Mimi nadhani ni muhimu kwanza tuweke vipaumbele vikuu vitano halafu ndio tupime viongozi kutokana na misimamo yao juu ya vipaumbele vyetu kama wananchi;
1. Maadili ya uongozi, hasa ufisadi - jinsi gani atatatua tatizo lililopo sasa;
2. Muungano (mfumo unaotufaa...)
3. Katiba (msimamo juu ya nini kiwemo na nini kisiwemo, na kwanini...)
4. Itikadi Na Dira ya Nchi (Ubepari? Ujamaa? Mwananchi wa kawaida, hasa vijijini maisha yake yataboreshwa vipi...)
5. Sera ya mambo ya nje - Je, sera yetu ni ipi? Baada ya mwalimu kuondoka, hatuna sera zaidi ya kusafiri safiri na kwenda kutengeneza marafiki; Ni muhimu tukatazama (Mahusiano na WTO, WorldBank na IMF na jinsi gani atapigania tufaidike zaidi na bila upendeleo kwenye biashara ya kimataifa - (hivi sasa viongozi wetu wakisafiri nje hawaendi kupigania maslahi ya wakulima na kutafuta bei nzuri bali kwenda kula tu posho za vikao, shopping...),jinsi gani atatatua tatizo la madeni, jinsi gani ataimarisha economic diplomacy - na nchi gani na kwanini? Role of China, USA, Iran, Brazil, tofauti na sasa ambapo tumekuwa ni shamba la bibi,dampo la biadhaa duni za nje, uwanja wa kujaribia sera za kukuza uchumi...n.k
Tukiwapima wagombea wote kwa vigezo kama hivi na vingine vingi tu, ndio tutajua iwapo tumepata RAIS BORA au tumepata BORA RAIS
Otherwise Tundu Lissu for President? Nitakuwa mstari wa mbele kwenye kampeni kumpigania;