Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Mimi kelo yangu uuzwaji wa madawa ya kelevya Sinza makabulini. Kuna mama mmoja anaitwa MAMA DOMI huyu mama anauza madawa mchana kweupe, akiripotiwa hukamatwa na polisi baada ya masaa mawili utamkuta mtaani kama kawa. Vijana wadogo wameharibika kweli, iliwapate madawa sometimes inabidi wajiingize kwenye uvibaka, wakipora au kukwapua wanapokosa wa kummuuzia utakuta wanabadilisha vitu vya wizi na madawa kwa huyu mama. Ukiibiwa kitu ukiwahi kwa huyu mama utakuta vitu vyako anasema kanunua, akipelekwa polisi kijitonyama anaachiwa faster. Kila polisi anamjua pale. Huyu mama sijui na ajenti wa kuuza madawa ya nani kwani inaonekana ni kigogo kwani simu tuu inatosha kumtoa huyu mama polisi na kufuta kesi. My take huyu mama anaweza kuonyesha mtandao wa madawa ya kulevya.
 
Tozo Daraja la Nyerere ni kero nyingine, Kwanini kupita darajani iwe gharama sawa au zaidi ya kivuko ambacho kinatumia mafuta,kinafanyiwa service ya mara kwa mara pamoja na kubadilisha spare chakavu? Mmepunguzia wananchi matatizo kwa kuwaongezea gharama za maisha!

umenena mkuu

inamaana kila unapopita ndo unalipia au ni kwa siku?
je bodaboda akipita mra kumi inakuwaje hapo?
badala ya kupunguza kero wameongezea kero nyingine mpyaaa...
 
Kero kubwa ni kwamba nchi imekuwa adui kwa wananchi...
1. Wafanya Biashara wadogo, wa kati na wakubwa wananyanyaswa bila msingi
2. Nchi imekuwa ya kijeshi badala ya kuhimarisha demokrasia
3. Uhuru wa kutoa maoni umefinywa sana na kupata habari imekuwa vigumu sana
4. Serikali inaendelea kutumia nguvu kubwa kudhibiti Uhuru wa wananchi...
 
Tanesco tabata liwiti ni kero kero kero. Wanawaambia wateja waje saa mojs na nusu siku ya jmamosi. Wao wanafika saa nne!! Wanatupotezea muda kwa nini? Rais tumbua majipu haya. Wanafanya kazi kwa mazoea
 
Kwa heshima na taadhima nakukubushia mkuu wetu wa nchi tunaomba kujua juu ya hatima ya mabehewa yale aliyo ya simamia Mwakyembe na kujitapa kuwa ni ya kisasa lakini mwisho wa siku tukaambiwa kuwa hayafai, Mh rais unasubiri nini kutumbua hilo jipu?
 
Rais John Magufuli amejinadi na ametekeleza ahadi yake ya kutumbua majibu ili kuboresha utendaji katika utumishi wa umma jambo ambalo ni jema.

DAWASCO ina jukumu la kusambaza maji safi na kuondoa maji taka Dar na Pwani, cha kushangaza sehemu kubwa ya miji haina maji japo kuna mipango mingi ya kuhakikisha maji yanawafikia watu wengi.

Shida yangu ni kuwa maji mengi sana yanapotea kwa kumwagika barabarani karibu kila kona ya mji. Huku mbweni kiasi kikubwa mno cha maji kinamwagika barabara ya kwenda ndege beach nimewapigia DAWASCO zaidi ya mara mbili na wanakuja lakini ni karibu mwezi mzima hawafanyi chochote.

Sasa unajiuliza kama DAWASCO wanatumia fedha kupump maji hayaendi kwa wateja yanapotea huku yakiaribu miundombinu kwa nini hawatumbuliwi?

Magufuli tupia jicho dawasco ni jipu linaloitaji huduma ya dharura
 
Rais John Magufuli amejinadi na ametekeleza ahadi yake ya kutumbua majibu ili kuboresha utendaji katika utumishi wa umma jambo ambalo ni jema.

DAWASCO ina jukumu la kusambaza maji safi na kuondoa maji taka Dar na Pwani, cha kushangaza sehemu kubwa ya miji haina maji japo kuna mipango mingi ya kuhakikisha maji yanawafikia watu wengi.

Shida yangu ni kuwa maji mengi sana yanapotea kwa kumwagika barabarani karibu kila kona ya mji. Huku mbweni kiasi kikubwa mno cha maji kinamwagika barabara ya kwenda ndege beach nimewapigia DAWASCO zaidi ya mara mbili na wanakuja lakini ni karibu mwezi mzima hawafanyi chochote.

Sasa unajiuliza kama DAWASCO wanatumia fedha kupump maji hayaendi kwa wateja yanapotea huku yakiaribu miundombinu kwa nini hawatumbuliwi?

Magufuli tupia jicho dawasco ni jipu linaloitaji huduma ya dharura
DAWASCO ni jipu si utani, huku mitaa ya tegeta na boko utakuta bomba zimepasuka maji yanatiririka Dawasco wanapita na Bajaj zao utafikiri lile suala linawahusu Tanesco au Idara ya Uhamiaji.

Kuna sehemu nyingine watu wanabishana kama pale pana chemchem au kuna bomba limepasuka maana hata msimu wa mvua ukipita madimbwi hayaaishi.

Lingine kuhusu bili hewa....kuna nyumba Sinza ililetwa bili ya Zaidi lakini na nusu kwa mwezi wakati wastani wa bili ulikuwa takribani 15,000 kwa mwezi. Dawasco wakaandikiwa barua hawakuwa na majibu hivyo tunavyoongea ile nyumba maji yanatoka na Dawasco hawapeleki tena bili hivyo kuna nini Dawasco huko...?
 
Uchimbaji wa mchanga katika mto nyakasangu mbweni imekuwa kero sugu ambayo imewashinda polisi, manispaa ya kinondoni, NEMC na vyombo vingine vya ulinzi na usalama.

Mto huu ni moja ya maeneo yaliyopigwa marufuku kuchimba mchanga lakini malori yanachukua mchanga, katika kufuatilia tumegundua huu ni mradi wa polisi wa wazo, maafisa wa NEMC, maafisa wa manispaa ya kinondoni, diwani na mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa dovya.

Namuomba mkuu wa mkoa mheshimiwa Makonda na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni washughulikie jambo hili maana bonde la mto linapanuka na kuathiri kwa kiwango kikubwa mazingira ya wakazi wa boko na Mbweni huku Polisi wa wazo wakifanya huu ni mradi wa kujipatia kipato.

Ni vyema sasa adha hii ikapata ufumbuzi wa kudumu nina imani Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya wakiwa ni vijana wanaweza kabisa kumaliza hii kero kwa kuwatumbua wahusika wote katika mtandao haramu wa kujipatia fedha kwa uharibifu mkubwa wa mazingira.

Karibu Makonda, karibu Hapi mtumbue mijipu pale polisi wazo, NEMC na Manispaa ya Kinondoni sisi tupone.
 
Big up JPM.

Jipu lililo Iva hili hapa AJIRA ZA VIHIYO, alikimbia mauaji ya kimball Rwanda inasemekana na yeye alihusika akapokelewa kambi mojawapo ya muda karagwe mkoani kagera, akiwa elimu ya msingi. Kambini aka pewa uhudumu kwenye zahanati ya kambi. Ma kambi yalipovunjwa akakwepa kurudishwa kwao.

Kwa hofu ya kujumuishwa kwenye kesi za mauaji akabadili jina toka Jina lake la awali la Gasana HaleliMana na kujiita Emily Bugingo. Alishikia na hospitali ya Jimbo Katoliki Rulenge kama muuguzi na Kuoa mke binti wa kihaya mwenye Asili ya Rwanda lakini baada ya kudaiwa vyeti na kuhoji kuhusu uhalali wake alimbia kwenda sehemu asikoweza kufahamika akainumua vyeti na kujifanya Tabibu na hivi sasa ameajiriwa na halmashauri ya Mkulanga.

Hajawahi kusomea uuguzi wala utabibu, aliwahi kufanya kama mchanga wa macho feki na hata cheti alichonacho alikwenda kununua ifakala, anaweza kuwa mtu hatari lakini kwa kwa kufanya kazi bila utaalamu anajatarisja maisha ya watu wetu.

Wahamiaji haramu hawako Kagera tena Dar ndo kichaka. Wengi wao ni vihiyo na wanamtumia udaifu wa rushwa kwa maafisa wetu wa uhamiaji kuishi nchini. Wasije wakatuletea zahma.

Mtajwa juu alikwisha fuata na maafisa wa uhamiaji lakini wakazimwa lakini kwa JPM watatapika nyonyo.
 
JIPU NILILO NALO MIMI NI ASKALI POLISI KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI MKOANI MBEYA, NJIA YA KUTOKEA MBEYA MJINI KUELEKEA CHUNYA. WAMEKUWA WAKIKUSANYA SHIRINGI 5000 KWA KILA GARI INAYO PITA NA KILA KITUO AMBACHO TRAFIKI HAO WANASIMAMA.

KUTOKEA MBEYA MJINI KUNA VITUO VINNE, YAANI ISANGA, KAWETELE VIPO VITUO VIWILI, LAKINI PIA CHUNYA MJINI KWENYE KIBAO CHA KUINGIA SHULE YA MSINGI. TABIA HI NIMEKUWA NIKIOBSERVE TOKEA MWAKA JANA NILIPO ANZA SHUGHULIZANGU HUKU CHUNYA MATUNDASI, NA MPAKA LEO HII NAMALIZA SHUGHULI ZANGU NA KUPANGA KURUDI DAR.

NINGEPENDA SERIKALI WAIFANYIE KAZI, KWASABABU HUU NI WIZI WA WAZIWAZI, USIIONE 5000 NI NDOGO, KWA SIKU GARI MOJA YA ABIRIA HUPITA MARA TANO, ZILE ZA CHUNYA MJINI, LAKINI ZA MAKONGOROSI MARA TATU YAANI KWENDA NA KURUDI, ZILE ZA ISANGAWANA MARA TATU MPAKA NNE NA ZA ITUMBI MARA TATU MPAKA NNE, MAGARI YOTE NI TAKRIBANI 16, KWA ROUTS ZOTE.

ACHA ZINGINE MAGARI MAKUBWA YA MIZIGO, YANAYO PELEKA MIGODINI AMBAZO HUTOLEA KUANZIA 20,00 MPAKA 50,000, WAKIPATA SABABU YA KUMSIMAMISHA, ZIPO GARI ZA TUMBAKU PIA HUTOLEWA PESA, NA ZILE ZA KUBEBA WATU WA MINADA.
 
Kama atapita hapa mwambie namkubali sana. Ila pia mchakato wa ajira aufanye haraka haraka tumechoka kukaa mtaani
 
Mkuu, kero zipo za kutosha.

Kero yangu ya kwanza ni ufisadi wa Lugumi ambao CCM wameamua kuufumbia macho kwa kuwa kampuni iliyofanya ufisadi huo inamilikiwa na kada wao (Kitwanga).
 
Jipu kuntu... lipo katika kiwanda cha kuzalisha umeme Kiwira Coal Mines - Ileje, Mbeya...

Wafanyakazi hawajalipwa mafao yao toka 2004, hatma yao haijulkani had leo.. wanaishia kudanganywa kila leo.
 
Majipu mengine...ni kufanya taratibu za manunuzi, ama madai juu ya haki yako unaipataje kuwa siri kwenye taasisi za umma.

Ukienda kwa HR anakuzubaisha, hoo tunafuatilia ...mfano ni vyuo vikuu na vyuo vya kati. Taratibu hizi ziwekwe wazi.
 
Mh. Rais ipo mifano mingi tu hasahasa kwenye mifuko ya jamii wamewekana ndungu wa viongozi wa mifuko hiyo na watoto wa vigogo wengine hawana hata shahada ndio unakuta wakuu wa vitengo.

Naomba umulike huko ili usaili uwe huru na wa haki unakuta kunafanyika usaili mara mbili kabla ya usaili wa ana kwa ana hawazingatii kuna watu wametoka mikoani huku majibu wamepeana tusaidie kwa hili.

Asante
 
Mh. Rais, idara ya Hazina iliyopo chini ya Wizara ya Fedha kuna mtu huwa anapereka orodha ndefu ya majina ya watumishi walio stafu pale NMB makao makuu.

Katika orodha hiyo huwa NMB inapokelewa na kijana K, huyo kijana kazi yake ni kuangalia kama majina aliyopewa pamoja na fedha hizo alizopewa za watumishi hao walikopa pale na kama walikopa walilipa au bado, kumbuka Hazina huwa inapeleka na fedha.

Katika orodha iendayo NMB, Rais Magufuli kuna watu walikuwa watumishi walishakufa, na akaunti zao zilishafungwa zamani, hizi fedha, fuatilia muvi toleo lijalo.

Ila kwa ufupi kuna washikaji huwa wanawatafuta vijana mitahani na kuwapa maijna hayo na kuwambia watenegeze document na kwenda kufungua akaunti pale, sikufichi, huuuu mchezo watu kibao wanapiga pesa na haujaanza leo, ulianza tangu enzi hizo za wazee wa Africa Mashariki.

Baada ya mtu kufunguliwa akaunti uingiziwa mamilioni ya fedha na kuchapa lapa.

Kama wanibishia omba orodha iliyoperekwa hapo, NMB makao makuu, wape vijana waanze kufuatilia utajua jinsi gani nchi hii imekosa wazalendo watu wanaiba mpaka mali za marehemu.

Mimi ni tifufuuuuuuuuuuuuuuuu!
 
Kupiga pesa ni rahisi sana kuna walimu wanaongezewaga interest na mikopo pamoja na posts za chini kama masijala wachemsha chai walinzi dah nawaoneaga huruma.

Hawa tawgulu ndio usiseme.
 
Back
Top Bottom