cuf na hatima yake ni kuharibiwa biashara zao,nafkiri unayakumbuka matukio kama hayo,nitakukumbusha ikiwa umesahau... lkn kwa sasa wameamua viongozi wa juu suala la wafanyabiashara liwe wazi ndani ya chama,na ndo mana Lwakatare akahoji kwa nini isiendelee kuwa siri?..
 
labda kuna kwa ukweli fulani kuhusu CUF na huyo mfanyabiashara anayewafadhiri, kwa maana mbili, moja ni kuwa Bwana Lipumba kwa kweli sasa zile cheche zake za maslahi ya taifa hazionekani kabisa, na misimamo yake sio kama ile mwanzo ya kupinga uozo wa ccm lakini sasa anaonekana yuko laini kidogo, lakini pili ni uchaguzi wa Busanda, ile hata kama mtu alikuwa hajuhi mambo ya kupambanua siasa, lakini pale hapakuwa sahihi kwa CUF kuweka mgombea kabisa kwani kwa pale kilikuwa ni kama chama kipya kabisa hakikuwa na influence hata kidogo,
lakini lamwisho, ni kuhusu uchaguzi wa magogoni, ndio ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kwa CUF kushindwa uchaguzi Zanzibar na kukiri hadharani kuwa ni kweli wameshindwa bila purukushani yoyote
time will tell
 
labda kuna kwa ukweli fulani kuhusu CUF na huyo mfanyabiashara anayewafadhiri, kwa maana mbili, moja ni kuwa Bwana Lipumba kwa kweli sasa zile cheche zake za maslahi ya taifa hazionekani kabisa, na misimamo yake sio kama ile mwanzo ya kupinga uozo wa ccm lakini sasa anaonekana yuko laini kidogo, lakini pili ni uchaguzi wa Busanda, ile hata kama mtu alikuwa hajuhi mambo ya kupambanua siasa, lakini pale hapakuwa sahihi kwa CUF kuweka mgombea kabisa kwani kwa pale kilikuwa ni kama chama kipya kabisa hakikuwa na influence hata kidogo,
lakini lamwisho, ni kuhusu uchaguzi wa magogoni, ndio ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kwa CUF kushindwa uchaguzi Zanzibar na kukiri hadharani kuwa ni kweli wameshindwa bila purukushani yoyote
time will tell

CCM mbona imekaa kimya? CUF mbona wamekaa kimya? Tunataka waseme, naona wanajua Watanzania ni wepesi kusahau na inethibitishwa na hapa jinsi michango ilivyofifia na kuhamia katika topic nyingine ambayo nayo itakufa ikiibuka mpya, hakuna utekelezaji wala ufuatiliaji.

Hapa kuna issue nzito, ama CCM imemtuma RA kuua upinzani, ama yeye RA anatumia hiyo ili kupata kinga kwa upande wa upinzani!! Yote si mema hata kidogo kwa mustakabali wa nchi yetu, na hakuna anayejali!!!!

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU TUFUMBUE MACHO WATANZANIA
 
"CCM mbona imekaa kimya? CUF mbona wamekaa kimya? Tunataka waseme, naona wanajua Watanzania ni wepesi kusahau na inethibitishwa na hapa jinsi michango ilivyofifia na kuhamia katika topic nyingine ambayo nayo itakufa ikiibuka mpya, hakuna utekelezaji wala ufuatiliaji.

Hapa kuna issue nzito, ama CCM imemtuma RA kuua upinzani, ama yeye RA anatumia hiyo ili kupata kinga kwa upande wa upinzani!! Yote si mema hata kidogo kwa mustakabali wa nchi yetu, na hakuna anayejali!!!!"

__________________________

Halisi:
Umenena ndugu yangu, hakuna anayejali. RA anaogopwa sana na serikali ya CCM -- anaweza hata kuamrisha JK ajiuzulu -- na kweli JK akajiuzulu, kwani anaogopa asije RA akamwaga mambo -- you know Kagoda, Afriteiner, Richmond etc -- kutoa evidence walikuwa pamoja.

Hali hii imekuwa inadhhofisha kipindi hiki cha kwanza cha utawala wa JK pamoja na mazuri aliyokuwa akitarajia kuyafanya kwa Watanzania.

Aidha inatisha kuona kuwa hali itajirudia hivyo hivyo katika kipindi chake cha pili, iwapo atakuwa Rais tena -- kama jinsi anavyotaka, na huku RA akiwa bado na 'mpini' wake -- kwani haitarajiwi atauachia -- kwani anaona ni kinga kubwa sana kwa ufisadi aliowafanyia Watanzania.

Namshauri JK ajitutumue angalau kidogo, apige moyo konde na aseme potelea mbali na aanze kumshughulikia mtu huyu -- na nina imani umma utakuwa nyuma yake. Mtu mmoja hawezi akaachiwa akasumbua umma mzima kama vile sote ni mambumbu kwake.

Hatari ni kwamba Ra anazidi kujizatiti na inaweza kufikia hatua ambayo JK hawezi kubakiwa na uwezo wowote wa kumshughulikia na ikawa kwamba yeye ndiyo atashughulikiwa.
 
"CCM mbona imekaa kimya? CUF mbona wamekaa kimya? Tunataka waseme, naona wanajua Watanzania ni wepesi kusahau na inethibitishwa na hapa jinsi michango ilivyofifia na kuhamia katika topic nyingine ambayo nayo itakufa ikiibuka mpya, hakuna utekelezaji wala ufuatiliaji.

Hapa kuna issue nzito, ama CCM imemtuma RA kuua upinzani, ama yeye RA anatumia hiyo ili kupata kinga kwa upande wa upinzani!! Yote si mema hata kidogo kwa mustakabali wa nchi yetu, na hakuna anayejali!!!!"
__________________________

Halisi:
Umenena ndugu yangu, hakuna anayejali. RA anaogopwa sana na serikali ya CCM -- anaweza hata kuamrisha JK ajiuzulu -- na kweli JK akajiuzulu, kwani anaogopa asije RA akamwaga mambo -- you know Kagoda, Afriteiner, Richmond etc -- kutoa evidence walikuwa pamoja.

Hali hii imekuwa inadhhofisha kipindi hiki cha kwanza cha utawala wa JK pamoja na mazuri aliyokuwa akitarajia kuyafanya kwa Watanzania.

Aidha inatisha kuona kuwa hali itajirudia hivyo hivyo katika kipindi chake cha pili, iwapo atakuwa Rais tena -- kama jinsi anavyotaka, na huku RA akiwa bado na 'mpini' wake -- kwani haitarajiwi atauachia -- kwani anaona ni kinga kubwa sana kwa ufisadi aliowafanyia Watanzania.

Namshauri JK ajitutumue angalau kidogo, apige moyo konde na aseme potelea mbali na aanze kumshughulikia mtu huyu -- na nina imani umma utakuwa nyuma yake. Mtu mmoja hawezi akaachiwa akasumbua umma mzima kama vile sote ni mambumbu kwake.

Hatari ni kwamba Ra anazidi kujizatiti na inaweza kufikia hatua ambayo JK hawezi kubakiwa na uwezo wowote wa kumshughulikia na ikawa kwamba yeye ndiyo atashughulikiwa.


Siamini kabisa kama mawazo haya yanatoka kwa mtanzania. Natamani kulia nashindwa. Umekata tamaa, unaishi maisha ya jana, mawazo yako yamekanamizwa, umekuwa mtumwa huna uhuru.

Ulichosema hapo hakiingii akilini hata kidogo. Unaposema RA anaweza kumwambia JK ajiuzulu! kwa kifupi una declare RA yuko juu zaidi ya JK.

Unaposma JK ajitutumue sijajua how, wakati juu yake yuko RA!

Unachoficha hapa ni kuwa JK na uwezo wa kufanya lolote! lakini bado unasema ajitutumue, wakati ni rais wa nchi, ivi unaua unachosema??

unataka kuvunja ndoa ya JK RA an EL, kwa maneno yako ya 'kichovu' kuwa eti JK alipanga kufanya mambo mazuri kwa watanzania?? mwongo wewe! mambo gani mazuri aliyopanga ?

Mapango wa hawa jamaa watatu ulianzia miaka 10 iliyopita, leo kwa sentensi zako za kitoto bado unaamini kuwa JK anakupenda!!!!!


wewe amka sasa acha mawazo haya ya kitumwa, fanya uwezavyo , hubiri kwa kila kiumbe kule kuwa CCM waondoke madarakani, RA alitumiwa na angetumiwa yeyote yule, hii ni sera ya CCM kutumia kodi zenu ili wazidi kukaa madarakani.

Mnapomsema RA inaonyesha jinsi gani msivyotaka kuvamia na kung'oa mzizi huu uitwao CCM.

Sentensi za aina zako ni nyingi kuwa tumuone JK msafi wakati ananuka yeye na serikali yake, sitasita kussema kwa mawazo yako wewe ni FISADI na adui namba moja kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

Nyie na mawazo yenu ya RA mnaficha ukweli RA atabaki tu maadam CCM ipo pale, LAO MOJA wote si akina mwakyembe wala akina kilango

kaa na mawazo yako hayo utaona mwisho wake

wewe na mawazo yako haya ya kifisadi endeleeni kuwadanganya hao hao kuwa tusiiseme CCM NA JK wake tumseme RA. kamtu kadogo kuliko kawaida! RA ashindane na usalama wa taifa, mahakama, jeshi, RA aongoze watanzania milioni 40 RA??

CCM wanaweza mpaka kuwachukulia wake zenu mkabaki kusema Rostam! pia kumbuka mafisadi walioifilisi na wanaoifilisi nchi hii ni wengi na wamekula hela nyingi kuliko kukaa kumsema RA aliyeiba na kupewa support na weusi kama wewe na mimi kwa kupitia CCM! wabaya ndugu zetu hawa hawa, tunaopanda daladala zao na wanatuchangia harusi zetu!

CCM has to go with all its roots, that is a solution
 
Come along JF members, to put 2 and 2 together to make four: The party that has one of its top brass frequently putting up in hotels in Dar ni kafu na i .na .ku .fa!!! Sasa kilichobaki, kama mwana JF mmoja alivyoshauri hapo juu ni SLAA, MBOWE na ZITTO kujihadhari na ma********* wanaohonga kutokana na fedha walizokwapua BoT mchana kweupeee tunazoziita ni za EPA.

Chadema does not need the dirty money from EPA. Walalahoi watawachangia wakihamasika kwa ujumbe wa UKOMBOZI.

Hakuna kulala, Mpaka Kieleweke!

Wewe unamjua freeman mbowe au unamsikia?that guy loves his dough mkuu!yupo katika system hujasikia anaenda kugombania ubunge 2010?akiwa bungeni anaongeza nguvu ya kumtete RA!does it ring the bell?
 
mpaka michuzi yupo payroll eti blog ya jamii !Am telling you inatia huruma sana the generation is being poisoned slowly!
 
Tatizo kubwa hapa ninaloliona wengi katika majadiliano haya tumebaki na labda nyingi mno! Na hapo ndipo wajanja hutumia kupenyesha uongo wao!
 
Lohhh, naona mambo yote hadharani. Kifo cha Zitto kitasafisha kweli Upinzani.

Hawa jamaa bila kujua, ndiyo kwanza wataanzisha Upinzani wa kweli kweli.

Nakumbuka sasa maneno ya Nyerere kuwa Upinzani wa kweli, utatoka CCM.
 
Lohhh, naona mambo yote hadharani. Kifo cha Zitto kitasafisha kweli Upinzani.

Hawa jamaa bila kujua, ndiyo kwanza wataanzisha Upinzani wa kweli kweli.

Nakumbuka sasa maneno ya Nyerere kuwa Upinzani wa kweli, utatoka CCM.

ni jambo zuri sana ukweli kujulikana, mara zote hapa jukwaani tumekua tukisema hiki chama kimejaa wasanii tumekua tukiambulia matusi toka kwa members haya sasa oneni uoza huu
 
William Malecela alishasema zamani sana kuwa Viongozi wetu ni reflection yetu Watanzania.

Hebu nionyeshe Chama ambacho hakina Wasanii Africa maana kwa Tanzania utasema nimekupa uwanja mdogo.
ni jambo zuri sana ukweli kujulikana, mara zote hapa jukwaani tumekua tukisema hiki chama kimejaa wasanii tumekua tukiambulia matusi toka kwa members haya sasa oneni uoza huu
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom