Timu kubwa hucheza kikubwa na timu inayocheza kibingwa hushinda mechi aijalishi imechezaje na katika mazingira yapi

Mtanzanias

JF-Expert Member
Jul 30, 2021
1,747
3,723
Nimeona yanga kwenye mechi ya coastal union nimejiridhisha kwamba msimu huu wamepania kufanya jambo ktk kuupigania ubingwa waliopoteza misimu 3 iliyopita, kuna kauli nazisikia zikisema yanga ilizidiwa umiliki wa mpira na coast lakini asiyeelewa ni kwamba yanga walikwenda mkwakwani wakijua ni pagumu na historia ya pale aikuwa upande wao ivyo walienda kwa taadhari zote kwa plani ya kucheza direct football na sio kuremba.

Kama ilivyozoeleka yanga kwa sasa wanaposess sana mpira lakini kocha nabi anapanga mbinu zake kulingana na timu anayocheza nayo au kiwanja anachochezea, Coastal union walikuwa wamebebeshwa mzigo mzito vichwani mwao kwanza ahadi ya milioni 50 pili presha ya mashabiki wao uwanjani ni vitu vilivyowavuruga Sana kisaikolojia ukizingatia walikuwa wanacheza na yanga ambayo imekuwa na mabadiliko makubwa ndani ya uwanja mpaka nje ya uwanja aikuwa yanga ile ya misimu 4 iliyopita.

Viashiria vya timu inayosaka ubingwa ni kushinda mechi ata Kama timu iyo imecheza vibaya, ata kama imekutana na timu ngumu kinachoangaliwa ni point 3 muhimu na hilo yanga wameshaanza kulionyesha bila shaka.

Ni vizuri timu zinazokwenda kucheza na yanga zikaheshimu ubora wake kwa sasa vinginevyo itaendelea kuvuna point na zile hadithi za kuhonga zitaendelea kwa wale wasiopenda kuukubali ukweli ya kuwa yanga ya sasa iko vizuri kiufundi na aina ya usajili walioufanya ni bab kubwa, inao wachezaji wanaoweza kuamua mechi mda wowote na dk yoyote, Iyo ni tabia ya timu inayocheza kibingwa!

NB: Hoja ujibiwa kwa hoja na sio viroja!
 
Yanga hatari ilikuwa ya mwinyi zahera ilikuwa hata dakika ya 90 wanaweza kusawazisha au kushinda mechi wakiwa na Ajibu pamoja na makambo na bado simba ilibeba ubingwa
Unataka kusema yanga hii ambayo ukibadilisha tu first eleven wanapoteana.
 
Yanga hatari ilikuwa ya mwinyi zahera ilikuwa hata dakika ya 90 wanaweza kusawazisha au kushinda mechi wakiwa na Ajibu pamoja na makambo na bado simba ilibeba ubingwa
Unataka kusema yanga hii ambayo ukibadilisha tu first eleven wanapoteana.
Ni mawazo yake yaheshimiwe, ya kwako siyo msahafu kwamba wewe ndo msemaji wa soka nchi hii ukishasema basi ndo ukweli.
 
Yanga hatari ilikuwa ya mwinyi zahera ilikuwa hata dakika ya 90 wanaweza kusawazisha au kushinda mechi wakiwa na Ajibu pamoja na makambo na bado simba ilibeba ubingwa
Unataka kusema yanga hii ambayo ukibadilisha tu first eleven wanapoteana.
Kama simba ndie aliyebeba ubingwa hatari ya hiyo yanga inakujaje?
 
Yanga hatari ilikuwa ya mwinyi zahera ilikuwa hata dakika ya 90 wanaweza kusawazisha au kushinda mechi wakiwa na Ajibu pamoja na makambo na bado simba ilibeba ubingwa
Unataka kusema yanga hii ambayo ukibadilisha tu first eleven wanapoteana.
We mwehu kweli wewe sio bure but ni mawazo yako unavyoona wewe pengine unalo jicho la tofauti, kwaiyo unataka kusema yanga ya mwinyi zahera ilikuwa na kikosi kipana na chenye quality prayers kuliko hiki cha sasa? Kwamba first eleven ikibadilika ya sasa yanga haipati matokeo ebu nitajie mechi moja ambayo yanga ilibadilisha first eleven na ikashindwa kupata matokeo
 
Umeelewa mada vizuri au ndo wale wale pipa na mfuniko, soma mada vizuri usikurupuke kuhalalisha maneno ya Rage wakati unazo akili timamu kabisa
mzee umeweka mada ijadiliwe au anashea takataka na Utopolo wenzio? nakuuliza Yanga ni bingwa wa kitu gani? acha kupayuka
 
Nimeona yanga kwenye mechi ya coastal union nimejiridhisha kwamba msimu huu wamepania kufanya jambo ktk kuupigania ubingwa waliopoteza misimu 3 iliyopita, kuna kauli nazisikia zikisema yanga ilizidiwa umiliki wa mpira na coast lakini asiyeelewa ni kwamba yanga walikwenda mkwakwani wakijua ni pagumu na historia ya pale aikuwa upande wao ivyo walienda kwa taadhari zote kwa plani ya kucheza direct football na sio kuremba.

Kama ilivyozoeleka yanga kwa sasa wanaposess sana mpira lakini kocha nabi anapanga mbinu zake kulingana na timu anayocheza nayo au kiwanja anachochezea, Coastal union walikuwa wamebebeshwa mzigo mzito vichwani mwao kwanza ahadi ya milioni 50 pili presha ya mashabiki wao uwanjani ni vitu vilivyowavuruga Sana kisaikolojia ukizingatia walikuwa wanacheza na yanga ambayo imekuwa na mabadiliko makubwa ndani ya uwanja mpaka nje ya uwanja aikuwa yanga ile ya misimu 4 iliyopita.

Viashiria vya timu inayosaka ubingwa ni kushinda mechi ata Kama timu iyo imecheza vibaya, ata kama imekutana na timu ngumu kinachoangaliwa ni point 3 muhimu na hilo yanga wameshaanza kulionyesha bila shaka.

Ni vizuri timu zinazokwenda kucheza na yanga zikaheshimu ubora wake kwa sasa vinginevyo itaendelea kuvuna point na zile hadithi za kuhonga zitaendelea kwa wale wasiopenda kuukubali ukweli ya kuwa yanga ya sasa iko vizuri kiufundi na aina ya usajili walioufanya ni bab kubwa, inao wachezaji wanaoweza kuamua mechi mda wowote na dk yoyote, Iyo ni tabia ya timu inayocheza kibingwa!

NB: Hoja ujibiwa kwa hoja na sio viroja!
Chukua Pepsi m- ntakurudishia hela yako tukikutana
 
mzee umeweka mada ijadiliwe au anashea takataka na Utopolo wenzio? nakuuliza Yanga ni bingwa wa kitu gani? acha kupayuka
Unaelewa maana ya kucheza kibingwa? Kucheza kibingwa ni kucheza kwa mamlaka ndani ya uwanja, wanacomand ushindi popote pale aijalishi wanakumbana na ugumu wa aina gani dhidi ya mpinzani na wanaamua mechi iyo ndo maana halisi ya kucheza kibingwa na sio tafsiri yako iyo unayoifikiria kichwani, ili uwe bingwa unatakiwa upate matokeo popote pale ata Kama ukicheza ovyo
 
Simba mabingwa
JamiiForums-723330518.jpg
 
Back
Top Bottom