Tofauti kati ya maneno haya.

presenter

Member
Nov 27, 2013
69
22
Habari za wakati huu wana jukwaa? Nina jambo linanitatiza kidogo wana jukwaa ninaomba msaada wenu ili niondoe mkanganyiko huu kichwani. Hivi kuna tofauti gani kati ya kulala na kusinzia? Nategemea majibu yenu wanajukwaa. Nawatakia jioni njema.
 
...kulala ni kujinyoosha kwenye mahali bapa au panapofanana na hapo wakati kusinzia ni matokeo ya usingizi. Unaweza kusinzia wakati umesimama,unaendesha gari hata wakati unakula. Ila mara nyingi mtu anayesinzia hupenda kulala ili asinzie vizuri...
 
...kulala ni kujinyoosha kwenye mahali bapa au panapofanana na hapo wakati kusinzia ni matokeo ya usingizi. Unaweza kusinzia wakati umesimama,unaendesha gari hata wakati unakula. Ila mara nyingi mtu anayesinzia hupenda kulala ili asinzie vizuri...

Ahsante kwa maelezo yako....
 
kulala ni nusu kufa na kusinzia do cha kuashiria kuwa mtu anataka kalala ni hayo tu
na kusinzia ndio kunaanza alafu kkulala ndio kuna fuata
 
Mi naona kulala ni kitendo cha kuuweka mwili sehemu bapa na kusinzia ni kitendo cha kupoteza fahamu kwa muda bila kupata mshtuko. Na inategemea kipi kinaweza kuanza, mfano mwingine anaweza kusinzia kwenye kochi akaenda kulala kitandani na akasinzia. Mwingine anaweza kulala kwanza na akawa anaongea baadae akasinzia
 
Mi naona kulala ni kitendo cha kuuweka mwili sehemu bapa na kusinzia ni kitendo cha kupoteza fahamu kwa muda bila kupata mshtuko. Na inategemea kipi kinaweza kuanza, mfano mwingine anaweza kusinzia kwenye kochi akaenda kulala kitandani na akasinzia. Mwingine anaweza kulala kwanza na akawa anaongea baadae akasinzia

Nikuulize swali hili ndugu...je mtu ambaye anakuwa analala na kushtuka ndan ya muda mfupi na wakati mwingine huweza kusikia mambo yanayoendelea tutasema anafanya nn?
 
Back
Top Bottom