Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,640
- 697,940
- Thread starter
- #61
Najaribu kukuelewa hapa lakini kuna ukakasi kwenye dhana nzima ya time travel hasa linapokuja suala la time synchronization between real time and fantasy time... I mean psychological time... Backward and future while at very present in a single live bodyTime travel ieleweke kama ni mawazo ya kufikirika ya kisayansi kwamba kusafiri kwa wakati kuna wezekana kwa mwili, ambapo jambo la teknolojia (chombo) linajitokeza kama nguzo muhimu. Maswala kama time na space (two different field), kwa vyovyote vile hayatenganishwi na wazo hili.
Jambo la msingi hapa kuelewa ni, kusafiri kwa wakati kimwili.
Time travel, licha kwamba ni suala la sayansi ya maumbile,lakini bado halionyeshi jinsi hiyo, itawezaje kudhibiti kifo?
Utata wake pia uko katika Space. Ukisoma utaona kuna space mbili: the first space time is slow and the second space time is faster. Je, ni vipi space moja haiwezi kuathiri nyingine kikani?
Time travel, hatahivyo haifafanui kivipi jinsi hiyo itazuia uharibifu wa mwili.
Hapo hapo, time travel inatupa kujiuliza: second field ni ipi?
Kifalsafa, time travel ina jibiwa kwa mtazamo huu: ETERNALISM, POSSIBILISM and PRESENTISM.
Kimsingi, mitazamo yote inatazama time travel kama jambo la MIND. Suala la time travel lina dhihirika kwenye mindi. Uwezekano au uwepo wake, ni kuliko pekee kwa Akili kwa sasa.
Time ndiyo hoja kuu kwenye mtazamo wa kifalsafa. Kwenye mind kuna time pia kwenye physical kuna time.
It is possible kwa mind to travel back while you are present vile vile inawezekana kwa mind to travel the future in time.
Je, time travel ina funua "ufufuko"?
Mtazamo wangu unazingatia ukweli wenyewe wa ufufuko pia ukweli wa mambo yanavyojifunua kwa nyakati mbalimbali. Hapa nataka kusema, sayansi haipaswi kupuuzwa hata kidogo, pamoja na kwamba inashughulika kutafuta kweli za maumbile, kwani ndiyo kwa yenyewe imethibitisha mambo yaliyo nje ya akili ya mwanadamu.
Ukweli ni kwamba maarifa ya sayansi, hakuna namna tunaweza kuwa nao, pasipo Mungu Mwenyewe. Kwa sababu hiyo, sayansi inakuwa maarifa muhimu yanayobainisha ufunuo wa Mungu; ingawa kwa kupapasa, mambo yapitayo akili ya mwanadamu.
Kwamba mwili mmoja katikati ya wakati halisi je unawezaje kusafiri kifikra hata kama ni ndotoni na Kuishi miaka kenda nyuma ama kuutangulia wakati na kufanya prediction ya yajayo? Nadhani unaipata point yangu hapa