Time Heist and Time Apocalypse: Jinsi muda unavyoathiri Maisha ya ulimwengu na vilivyomo

Yeah.. 2Peter .5

Ah Safi sana.

Mara nyingine kwenye mashauri ya 'vitabu' vya dini kuna madini mazuri sana. Tushukuru...

===
2 Petro 1

1 Simoni Petro, mtumwa na mtume wa Yesu Kristo, kwa wale waliopata imani moja na sisi, yenye thamani, katika hali ya Mungu wetu, na Mwokozi Yesu Kristo.
2 Neema na iwe kwenu na amani iongezwe katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu.
3 Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.
4 Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa.
5 Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, na katika wema wenu maarifa,
6 na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu saburi, na katika saburi yenu utauwa,
7 na katika utauwa wenu upendano wa ndugu, na katika upendano wa ndugu, upendo.
8 Maana mambo hayo yakiwa kwenu na kujaa tele, yawafanya ninyi kuwa si wavivu wala si watu wasio na matunda, kwa kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.
9 Maana yeye asiyekuwa na hayo ni kipofu, hawezi kuona vitu vilivyo mbali, amesahau kule kutakaswa dhambi zake za zamani.
10 Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.
11 Maana hivi mtaruzukiwa kwa ukarimu kuingia katika ufalme wa milele wa Bwana wetu, Mwokozi wetu Yesu Kristo.
12 Kwa hiyo nitakuwa tayari kuwakumbusha hayo siku zote, ijapokuwa mnayajua na kuthibitishwa katika kweli mliyo nayo.
13 Nami naona ni haki, maadamu nipo mimi katika maskani hii, kuwaamsha kwa kuwakumbusha.

===

SURA 7

Arkelausi atawala mamlaka. Mariamu na Elizabeti pamoja na wana wao wapo Soani na wafundishwa na Elihu na Salome. Somo la Utangulizi la Elihu. Asimulia juu ya mfasiri.

Mwana wa Herode, Arkelausi, alitawala mamlaka yote katika Yerusalemu. Alikuwa ni mbinafsi, Mfalme mkatili, aliwaua wale wote wasiompa heshima yeye. 2 Aliita barazani wote wenye hekima zaidi juu ya watu na kuwauliza kuhusu mtoto mchanga mwenye kudaiwa kustahiki kiti cha ufalme wake. 3 Baraza likasema kwamba wote wawili Yohana na Yesu walikuwa wameshakufa; basi na yeye akaridhishwa. 4 Sasa Yosefu, Maria na Wana wao walikuwa chini katika Soani, na Yohana alikuwa na mama yake katika vilima vya Yudea. 5 Elihu na Salome wakawatuma wajumbe kuharakisha kuwatafuta Elizabeti na Yohana. Waliwapata nao wakawaleta wao Soani. 6 Sasa, Mariamu na Elizabeti walikuwa wakistaajabia sana kwa sababu ya kukombolewa kwao. 7 Elihu akasema, si ajabu, hakuna matokeo tu; kanuni hutawala kuendesha matukio yote. 8 Kutokea nyakati za nyuma sana ilishapangwa kwamba mtalikuja kuwa nasi, na katika shule hii yenye kutunzwa kusudio safi ili kufundishwa. 9 Elihu na Salome wakawachukua Mariamu na Elizabeti nje kwenye ua takatifu karibu na pale ambako wao walikuwa na desturi kufundisha. 10 Elihu akawaambia Mariamu na Elizabeti, mwaweza kujionelea furaha ninyi wenyewe mmebarikiwa mara tatu, kwa kuwa ninyi ni mama wateule wa wana walioahadiwa kipindi kirefu, 11 Wao ambao ilivyopangwa kuwekewa mkono kuja kuweka mwamba mgumu imara msingi jiwe wa uhakika ambao juu yake hekalu la mtu kamilifu litasimama--hekalu ambalo halitaweza kamwe kubomolewa. 12 Twauhesabu wakati kwa mizunguko ya zama za vipindi, na lango kwa kila zama twasema akilini ya kuwa ni jiwe la maili katika safari ya kundi la watu wa sifa ya namna moja. 13 Zama zimepita; lango kuelekea kwenye zama ingine lafunguka wazi katika kugusa kwa wakati. Hii ni zama ya maandalizi ya nafsi roho, ufalme wa Imanueli, wa Mungu katika mtu; 14 Na hawa, wana wenu, watakuwa ni wa kwanza kueleza habari, na kuhubiri injili ya mapenzi mema kwa watu, na amani duniani. 15 Kazi kubwa ni yao; kwa kuwa watu wa miili ya nyama hawataki Nuru, wao walipenda giza, na pale ambapo nuru yang'ara gizani wao hawaitambui. 16 Twawaita hawa wana, Wafunuaji wa mwanga; lakini inawapasa kuwa na nuru kabla ya wao kuweza kufunua nuru. 17 Na yawalazimu kuwafundisha wana wenu, na kuzitia moto nafsi-roho zao kwa upendo na msisimko mtakatifu, na kuwafanya wao kuwa macho fahamuni na mpango wao mahsusi kwa wana za watu. 18 Wafundisheni kwamba Mungu na Mwanadamu ni moja; ila kwamba kupitia mawazo ya mwili wa nyama na maneno na matendo, mwanadamu hujirarua mwenyewe mbali na Mungu; kujishusha hadhi yeye mwenyewe. 19 Fundisheni ya kwamba Pumzi Takatifu italiwafanya wao moja tena, kurejesha hali ya kwenda kwa utangamano; 20 Kwamba hakuna chochote chenye kuweza kuwafanya moja ila Upendo; kwamba Mungu ameupenda sana ulimwengu hata kumvika mwana wake katika nyama ili kwamba mwanadamu aweze kutambua. 21 Mwokozi pekee wa ulimwengu ni upendo, na Yesu, mwana wa Mariamu, aja kudhahirisha pendo hilo kwa watu. 22 Sasa, pendo haliwezi kudhahirika mpaka njia yake iandaliwe, na hakuna chochote chenye kuweza kuivunjilia mbali miamba na kuangusha chini vilima vilivyo kwea juu sana na kujazia juu mabonde, na hivyo kutayarisha njia, ila usafi wa moyo. 23 Lakini usafi wa moyo katika maisha wanadamu hawatambui; na hivyo, huo, pia, waja katika mwili wa nyama. 24 Nawe Elizabeti, umebarikiwa kwa kuwa mwana wako ni Usafi wa moyo kufanyika nyama, na yeye ataifanya njia kwa Pendo. 25 Zama hii itatambua ila kidogo tu juu ya kazi ya Usafi wa Moyo na Upendo; lakini hakuna neno limepotea, kwa kuwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Mungu ingizo lafanyika kwa kila wazo, na neno, na tendo; 26 Na pale ambapo ulimwengu u tayari kupokea, lo, Mungu atamtuma mjumbe kufungua kitabu na kunakili kutoka kwenye kurasa zake zilizohifadhika patakatifu ujumbe wote wa Usafi wa Moyo na Upendo. 27 Na kisha tena kila mtu wa juu ya nchi atayasoma maneno ya uhai katika lugha ya nchi yake ya kuzaliwa, na wanadamu wataiona nuru, kutembea katika nuru na kuwa nuru. 28 Na mwanadamu tena atakuwa mmoja na Mungu.
===

Yakushahibiana na haya zaidi hi haya hapa (kiungo).
 
View attachment 1432660
(Picha ikionyesha Warmhole na Nyota mbalimbali)

Salute Comrades.
Kwa references ya vitabu vya imani za dini mbalimbali zinasema kua hapo zamani Mungu aliumba ulimwengu, akaumba vyote vilivyomo ndani ya siku sita. Upande wa tafiti za kisayansi zinasema kua hapo zamani miaka billion kadhaa iliyopita kulitokea mlipuko mkubwa huko angani ambao wanauita The big Bang, mlipuko huo ulipelekea kutengenezwa kwa sayari na kuleta uhai wa viumbe mbalimbali kwenye sayari hizo (Earth) kupitia Evolution. Mimi ni muamini sio mwanasayansi, hivyo mada yangu itaegemea kwenye imani kwa kiasi Fulani.

Inasemekana Mungu aliumba kila kitu ndani ya siku sita tu na kukabidhi yote aliyoyaumba mikononi mwa mawanadamu (Kiumbe wake pendwa zaidi). Moja kati ya vitu ambavyo vitabu vya imani havielezi kama viliumbwa na Mungu ni MUDA, hakuna sehemu yoyote utakuta wameeleza muda uliumbwa, lakini logically muda uliumbwa.

Fundamental physical quantinty inasema kwamba SI-unit ya muda ni Second, minute,year,months etc. Ili muda uwepo inatakiwa kuwe na solar system, katika soler system sayari zinazunguka jua..zinapozunguka jua tunapata matokeo ya musiku na mchana. Katika usiku na mchana huo ndio tunaweza hesabu sekunde,dakika mwezi au mwaka. Jua ndio linasababisha ruweze kuhesabu muda au tuseme kwamba ndio inafanya existence ya muda. Since jua likizima basi muda utapotea pia uhai wa viumbe vilivyopo kwenye dunia unaweza kuwa extincted/toweka. Jua limepewa dhamana ya kushikilia uhai wa viumbe vilivyopo kwenye sayari hizi (Earth), ndio maana baadhi ya jamii huabudu Jua wakiamini ni Mungu,wengine huenda mbali zaidi wakisema kua hallo ambazo zimechorwa kwenye picha ya yesu ni jua..Hallo ni dura ambalo lipo juu ya kichwa cha picha ya yesu ikimaanisha “Aliye mtakatifu”

...

Labada itakupendeza kuyaakisi haya akilini.

Kutoka: Mwongozo Hai kuelekea Uhuru Halisi seh. III
5 Septemba 2011 saa 12:23 Asubuhi

Dunia hii ambayo Aristotle alilenga kuichunguza kwa kuitazama kwa macho haiwezekani kamwe kuona ‘siri za mbingu’ kama vile mti wenyewe usivyoweza kuonekana hata katika mbegu yake. Basi Hekima itaelekeza kuelewa utangamano wa dhahiriko na ‘Neno la Uzima’ kwa vitu vyote kwa jinsi ya kwamba, kukua na kuongezeka ndiyo amri ambayo kila chenye ‘chembe-nia’ ya ‘kuwa’ huja kutii ili kuchukua nafasi. Lakini katika sura hasa ya mwili wa kudhahirika hakuwezi kuwa na refu lisilo na ncha... Na hivi hili linaleta utanabaishaji wa namna moja juu ya amri hii na ustahimilishwaji wake. Vitu vyote hujitokeza kwa jinsi ya pumzi ya namna yake ambayo itadhahirisha ukiasi wake katika minajili ya kuchambua ‘ukuaji’ na ‘wakati’. Lakini kikubwa hasa katika kudhahirika si mwili wenyewe wenye kudhahirisha hayo mawili... Mti hukua toka kwenye mbegu hadi kuwa kima chake na si kukua mpaka kulifikia jua lenyewe. Pale kipindi chake cha mwili wa dhahiriko umefika tamati basi tayari kutakuwa na mbegu nyingi zilizotapanywa kungine ; kupitia mbegu hizo hamu yake ile ile inaweza kuhifadhika mwili na kukirimika kukua. Na hivyo hata kama chembe-nia imekuwa ni yenye ‘jinsi ya u-moja’ katika mkondo wa madhahirisho daima katika marefu na mapana yake kutafanyika kitovu cha mwendelezo zaidi wa mchezo ule ule na kutohitaji refu lisilo na mwisho katika mwili ule ule.

Na huo utakuwa ni mzunguko kwa safari iliyo ni ile ile.

Vile vile dalili ya kwamba safari zote ni mizizi iishiayo kwenye shina moja la ‘wakati’ ; zile safari zenye kupandizwa huku na kule katika jamvi la wakati pasipo kumaanisha ‘unyoofu wa wakati’ ila tu mseto wa yote yenye kuweza kuonekana/kudhahirika.

Hapa twastahili kujifunza shauri la kupanda na kushuka ; kwenda mbali na kurudi nyumbani.

Katika visa vitokenavyo na maisha ya Yesu kina kile kinachoongelea ‘siku arobaini’ za mfungo ‘jangwani’ na mashauri ya ndani ya Yesu katika kushukiwa na ‘roho wa ubatizo’ ; na hivi kukaa kwake pembeni ili kuitafari dhamira yake juu ya sura na sifa ya huduma iliyoihisi kuhitaji kuitekeleza ndani ya jamii yake. Kwani na baada ya hapo ndipo inapotajwa kuanza huduma yake ya kutangaza ‘habari njema’ kwa watu wote. Labda ni yeye mwenyewe aliyekujashuhudia hata yale aliyokuwa mioyoni mwake wakati akipitia hayo—kwa watu wengine ; ama ni mtu mwingine aliyekujahifadhi kisa fulani kwa mchanganyiko wa tukio halisi na mashauri yaendenayo na hilo tukio katika simulizi la kufundishia jambo fulani lihitajikalo kupokelewa na wanajamii katika vina mbali mbali. Kwa kuwa tunajua kwa miaka mingi hata baada ya Yesu kupotea katika ardhi ya Palestina, simulizi la visa na mafundisho yake yalikuwa bado kuandikwa rasmi ila tu kuwa ni mtindo wa makusanyiko wa mafundisho madogo madogo ya kurithishwa kwa masimulizi na nyaraka za barua miongoni mwa ule umma uliokuwa ukifuatisha huduma yake kwa mapana ya jamii zingine.

Na hivi hili ni kweli katika kisomo cha historia, watu wa siku za nyuma si walikuwa ni watunza kumbu kumbu la mtiririko sahili kabisa ila tu walikuwa na namna za uandishi ambazo zilikuwa zikichanganya ‘usahihi’ wa tukio na ushairi ; vile vile ushairi wa mafumbo, ishara za kukoreza hisia na mapambio katika simulizi. Hakukuwa na jinsi ya uandishi kama ulivyokatika ulimwengu wa leo wa habari na historia juu ya mtu, jambo ama tukio.

Mtu yeyote kwa mfano, anayedhani kisa cha ‘nyoka’ aliyeongea na mwanadamu ni kweli ya kihistoria huyo atakuwa anajichanganya mwenyewe... Hakuna kitu kama hicho kinachoweza kutokea katika hali ya kawaida ila tu kwa namna ya ishara ya ukweli fulani ifananayo na picha hiyo—inayoweza kuhifadhika katika simulizi la wahusika waliohaishwa na wengine waliobunika sura. Basi ni jinsi hiyo hiyo binadamu anatokea kwenye silika ya kupenda kuchanganya ukweli wa kimatukio na upambo wa kufikirika ili kupeleka mbele na kufikisha ujumbe kwa mwingine.

Siku za nyuma watu hawakuwa na utajiri wa vifaa vya kuandikia na kuhifadhia maandishi ama kufyatua nakala na hivyo uwezo wao ulikuwa na kikomo katika uadilifu wa ‘habari halisi’ juu ya mtu ama jambo. Ndicho hichi kikomo hasa kilichobidisha kutia ‘nakshi’ habari inayopaswa kubaki katika jamii ili kuwa na utamu na urembo vile pia kuvuta masikio na hisia ; na hivyo kufanya watu wepende kuvitunza visa vya kusimulika na kuvirithisha kwa wengine.

Hii pia inahusu visa vya mashujaa na miungu wa makabila.

Haya yalikuwa ni fasihi ya aina yake ni yenye kumulika ukuwakujia wa kiakili, sanaa na mawasiliano ya kijamii katika kuhifadhi ‘vihamba’ vyake vya maadili na busara yenye namna yake kheri katika kudumu kwa utamaduni wao.

Basi lile shauri la Yesu katika kuishi pekee ‘jangwani’ kunaleta simulizi la ‘majaribu matatu’ kwa Yesu toka kwa ‘Ibilisi’. Kukipangilia kisa ili kuleta maana bora ya uwezekano inaweza kusemwa hivi : Baada ya ‘Ubatizo’ wenye kusimulika pale Yordani, Yesu alifunguka fahamu kwa jinsi ya ‘Ufunuo’ wa jinsi ya rohoni na ulimteka sana akili kiasi cha kuhitaji kujitenga na watu na shughuli zao za kila siku ili apate kutafakari uingiliano wa ‘ufunuo’ huo na ‘ustawi’ wa jamii yake ikiwa kuna chochote chenye kuweza kufaa hasa. Jangwa si tu kumaanisha ukavu wa nchi na michanga, lakini ni kujitenga mbali kiakili hadi hali isiyo na msaada wowote kwa wakati na mahala kwa jinsi ya utumikivu wa mwili. Kudumu pale tu ambapo fahamu yatawala na mtu kujimulika yeye mwenyewe na hapo kabisa alipo.

Siku ‘arobaini’ si lazima iwe ni siku arobaini kwa jinsi ya hesabu ya kawaida. Arobaini ni mzingo wa mraba kwa jinsi ya pande za vizio vya kadri ya ukumi-ukumi vya urefu wa mapana yake—kama ilivyohesabu ya vidole vya miguu na mikono na ishara ya ukamilifu wa ncha zote za nia kwa kuuchora wakati kwa namna yake ya ndani ya mwanadamu. Kufunga ni ishara ya kujinyima mahitaji ya kawaida ya mwili na ili labda pia kuzijua siri zake kukutana ‘pumzi ya uzima’ isiyotokana na asili ya mwili wenyewe ila kukutana na mwili katika namna ya utangamano wa aina yake. Haya yote kutokea kwa yule mtu anayekirimika kujua ukweli wa kanuni za ‘kuishi kwa mwili’ na uweza wa nguvu wa pumzi isiyoonekana kwa macho na kuzitambua nguvu zake zenye kuhaisha na kutenda kazi kwa maajabu yake ya utangamanifu na ‘uumushaji’. Kwa mtu asiyekirimika ; hili limeleta utamaduni wa kuiga kufunga kwa minajili ya ‘toba’ ; ukirifu wa dhamira mbaya zitokanazo na tamaa ya mwili, mawazo mabaya na dhamira mbovu juu ya maisha ya mwanadamu mwenyewe kupitia kujitazama. Lakini katika mfano wa Yesu, hakuna ishara hasa ya ‘toba’ bali kuna ‘upimwaji’ wa dhamira yake juu ya mambo fulani na kusudi ‘vimvuli’ vya jinsi ya ‘mashauri ya juu’ ipate kutathminika na kujengewa ‘msimamo wa nia’ ya kuhudumia jamii ikiwa mashauri hayo ni mazito kuliko wastani wa kawaida wa watu kuelewa na kutangamanishia kazi—kama jinsi ilivyo katika hali ya kawaida wanadamu hawatambui hakika ya uwepo wa ‘pumzi ya uzima’ ila tu wakimaizi jinsi yake ya kudhahirika waitwavyo hiyo ni ‘pumzi ya uhai’ kwa mwili.

Basi katika kisa cha Yesu jangwani husemwa alijaribiwa na Ibilisi nayeye akamshinda huyo na hivi kuwa ni ‘mwokozi’ kwa wengine wote waliokatika ‘himaya’ ya Ibilisi kupitia huduma yake ‘kulishuhudia neno’ na habari njema. Na hivi tukague ‘majaribu’ na ‘Ibilisi’ katika muktadha mzima wa mambo na mtu mwenyewe.

Kutokana na kuchukulia masimulizi juu ya ‘mambo ya kiroho’ kwa juu juu ; watu wengi hudhani Ibilisi ama shetani ni nafsi iliyo nje na nia-utu wao. Hiyo si kweli. Ibilisi ni mtu mwenyewe na ‘kisogo’ cha dhamira yake. Wengine huchukulia visa vyote vya namna kama ile ya masimulizi ya vita ‘mbinguni’ vya malaika ‘wema’ na ‘wabaya’—wabaya kushindwa na ‘kutupwa’ duniani ; kuwa ni tukio la ‘kihistoria’. Hiyo si kweli. Haijawahi kutokea hasa kwa mtiririko wa masimulizi. Ukweli ni kwamba vita hivyo haina mahala pa jana, wala kesho kwa kuwa vita hiyo ipo hapa na sasa. Na hili halina budi kudadavuliwa fumbo lake.

Uzima wa milele ni ‘Kweli’ iliyopo na hali isiyoshikwa na ‘wakati’ wowote. Madhahirisho yote yanachukua sura na hivyo ‘muda’ kubidi kutokea kujiazimu mbainisho wa ‘Kweli’ na ‘si Kweli’. Lakini hakuwezi kuwa na ‘si Kweli’ ila tu kwa kuwa inakirimika ‘ndani na nje’ ya ‘Kweli’. Vyote vinavyofanyika katika ‘usikweli’ hata ikitokea kuwa ni vilivyohaishwa vikijitambua kwa jinsi ya ‘wakati’ wake haviwezi kung’amua ‘Kweli’. Itokeapo kile kilichohaishwa katika ‘usikweli’ ‘kikataamulika’ kuwa moja na ‘Kweli’ hicho kinamaizi mara moja wakati wote si tu ni chochote ila ile ‘Kweli’ katika ukamilifu wake usiyogawanyika na wala kupotoka katika jinsi ya maonekano yote kama ‘sura ya wakati’ yaani madhahirisho na matukio. Na hivi jinsi yote ya viumbe vinavyofanyika katika madhahirisho kufungwa na kamba zake zenye kugundisha dhamira na utashi wa hivyo viumbe na ulimwengu wa madhahirisho yake. Bila ya hizo kamba ‘Usikweli’ hauwezi ‘kuishi’ ndani na nje ya ‘Kweli’.

Kisomo cha leo juu ya akili na fahamu ndicho kitasaidia kung’amua lugha za watu wa zamani katika kuzungumzia mashauri mbali mbali yenye kugusa moja kwa moja utabia ya mtu, imani, utambuzi, fahamu mbalali, fahamu jua, utofahamu kumbaizi, na ufahamu-jua kumbaizi. Kwa kuwa haya yote, kwa mtu, yana mapelekeo ya moja kwa moja kwa ishara za nidhamu ama mapepe, kuhangaika ama kutulia , ‘ugonjwa’ ama kuwa ‘sawa’.

Imani inamuunganisha mtu na ‘sura ya kheri’, utambuzi ni kitendo cha akili kwa wakati kumaizi uso wa jambo lilotwalo na fahamu za mwili, ama kumaizi jambo liletwalo na mawazo au fikra. Utambuzi hutokea katikati ya fahamu mbalali na fahamu jua—yaani ziwa la mawazo tuli ilivyomfano wa mbalamwezi iliyodakwa na maji kama ‘fahamu mbalali’ na hivyo fahamu jua kuwa ni mchemko wa mawazo mapya ambapo katika uso wake ndiyo mawazo mapya huzaliwa na kuwa ya moto kwa wakati halafu yakapoa na kwenda chini kwenye baridi.

Jamii inahitaji kisomo endelevu katika muktadha wa kutambua upana na kujifunza ili kutumia maarifa katika minajili ya taaluma za saikolojia ya kawaida na saikolojia ya paranomo. Miongoni mwa wanajamii wenye kuzungumza kiswahili ni hamu yangu maneno mbalimbali ya kiingereza yapate tafsiri ya moja kwa moja kutoka kwenye yale ya kiingereza ; iwe kwa kutohoa, ama labda kuweka tafsiri-mbinu. Hii itarahisisha kupanua haraka uwanja kwa visomo kwa kuwa maarifa katika lugha ya kiingereza yamepanuka sana na yanaendelea kupanuka kila kukicha. Na mimi nimetumia tafsiri-mbinu kama ‘fahamu mbalali’ kuwa sawa na ‘subconscious mind level/domain’, ‘fahamu jua’ kuwa kama ‘conscious mind level/activity’, ‘utambuzi’ kuwa kama ‘Cognition ; ~ Process’, ‘utofahamu kumbaizi’ kuwa kama ‘collective unconsciousness’. ‘Ufahamu jua kumbaizi’ kuwa kama ‘Superconscious/ness State of Mind’. Kuwa maneno haya yatawezesha kudadavua ilivyobora zaidi mashauri juu ya mtu, maumbile ya asili, habari na mawasiliano.

Haya hayakamiliki bila kisomo cha sibatenia ‘Cybernetics’ na saikolojia kwa jinsi uchanganuzi wa vitendo vya kiuchunguzi wakutoka nje. Lakini kwa namna ya uchunguzi kutoka ndani, sayansi haitanabahi hili hasa kwa sasa, lakini ni makusudi yangu umma wa waswahili waanze pia na jinsi hii ya uchunguzi katika mwili wa visomo vyake vyote vipasavyokuwepo na kwa manufaa yake. Kuwepo na uhifadhi wa mashauri na visomo kwa manufaa ya wengi.

Mtu anapochunguza ulimwengu toka ndani yake hujenga uelewa hata wa mambo yasiyothibitishika kwa mwingine ila tu kueleweka haraka au hata maramoja kwa mwingine aliyepita katika njia yenye kufanania ya kiuchunguzi. Ni kisomo hichi chenye kumulika mashauri ya Paranomo ‘Paranormal’ –ugutu wa hisia za fahamu hata nje ya jinsi mwili wa mtu ; na Uwimbiakili ‘Psychic’— kadri ya kuweza kuona mambo nje ya macho ya kawaida ama kushawishi/kushawishika na kupokea ‘picha’, ‘nia’ au ‘neno/fikra’ kwa jinsi ya akili na pasipo sura dhahiri ya kimaada. Kuwepo na uhifadhi wa mashauri na visomo kwa manufaa ya wengine pia wenye nia kupenyeza ndani zao.

Na binadamu anapokuwa na mwongozo bora huitengeneza njia kwa ajili ya ile ‘Hekima’ na kisomo chake toka hapo ni huwa ni chenye manufaa si kwa jinsi ya nje tu ila ya ndani pia. Kisomo cha leo kinamfaa mtu kwa jinsi ya nje lakini kikamwacha yeye maskini katika hazina ya utu wake. Na hivi haijalishi binadamu anakiri ama kutambua ‘udumavu’ wake katika hilo, kuelewa kanuni za mambo ya kiroho si ‘hiyari’ ni lazima kwa mwanadamu yeyote mwenyekutafuta kukirimu mengine na hali yeye ni mwenyewe kukirimiwa. Na kusudi pia ustawi wake upate kuinukia juu kuakisi chanuo kamili la ua katika kukatiza kwa kipindi cha muda uhitajikao.

Na hivi tutazame mtu, mdhahiriko wa nyakati za mtu na nafasi ya huo katika wakati mzima wa madhahirisho yote na hivyo wakati.

Kisa cha Yesu ‘jangwani’ kilikuwa ni mkato wa shauri zima kuhusu uakilifu na ‘mbegu’ zake za msukumo katika mtu ili kuchukua sura katika ustawi wa binadamu.

Jaribu la kwanza husimulika lilitokana na ‘njaa’. Aliposikia njaa Ibilisi akaja akamwambia mbona yeye ni mtu mwenye kufanyika uwezo sasa, maana anaweza kuyaambia mawe yageuke kuwa mkate nayo yakatii ‘neno’ lake, si afanye hivyo tu ? Tofauti na inavyochukulika juu juu, shauri la mkate ni lugha ya ishara kuhusu tabia za ‘utafunaji’ ili kushibisha matumbo kama mwenendo wa tabia moja inayoweza kumgeuza mtu kuwa ni mbinafsi. Yesu alipofunuka katika ufahamu wa kristo, baada ya ubatizo wa mto yordani, alingia katika ufahamu jua kumbaizi ; kwa jinsi hiyo aliweza kuona vitu vyote wa jinsi yake ya kuwa ni namna ya mitetemo katika ‘bahari’ ya madhahirisho yake. Alijua vivyo hivyo kila kadri ya kitetemo hushikilia hadhi ya usifa wa kitu na hivi mtu yeyote kutoka katika kina fulani cha utambuzi ndani ya fahamu kumbaizi akiweka nia ya mitetemo ya kitu chaguo lake katika macho ya kawaida ; kusudio ya hicho kubadilika, haraka madhahirisho ya umbo la kitu hubadilika kuitikia taswira ya akitakacho kwa ‘neno la lake’ ndani ya fahamu jua kumbaizi.

Ilikuwa ni fahamu ya jinsi ya akili ya kawaida na mashauri kutoka katika vina vya fahamu mbalali kuwa kwamba Yesu alipotuama kutoka kwenye vilele vya ufahamu wa juu ; alikumbuka njaa yake na kufikiria kama akili yake ya zamani ‘ilivyozoea’. Kwani ndiyo hiyo ilijifikirisha ikiwa kila kitu kinaweza ‘kujazwa pumzi’ kikabailika mitetemo hadhi na sura si anaweza tu hata kugeuza jiwe la pembeni ili kuwa mkate ili kuondoa njaa ? Lakini hapo hapo dhamira yake ya kheri hata katika fahamu jua yake ndiyo iliyomkumbusha hilo sio sahihi hasa. Kwa kuwa katika mpango mzima, kila dhahirisho lina nafasi yake na hivi si busara kwa kuwa mtu ni aliyetaamulika kujua siri za kubadilisha maumbo basi aende kufanya hivyo ili kujiridhisha hitaji lake kimwili. ‘Hekima’ ikamjia zaidi katika mashauri yake ya kwamba ikiwa kila kitu kinaweza kustahimilishwa na ‘pumzi ya uzima’ si ni hivyo hivyo na yeye aweza kustahilishwa kwa ndani pasipo kuhitaji kubadili jiwe kuwa mkate, kwa kuwa jinsi hiyo ingalikuwa ni tu mzunguko wa ubatili wa vitendo. Basi ndipo busara ilipomkaa Yesu kuzidi mashauri yake yote ya akili ya kawaida katika kuyatambua ‘matatizo’ ya mahitaji ya kimwili ; vile si busara kutosheleza kimoja kwa gharama ya kukibadili umbo kingine bila ridhaa yake. Kwa kuwa vitu vyote vina uhai wa aina yake katika mpango mzima hata kama macho ya kawaida hayang’amui hili. Na ndiyo jicho la staha—mara alipotambua hilo ‘akaomba’ hiyo pumzi kumkirimu, na ikiwa hivyo na njaa yake ikatokewa bila ya kutia chochote mdomoni.

Jaribio la pili husimulika kuchukuliwa kwa Yesu hadi kwenye ‘kinara cha hekalu’ halafu kuambiwa na Ibilisi atijupe chini kuthibitisha ufadhiliko wake kwa Mungu. Kuwa juu katika kinara cha hekalu ni ishara ya mtu kuwa katika mahala pa kutanabahi ukamilifu wa maadili yenye kuendana na kanuni za kiroho katika hali yake ya ‘kuinuliwa’. Katika kueleza mahusiano ya mambo ya ulimwengu wa kawaida na ule uliofichika, mambo ya dunia hutajwa ni ya chini na yale ya kiroho hutajwa ni ya juu. Mtu mwenye kuingia kutahamaki moja kwa moja mambo ya juu hutajwa ni mtu aliyeinuliwa katika ‘utukufu’ wa ile ‘Kweli’ na tena ndiyo fahari ya ‘Mbingu’—kwa kadri ya ukamilifu wake unavyoruhusu kukwea juu sana ilivyosawa na kusema kupenya ndani sana katika siri ya ‘Uzima’. Na hivyo kipande cha simulizi hili ni kielezi cha pale mtu aliyekatika ngazi za juu za utambuzi wa kiroho, dhamira ya utu-nia ya mazoea ya kinadamu hujakumshawishi kujaribu kuchepuka na ukweli wa kanuni anazotahamki dhidi ya zile kawaida ; lakini kwa mujibu wa kisa cha Yesu, alitambua hilo sio lazima kwani ulimwengu wa ‘kuinuliwa’ si wa mashaka na hivyo hakuna la kupimwa hasa kwa kulinganisha sura za mienendo yake ya hali. Na nguvu idhihirishayo kani mtuo kwa dunia, kuvivuta vitu vyote juu sura ya dunia kwenda chini, hainachochote cha ‘kujaribiwa’ kwa kanuni ya ‘kupea juu’ kujako na hali ya kuzama katika ‘hazina isiyokauka’ ya kiroho. Kwa kuwa kani mtuo ni ‘dhahiriko la wakati’ na angali watu si wenye kutambua hilo moja kwa moja ; ili kutunza na kuhifadhi vyote juu ya uso wa dunia kwa sura yake.

Ufunuo wa kiroho, japo humwingia mtu katika ‘vipindi vya muda’ mfupi ama mrefu, hii inaendana na uwezo wa mtu ‘kujikwatua’ toka hali moja ya ufahamu wa kawaida na kuingia katika ufahamu ulioinulika ; tena ndani ya vipindi hivyo dhana ya ‘wakati’ hupwaya kabisa shauri lake. Basi ‘kujitupa’ ili kuanguka chini ni ishara ya mmoja kushawishika kwa jinsi yake kujaribu kulazimishia matarajio kati ya ulimwengu wa wakati na ule usio wakati. Hii hutokeo pale mtu anapokuwa ni ‘mgeni’ wa kutahamaki ulimwengu upitao wakati, na hivi sehemu ya uakili wake yenye bado kujifunga na utu-nia wake kumshawishi kufikiri michakato ya mambo kwa mazoea yake ‘yalioandikwa’. Lakini mtu huyu mgeni yampasa kufanya chaguo kutoka katika ‘uchanga’ na ugeni hadi katika imani ya yote ya jinsi ya chini na ya juu na hivyo ‘Kweli/Mungu’. Kila linalotokea duniani kwa mapana yake yote ni kwa kheri ya vyote vya kwake ; lakini binadamu wenye ushawishi wa dhamira na utashi ndani ya nafsi zao, na katika upofu juu ya kuwepo kwa kanuni za ukamilifu wa juu katika ‘kinara cha hekalu’ ; wao hujikwaa na mambo ya dunia na kujichanganya wenyewe katika tafsiri za matokeo ya matendo yao ; ikiwa watashtukia kukumbuka siri za ‘kukwatuka’, wao watakuwa wana wa ‘Mungu’ wa vyote na hivyo wataweza kuinuliwa toka kwenye uharibifu hadi kwenye kheri halisi na kwa neema zake.

Jaribu la tatu la Ibilisi kwa Yesu husimulika habari ya yeye kupandishwa hadi juu kwenye kilele cha mlima na kuoneshwa miliki yote na fahari ya nchi ; halafu Ibilisi kumtaka Yesu amsujudie ili apate hivyo vyote kuwa mali yake. Katika kielezi hiki, ndiyo sura ya unafsi wa mtu huja ‘kutahinika’ katika kujichukulia kwake dhidi ya kumbukumbu na mapambo yake ndani ya nyakati. Ni jaribio katika uwanda wa uadilifu wa kimawazo, ambapo mtu ‘mgeni’ katika utaamuliko wa kiroho hupimika dhamira katika kile akionacho kustahili heshima ya nidhamu yake kiroho. Ikiwa kwa jinsi yoyote anapenda kujifunga na fahari za nchi na ‘kumbukumbu’ ya jina lake, basi yeye atakuwa amemuangukia Ibilisi ili kumuabudu, na yeye ataishi daima kukirimiwa kwa kiasi cha Ibilisi kuweza kumwongoza.

Katika hali ya kawaida watu huishi wakazaliana na kustawi. Jamii pana katika kilele cha jicho moja, huzaa dhamira ya mtu kuishi kutimiza ‘wajibu’ wake miongoni mwa wanajamii wake. Wanajamii wanajinsi yao ya kutambuana na kuheshimiana miongoni mwao. Kuwa mtu wa kaya, mume ama mke kuna heshima yake, watoto na mali ni ndoto ya uhakika kwa ustawi, miliki na urithi juu ya sura ya nchi. Kaya hukumbukwa kwa majina ya koo zao na heshima walizojijengea katika jamii yao pana. Binadamu huzaliwa na kufa, si chochote kati ya watoto wala nazo mali; ambavyo mtu hupita navyo katika mlango wa mauti. Na hivi ni sehemu tu ya mapenzi mema kwa vizazi, na tena kwa jinsi ya ukaribu wa damu, vizazi hurithishana urithi wao. Binadamu ainuapo macho yake juu humaizi jinsi yeye alivyo ni ‘mweupe’ na mtupu wa hazina ya kweli ; hili hujengea hofu kwake yeye ya utupu wa ubinadamu wake dhidi ya kadhia zake za maisha. Na hivi binadamu wa jinsi ya ndani kabisa ambapo hutafuta kujijengea ‘jina’ ambalo kwa hilo maisha ‘yatawakumbuka’. Jina hilo si chochote ila muakisiko wa fahari zote na maisha kama vile inavyoazimu ‘kujijua’ katika ulimwengu wa madhahirisho na wakati. Lakini ‘jina’ hilo huwa ndio kiegemeo cha jitihada zake zote dhidi ya majaliwa yake. Na vivyo hivyo, mwanadamu katika ‘kuinuliwa’ ndani ya ufahamu wa kristo ; adui wa mwisho kumkatalia mkataba naye ni nafsi yake yeye mwenyewe iendeshwayo na nafsi-roho yake na hali ni muakisiko uliopinduka sura na hadhi toka kwenye mbegu ya kweli yake ya milele. Kwa kuwa sura ile ile ambayo mtu huamini utu wake ulivyo na mipaka, yeye hawezi kumuona ‘mungu’ ila tu kwa jinsi hiyo hiyo na ‘kumuabudu’ kwake ni kutaka upendeleo katika majaliwa yake kwa kadri ya udhanifu wake.

Kwa hivyo kwa sehemu hii katika jaribio la tatu inaweza kufafanuliwa kuwa Yesu alikataa sehemu ya unafsi wake ambao ndiyo huwa ni msingi wa kutafuta jina na umaarufu miongoni mwa watu wa mataifa, na fahari zao zote, kwa jinsi zote ambazo binadamu hufanya kwa kushindana na saa za kusogea kwa mauti zao. Na kuanzia hapo kukiri Nia moja na ‘Kweli’ ambayo ni utumishi pale panapohitajika ; pasipo kuendeleza kulea ubatili na kujilisha upepo. Pia hapa ndipo tunajifunza juu ya nidhamu ya heshima kwa watu na wanajamii—Wake kwa waume na watoto ; pasipo misingi ya kutafuta ‘ukuu’, utawala na sifa za kawaida za watu wasiohisi mambo makuu yenye kuneemesha na kustahimilisha maisha yao.

Na ndiyo jinsi Yesu aliishi ni ‘Mfalme Mfilosofia’ miongoni mwa watu wale ambao hawakumtambua—maana tafsiri za wenyeji wake zilikuwa na mapokeo ya kutarajika kuja kwa ‘nabii kiongozi’ mkombozi na mwenyekuleta ‘mamlaka’ mapya ya wayahudi.

Husemwa baada ya kushinda majaribio hayo matatu Ibilisi alimwacha na halafu ‘malaika’ wakamchukua Yesu na kumhudumia. Na ndipo baada ya hapo alianza huduma yake kwa wanajamii wake akionesha uwezo mkubwa wa kuleta mashauri mapya na kufundisha. Akizungumza jinsi ya ‘kuingia’ katika ‘ufalme’ kwa uhitaji wa kujisafisha kwanza, kubatizwa kama ilivyoishara ya tendo la kuzamishwa kwenye maji na kuibuliwa lililofanywa na binamu yake Yohana ili kupata ‘jina’ jipya... Jina lakuwa ‘mwana wa mungu’ na vile Paulo alizungumza kuwa ni ‘Kiumbe Kipya’ na ‘Mtu Mpya’. Isivyo kama katika utumikivu mwingine wa maisha ya kila siku pamoja na uadilifu wake.

Basi tukague ishara za ‘maji’, ‘Ibilisi’, ‘Malaika’ na kitendo sanaa cha kupata jina jipya la kuingia ‘Ufalme wa Mbingu’.

Mafundisho yenye kuzidia mbali uelewa wa maumbile ya kawaida ya mtu na uzima ; huwa ndani ya kisomo cha kumuelewa mtu na hasa kule ‘alikochipukia’ na hivi ‘kuwepo’—yaani ndivyo tunaita hii leo ni Ontolojia. Mashauri ya ontolojia katika vizazi vya watu mbalimbali duniani, mara nyingi hufutikwa na lugha za ishara kuliko habari kamili. Ulimwengu wa leo ni ulimwengu wa habari na mashauri ya moja kwa moja katika ufundi na utumikishi wa taarifa/maarifa halisi katika wakati.

Ni kutokana na hili la wakati tulipo sasa lipo hitaji la kutafuta lugha mpya ambapo masimulizi yote ya kiontolojia yaliyopata kuwepo miongoni mwa mataifa na makabila ya wanadamu yatapata mahali pake pa kuelezwa na kuweza kufafanulika muktadha wake katika sura kamili ya mambo na mkunjuko wa wakati.

Hili linawezekana kupitia kisomo cha ‘Akitipu’ zenye kuongoza ramani za msukuko wa sura mbali mbali za michakato ya ukuaji na ustawi wa jamii katika kukatiza kwa vipindi maalum vya mng’amuliko fulani wa mzunguko kamili ya kuja na kuondoka kwa vilele vya ustawi wa wanadamu. Ingawa watu hudhani mambo yanayotekea ni mapya, pamoja na upya wake huwa kuna mtindo ambao madhahiriko yote kujifinyanga katika wakati.

Ndani ya madhahiriko yote kuna vichochezi vya sura ambayo hupelekea hata viumbe hai wenye utashi kama mwanadamu pamoja na mambo yao yote kuwa ndani ya vichochezi hivyo. Hivi huweza kuchukua sura ya kama hata dhamira ya mtu na kumbe ni sehemu tu ‘mpango mzima’ wa uzima wote hata kupitiliza ‘wakati’ wenyewe. Navyo ni sehemu ya uzima wote lakini kwa jinsi ya namna yake ya ajabu ; kuwa ni kama ‘mchanganyiko’ wa ukamilifu wa jinsi ya mafikara ya yote yenye kuwezekana(yasiyodhahiri kwa macho), yale yaliyokwisha kudhahirika na yale ambayo bado hayajadhahirika. Binadamu ni sehemu wa haya kwa mujibu na tena kadri ya alivyofanyika ndani yake kwa ‘ngozi za mifanyiko’ mbali mbali na pia ngazi mbali mbali za ufahamu na utambuzi kwa wakati katika kumfungamanishia yeye na hayo yote. Ndiyo haya hasa makutano ndani yake yahusishayoufahamu jua, fahamu mbalali na utofahamu kumbaizi.

Basi katika kisomo cha Akitipu tunajitahidi kutafuta kuujua ule ‘wavu’ uliotanda kote na kukokota misuko ya madhahirisho mbalimbali kutoka katika ‘bahari’ isiyoonekana ‘ya ukamilifu wa jinsi ya mafikara ya yote yenye kuwezekana’. Kwa kutumia akitipu tunatafuta kutambua tabia za watu na dalili za mienendo yao yote, kutokea na kupotea, kufumika ustawi na kutoweka kwake, mtandao wake wa nje na ule wa ndani wa mahusiano ya watu na uzima wao. Vivyo hivyo kwa Dunia, Nyota na vyote vyenye kuonekana katika udhahiri wa macho hata pia katika kaleidoskopi zake zote. Ni kama vile haswa kusemwa ‘jeometria ya wakati’ na uso wa maumbile yake.

Hayo tukijaribu ‘kuyaona’ yakichukua sura katika ‘bahari’ ya ‘uzima wa milele’ ; Nuru iangazayo yote na kufanya yote na hali hayo yote si chochote kubakia tu ile ‘Kweli’.

‘Ibilisi’ na ‘Malaika’ ni Akitipu. Binadamu hawezi kumaizi baadhi ya tabia za kufanyika matokeo ndani ya maisha yake ili kwa lugha ya akitipu zilizohuishwa. Hili linaweza kueleweka vizuri ikiwa mfanyiko wa ubongo wa binadamu unavyoweza kupenyezwa kisomo chake.

Binadamu ana ubongo uligawanyika katika pande mbili—ubongo wa kushoto na ubongo wa kulia. Japo kunamgawanyiko huu, kila pande ni jinsi ya kioo kabisa na mwingine. Jinsi hiyo pia inafanya kama vile isivyowezekana mkono wa kulia ukabadilishwa kuwekwa upande wa kushoto, kama hivyo hivyo kinyume chake.

Ubongo wa upande wa kulia kwa mfano huonekana kuwa ‘hai’ na vitendo vilivyokatika namna ya ‘picha’ na sura zote zenye kufanana na hivyo. Ubongo wa upande wa kushoto huonekana kuwa ‘hai’ na vitendo vya uchanganuzi na vitendo vya kufikiri. Kwa jinsi hiyo mazungumzo na kumbukumbu ni mchakato unaohusisha namna ya utangamano wa pande zote mbili za ubongo. Ukiondoa umahususi wa ubongo kama namna ya misokoto mirefu iliyojikunjamania ndani na hivi ‘kukoleza’ ukali kwa ‘fahamu’ zitokanazo na mikondo yote ya neva za fahamu katika usakiti wake. Kwa kawaida binadamu ana fahamu hai na tuli yaani zile ambazo kwa wakati anazitambua kuendelea katika mwili wake na zile asizozitambua na angali zipo.

Ngozi yote mwanadamu ina vipokezi vya taarifa ambavyo ni muhimu katika ‘kuhuisha’ utabia wa mtu dhidi ya mazingira yake. Vivyo hivyo huwa kwa fahamu zote tano. Kupitia ubongo ulioanzia katika uti wa mgongo fahamu zote za mwili wa mwanadamu huishia kunyongorotea mahala fulani katika ubongo uliokatika fuvu la kichwa. Sayansi hadi hii leo ni yenye kasumba ya kwamba ubongo ndiyo mashine kuu ya mwili yenye kuratibu kila kitu... Hii siyo lazima kuwa kweli ; kwa nje ni rahisi kudhani hivyo ila ikiwa mfanyiko wa mwili kuanzia katika seli moja hadi kuja kuwa muundiko wa mjumuiko wa seli nyingi katika mwili uliokomaa utazamamwa vizuri kunauwezekano wa kung’amua uhusiano wa ‘mishipa-sauti’ ya moyo na ‘kitovu-moto’ cha ubongo—hivi viwili ndivyo hufanya uzima wa mtu na viumbe vingine vyenye jinsi hii ya mfanyiko.

Kutoka kwenye ‘kitovu-moto’ cha ubongo mwanga-habari huwaka na kuangazia mwili wote taarifa za uwezekano wa kujisuka kwake na ubongo ndiyo mtandao wa kwanza kutumia tumia sehemu ya huo mwanga kusuka na kuratibu mienendo yote hata mwa mujibu wa ‘maandishi’ yalitungika na mwili wenyewe na tena yenye kuhama toka mwili mmoja hadi mwingine kwa jinsi ya matendo ya mwili kama kujamiiana. Ni ubongo huo huo pia ambao huweza kubadili taarifa za mwili kuwa mawazo na hisia na hivyo hivyo kubadili fikra kuwa nia kwa kufungua sakiti za kuamsha matendo ya mwili ambavyo mwili hutumika kama chombo cha kudhahiria nia fulani itokanayo na ‘mmiliki’ wa mwili wenyewe. Tofauti na inavyodhanika kwamba kitendo cha kufikiri hutokea kwenye ubongo, hiyo inaweza kuwa siyo kweli yenyewe hasa ; ubongo ni daraja lililo kama transmita na risiva ya mahala penye kuweza kuchakatisha mawazo. Na hapo hapo ubongo unaweza kuwa ni kama ‘lensi’ inayokusanya ukali wa mawimbi ya mawazo ili yang’amulike kwa jinsi ya ‘utambuzi’ wa kimwili—kama vile habari za kimwili kwa jinsi hiyo hiyo zaweza kuchakatuliwishia mawazo.

Ni nia yangu miongoni mwa wanajamii wa kitanzania kuwe na fikra za ziada na pana zaidi katika kuzidi kupanua kisomo kizima cha mwili, fahamu na utambuzi hata kupita yale mashauri ya kisayansi yaliyopokelewa pamoja na utokamilifu wake. Azma yangu ingalikuwa ni kusongesha mbele yale yaliyopokelewa kwa kisomo zaidi pale ambapo nafasi inaruhusu kwa mtu kufanya uchunguzi wa kina—katika mwelekeo wowote ule bila kuhofu mwelekeo usio wa kawaida wa mambo. Siku zote kuna ugumu kuvunjilia mbali mipaka, lakini hili halipaswi kuendekezwa daima. Watu wafanye visomo kwa faida binafsi na kwa faida ya wote. Isiwe tu kwamba mtu apaswa kufanya mambo kwa faida ya wote na hali faida yake ‘binafsi’ haina maana ; ni upuuzi pia mambo kuwa hivi. Na hivi jukumu la wanajamii wote kuhakikisha uchunguzi na utafiti wa jinsi zote mbili unakubalika na kutengenezewa mazingira bora ya kumea kwake.

Chimbuko la ‘moto’ wa kitovu cha ubongo si ubongo, na hivi kinyume na udhanifu wa mtu kuwa ni mwili, mtu si mwili. Mwili hujisuka kwa jinsi ya elementi za mwili wa dunia na hewa. Lakini ‘utu halisi’ wa mtu haufanyiki hasa kwa elementi za dunia na hewa ya kuvutwa puani. Kuna kasumba katika kisomo cha hata sayansi ya leo kusema kwamba kila anachofanyikia mwanadamu kimwili ni kwa nguvu za mienendo ya kubomoka na kujengeka kwa chembe chembe za chakula zake, akistasabahi hayo kwa lugha ya kisomo chake cha baiyolojia, kemia na fizikia. Kusema kuwa misingi ya mabadilishano ya kinishati yaambatanayo na kubomoka na kujengeka, nishati husharabiwa ama kutolewa kutumika katika kitendo cha kazi na ndivyo fizikia hushughulika na haya. Kwamba hadhi ya maumbile chembe huja kubainisha mpangilio wa kuundika kwa vitu vyenye kustahili kuitwa ni 'maada'; na hivi chembe chembe za jinsi mbali mbali zina jinsi mbalimbali za kufungamana ili kuchukua sura mpya ya kuundika sifa na hadhi, ndivyo kemia huambaa na mashauri vya visomo vyake. Pia kuwa chembe chembe za maada huweza kujijenga katika mfumo wenye 'uhai' na kudhihirisha taratibu zenye kukubalika kuwa ni 'hai' kwa kadiri ya visomo vyenye kutajwa chini ya jina la Baiyolojia.

Kisomo cha baiyolojia hudhanifu 'uhai' ni sifakazi itokanayo na tabia za kifizikia na kikemikali tu. Hii ni Si kweli; ndiyo maana kisomo cha baiyolojia si ni 'kikamilifu' hasa. Si yote ni yenye kufahamika vema katika mifumo vya viumbe hai na mienendo yake. Ni mapenzi yangu jamii ya watanzania walitambue hili na kulijengea mkondo kwa mawezekano ya kuchimba na kutanuka zaidi. Kufanya hivi si tu kutaongeza maarifa lakini pia ndiko hasa kutatuletea majibu kwa baaddhi ya matatizo yanayoweza kujitokeza kwa wakati na jamii ikakosa suluhu na ukwamuzi. Maradhi yatokanayo na mambo kama ubovu katika mishipa ya fahamu, mjengeko mbovu wa mwili kwa kuzaliwa na jinsi zote za maradhi yenye kupelekea msuko tenge wa miili ni shughuli inayotaka uwanja wa ujuzi na maarifa kutanuliwa. Kuambaa ambaa na visomo kwa jinsi ya Aristotle hufanya jamii ya wengi ikiwemo hii ya watanzania kudhani kila 'ukweli' lazima ukadirike kwa jinsi yake dhahiri; na kama lipo jambo lisilo ni dhahiri basi hiyo ni 'si sayansi'. Huu ni upumbavu. Azma yangu ni kutaja bayana kuna mambo katika kisomo daima hayatakuwa dhahiri lakini upo ufundi mbadala kwa jinsi ya vile vitendo kiaristotle unaoweza kunatabahi vina vipya vya visomo. Na hii ndiyo lengo mojawapo la Oganam ya karne ya 21 juu ya njia ya tatu.

Upande huu wa kisomo usiohitaji upekee wa mbinu za kiaristotle, umekuwepo hata kabla ya Aristotle na ni mwenye umri mkubwa kama mwanadamu mwenyewe. Baada ya Aristotle kuwepo kiwakati, ni kwamba tu binadamu aliamua kutendea haki fahamu zake za mwili kwa maarifa na visomo vyenye kufaa 'kumbukumbu' lake. Kwa kuwa kisomo hiki pia kina utumikivu wake wenye nguvu katika kuimarisha misingi ya ustawi na maendeleo ya watu yenye 'kupangilika'. Labda kote duniani binadamu wamekuwa na jinsi ya visomo vyao ndani ya jamii lakini kutokulenga kuleta jinsi ya mpangilio kwa ustawi wao kwa jinsi ya moja kwa moja hiyo iliishia kufanya visomo vyao visiwe rasmi katika minajili ya mapana ya jamii. Na hivi mengi yaliishia katika mahusiano ya mtu na mtu na ama ikitokea yakafahamika kwa wengi huwa ni tu habari isiyoweza kukitwishwa chini misingi yake.

Ni jambo sililofahamika kwa watu wengi kuwa hata 'wanasayansi' wa mwanzo katika chimbuko la mapana ya visomo vya leo walikuwa ni watu wenye kujaribu kupatanisha maarifa ya kuonekana na yale yasiyo yakuonekana. Bacon aliyevuvia kizazi cha wanasayansi wa mwamzo mbinu bora za visomo na kutokomeza kasumba katika kuelewa mashauri ya asili; yeye mwenyewe alikuwa ni mtu wa 'utambuzi' wa jinsi ya kiroho. Watu wengi tu kama Robert Boyle(fizikia, --gesi na mtanuko, mgandamizo, joto), Isaac Newton(fikizikia,-- mwanga, mienendo ya miili na nguvu tawalifu), Johanes Kepler(fizikia, -- mienendo ya miili ya mbinguni, mizunguko yake, umbali toka juani na urefu wa vipindi vya mizunguko kamili), Rene Descartes(Hisabati, fizikia--Jeometria bapa, aljebra) Leonardo da Vinci(sanaa na fizikia, --ubunifu, uvumbuzi na udhanifu wa kimstakabhari) Michael Faraday(fizikia na kemia, --umeme na usumaku, mpitisho wa umeme katika vimiminika vya tindikali/chumvi chumvi), Blaise Paschal(Fizikia, Hisabati,--mgandamizo na ombwe katika mtungiko wa gesi katika chombo, jeometria bapa, nadharia yumkinifu, mienendo ya vimiminika, dhahania ya mwendo pepetua), John Locke(Baiyolojia/Tiba,--sayansi za jamii, sheria na haki za raia), Benjamin Franklin (fizikia,--nguvu za umeme radi)Thomas Jefferson(hisabati, historia,--sayansi za jamii, mwandishi la tamko la uhuru la marekani, msanifu wa utenganisho wa tawala ya nchi na dini, utambuzi wa upekee wa kila raia, udhanifu wa sheria 'isiyompa' mtu 'liberiti' ila kutambua hiyo katika mtu, upingaji wa mtaasisisho za mabenki, upingaji wa dhana ya madeni ya kurithi kulingana na amana za kibenki, dhahania ya katiba kutokuwa 'msahafu' katika vizazi vya wanajamii, upingifu wa nguvu za majaji wa mahakama kuu kuwa ni wa 'mwisho') nk walikuwa ni wajumbe wa jumuiya za siri zilizoazimia kuleta mwamko wa 'hekima' ya zamani katika mwili mpya wa mawazo na kisomo cha mwanadamu.

Wengi miongoni mwa hawa wakisambaza machapisho ya mashauri anuai juu 'nguvu' zisukumazo maisha na maajaliwa ya mwanadamu—kufanya hivi kwa wazi wazi na wengine kufanya hivi kwa kuficha utambulisho wao halisi ili kulinda shughuli zao katika ofisi za umma, taasisi za kidini au hata ajira zao katika taasisi za elimu za juu. Wengine wakifanya hayo kwa kuchanganya baadhi ya visa vya mafundisho ya Yesu na wasikirifu wengine waliopata kujitokeza kabla na hata baada yake katika kuchochea udadisi wa mafumbo yenye kuambatana na mapokeo. Wengi miongoni mwa hawa wakianzia kwenye misingi ya mapokeo yenye kuzungumza juu ya mawezekano ya ubadiliko wa maumbo na hadhi kutokana na 'nguvu' za ndani za 'mfilosofia' mwenye busara. Vile visa hasa vya 'ma-alkimiya' wenye kutafuta mbinu za kubadili chuma cha 'daraja la chini' kuwa 'dhahabu safi' kwa kutafuta 'jiwe la mfilosofia' lenye kuleta uwezo. Bacon alikosoa mtindo wa majaribio ya kisayansi yenye kutarajia 'miujiza' labda kwa kuwa alikuwa akijua sehemu nyingi ya visa vya mapokeo ni tu masimulizi ya ishara lakini si lazima iwe kama inavyosemwa kwa juu juu. Wanasayansi wengi wa siku hizo za mwamko ndiyo waliingia hasa kwenye kuvunjika kwa ndoa ya kupendana na mabadiliko ya 'miujiza'; na kujikita kwenye vitendo vyenye kuweza kurudiwa na kutoa matokeo yale yale ikiwa viwango vile vile vya majaribio vikizingatiwa ili kusimamisha 'ukweli' wa jambo.

Hili si kwamba linabatilisha mafumbo yaliyomo katika mapokeo ya alkimiya kwa mfano. Hujulikina hata Yesu alikuwa akifundisha alkimiya ingawaje mapokeo mengi yalivuka vizazi kwa kuvutikia kwao na siri za 'miujiza'. Udadisi ndio daima humuongoza mtu wa kiuchunguzi na huo daima huanza na pale ulimbo wake unapomnasa katika kutahayari fumbo fulani. Wanasayansi wa mwanzo walinata kwenye ulimbo wa 'miujiza kamili'; majaribio yenye kuweza kufanya na kuthibitisha kisomo kilichosimama na si kusifika kwa mazingaombwe. Ingawa wengi walikuja kupendezwa na 'sanaa' hii yenye ushawishi wa maarifa dhahiri; wapo wengine ambao walizidi kuvutika kwenye mengi 'yasiyoarifika'. Hayo ambayo 'hayaarifiki' bado yanafutika mapana yote ya visomo vya mwanadamu ijapokuwa mwanadamu sasa anakuwa 'mjanja' sana kukwepa mashauri yanayoelekea kwenye mafumbo ya maumbile, nishati na uzima. Na kwa kuwa uwingi wa umma hauna namna mahsusi ya uchimbaji wa kisomo, maarifa mengi yana ukomo wa tasnifu zenye 'kusifika' kuwa ni bora—si kwa kuwa zinakidhi 'uhakika' ila tu kwa dhahania zake zilizo na 'mahadhi'; kwa kutambulika hivyo miongoni mwa wanataasisi wengi chini ya mashauri yake.

Basi pamoja na maendeleo yote ya sayansi katika siku hizi; upo upande wake uliona athari kubwa na mbaya zitokazo na wanataaluma kuwa na 'upofu' wa kujitakia juu ya upande mwingine wa kisomo usiohitaji mashauri yatokanayo na 'vipimo' vya utazamaji. Katika shauri hili tunaweza kuingia moja kwa moja katika kutazama kwa juu na 'kuhisi' jambo lililo 'geni' katika kukubalika.

Wanataaluma wa baiyolojia wanaweza kusema kifaranga aliyetokana na yai la kuku amefanyika kutokana na ule ute uliokuwamo kabla ya yeye kutungika na kukamilika kuja kutotolewa. Na siajabu hili limezaa shauri ya yai kuwa mboga yenye 'virutubisho' vyote vya mwili. Hii ni kwa kuwa katika mashauri yajayo na kisomo cha kemia, fizikia na hisabati; nishati yote iliyostahimilisha mabadiliko ya utokeaji na ukuaji wa kifaranga ndani ya yai ni jumla ya nishati iliyohifadhika ndani ya ute na kiini kwa kuhifadhika dhidi ya halijoto izungukayo yai. Ujazo wa yai ndiyo huja kuwa ujazo wa mwili wa kifaranga na pia chembechembe zote alifanyika kifaranga na ndizo zilezile zilizofanya ute mwanzoni. Sasa yai ni kati ya maumbile ya ajabu ya uhai; udhanifu wa kawaida wa kisayansi kulingana na mashauri yaliyotangulia yataleta tasnifu isiyokuwa ya ukweli juu ya yai na hatua za mtokezo wa kifanga. Kwa jinsi hiyo hiyo ya kutazama maumbile kwa nje imepata kuonekana kuwa kuku anaweza asile virutubisho vyenye kubeba madini ya kalsium na badala yake akawa anakula hata chembe za udongo zenye 'mika' ambayo ndiyo huwa na madini ya potasiamu. Uchunguzi unaonesha kadri kuku alapo 'mika' na akakosa kula chakula chenye madini ya kalsium kwa muda mrefu bado anaweza kutaga mayai yenye maganda ya kalsiumu ya kutosha. Lakini kuku anayekosa 'mika' na kalsium huishia kutokutaga mayai imara yenye kalsiumu. Yapo majibu kadhaa yanayoweza kudadavuliwa kutokana na matokeo ya uchunguzi huu lakini nichague moja ambalo hushangaza wachunguzi; inaonekana viumbe katika mchakato wa kuishi si lazima wale 'kiasi' kwa 'kiasi' cha madini na vitamini ili kuwa na 'afya bora' kama visomo vya leo vya sayansi ya virutubisho inavyoshawishi ukubali kwa watu. Na tena uchunguzi unaonesha hata kama kiasi cha kalsiumu kipindi cha ute ikipimwa na kuja kulinganisha na kiasi cha kalsiamu inayouunda mifupa ya kifaranga hivi viwili vipimo havina uadilifu. Mwili wa kifaranga una kalsiumu nyingi kuliko inavyowezekana kabla kutungika kwake toka kwenye ute... Je, mifumo hai inaweza 'kujitengenezea' madini na virutubisho vya jinsi tofauti hadhi na maumbile yake ya msingi? Kulingana na yai jibu la swali hili ni NDIYO.

Sayansi katika shauri hili inajiwekea mikingamo yake yenyewe kwa kung'ang'ania 'vipimo' na 'kiasi' hadi katika mifumo ya viumbe hai na kumbe namna za viumbe hai vinapitiliza kweli ndogo ndogo za kisayansi. Kulingana na hili peke yake kwa mfano, jamii hufundishwa matumizi ya mbolea za 'chumvi chumvi' katika kilimo ili 'kukuzia' mazao vizuri na haraka. Lakini ukweli wa kuchunguza ni kwamba ardhi yenye kutiwa mbolea za chumvi huonesha dalili za kukuza mazao haraka lakini baada ya misimu michache rutuba ya ardhi huathirika vibaya, na ile 'neema na hakika' ya mazao huanza kudorora na kupelekea hali ya mazao na mavuno kuwa mbaya.

Kisomo cha kemia na fizikia kinamapungufu yake makubwa kabisa pale mashauri yake yanapochukuliwa kwa 'ujumla' wake na kubebeka toka kungine. Kwa mfano mwingine, hudhanika kuwa nguvu zinazostawisha mwili wa viumbe wanyama hutokana na chakula pekee... Yapo majaribio yanayoweza hata kubatilisha hili shauri na mojawapo ni kama lile la mafundi wa kufunga wenye kuweza kukaa masiku, majuma na hata miezi pasipo kula. Vimekuwepo visa vya watu wachache wenye kudhihirisha hili miongoni mwa wanajamii lakini ni wanasayansi wachache wamebahatika kuchunguza finomena hii na kushuhudia 'jambo lisilolakawaida' kuendelea katika miili ya watu kama hawa.

Inafahamika kuwa mimea ya nchi kavu huwa na jinsi yake 'kujitengenezea chakula' kwa kitendo kinachotajwa ni 'usanisi na mwanga wa jua'. Aghalabu ni kwenye mimea na katika mwili wa wanadamu hudhahirika uwezekano wa 'kutengeneza chakula' ama 'vitamini' kutokana na mwanga wa jua; lakini si ile sehemu ya ukweli mwingine usiobayanika kwa wachunguzi wa jinsi ya macho na vipimo.

Miongoni mwa watu wa Bara la Uchina kumekuwepo kwa mashauri juu ya 'nguvu' yenye kustahimilisha miili 'kutoka ndani'; yaani kana kwamba chakula, maji na hewa kukidhi mahitaji ya 'nje' ya mwili lakini mienendo ya uhai wa mwili hustahimilishwa hasa na nguvu yenye kutajwa ni 'Chi'. Ni 'Chi' yenye kusharabiwa na viumbe hai vyote na kuhuisha maada zake ili kuchuka sura ya 'uzima' wa kimwili. Uzima huu hutajwa kuwa unajinsia za namna mbili katika moja—Yin na Yang. Kuna msemo katika lugha ya kiswahili usemao Lila na Fila havitangamani; kuna uwezokano usemi huu umetoka na mashauri ya Yin na Yang. Kulingana ya 'hekima' juu ya Yin na Yang katika 'Chi', husemwa uzima wa vitu hutegemea utangamano wa Yin na Yang ili viwe 'bukheri wa afya'. Viwili hivi visipotangamana huwa kuja kuwa ni 'maradhi' na si uzima katika mwili wa kiumbe. 'Chi' ni Pumzi ya uzima isiyodhahirika machoni lakini ikabainishwa kwa ishara za matokeo ya hali na hadhi ya viumbe hai. 'Chi' ipo kote na inapenya kote ingawaje yaweza 'kukadirika kujikusanya' pahala penye 'mgongo' wa umbile kama mlimani... Tokea siku za zamani kilele cha mafunzo ya sanaa za mapigano kilifanyika milimani ambako shauri kuu juu ya kutambua 'Chi' lilichukua mkondo wake.

'Kung Fu' ina tafsiri ya kusema 'muda wa kucheza' na ndivyo hivi katika maisha kila kitu ni mchezo. Sanaa za mapigano hukamilika ndani ya mtu kwa kutambua uwezo wa 'Chi' katika kukamilisha sanaa yake hiyo. Na ndivyo mafunzo kamili ya msanii kukamilika kwa kitendo kinachosemekana ni 'kuutupisha' akili; kwani katika hali hiyo ya utupu akili ya mwanadamu inaweza kuwa 'kioo kamili' cha kuakisi mienendo na nguvu ya 'Chi' katika kuchochea 'michezo' yote. Na hivi mtu yeyote mwenye kufikia daraja la 'usafi wa kiakili' husemwa hawezi kushindwa katika pigano lolote na mchezaji yeyote. Na ndivyo hivi hivi hata miongoni mwa masamurai wa Ujapani, ilijulikana kuwa 'ukamilifu' wa mfundwaji wa sanaa ya mapigano hukamilika kimafunzo yake pale anapofikia kutoka 'sawa' katika mapigano na mtu mwingine aliyemjuzi kwa kutangulia. Kwa kuwa katika hali ambayo mtu huwa ni 'mtupu' katika akili aweza kumaizi mara moja hata nia iliyojificha ya mpiganaji mwenzie na hivi akarudisha majibu ya kipigano kubatilisha athari zake. Hichi ni kitendo cha 'muda mfupi' kufanyika lakini pia hutokea 'pasipo muda'--siri yenyewe hasa ya athari ya 'mruko wa kikwantumu'.

'Chi' ndiyo 'Kani--The Force' ilivyo katika filamu za Vita katika Manyota—Star Wars; katika fasihi picha za sinema kama zilivyobuniwa na George Lucas. Dhana ya Lila na Fila ikiwakilishwa na mchezo wa vita kati ya mrengo wa ma-Jedayi na ma-Sithi. Ma-Jedayi wakifanya bidii sana ili waweze kutumia 'Kani' ili kuzikabili kuzishinda nguvu na fujo za ma-Sithi katika mapambano ya Himaya za madola katika ustawi wa Nyotani.

Shauri la 'Chi' ni sehemu ya utambuzi wa kisayansi usiotaka mtindo wa kiaristotle 'kuthibitisha' ukweli wa jambo. Jamii za mashariki walijua namna ya vitendo vyenye 'kuthibitisha' uwezekano wake wa kuwepo. Ikiwa kisomo cha 'Chi' kitapanuliwa kugusa mashauri mengine mengi katika uwanja, wa fizikia, kemia na baiyolojia, sayansi itakuwa ni 'kamili' na 'upanga' ule hasa wa Jedayi. Oganam ya karne ya 21 juu ya njia ya Tatu inaazimu hili.

Kulikuwepo na shauri la kitu kama 'Chi' katika jamii za wanasayansi wa mwanzoni; wao walisikia hayo kutoka katika mapokeo kutajwa kama 'Etha Iwakayo' . Majaribio ya 'kuthibitisha' uwepo ya etha hayakufaulu kutokana na msingi wenyewe hasa wa udhanifu katika kubuni kitendo cha uchunguzi. Mpaka hivi leo husemwa hakuna etha; lakini huu ni upofu tu... na ni swala la kiufundi. Etha 'HAIPIMIKI' na wala haina 'Ukiasi' wowote. Maumbile ndiyo yenye kuzaa picha kama vile 'Chi' imejikusanya kwa wingi hapa ama pale, lakini katika maumbile 'ukweli' ni msigano. Sayansi kwa jinsi ya vitendo vyake imekosa kufaulu kudadavua shauri la uwepo wa Etha kwa kuwa ndiyo hiyo inayodhahirisha hata 'wakati' wa mwanga 'kusafiri'. Msingi wa kitendo uchunguzi cha Michelson-Morley ulipanga sura la jaribio lao kwa udhanifu wa etha 'iliyosimama'.

Etha na 'Chi' ndivyo viwili hasa vilivyotajwa toka zamani kuufanya ulimwengu wote.

Vitu hivi ni 'Nuru' na 'Pumzi ya Uzima'. Madhahirisho yote ni 'Maumbo/Wakati'. Na hivyo kila chenye kufanyika katika madhahirisho kina 'kadri' ya chembe tatu katika moja. Jinsi moja ya Tatu kama 'Nuru/neno', jinsi moja ya Tatu kama 'Pumzi ya Uzima/kuchukua sura ya Umbo' na jinsi moja ya Tatu kama 'Nia'. Kwa ujumla wake wa moja na moja na moja, ulimwengu wote mzima ni 'Kiumbe Hai' –tofauti na mapungufu ya kimtazamo yaliyomo katika utaasisi wa sayansi ya leo katika kukubalika.

Vyenye kufanyika 'ndani' ya ulimwengu huchukua sura yake kwa daraja la 'Nia' kati ya kile kinachodhahirika na 'Ulimwengu'. Vile vile kinachohuishwa katika ulimwengu huchukua sura yake kwa daraja la 'Nia' na 'Pumzi ya Uzima' kwa jinsi ya 'Ulimwengu Hai'. Ulimwengu wote uliodhahirika ni 'Neno linaloishi'. Binadamu amefanyika kwa mfano wa 'Neno Linaloishi' lakini kwa funguo ya 'Nia' anao utashi wa kuamua kuzitambua siri za 'uzima wa milele' ama kusadiki 'mwili wa mauti' na kughafilika na adha zake zote. Siri ya maumbile na 'uzima' inashikiliwa na 'Utangamano uliofichika' uliyo pia ni muktadha wa 'Nia'.

Nyoka kujiviringishia katika Yai ni ishara ya 'Nia' na 'Uwezo' unaofanyikia ndani ya Yai--haya katika kutoa kielelezo cha 'Uzima wa Ulimwengu'. Kwa kuwa nyoka ni kadri ya unyoofu wa mantiki na utumikivu katika 'visomo' vyenye kutanabahi 'viasi'; na hivi ndivyo imekuwa nyoka ni kielelezo cha werevu. Mviringisho ni sifa ya kike ya uumbaji 'inayosiganisha' unyoofu na hivyo nyoka huwa ni alama kwa vyote viwili—akili yenye kumaizi mwelekeo na ile yenye kumaizi 'hadhi' ya mwelekeo. Ni hivi viwili vinavyozaa utambuzi wa 'wakati' katika mtu. Katika maisha, uwezekano wa wakati kutokea ni kwa sababu tu ya uwepo wa 'jinsi ya kiume' na 'jinsi ya kike'. Viwili hivi vikiwa katika 'Ndoa kamili'; hakuna 'wakati' na ni 'Uzima Kamili'. Lakini katika maumbile yaliyohuishwa 'Ndoa' ya 'jinsi ya Kiume' na 'jinsi ya kike' huja kwa utangamano maalum. Katika kila kile cha kiume kuna sehemu ya ukike na katika kila kile cha kike kuna sehemu ya ukiume... hii huleta 'mvutano' kati ya 'jinsi ya kiume' na ile 'jinsi ya kike'. Yin na Yang ni kielelezo cha 'Jinsi ya Kike' na 'Jinsi ya Kiume'.

Katika jinsi ya mfumo ndani ya mfumo, 'Nia' ndiyo hufanya 'Mwana'--hadhi ya chembe yenye mwelekeo na kutafuta 'kudhahirika'--ilivyo mbegu. Uzima ni 'uambukizaji uhai' na hivyo katika viumbe hai vyote vyenye kufanya jinsi ya 'uzazi' ; mazao yake hustahimilishwa na 'Uzima wa Vyote' na ulioko kote. Katika maungano ya kimaumbile ‘nia ya msingi’ ni habari/neno la jinsi ya chini, lakini 'Nia kuu’ huja kwa nafsi-roho na hasa katika kumzungumzia mwanadamu. Hata hivyo nia zote huneemeshwa na 'Uzima wa Milele' na huku zenyewe zikiakisi 'marefu' ya uhai. Marefu ya uhai ni neno liliandikwa katika jinsi ya msokoto wa chembe za kimwili. Pumzi ijazapo 'nguvu' neno hili, lenyewe huhaisha mienendo ya kimaada kukirimu hadhi ya kuwa ni kiumbe hai mpaka pale mwili huo utavyokosa 'kusharabu' pumzi kwa uadilifu wake.

Yai hujakutotoa vifaranga kwa mchakato unahusisha 'maada za ndani' yake na nguvu zisizotokana na maada yenyewe moja kwa moja. 'Namna' ya nuru na pumzi huhaisha kiumbe kipya katika yai na kusuka mwili wake katika mazingira fulani. Hili haliko katika yai tu, seli zote za uhai zinadumishwa nguvu kwa 'jinsi ya nuru' na 'jinsi ya pumzi' isiyoonekana kwa vipimo. Jinsi hii ya hivi viwili kudakwa na 'pete' ya uhai inayojulikana katika uwanja wa sayansi kama DNA. Umbo la 'pete' ni umbo lenye uwezo usiowakawaida wa 'mpitisho' wa 'wakati' na 'habari/neno' lisilo na umahala.

Inafahamika katika sayansi kuwa katikati ya seli yenye uhai kuna kiini chenye kuongoza mienendo yote ya mabadiliko ya uhai wa seli husika na humo ndani yake hukutwa 'jinsi ya misokoto pacha' inayopachikwa jina la 'utepe wa DNA'. Utepe huu huwa hasa ni 'pete' ya misokoto ya 'nyuzi' mbili ambazo hujizungusha kujisokota kulingana na kiasi cha ukali wa 'tindikali' iliyomo katika mfumo wake na hivi kusema kadri ijisokotavyo ndivyo 'maji maji' husukumwa nje na mnyongoroto kuwa mkali zaidi (B DNA, muundo wa uonekanao katika seli za kawaida za wanyama). Maji ni chombo shikilivu muhimu katika muonekano wa DNA kwa wakati. 'Maneno manne' yanayofanya DNA ni adenaini A—adenine, sitosaini C—cytosine, guanaini G—guanine na Thaimaini T—Thymine. Haya ndiyo hujirudia rudia katika msuko wote wa DNA katika 'kuchora' picha yake ya muundiko. Hizi hufanyika kwa maada zenye mfanyiko wa kuunda mienendo hai ya seli na uwepo wake katika vimimika vya kwenye seli hurahisisha msuko zaidi wa DNA pale seli inapoelekea kugawanyika na hivyo kuhitaji 'DNA pacha' ya kuendeleza 'Habari' za ususi wa seli na shughuli zake nyingine zote.

Uchunguzi wa DNA katika ugani wa fizikia umepata kufunua mawezekano yasiyo ya kawaida yatokanayo na hiyo. Gariaev kutoka Urusi, mwaka 1985 aligundua 'Athari Kizuka'--Fanthom Effect, alipokuwa wakifanyia kazi 'upipichumwa'-upigaji picha za kiuchunguzi mwanga—spectroscopy, kwa 'ribosamu' na 'kolagini'; katika taasisi ya fizikia, Urusi. Matokeo ya utafiti wake kamili alikuja kuchapisha mwaka 1991 na baadaye kutoa kitabu kulingana na kikundi chake cha kisomo maalum kilichopendekeza humo kitabuni shauri la natharia ya 'Jinomi yenye Msingi wa Mawimbi'--Wave Based Genome. 'Athari Kizuka' huonesha wazi machoni jinsi ya ugani mpya yenye kuvutia udadisi katika kuzungumzia vijinafasi vidogo vidogo vya muundiko 'ndani' ya ombwe—vacuum substructure; kwa kumulikia hiyo sehemu yenye 'Athari Kizuka' kwa Biru(jinsi ya mwanga isiyo ni mseto wa mawimbi mbalimbali ila namna ya namna ya mkusanyiko wa mawimbi mengi ya jinsi ya wimbi moja lenye nguvu na mwelekeo bayana, Laser) pamoja na namna ya mwanga wa kawaida. Na kama ilivyo ada, japo itifaki za jaribio ni zenye kubana ugumu, jaribio liliweza kurudiwa Moscow na huko Starnford na hivi ni 'ukweli' wenye kuthibitika.

Mawaidha ndani ya shauri la Jinomi yenye Msingi wa Mawimbi ni yenye kudadavua ukweli wa kwamba palipo na DNA pana sifakazi kama ngamuzi/kompyuta ya uhai ambapo ‘jinsi ya mawimbi’ huchimbuka--yenye sifa kuu tatu za kimsingi (1) kama 'vijineno' vilivyo katika muktadha wa lugha ya mwanadamu (2) Kromosamu, ambamo ndani yake huwepo DNA, ina hadhi ya kuweza kufanikisha sifakazi mbili--kurusha na kupokea mawimbi yachukuayo 'vijineno' na vile vile kung'amua maana wakati wa kupokea; kufungashia maana wakati wa marusho na (3) Kromosamu hufanya kazi kama 'chanja' za utengenezaji hologramu(holografia).

Holografia ni neno lenye kuwakilisha ufundi wa 'kupiga picha' wenye kuleta taswira ya mwonekano wa vina vya pembe zote tatu za uono yaani '3D'. Ufundi huu huja kwa kugonganisha 'miale' miwili toka katika 'chanzo cha mwanga' kulengwa kuishia kwenye uso wa 'kihifadhi picha'. Mmoja kutoka katika chanzo ni wenyekuja kuakisika toka kwenye 'kipigwacho picha' hadi kwenye uso wa 'kihifadhi picha'; na mwingine moja kwa moja toka kwenye chanzo kile kile, na kwa wakati mmoja--kwa jinsi tu iliyogawanyika njia; kwenda hadi kwenye uso wa 'kihifadhi picha'. Miale hiyo ili kufanya hologramu ['holo'-kamili, 'grafe'-andiko/mchoro/picha; kigiriki] yapasakuwa na 'unyoofu' na 'ukali' sawa wa jinsi ya mawimbi yake. Hili hufanikishwa kwa kutumia 'jinsi ya chanja' ya mpenyesho mwanga iliyo na mwachano sawa kwa 'nyufa' zake ndogo ndogo sana kadri ya 'urefu wa wimbi' la kuchujwa kupenyezea mbele. Vile vile hili linawezekana kwa kutumia biru, namna ya nuru yenye 'rangi moja' isiyo na asili ya 'mchangamano' ili kudhahirisha kadiri ya zile rangi za sekondari... Haya yote katika mpangilio maalum huwezesha upigaji picha yenye 'taswira ya ujazo' ilivyokutokea kama kile kitu kilichopigwa kilivyonekana kabla ya kupigwa picha ya holografia. Hii inamaana mara baada ya kupiga picha ya holografia, kile kitu kilichopigwa picha kikiondolewa lakini mwanga wa 'miale rangi moja nyoofu' kumulika pale pale palipopata kuwa na kitu na hapo hapo kumulika 'kihifadhi picha' basi kile kitu 'kitajitokeza' kuonekana kama vile kimewekwa tena mahala pale pale na kwa ujazo wake...

Hivyo ndivyo mfano pia 'Athari Kizuka' inavyokuwevyo kwa 'kuzuka' katika sehemu na hali kilichoasili ya kweli hakipo tena.

Jinsi hii ya shughuli itendekayo ndani ya seli za uhai inafunua ufunguo muhimu sana wa maarifa. Penye DNA pana 'kalamu' za kuandika/kuchora maumbo ya uhai na nyenendo zake za tabia katika miili ya viumbe hai. 'Sura ya umbo' katika fumbo lake, haiko popote pa umahala na ndivyo kuwa sayansi ya baiyolojia inayokubalika katika taasisi nzima; hudhanifu 'habari' yote ya msuko wa mwili huifadhiwa katika DNA. Lakini kumbe DNA hiyo hiyo ikianza kuhusishwa na vitu kama 'Mwanga' ama 'Sauti' huanza kuonesha dalili zisizokuwa za kawaida! Yumkini kusema sura ya viumbe hai ni 'kizuka' kitokanacho picha iliyoko 'mahala' pasikoonekanika. Hili katika kisomo cha uchunguzi ndani ya ugani wa baiyolojia, kimeleta nadharia ya 'Baiyoholografia ya Kikwantumu'--Quantum Bioholography.

Sauti nayo kwa jinsi ile ile ya 'kuchanjisha' mawimbi yaweza kuleta namna ya 'holografia ya kisauti' ambayo nayo hutumika katika kukadirisha chanzo cha sauti inayopimwa kule inakotokea.

'Mawimbi' na mfanyiko wa 'Unyoofu' kurahisisha mdhahiriko wa sura ya jinsi ya 'umbo hai' ndiyo ile alama ya Asclepius; Nyoka anayejivingirishia katika jiti.

Asclepius, mganga na tabibu wa kiyunani anayekuja kuwakilishwa katika ngano za kiyunani kama yule mtu aliyetupwa nyotani na kuwa 'ukanda nyota' wa Ophiuchus—'Mbeba Nyoka'. Huo upo katikati ya sekta ya Nge na Mshale; na hivi baadhi ya wanajimu wasiofuatisha mtindo wa mgawanyo wa nyuzi 30 za Zodiaki, huita Ophiuchus kama alama ya 13. Kusemwa kwamba alama 12 hujumuisha Dunia, Jua, Mwezi na Sayari lakini kuhusisha alama ya 13 ni kupenya zaidi kwenye kutambua mwenendo mzima wa mfumo wa Jua katika mfumo mwingine mpana wa 'mafungu unyota' ambako mfumo wetu wa Jua nao huzingusha dhidi ya ukati wake.

Husemwa Asclepius alijifunza siri za 'kughairisha' mauti baada ya kutia machoni nyoka wawili 'wakipeana' mzizi wa uponyaji, na hivi Ziusi, Mungu mkuu wa wayunani, ili kuepusha binadamu wasiwe 'watokufa' alimuua yeye kwa nguvu za radi na kutupia taswira yake nyotani.

Kisa hiki kizuri ni fumbo tu linalozungumzia 'udadisi' na 'hamasa ya kuingiliana kimwili'; kwa kuwa kupeana mzizi ni mbadala wa tendo la kupandikiza upya 'uhai' ambayo ndiyo hutawala 'sindano' ya Nge—nayo hutawaliwa kwa hayo; na nguvu za radi ni alama ya Mshale—alama ya yule mtu mwenye kasi na kulenga kufika katika mbingu; ambayo ni kama vile Asclesius alisulubiwa kwa kupigwa nao.

Nyoka kupeana mzizi pia huwa na kielelezo mbadala cha Nyoka Ouroboros pale 'wakati' unapogusiwa.

Ouroboros ni ile alama ya nyoka anayefukuzia kuungata mkia wake mwenyewe na hivi kutengeneza mduara kamili wa kujikunja. Ni alama ya fumbo la 'milele' ya wakati. Katika Pentauki, vile vitabu vitano vya Musa kutoka jamii ile ya watu kutoka mashariki ya kati, Israeli, huwa kina kisa cha nyoka 'amgongae' mwanadamu kisigino na mwanadamu yule 'aliyeandikwa shurti' la kumgonga huyo nyoka kichwa popote atakapompata. Lugha hizi za vielelezi ni mafumbo ya mfanyiko wa 'uzima' na madhahirisho yote katika wakati wote. Huitwa ni kama simulizi la 'Mwanzo' lakini hii ni kwa kuwa mwanzo wa vyote ni suala lenye kuvuta udadisi wa wanadamu wote katika kutafuta asili ya mambo yote na wakati wote.

Ukweli wa simulizi lenyewe ni kitendo kisicho cha jana wala kesho ila kutegemea tu na 'busara' ya yule aliyekusudiwa kukirimika kwa 'hekima' ya jinsi ya rohoni. Binadamu anayegongwa na nyoka ni ishara ya mauti isiyoepukwa na tena ijayo kwa mtu kwa kuviziwa—pale mtu alipojisahau kabisa kwa nyuma yaani kisiginoni. Vile pia kufanana na kile kisa cha 'Achelis' wa vita vya Troyi katika uyunani ya kale—aliyekuwa shujaa wa mapigano lakini udhaifu wake ulikuwa kisiginoni na ndivyo alikuja kuuliwa kwa kugongwa mshale katika kisigino na siyo kungineko kote katika mwili wake.

Hatua za mwanadamu ni msongo wa vizazi na mwendo wa safari yake ya ubinadamu. Vizazi vya mwandamu havikamiliki ila kwa kuandamwa na mauti. Na hivi shauri kuu la mwanadamu katika kuishi kwake ni kutafuta ile siri ya 'kutokufa'. Jinsi moja wapo ni kuendeleza hatua za uzazi wake; lakini hiyo siyo suluhu hasa. Yeye inampasa kumtafuta yule 'nyoka' mviziaji na 'kumuua' kabisa kwa kumponda si kwingineko kungine ila kichwani. Uadui wa nyoka na mwanadamu ni fumbo la wakati na kutupia kwake mkono dhamira ya kuishi kwa mwanadamu kusivyo na hakika ya kudumu. Sehemu ya ukweli wa maisha ambao husabisha mtu kufa daima utamchochea mwanadamu kutafuta maarifa na ukweli wa shauri lake la kuwa hai.

Na binadamu hawezi kuwa na amani mpaka afumbue fumbo la 'wakati' na 'uzima'. Uvumbuzi wa tendo la kujamiiana katika mwanadamu unaleta na adha ya 'kutambua' hakika ya mauti. Kwa kuwa uzazi ni ncha moja; na mauti ni ile ingine katika fimbo ya wakati—hakika ya kwamba 'hakuna refu lisilo na ncha'; kila chenye mwanzo hakikosi mwisho. Maisha na vitimbi vyote vya mwandamu kujisokotea katika 'wakati'.
***
Hmmm
 
Labada itakupendeza kuyaakisi haya akilini.

Kutoka: Mwongozo Hai kuelekea Uhuru Halisi seh. III
5 Septemba 2011 saa 12:23 Asubuhi

Dunia hii ambayo Aristotle alilenga kuichunguza kwa kuitazama kwa macho haiwezekani kamwe kuona ‘siri za mbingu’ kama vile mti wenyewe usivyoweza kuonekana hata katika mbegu yake. Basi Hekima itaelekeza kuelewa utangamano wa dhahiriko na ‘Neno la Uzima’ kwa vitu vyote kwa jinsi ya kwamba, kukua na kuongezeka ndiyo amri ambayo kila chenye ‘chembe-nia’ ya ‘kuwa’ huja kutii ili kuchukua nafasi. Lakini katika sura hasa ya mwili wa kudhahirika hakuwezi kuwa na refu lisilo na ncha... Na hivi hili linaleta utanabaishaji wa namna moja juu ya amri hii na ustahimilishwaji wake. Vitu vyote hujitokeza kwa jinsi ya pumzi ya namna yake ambayo itadhahirisha ukiasi wake katika minajili ya kuchambua ‘ukuaji’ na ‘wakati’. Lakini kikubwa hasa katika kudhahirika si mwili wenyewe wenye kudhahirisha hayo mawili... Mti hukua toka kwenye mbegu hadi kuwa kima chake na si kukua mpaka kulifikia jua lenyewe. Pale kipindi chake cha mwili wa dhahiriko umefika tamati basi tayari kutakuwa na mbegu nyingi zilizotapanywa kungine ; kupitia mbegu hizo hamu yake ile ile inaweza kuhifadhika mwili na kukirimika kukua. Na hivyo hata kama chembe-nia imekuwa ni yenye ‘jinsi ya u-moja’ katika mkondo wa madhahirisho daima katika marefu na mapana yake kutafanyika kitovu cha mwendelezo zaidi wa mchezo ule ule na kutohitaji refu lisilo na mwisho katika mwili ule ule.

Na huo utakuwa ni mzunguko kwa safari iliyo ni ile ile.

Vile vile dalili ya kwamba safari zote ni mizizi iishiayo kwenye shina moja la ‘wakati’ ; zile safari zenye kupandizwa huku na kule katika jamvi la wakati pasipo kumaanisha ‘unyoofu wa wakati’ ila tu mseto wa yote yenye kuweza kuonekana/kudhahirika.

Hapa twastahili kujifunza shauri la kupanda na kushuka ; kwenda mbali na kurudi nyumbani.

Katika visa vitokenavyo na maisha ya Yesu kina kile kinachoongelea ‘siku arobaini’ za mfungo ‘jangwani’ na mashauri ya ndani ya Yesu katika kushukiwa na ‘roho wa ubatizo’ ; na hivi kukaa kwake pembeni ili kuitafari dhamira yake juu ya sura na sifa ya huduma iliyoihisi kuhitaji kuitekeleza ndani ya jamii yake. Kwani na baada ya hapo ndipo inapotajwa kuanza huduma yake ya kutangaza ‘habari njema’ kwa watu wote. Labda ni yeye mwenyewe aliyekujashuhudia hata yale aliyokuwa mioyoni mwake wakati akipitia hayo—kwa watu wengine ; ama ni mtu mwingine aliyekujahifadhi kisa fulani kwa mchanganyiko wa tukio halisi na mashauri yaendenayo na hilo tukio katika simulizi la kufundishia jambo fulani lihitajikalo kupokelewa na wanajamii katika vina mbali mbali. Kwa kuwa tunajua kwa miaka mingi hata baada ya Yesu kupotea katika ardhi ya Palestina, simulizi la visa na mafundisho yake yalikuwa bado kuandikwa rasmi ila tu kuwa ni mtindo wa makusanyiko wa mafundisho madogo madogo ya kurithishwa kwa masimulizi na nyaraka za barua miongoni mwa ule umma uliokuwa ukifuatisha huduma yake kwa mapana ya jamii zingine.

Na hivi hili ni kweli katika kisomo cha historia, watu wa siku za nyuma si walikuwa ni watunza kumbu kumbu la mtiririko sahili kabisa ila tu walikuwa na namna za uandishi ambazo zilikuwa zikichanganya ‘usahihi’ wa tukio na ushairi ; vile vile ushairi wa mafumbo, ishara za kukoreza hisia na mapambio katika simulizi. Hakukuwa na jinsi ya uandishi kama ulivyokatika ulimwengu wa leo wa habari na historia juu ya mtu, jambo ama tukio.

Mtu yeyote kwa mfano, anayedhani kisa cha ‘nyoka’ aliyeongea na mwanadamu ni kweli ya kihistoria huyo atakuwa anajichanganya mwenyewe... Hakuna kitu kama hicho kinachoweza kutokea katika hali ya kawaida ila tu kwa namna ya ishara ya ukweli fulani ifananayo na picha hiyo—inayoweza kuhifadhika katika simulizi la wahusika waliohaishwa na wengine waliobunika sura. Basi ni jinsi hiyo hiyo binadamu anatokea kwenye silika ya kupenda kuchanganya ukweli wa kimatukio na upambo wa kufikirika ili kupeleka mbele na kufikisha ujumbe kwa mwingine.

Siku za nyuma watu hawakuwa na utajiri wa vifaa vya kuandikia na kuhifadhia maandishi ama kufyatua nakala na hivyo uwezo wao ulikuwa na kikomo katika uadilifu wa ‘habari halisi’ juu ya mtu ama jambo. Ndicho hichi kikomo hasa kilichobidisha kutia ‘nakshi’ habari inayopaswa kubaki katika jamii ili kuwa na utamu na urembo vile pia kuvuta masikio na hisia ; na hivyo kufanya watu wepende kuvitunza visa vya kusimulika na kuvirithisha kwa wengine.

Hii pia inahusu visa vya mashujaa na miungu wa makabila.

Haya yalikuwa ni fasihi ya aina yake ni yenye kumulika ukuwakujia wa kiakili, sanaa na mawasiliano ya kijamii katika kuhifadhi ‘vihamba’ vyake vya maadili na busara yenye namna yake kheri katika kudumu kwa utamaduni wao.

Basi lile shauri la Yesu katika kuishi pekee ‘jangwani’ kunaleta simulizi la ‘majaribu matatu’ kwa Yesu toka kwa ‘Ibilisi’. Kukipangilia kisa ili kuleta maana bora ya uwezekano inaweza kusemwa hivi : Baada ya ‘Ubatizo’ wenye kusimulika pale Yordani, Yesu alifunguka fahamu kwa jinsi ya ‘Ufunuo’ wa jinsi ya rohoni na ulimteka sana akili kiasi cha kuhitaji kujitenga na watu na shughuli zao za kila siku ili apate kutafakari uingiliano wa ‘ufunuo’ huo na ‘ustawi’ wa jamii yake ikiwa kuna chochote chenye kuweza kufaa hasa. Jangwa si tu kumaanisha ukavu wa nchi na michanga, lakini ni kujitenga mbali kiakili hadi hali isiyo na msaada wowote kwa wakati na mahala kwa jinsi ya utumikivu wa mwili. Kudumu pale tu ambapo fahamu yatawala na mtu kujimulika yeye mwenyewe na hapo kabisa alipo.

Siku ‘arobaini’ si lazima iwe ni siku arobaini kwa jinsi ya hesabu ya kawaida. Arobaini ni mzingo wa mraba kwa jinsi ya pande za vizio vya kadri ya ukumi-ukumi vya urefu wa mapana yake—kama ilivyohesabu ya vidole vya miguu na mikono na ishara ya ukamilifu wa ncha zote za nia kwa kuuchora wakati kwa namna yake ya ndani ya mwanadamu. Kufunga ni ishara ya kujinyima mahitaji ya kawaida ya mwili na ili labda pia kuzijua siri zake kukutana ‘pumzi ya uzima’ isiyotokana na asili ya mwili wenyewe ila kukutana na mwili katika namna ya utangamano wa aina yake. Haya yote kutokea kwa yule mtu anayekirimika kujua ukweli wa kanuni za ‘kuishi kwa mwili’ na uweza wa nguvu wa pumzi isiyoonekana kwa macho na kuzitambua nguvu zake zenye kuhaisha na kutenda kazi kwa maajabu yake ya utangamanifu na ‘uumushaji’. Kwa mtu asiyekirimika ; hili limeleta utamaduni wa kuiga kufunga kwa minajili ya ‘toba’ ; ukirifu wa dhamira mbaya zitokanazo na tamaa ya mwili, mawazo mabaya na dhamira mbovu juu ya maisha ya mwanadamu mwenyewe kupitia kujitazama. Lakini katika mfano wa Yesu, hakuna ishara hasa ya ‘toba’ bali kuna ‘upimwaji’ wa dhamira yake juu ya mambo fulani na kusudi ‘vimvuli’ vya jinsi ya ‘mashauri ya juu’ ipate kutathminika na kujengewa ‘msimamo wa nia’ ya kuhudumia jamii ikiwa mashauri hayo ni mazito kuliko wastani wa kawaida wa watu kuelewa na kutangamanishia kazi—kama jinsi ilivyo katika hali ya kawaida wanadamu hawatambui hakika ya uwepo wa ‘pumzi ya uzima’ ila tu wakimaizi jinsi yake ya kudhahirika waitwavyo hiyo ni ‘pumzi ya uhai’ kwa mwili.

Basi katika kisa cha Yesu jangwani husemwa alijaribiwa na Ibilisi nayeye akamshinda huyo na hivi kuwa ni ‘mwokozi’ kwa wengine wote waliokatika ‘himaya’ ya Ibilisi kupitia huduma yake ‘kulishuhudia neno’ na habari njema. Na hivi tukague ‘majaribu’ na ‘Ibilisi’ katika muktadha mzima wa mambo na mtu mwenyewe.

Kutokana na kuchukulia masimulizi juu ya ‘mambo ya kiroho’ kwa juu juu ; watu wengi hudhani Ibilisi ama shetani ni nafsi iliyo nje na nia-utu wao. Hiyo si kweli. Ibilisi ni mtu mwenyewe na ‘kisogo’ cha dhamira yake. Wengine huchukulia visa vyote vya namna kama ile ya masimulizi ya vita ‘mbinguni’ vya malaika ‘wema’ na ‘wabaya’—wabaya kushindwa na ‘kutupwa’ duniani ; kuwa ni tukio la ‘kihistoria’. Hiyo si kweli. Haijawahi kutokea hasa kwa mtiririko wa masimulizi. Ukweli ni kwamba vita hivyo haina mahala pa jana, wala kesho kwa kuwa vita hiyo ipo hapa na sasa. Na hili halina budi kudadavuliwa fumbo lake.

Uzima wa milele ni ‘Kweli’ iliyopo na hali isiyoshikwa na ‘wakati’ wowote. Madhahirisho yote yanachukua sura na hivyo ‘muda’ kubidi kutokea kujiazimu mbainisho wa ‘Kweli’ na ‘si Kweli’. Lakini hakuwezi kuwa na ‘si Kweli’ ila tu kwa kuwa inakirimika ‘ndani na nje’ ya ‘Kweli’. Vyote vinavyofanyika katika ‘usikweli’ hata ikitokea kuwa ni vilivyohaishwa vikijitambua kwa jinsi ya ‘wakati’ wake haviwezi kung’amua ‘Kweli’. Itokeapo kile kilichohaishwa katika ‘usikweli’ ‘kikataamulika’ kuwa moja na ‘Kweli’ hicho kinamaizi mara moja wakati wote si tu ni chochote ila ile ‘Kweli’ katika ukamilifu wake usiyogawanyika na wala kupotoka katika jinsi ya maonekano yote kama ‘sura ya wakati’ yaani madhahirisho na matukio. Na hivi jinsi yote ya viumbe vinavyofanyika katika madhahirisho kufungwa na kamba zake zenye kugundisha dhamira na utashi wa hivyo viumbe na ulimwengu wa madhahirisho yake. Bila ya hizo kamba ‘Usikweli’ hauwezi ‘kuishi’ ndani na nje ya ‘Kweli’.

Kisomo cha leo juu ya akili na fahamu ndicho kitasaidia kung’amua lugha za watu wa zamani katika kuzungumzia mashauri mbali mbali yenye kugusa moja kwa moja utabia ya mtu, imani, utambuzi, fahamu mbalali, fahamu jua, utofahamu kumbaizi, na ufahamu-jua kumbaizi. Kwa kuwa haya yote, kwa mtu, yana mapelekeo ya moja kwa moja kwa ishara za nidhamu ama mapepe, kuhangaika ama kutulia , ‘ugonjwa’ ama kuwa ‘sawa’.

Imani inamuunganisha mtu na ‘sura ya kheri’, utambuzi ni kitendo cha akili kwa wakati kumaizi uso wa jambo lilotwalo na fahamu za mwili, ama kumaizi jambo liletwalo na mawazo au fikra. Utambuzi hutokea katikati ya fahamu mbalali na fahamu jua—yaani ziwa la mawazo tuli ilivyomfano wa mbalamwezi iliyodakwa na maji kama ‘fahamu mbalali’ na hivyo fahamu jua kuwa ni mchemko wa mawazo mapya ambapo katika uso wake ndiyo mawazo mapya huzaliwa na kuwa ya moto kwa wakati halafu yakapoa na kwenda chini kwenye baridi.

Jamii inahitaji kisomo endelevu katika muktadha wa kutambua upana na kujifunza ili kutumia maarifa katika minajili ya taaluma za saikolojia ya kawaida na saikolojia ya paranomo. Miongoni mwa wanajamii wenye kuzungumza kiswahili ni hamu yangu maneno mbalimbali ya kiingereza yapate tafsiri ya moja kwa moja kutoka kwenye yale ya kiingereza ; iwe kwa kutohoa, ama labda kuweka tafsiri-mbinu. Hii itarahisisha kupanua haraka uwanja kwa visomo kwa kuwa maarifa katika lugha ya kiingereza yamepanuka sana na yanaendelea kupanuka kila kukicha. Na mimi nimetumia tafsiri-mbinu kama ‘fahamu mbalali’ kuwa sawa na ‘subconscious mind level/domain’, ‘fahamu jua’ kuwa kama ‘conscious mind level/activity’, ‘utambuzi’ kuwa kama ‘Cognition ; ~ Process’, ‘utofahamu kumbaizi’ kuwa kama ‘collective unconsciousness’. ‘Ufahamu jua kumbaizi’ kuwa kama ‘Superconscious/ness State of Mind’. Kuwa maneno haya yatawezesha kudadavua ilivyobora zaidi mashauri juu ya mtu, maumbile ya asili, habari na mawasiliano.

Haya hayakamiliki bila kisomo cha sibatenia ‘Cybernetics’ na saikolojia kwa jinsi uchanganuzi wa vitendo vya kiuchunguzi wakutoka nje. Lakini kwa namna ya uchunguzi kutoka ndani, sayansi haitanabahi hili hasa kwa sasa, lakini ni makusudi yangu umma wa waswahili waanze pia na jinsi hii ya uchunguzi katika mwili wa visomo vyake vyote vipasavyokuwepo na kwa manufaa yake. Kuwepo na uhifadhi wa mashauri na visomo kwa manufaa ya wengi.

Mtu anapochunguza ulimwengu toka ndani yake hujenga uelewa hata wa mambo yasiyothibitishika kwa mwingine ila tu kueleweka haraka au hata maramoja kwa mwingine aliyepita katika njia yenye kufanania ya kiuchunguzi. Ni kisomo hichi chenye kumulika mashauri ya Paranomo ‘Paranormal’ –ugutu wa hisia za fahamu hata nje ya jinsi mwili wa mtu ; na Uwimbiakili ‘Psychic’— kadri ya kuweza kuona mambo nje ya macho ya kawaida ama kushawishi/kushawishika na kupokea ‘picha’, ‘nia’ au ‘neno/fikra’ kwa jinsi ya akili na pasipo sura dhahiri ya kimaada. Kuwepo na uhifadhi wa mashauri na visomo kwa manufaa ya wengine pia wenye nia kupenyeza ndani zao.

Na binadamu anapokuwa na mwongozo bora huitengeneza njia kwa ajili ya ile ‘Hekima’ na kisomo chake toka hapo ni huwa ni chenye manufaa si kwa jinsi ya nje tu ila ya ndani pia. Kisomo cha leo kinamfaa mtu kwa jinsi ya nje lakini kikamwacha yeye maskini katika hazina ya utu wake. Na hivi haijalishi binadamu anakiri ama kutambua ‘udumavu’ wake katika hilo, kuelewa kanuni za mambo ya kiroho si ‘hiyari’ ni lazima kwa mwanadamu yeyote mwenyekutafuta kukirimu mengine na hali yeye ni mwenyewe kukirimiwa. Na kusudi pia ustawi wake upate kuinukia juu kuakisi chanuo kamili la ua katika kukatiza kwa kipindi cha muda uhitajikao.

Na hivi tutazame mtu, mdhahiriko wa nyakati za mtu na nafasi ya huo katika wakati mzima wa madhahirisho yote na hivyo wakati.

Kisa cha Yesu ‘jangwani’ kilikuwa ni mkato wa shauri zima kuhusu uakilifu na ‘mbegu’ zake za msukumo katika mtu ili kuchukua sura katika ustawi wa binadamu.

Jaribu la kwanza husimulika lilitokana na ‘njaa’. Aliposikia njaa Ibilisi akaja akamwambia mbona yeye ni mtu mwenye kufanyika uwezo sasa, maana anaweza kuyaambia mawe yageuke kuwa mkate nayo yakatii ‘neno’ lake, si afanye hivyo tu ? Tofauti na inavyochukulika juu juu, shauri la mkate ni lugha ya ishara kuhusu tabia za ‘utafunaji’ ili kushibisha matumbo kama mwenendo wa tabia moja inayoweza kumgeuza mtu kuwa ni mbinafsi. Yesu alipofunuka katika ufahamu wa kristo, baada ya ubatizo wa mto yordani, alingia katika ufahamu jua kumbaizi ; kwa jinsi hiyo aliweza kuona vitu vyote wa jinsi yake ya kuwa ni namna ya mitetemo katika ‘bahari’ ya madhahirisho yake. Alijua vivyo hivyo kila kadri ya kitetemo hushikilia hadhi ya usifa wa kitu na hivi mtu yeyote kutoka katika kina fulani cha utambuzi ndani ya fahamu kumbaizi akiweka nia ya mitetemo ya kitu chaguo lake katika macho ya kawaida ; kusudio ya hicho kubadilika, haraka madhahirisho ya umbo la kitu hubadilika kuitikia taswira ya akitakacho kwa ‘neno la lake’ ndani ya fahamu jua kumbaizi.

Ilikuwa ni fahamu ya jinsi ya akili ya kawaida na mashauri kutoka katika vina vya fahamu mbalali kuwa kwamba Yesu alipotuama kutoka kwenye vilele vya ufahamu wa juu ; alikumbuka njaa yake na kufikiria kama akili yake ya zamani ‘ilivyozoea’. Kwani ndiyo hiyo ilijifikirisha ikiwa kila kitu kinaweza ‘kujazwa pumzi’ kikabailika mitetemo hadhi na sura si anaweza tu hata kugeuza jiwe la pembeni ili kuwa mkate ili kuondoa njaa ? Lakini hapo hapo dhamira yake ya kheri hata katika fahamu jua yake ndiyo iliyomkumbusha hilo sio sahihi hasa. Kwa kuwa katika mpango mzima, kila dhahirisho lina nafasi yake na hivi si busara kwa kuwa mtu ni aliyetaamulika kujua siri za kubadilisha maumbo basi aende kufanya hivyo ili kujiridhisha hitaji lake kimwili. ‘Hekima’ ikamjia zaidi katika mashauri yake ya kwamba ikiwa kila kitu kinaweza kustahimilishwa na ‘pumzi ya uzima’ si ni hivyo hivyo na yeye aweza kustahilishwa kwa ndani pasipo kuhitaji kubadili jiwe kuwa mkate, kwa kuwa jinsi hiyo ingalikuwa ni tu mzunguko wa ubatili wa vitendo. Basi ndipo busara ilipomkaa Yesu kuzidi mashauri yake yote ya akili ya kawaida katika kuyatambua ‘matatizo’ ya mahitaji ya kimwili ; vile si busara kutosheleza kimoja kwa gharama ya kukibadili umbo kingine bila ridhaa yake. Kwa kuwa vitu vyote vina uhai wa aina yake katika mpango mzima hata kama macho ya kawaida hayang’amui hili. Na ndiyo jicho la staha—mara alipotambua hilo ‘akaomba’ hiyo pumzi kumkirimu, na ikiwa hivyo na njaa yake ikatokewa bila ya kutia chochote mdomoni.

Jaribio la pili husimulika kuchukuliwa kwa Yesu hadi kwenye ‘kinara cha hekalu’ halafu kuambiwa na Ibilisi atijupe chini kuthibitisha ufadhiliko wake kwa Mungu. Kuwa juu katika kinara cha hekalu ni ishara ya mtu kuwa katika mahala pa kutanabahi ukamilifu wa maadili yenye kuendana na kanuni za kiroho katika hali yake ya ‘kuinuliwa’. Katika kueleza mahusiano ya mambo ya ulimwengu wa kawaida na ule uliofichika, mambo ya dunia hutajwa ni ya chini na yale ya kiroho hutajwa ni ya juu. Mtu mwenye kuingia kutahamaki moja kwa moja mambo ya juu hutajwa ni mtu aliyeinuliwa katika ‘utukufu’ wa ile ‘Kweli’ na tena ndiyo fahari ya ‘Mbingu’—kwa kadri ya ukamilifu wake unavyoruhusu kukwea juu sana ilivyosawa na kusema kupenya ndani sana katika siri ya ‘Uzima’. Na hivyo kipande cha simulizi hili ni kielezi cha pale mtu aliyekatika ngazi za juu za utambuzi wa kiroho, dhamira ya utu-nia ya mazoea ya kinadamu hujakumshawishi kujaribu kuchepuka na ukweli wa kanuni anazotahamki dhidi ya zile kawaida ; lakini kwa mujibu wa kisa cha Yesu, alitambua hilo sio lazima kwani ulimwengu wa ‘kuinuliwa’ si wa mashaka na hivyo hakuna la kupimwa hasa kwa kulinganisha sura za mienendo yake ya hali. Na nguvu idhihirishayo kani mtuo kwa dunia, kuvivuta vitu vyote juu sura ya dunia kwenda chini, hainachochote cha ‘kujaribiwa’ kwa kanuni ya ‘kupea juu’ kujako na hali ya kuzama katika ‘hazina isiyokauka’ ya kiroho. Kwa kuwa kani mtuo ni ‘dhahiriko la wakati’ na angali watu si wenye kutambua hilo moja kwa moja ; ili kutunza na kuhifadhi vyote juu ya uso wa dunia kwa sura yake.

Ufunuo wa kiroho, japo humwingia mtu katika ‘vipindi vya muda’ mfupi ama mrefu, hii inaendana na uwezo wa mtu ‘kujikwatua’ toka hali moja ya ufahamu wa kawaida na kuingia katika ufahamu ulioinulika ; tena ndani ya vipindi hivyo dhana ya ‘wakati’ hupwaya kabisa shauri lake. Basi ‘kujitupa’ ili kuanguka chini ni ishara ya mmoja kushawishika kwa jinsi yake kujaribu kulazimishia matarajio kati ya ulimwengu wa wakati na ule usio wakati. Hii hutokeo pale mtu anapokuwa ni ‘mgeni’ wa kutahamaki ulimwengu upitao wakati, na hivi sehemu ya uakili wake yenye bado kujifunga na utu-nia wake kumshawishi kufikiri michakato ya mambo kwa mazoea yake ‘yalioandikwa’. Lakini mtu huyu mgeni yampasa kufanya chaguo kutoka katika ‘uchanga’ na ugeni hadi katika imani ya yote ya jinsi ya chini na ya juu na hivyo ‘Kweli/Mungu’. Kila linalotokea duniani kwa mapana yake yote ni kwa kheri ya vyote vya kwake ; lakini binadamu wenye ushawishi wa dhamira na utashi ndani ya nafsi zao, na katika upofu juu ya kuwepo kwa kanuni za ukamilifu wa juu katika ‘kinara cha hekalu’ ; wao hujikwaa na mambo ya dunia na kujichanganya wenyewe katika tafsiri za matokeo ya matendo yao ; ikiwa watashtukia kukumbuka siri za ‘kukwatuka’, wao watakuwa wana wa ‘Mungu’ wa vyote na hivyo wataweza kuinuliwa toka kwenye uharibifu hadi kwenye kheri halisi na kwa neema zake.

Jaribu la tatu la Ibilisi kwa Yesu husimulika habari ya yeye kupandishwa hadi juu kwenye kilele cha mlima na kuoneshwa miliki yote na fahari ya nchi ; halafu Ibilisi kumtaka Yesu amsujudie ili apate hivyo vyote kuwa mali yake. Katika kielezi hiki, ndiyo sura ya unafsi wa mtu huja ‘kutahinika’ katika kujichukulia kwake dhidi ya kumbukumbu na mapambo yake ndani ya nyakati. Ni jaribio katika uwanda wa uadilifu wa kimawazo, ambapo mtu ‘mgeni’ katika utaamuliko wa kiroho hupimika dhamira katika kile akionacho kustahili heshima ya nidhamu yake kiroho. Ikiwa kwa jinsi yoyote anapenda kujifunga na fahari za nchi na ‘kumbukumbu’ ya jina lake, basi yeye atakuwa amemuangukia Ibilisi ili kumuabudu, na yeye ataishi daima kukirimiwa kwa kiasi cha Ibilisi kuweza kumwongoza.

Katika hali ya kawaida watu huishi wakazaliana na kustawi. Jamii pana katika kilele cha jicho moja, huzaa dhamira ya mtu kuishi kutimiza ‘wajibu’ wake miongoni mwa wanajamii wake. Wanajamii wanajinsi yao ya kutambuana na kuheshimiana miongoni mwao. Kuwa mtu wa kaya, mume ama mke kuna heshima yake, watoto na mali ni ndoto ya uhakika kwa ustawi, miliki na urithi juu ya sura ya nchi. Kaya hukumbukwa kwa majina ya koo zao na heshima walizojijengea katika jamii yao pana. Binadamu huzaliwa na kufa, si chochote kati ya watoto wala nazo mali; ambavyo mtu hupita navyo katika mlango wa mauti. Na hivi ni sehemu tu ya mapenzi mema kwa vizazi, na tena kwa jinsi ya ukaribu wa damu, vizazi hurithishana urithi wao. Binadamu ainuapo macho yake juu humaizi jinsi yeye alivyo ni ‘mweupe’ na mtupu wa hazina ya kweli ; hili hujengea hofu kwake yeye ya utupu wa ubinadamu wake dhidi ya kadhia zake za maisha. Na hivi binadamu wa jinsi ya ndani kabisa ambapo hutafuta kujijengea ‘jina’ ambalo kwa hilo maisha ‘yatawakumbuka’. Jina hilo si chochote ila muakisiko wa fahari zote na maisha kama vile inavyoazimu ‘kujijua’ katika ulimwengu wa madhahirisho na wakati. Lakini ‘jina’ hilo huwa ndio kiegemeo cha jitihada zake zote dhidi ya majaliwa yake. Na vivyo hivyo, mwanadamu katika ‘kuinuliwa’ ndani ya ufahamu wa kristo ; adui wa mwisho kumkatalia mkataba naye ni nafsi yake yeye mwenyewe iendeshwayo na nafsi-roho yake na hali ni muakisiko uliopinduka sura na hadhi toka kwenye mbegu ya kweli yake ya milele. Kwa kuwa sura ile ile ambayo mtu huamini utu wake ulivyo na mipaka, yeye hawezi kumuona ‘mungu’ ila tu kwa jinsi hiyo hiyo na ‘kumuabudu’ kwake ni kutaka upendeleo katika majaliwa yake kwa kadri ya udhanifu wake.

Kwa hivyo kwa sehemu hii katika jaribio la tatu inaweza kufafanuliwa kuwa Yesu alikataa sehemu ya unafsi wake ambao ndiyo huwa ni msingi wa kutafuta jina na umaarufu miongoni mwa watu wa mataifa, na fahari zao zote, kwa jinsi zote ambazo binadamu hufanya kwa kushindana na saa za kusogea kwa mauti zao. Na kuanzia hapo kukiri Nia moja na ‘Kweli’ ambayo ni utumishi pale panapohitajika ; pasipo kuendeleza kulea ubatili na kujilisha upepo. Pia hapa ndipo tunajifunza juu ya nidhamu ya heshima kwa watu na wanajamii—Wake kwa waume na watoto ; pasipo misingi ya kutafuta ‘ukuu’, utawala na sifa za kawaida za watu wasiohisi mambo makuu yenye kuneemesha na kustahimilisha maisha yao.

Na ndiyo jinsi Yesu aliishi ni ‘Mfalme Mfilosofia’ miongoni mwa watu wale ambao hawakumtambua—maana tafsiri za wenyeji wake zilikuwa na mapokeo ya kutarajika kuja kwa ‘nabii kiongozi’ mkombozi na mwenyekuleta ‘mamlaka’ mapya ya wayahudi.

Husemwa baada ya kushinda majaribio hayo matatu Ibilisi alimwacha na halafu ‘malaika’ wakamchukua Yesu na kumhudumia. Na ndipo baada ya hapo alianza huduma yake kwa wanajamii wake akionesha uwezo mkubwa wa kuleta mashauri mapya na kufundisha. Akizungumza jinsi ya ‘kuingia’ katika ‘ufalme’ kwa uhitaji wa kujisafisha kwanza, kubatizwa kama ilivyoishara ya tendo la kuzamishwa kwenye maji na kuibuliwa lililofanywa na binamu yake Yohana ili kupata ‘jina’ jipya... Jina lakuwa ‘mwana wa mungu’ na vile Paulo alizungumza kuwa ni ‘Kiumbe Kipya’ na ‘Mtu Mpya’. Isivyo kama katika utumikivu mwingine wa maisha ya kila siku pamoja na uadilifu wake.

Basi tukague ishara za ‘maji’, ‘Ibilisi’, ‘Malaika’ na kitendo sanaa cha kupata jina jipya la kuingia ‘Ufalme wa Mbingu’.

Mafundisho yenye kuzidia mbali uelewa wa maumbile ya kawaida ya mtu na uzima ; huwa ndani ya kisomo cha kumuelewa mtu na hasa kule ‘alikochipukia’ na hivi ‘kuwepo’—yaani ndivyo tunaita hii leo ni Ontolojia. Mashauri ya ontolojia katika vizazi vya watu mbalimbali duniani, mara nyingi hufutikwa na lugha za ishara kuliko habari kamili. Ulimwengu wa leo ni ulimwengu wa habari na mashauri ya moja kwa moja katika ufundi na utumikishi wa taarifa/maarifa halisi katika wakati.

Ni kutokana na hili la wakati tulipo sasa lipo hitaji la kutafuta lugha mpya ambapo masimulizi yote ya kiontolojia yaliyopata kuwepo miongoni mwa mataifa na makabila ya wanadamu yatapata mahali pake pa kuelezwa na kuweza kufafanulika muktadha wake katika sura kamili ya mambo na mkunjuko wa wakati.

Hili linawezekana kupitia kisomo cha ‘Akitipu’ zenye kuongoza ramani za msukuko wa sura mbali mbali za michakato ya ukuaji na ustawi wa jamii katika kukatiza kwa vipindi maalum vya mng’amuliko fulani wa mzunguko kamili ya kuja na kuondoka kwa vilele vya ustawi wa wanadamu. Ingawa watu hudhani mambo yanayotekea ni mapya, pamoja na upya wake huwa kuna mtindo ambao madhahiriko yote kujifinyanga katika wakati.

Ndani ya madhahiriko yote kuna vichochezi vya sura ambayo hupelekea hata viumbe hai wenye utashi kama mwanadamu pamoja na mambo yao yote kuwa ndani ya vichochezi hivyo. Hivi huweza kuchukua sura ya kama hata dhamira ya mtu na kumbe ni sehemu tu ‘mpango mzima’ wa uzima wote hata kupitiliza ‘wakati’ wenyewe. Navyo ni sehemu ya uzima wote lakini kwa jinsi ya namna yake ya ajabu ; kuwa ni kama ‘mchanganyiko’ wa ukamilifu wa jinsi ya mafikara ya yote yenye kuwezekana(yasiyodhahiri kwa macho), yale yaliyokwisha kudhahirika na yale ambayo bado hayajadhahirika. Binadamu ni sehemu wa haya kwa mujibu na tena kadri ya alivyofanyika ndani yake kwa ‘ngozi za mifanyiko’ mbali mbali na pia ngazi mbali mbali za ufahamu na utambuzi kwa wakati katika kumfungamanishia yeye na hayo yote. Ndiyo haya hasa makutano ndani yake yahusishayoufahamu jua, fahamu mbalali na utofahamu kumbaizi.

Basi katika kisomo cha Akitipu tunajitahidi kutafuta kuujua ule ‘wavu’ uliotanda kote na kukokota misuko ya madhahirisho mbalimbali kutoka katika ‘bahari’ isiyoonekana ‘ya ukamilifu wa jinsi ya mafikara ya yote yenye kuwezekana’. Kwa kutumia akitipu tunatafuta kutambua tabia za watu na dalili za mienendo yao yote, kutokea na kupotea, kufumika ustawi na kutoweka kwake, mtandao wake wa nje na ule wa ndani wa mahusiano ya watu na uzima wao. Vivyo hivyo kwa Dunia, Nyota na vyote vyenye kuonekana katika udhahiri wa macho hata pia katika kaleidoskopi zake zote. Ni kama vile haswa kusemwa ‘jeometria ya wakati’ na uso wa maumbile yake.

Hayo tukijaribu ‘kuyaona’ yakichukua sura katika ‘bahari’ ya ‘uzima wa milele’ ; Nuru iangazayo yote na kufanya yote na hali hayo yote si chochote kubakia tu ile ‘Kweli’.

‘Ibilisi’ na ‘Malaika’ ni Akitipu. Binadamu hawezi kumaizi baadhi ya tabia za kufanyika matokeo ndani ya maisha yake ili kwa lugha ya akitipu zilizohuishwa. Hili linaweza kueleweka vizuri ikiwa mfanyiko wa ubongo wa binadamu unavyoweza kupenyezwa kisomo chake.

Binadamu ana ubongo uligawanyika katika pande mbili—ubongo wa kushoto na ubongo wa kulia. Japo kunamgawanyiko huu, kila pande ni jinsi ya kioo kabisa na mwingine. Jinsi hiyo pia inafanya kama vile isivyowezekana mkono wa kulia ukabadilishwa kuwekwa upande wa kushoto, kama hivyo hivyo kinyume chake.

Ubongo wa upande wa kulia kwa mfano huonekana kuwa ‘hai’ na vitendo vilivyokatika namna ya ‘picha’ na sura zote zenye kufanana na hivyo. Ubongo wa upande wa kushoto huonekana kuwa ‘hai’ na vitendo vya uchanganuzi na vitendo vya kufikiri. Kwa jinsi hiyo mazungumzo na kumbukumbu ni mchakato unaohusisha namna ya utangamano wa pande zote mbili za ubongo. Ukiondoa umahususi wa ubongo kama namna ya misokoto mirefu iliyojikunjamania ndani na hivi ‘kukoleza’ ukali kwa ‘fahamu’ zitokanazo na mikondo yote ya neva za fahamu katika usakiti wake. Kwa kawaida binadamu ana fahamu hai na tuli yaani zile ambazo kwa wakati anazitambua kuendelea katika mwili wake na zile asizozitambua na angali zipo.

Ngozi yote mwanadamu ina vipokezi vya taarifa ambavyo ni muhimu katika ‘kuhuisha’ utabia wa mtu dhidi ya mazingira yake. Vivyo hivyo huwa kwa fahamu zote tano. Kupitia ubongo ulioanzia katika uti wa mgongo fahamu zote za mwili wa mwanadamu huishia kunyongorotea mahala fulani katika ubongo uliokatika fuvu la kichwa. Sayansi hadi hii leo ni yenye kasumba ya kwamba ubongo ndiyo mashine kuu ya mwili yenye kuratibu kila kitu... Hii siyo lazima kuwa kweli ; kwa nje ni rahisi kudhani hivyo ila ikiwa mfanyiko wa mwili kuanzia katika seli moja hadi kuja kuwa muundiko wa mjumuiko wa seli nyingi katika mwili uliokomaa utazamamwa vizuri kunauwezekano wa kung’amua uhusiano wa ‘mishipa-sauti’ ya moyo na ‘kitovu-moto’ cha ubongo—hivi viwili ndivyo hufanya uzima wa mtu na viumbe vingine vyenye jinsi hii ya mfanyiko.

Kutoka kwenye ‘kitovu-moto’ cha ubongo mwanga-habari huwaka na kuangazia mwili wote taarifa za uwezekano wa kujisuka kwake na ubongo ndiyo mtandao wa kwanza kutumia tumia sehemu ya huo mwanga kusuka na kuratibu mienendo yote hata mwa mujibu wa ‘maandishi’ yalitungika na mwili wenyewe na tena yenye kuhama toka mwili mmoja hadi mwingine kwa jinsi ya matendo ya mwili kama kujamiiana. Ni ubongo huo huo pia ambao huweza kubadili taarifa za mwili kuwa mawazo na hisia na hivyo hivyo kubadili fikra kuwa nia kwa kufungua sakiti za kuamsha matendo ya mwili ambavyo mwili hutumika kama chombo cha kudhahiria nia fulani itokanayo na ‘mmiliki’ wa mwili wenyewe. Tofauti na inavyodhanika kwamba kitendo cha kufikiri hutokea kwenye ubongo, hiyo inaweza kuwa siyo kweli yenyewe hasa ; ubongo ni daraja lililo kama transmita na risiva ya mahala penye kuweza kuchakatisha mawazo. Na hapo hapo ubongo unaweza kuwa ni kama ‘lensi’ inayokusanya ukali wa mawimbi ya mawazo ili yang’amulike kwa jinsi ya ‘utambuzi’ wa kimwili—kama vile habari za kimwili kwa jinsi hiyo hiyo zaweza kuchakatuliwishia mawazo.

Ni nia yangu miongoni mwa wanajamii wa kitanzania kuwe na fikra za ziada na pana zaidi katika kuzidi kupanua kisomo kizima cha mwili, fahamu na utambuzi hata kupita yale mashauri ya kisayansi yaliyopokelewa pamoja na utokamilifu wake. Azma yangu ingalikuwa ni kusongesha mbele yale yaliyopokelewa kwa kisomo zaidi pale ambapo nafasi inaruhusu kwa mtu kufanya uchunguzi wa kina—katika mwelekeo wowote ule bila kuhofu mwelekeo usio wa kawaida wa mambo. Siku zote kuna ugumu kuvunjilia mbali mipaka, lakini hili halipaswi kuendekezwa daima. Watu wafanye visomo kwa faida binafsi na kwa faida ya wote. Isiwe tu kwamba mtu apaswa kufanya mambo kwa faida ya wote na hali faida yake ‘binafsi’ haina maana ; ni upuuzi pia mambo kuwa hivi. Na hivi jukumu la wanajamii wote kuhakikisha uchunguzi na utafiti wa jinsi zote mbili unakubalika na kutengenezewa mazingira bora ya kumea kwake.

Chimbuko la ‘moto’ wa kitovu cha ubongo si ubongo, na hivi kinyume na udhanifu wa mtu kuwa ni mwili, mtu si mwili. Mwili hujisuka kwa jinsi ya elementi za mwili wa dunia na hewa. Lakini ‘utu halisi’ wa mtu haufanyiki hasa kwa elementi za dunia na hewa ya kuvutwa puani. Kuna kasumba katika kisomo cha hata sayansi ya leo kusema kwamba kila anachofanyikia mwanadamu kimwili ni kwa nguvu za mienendo ya kubomoka na kujengeka kwa chembe chembe za chakula zake, akistasabahi hayo kwa lugha ya kisomo chake cha baiyolojia, kemia na fizikia. Kusema kuwa misingi ya mabadilishano ya kinishati yaambatanayo na kubomoka na kujengeka, nishati husharabiwa ama kutolewa kutumika katika kitendo cha kazi na ndivyo fizikia hushughulika na haya. Kwamba hadhi ya maumbile chembe huja kubainisha mpangilio wa kuundika kwa vitu vyenye kustahili kuitwa ni 'maada'; na hivi chembe chembe za jinsi mbali mbali zina jinsi mbalimbali za kufungamana ili kuchukua sura mpya ya kuundika sifa na hadhi, ndivyo kemia huambaa na mashauri vya visomo vyake. Pia kuwa chembe chembe za maada huweza kujijenga katika mfumo wenye 'uhai' na kudhihirisha taratibu zenye kukubalika kuwa ni 'hai' kwa kadiri ya visomo vyenye kutajwa chini ya jina la Baiyolojia.

Kisomo cha baiyolojia hudhanifu 'uhai' ni sifakazi itokanayo na tabia za kifizikia na kikemikali tu. Hii ni Si kweli; ndiyo maana kisomo cha baiyolojia si ni 'kikamilifu' hasa. Si yote ni yenye kufahamika vema katika mifumo vya viumbe hai na mienendo yake. Ni mapenzi yangu jamii ya watanzania walitambue hili na kulijengea mkondo kwa mawezekano ya kuchimba na kutanuka zaidi. Kufanya hivi si tu kutaongeza maarifa lakini pia ndiko hasa kutatuletea majibu kwa baaddhi ya matatizo yanayoweza kujitokeza kwa wakati na jamii ikakosa suluhu na ukwamuzi. Maradhi yatokanayo na mambo kama ubovu katika mishipa ya fahamu, mjengeko mbovu wa mwili kwa kuzaliwa na jinsi zote za maradhi yenye kupelekea msuko tenge wa miili ni shughuli inayotaka uwanja wa ujuzi na maarifa kutanuliwa. Kuambaa ambaa na visomo kwa jinsi ya Aristotle hufanya jamii ya wengi ikiwemo hii ya watanzania kudhani kila 'ukweli' lazima ukadirike kwa jinsi yake dhahiri; na kama lipo jambo lisilo ni dhahiri basi hiyo ni 'si sayansi'. Huu ni upumbavu. Azma yangu ni kutaja bayana kuna mambo katika kisomo daima hayatakuwa dhahiri lakini upo ufundi mbadala kwa jinsi ya vile vitendo kiaristotle unaoweza kunatabahi vina vipya vya visomo. Na hii ndiyo lengo mojawapo la Oganam ya karne ya 21 juu ya njia ya tatu.

Upande huu wa kisomo usiohitaji upekee wa mbinu za kiaristotle, umekuwepo hata kabla ya Aristotle na ni mwenye umri mkubwa kama mwanadamu mwenyewe. Baada ya Aristotle kuwepo kiwakati, ni kwamba tu binadamu aliamua kutendea haki fahamu zake za mwili kwa maarifa na visomo vyenye kufaa 'kumbukumbu' lake. Kwa kuwa kisomo hiki pia kina utumikivu wake wenye nguvu katika kuimarisha misingi ya ustawi na maendeleo ya watu yenye 'kupangilika'. Labda kote duniani binadamu wamekuwa na jinsi ya visomo vyao ndani ya jamii lakini kutokulenga kuleta jinsi ya mpangilio kwa ustawi wao kwa jinsi ya moja kwa moja hiyo iliishia kufanya visomo vyao visiwe rasmi katika minajili ya mapana ya jamii. Na hivi mengi yaliishia katika mahusiano ya mtu na mtu na ama ikitokea yakafahamika kwa wengi huwa ni tu habari isiyoweza kukitwishwa chini misingi yake.

Ni jambo sililofahamika kwa watu wengi kuwa hata 'wanasayansi' wa mwanzo katika chimbuko la mapana ya visomo vya leo walikuwa ni watu wenye kujaribu kupatanisha maarifa ya kuonekana na yale yasiyo yakuonekana. Bacon aliyevuvia kizazi cha wanasayansi wa mwamzo mbinu bora za visomo na kutokomeza kasumba katika kuelewa mashauri ya asili; yeye mwenyewe alikuwa ni mtu wa 'utambuzi' wa jinsi ya kiroho. Watu wengi tu kama Robert Boyle(fizikia, --gesi na mtanuko, mgandamizo, joto), Isaac Newton(fikizikia,-- mwanga, mienendo ya miili na nguvu tawalifu), Johanes Kepler(fizikia, -- mienendo ya miili ya mbinguni, mizunguko yake, umbali toka juani na urefu wa vipindi vya mizunguko kamili), Rene Descartes(Hisabati, fizikia--Jeometria bapa, aljebra) Leonardo da Vinci(sanaa na fizikia, --ubunifu, uvumbuzi na udhanifu wa kimstakabhari) Michael Faraday(fizikia na kemia, --umeme na usumaku, mpitisho wa umeme katika vimiminika vya tindikali/chumvi chumvi), Blaise Paschal(Fizikia, Hisabati,--mgandamizo na ombwe katika mtungiko wa gesi katika chombo, jeometria bapa, nadharia yumkinifu, mienendo ya vimiminika, dhahania ya mwendo pepetua), John Locke(Baiyolojia/Tiba,--sayansi za jamii, sheria na haki za raia), Benjamin Franklin (fizikia,--nguvu za umeme radi)Thomas Jefferson(hisabati, historia,--sayansi za jamii, mwandishi la tamko la uhuru la marekani, msanifu wa utenganisho wa tawala ya nchi na dini, utambuzi wa upekee wa kila raia, udhanifu wa sheria 'isiyompa' mtu 'liberiti' ila kutambua hiyo katika mtu, upingaji wa mtaasisisho za mabenki, upingaji wa dhana ya madeni ya kurithi kulingana na amana za kibenki, dhahania ya katiba kutokuwa 'msahafu' katika vizazi vya wanajamii, upingifu wa nguvu za majaji wa mahakama kuu kuwa ni wa 'mwisho') nk walikuwa ni wajumbe wa jumuiya za siri zilizoazimia kuleta mwamko wa 'hekima' ya zamani katika mwili mpya wa mawazo na kisomo cha mwanadamu.

Wengi miongoni mwa hawa wakisambaza machapisho ya mashauri anuai juu 'nguvu' zisukumazo maisha na maajaliwa ya mwanadamu—kufanya hivi kwa wazi wazi na wengine kufanya hivi kwa kuficha utambulisho wao halisi ili kulinda shughuli zao katika ofisi za umma, taasisi za kidini au hata ajira zao katika taasisi za elimu za juu. Wengine wakifanya hayo kwa kuchanganya baadhi ya visa vya mafundisho ya Yesu na wasikirifu wengine waliopata kujitokeza kabla na hata baada yake katika kuchochea udadisi wa mafumbo yenye kuambatana na mapokeo. Wengi miongoni mwa hawa wakianzia kwenye misingi ya mapokeo yenye kuzungumza juu ya mawezekano ya ubadiliko wa maumbo na hadhi kutokana na 'nguvu' za ndani za 'mfilosofia' mwenye busara. Vile visa hasa vya 'ma-alkimiya' wenye kutafuta mbinu za kubadili chuma cha 'daraja la chini' kuwa 'dhahabu safi' kwa kutafuta 'jiwe la mfilosofia' lenye kuleta uwezo. Bacon alikosoa mtindo wa majaribio ya kisayansi yenye kutarajia 'miujiza' labda kwa kuwa alikuwa akijua sehemu nyingi ya visa vya mapokeo ni tu masimulizi ya ishara lakini si lazima iwe kama inavyosemwa kwa juu juu. Wanasayansi wengi wa siku hizo za mwamko ndiyo waliingia hasa kwenye kuvunjika kwa ndoa ya kupendana na mabadiliko ya 'miujiza'; na kujikita kwenye vitendo vyenye kuweza kurudiwa na kutoa matokeo yale yale ikiwa viwango vile vile vya majaribio vikizingatiwa ili kusimamisha 'ukweli' wa jambo.

Hili si kwamba linabatilisha mafumbo yaliyomo katika mapokeo ya alkimiya kwa mfano. Hujulikina hata Yesu alikuwa akifundisha alkimiya ingawaje mapokeo mengi yalivuka vizazi kwa kuvutikia kwao na siri za 'miujiza'. Udadisi ndio daima humuongoza mtu wa kiuchunguzi na huo daima huanza na pale ulimbo wake unapomnasa katika kutahayari fumbo fulani. Wanasayansi wa mwanzo walinata kwenye ulimbo wa 'miujiza kamili'; majaribio yenye kuweza kufanya na kuthibitisha kisomo kilichosimama na si kusifika kwa mazingaombwe. Ingawa wengi walikuja kupendezwa na 'sanaa' hii yenye ushawishi wa maarifa dhahiri; wapo wengine ambao walizidi kuvutika kwenye mengi 'yasiyoarifika'. Hayo ambayo 'hayaarifiki' bado yanafutika mapana yote ya visomo vya mwanadamu ijapokuwa mwanadamu sasa anakuwa 'mjanja' sana kukwepa mashauri yanayoelekea kwenye mafumbo ya maumbile, nishati na uzima. Na kwa kuwa uwingi wa umma hauna namna mahsusi ya uchimbaji wa kisomo, maarifa mengi yana ukomo wa tasnifu zenye 'kusifika' kuwa ni bora—si kwa kuwa zinakidhi 'uhakika' ila tu kwa dhahania zake zilizo na 'mahadhi'; kwa kutambulika hivyo miongoni mwa wanataasisi wengi chini ya mashauri yake.

Basi pamoja na maendeleo yote ya sayansi katika siku hizi; upo upande wake uliona athari kubwa na mbaya zitokazo na wanataaluma kuwa na 'upofu' wa kujitakia juu ya upande mwingine wa kisomo usiohitaji mashauri yatokanayo na 'vipimo' vya utazamaji. Katika shauri hili tunaweza kuingia moja kwa moja katika kutazama kwa juu na 'kuhisi' jambo lililo 'geni' katika kukubalika.

Wanataaluma wa baiyolojia wanaweza kusema kifaranga aliyetokana na yai la kuku amefanyika kutokana na ule ute uliokuwamo kabla ya yeye kutungika na kukamilika kuja kutotolewa. Na siajabu hili limezaa shauri ya yai kuwa mboga yenye 'virutubisho' vyote vya mwili. Hii ni kwa kuwa katika mashauri yajayo na kisomo cha kemia, fizikia na hisabati; nishati yote iliyostahimilisha mabadiliko ya utokeaji na ukuaji wa kifaranga ndani ya yai ni jumla ya nishati iliyohifadhika ndani ya ute na kiini kwa kuhifadhika dhidi ya halijoto izungukayo yai. Ujazo wa yai ndiyo huja kuwa ujazo wa mwili wa kifaranga na pia chembechembe zote alifanyika kifaranga na ndizo zilezile zilizofanya ute mwanzoni. Sasa yai ni kati ya maumbile ya ajabu ya uhai; udhanifu wa kawaida wa kisayansi kulingana na mashauri yaliyotangulia yataleta tasnifu isiyokuwa ya ukweli juu ya yai na hatua za mtokezo wa kifanga. Kwa jinsi hiyo hiyo ya kutazama maumbile kwa nje imepata kuonekana kuwa kuku anaweza asile virutubisho vyenye kubeba madini ya kalsium na badala yake akawa anakula hata chembe za udongo zenye 'mika' ambayo ndiyo huwa na madini ya potasiamu. Uchunguzi unaonesha kadri kuku alapo 'mika' na akakosa kula chakula chenye madini ya kalsium kwa muda mrefu bado anaweza kutaga mayai yenye maganda ya kalsiumu ya kutosha. Lakini kuku anayekosa 'mika' na kalsium huishia kutokutaga mayai imara yenye kalsiumu. Yapo majibu kadhaa yanayoweza kudadavuliwa kutokana na matokeo ya uchunguzi huu lakini nichague moja ambalo hushangaza wachunguzi; inaonekana viumbe katika mchakato wa kuishi si lazima wale 'kiasi' kwa 'kiasi' cha madini na vitamini ili kuwa na 'afya bora' kama visomo vya leo vya sayansi ya virutubisho inavyoshawishi ukubali kwa watu. Na tena uchunguzi unaonesha hata kama kiasi cha kalsiumu kipindi cha ute ikipimwa na kuja kulinganisha na kiasi cha kalsiamu inayouunda mifupa ya kifaranga hivi viwili vipimo havina uadilifu. Mwili wa kifaranga una kalsiumu nyingi kuliko inavyowezekana kabla kutungika kwake toka kwenye ute... Je, mifumo hai inaweza 'kujitengenezea' madini na virutubisho vya jinsi tofauti hadhi na maumbile yake ya msingi? Kulingana na yai jibu la swali hili ni NDIYO.

Sayansi katika shauri hili inajiwekea mikingamo yake yenyewe kwa kung'ang'ania 'vipimo' na 'kiasi' hadi katika mifumo ya viumbe hai na kumbe namna za viumbe hai vinapitiliza kweli ndogo ndogo za kisayansi. Kulingana na hili peke yake kwa mfano, jamii hufundishwa matumizi ya mbolea za 'chumvi chumvi' katika kilimo ili 'kukuzia' mazao vizuri na haraka. Lakini ukweli wa kuchunguza ni kwamba ardhi yenye kutiwa mbolea za chumvi huonesha dalili za kukuza mazao haraka lakini baada ya misimu michache rutuba ya ardhi huathirika vibaya, na ile 'neema na hakika' ya mazao huanza kudorora na kupelekea hali ya mazao na mavuno kuwa mbaya.

Kisomo cha kemia na fizikia kinamapungufu yake makubwa kabisa pale mashauri yake yanapochukuliwa kwa 'ujumla' wake na kubebeka toka kungine. Kwa mfano mwingine, hudhanika kuwa nguvu zinazostawisha mwili wa viumbe wanyama hutokana na chakula pekee... Yapo majaribio yanayoweza hata kubatilisha hili shauri na mojawapo ni kama lile la mafundi wa kufunga wenye kuweza kukaa masiku, majuma na hata miezi pasipo kula. Vimekuwepo visa vya watu wachache wenye kudhihirisha hili miongoni mwa wanajamii lakini ni wanasayansi wachache wamebahatika kuchunguza finomena hii na kushuhudia 'jambo lisilolakawaida' kuendelea katika miili ya watu kama hawa.

Inafahamika kuwa mimea ya nchi kavu huwa na jinsi yake 'kujitengenezea chakula' kwa kitendo kinachotajwa ni 'usanisi na mwanga wa jua'. Aghalabu ni kwenye mimea na katika mwili wa wanadamu hudhahirika uwezekano wa 'kutengeneza chakula' ama 'vitamini' kutokana na mwanga wa jua; lakini si ile sehemu ya ukweli mwingine usiobayanika kwa wachunguzi wa jinsi ya macho na vipimo.

Miongoni mwa watu wa Bara la Uchina kumekuwepo kwa mashauri juu ya 'nguvu' yenye kustahimilisha miili 'kutoka ndani'; yaani kana kwamba chakula, maji na hewa kukidhi mahitaji ya 'nje' ya mwili lakini mienendo ya uhai wa mwili hustahimilishwa hasa na nguvu yenye kutajwa ni 'Chi'. Ni 'Chi' yenye kusharabiwa na viumbe hai vyote na kuhuisha maada zake ili kuchuka sura ya 'uzima' wa kimwili. Uzima huu hutajwa kuwa unajinsia za namna mbili katika moja—Yin na Yang. Kuna msemo katika lugha ya kiswahili usemao Lila na Fila havitangamani; kuna uwezokano usemi huu umetoka na mashauri ya Yin na Yang. Kulingana ya 'hekima' juu ya Yin na Yang katika 'Chi', husemwa uzima wa vitu hutegemea utangamano wa Yin na Yang ili viwe 'bukheri wa afya'. Viwili hivi visipotangamana huwa kuja kuwa ni 'maradhi' na si uzima katika mwili wa kiumbe. 'Chi' ni Pumzi ya uzima isiyodhahirika machoni lakini ikabainishwa kwa ishara za matokeo ya hali na hadhi ya viumbe hai. 'Chi' ipo kote na inapenya kote ingawaje yaweza 'kukadirika kujikusanya' pahala penye 'mgongo' wa umbile kama mlimani... Tokea siku za zamani kilele cha mafunzo ya sanaa za mapigano kilifanyika milimani ambako shauri kuu juu ya kutambua 'Chi' lilichukua mkondo wake.

'Kung Fu' ina tafsiri ya kusema 'muda wa kucheza' na ndivyo hivi katika maisha kila kitu ni mchezo. Sanaa za mapigano hukamilika ndani ya mtu kwa kutambua uwezo wa 'Chi' katika kukamilisha sanaa yake hiyo. Na ndivyo mafunzo kamili ya msanii kukamilika kwa kitendo kinachosemekana ni 'kuutupisha' akili; kwani katika hali hiyo ya utupu akili ya mwanadamu inaweza kuwa 'kioo kamili' cha kuakisi mienendo na nguvu ya 'Chi' katika kuchochea 'michezo' yote. Na hivi mtu yeyote mwenye kufikia daraja la 'usafi wa kiakili' husemwa hawezi kushindwa katika pigano lolote na mchezaji yeyote. Na ndivyo hivi hivi hata miongoni mwa masamurai wa Ujapani, ilijulikana kuwa 'ukamilifu' wa mfundwaji wa sanaa ya mapigano hukamilika kimafunzo yake pale anapofikia kutoka 'sawa' katika mapigano na mtu mwingine aliyemjuzi kwa kutangulia. Kwa kuwa katika hali ambayo mtu huwa ni 'mtupu' katika akili aweza kumaizi mara moja hata nia iliyojificha ya mpiganaji mwenzie na hivi akarudisha majibu ya kipigano kubatilisha athari zake. Hichi ni kitendo cha 'muda mfupi' kufanyika lakini pia hutokea 'pasipo muda'--siri yenyewe hasa ya athari ya 'mruko wa kikwantumu'.

'Chi' ndiyo 'Kani--The Force' ilivyo katika filamu za Vita katika Manyota—Star Wars; katika fasihi picha za sinema kama zilivyobuniwa na George Lucas. Dhana ya Lila na Fila ikiwakilishwa na mchezo wa vita kati ya mrengo wa ma-Jedayi na ma-Sithi. Ma-Jedayi wakifanya bidii sana ili waweze kutumia 'Kani' ili kuzikabili kuzishinda nguvu na fujo za ma-Sithi katika mapambano ya Himaya za madola katika ustawi wa Nyotani.

Shauri la 'Chi' ni sehemu ya utambuzi wa kisayansi usiotaka mtindo wa kiaristotle 'kuthibitisha' ukweli wa jambo. Jamii za mashariki walijua namna ya vitendo vyenye 'kuthibitisha' uwezekano wake wa kuwepo. Ikiwa kisomo cha 'Chi' kitapanuliwa kugusa mashauri mengine mengi katika uwanja, wa fizikia, kemia na baiyolojia, sayansi itakuwa ni 'kamili' na 'upanga' ule hasa wa Jedayi. Oganam ya karne ya 21 juu ya njia ya Tatu inaazimu hili.

Kulikuwepo na shauri la kitu kama 'Chi' katika jamii za wanasayansi wa mwanzoni; wao walisikia hayo kutoka katika mapokeo kutajwa kama 'Etha Iwakayo' . Majaribio ya 'kuthibitisha' uwepo ya etha hayakufaulu kutokana na msingi wenyewe hasa wa udhanifu katika kubuni kitendo cha uchunguzi. Mpaka hivi leo husemwa hakuna etha; lakini huu ni upofu tu... na ni swala la kiufundi. Etha 'HAIPIMIKI' na wala haina 'Ukiasi' wowote. Maumbile ndiyo yenye kuzaa picha kama vile 'Chi' imejikusanya kwa wingi hapa ama pale, lakini katika maumbile 'ukweli' ni msigano. Sayansi kwa jinsi ya vitendo vyake imekosa kufaulu kudadavua shauri la uwepo wa Etha kwa kuwa ndiyo hiyo inayodhahirisha hata 'wakati' wa mwanga 'kusafiri'. Msingi wa kitendo uchunguzi cha Michelson-Morley ulipanga sura la jaribio lao kwa udhanifu wa etha 'iliyosimama'.

Etha na 'Chi' ndivyo viwili hasa vilivyotajwa toka zamani kuufanya ulimwengu wote.

Vitu hivi ni 'Nuru' na 'Pumzi ya Uzima'. Madhahirisho yote ni 'Maumbo/Wakati'. Na hivyo kila chenye kufanyika katika madhahirisho kina 'kadri' ya chembe tatu katika moja. Jinsi moja ya Tatu kama 'Nuru/neno', jinsi moja ya Tatu kama 'Pumzi ya Uzima/kuchukua sura ya Umbo' na jinsi moja ya Tatu kama 'Nia'. Kwa ujumla wake wa moja na moja na moja, ulimwengu wote mzima ni 'Kiumbe Hai' –tofauti na mapungufu ya kimtazamo yaliyomo katika utaasisi wa sayansi ya leo katika kukubalika.

Vyenye kufanyika 'ndani' ya ulimwengu huchukua sura yake kwa daraja la 'Nia' kati ya kile kinachodhahirika na 'Ulimwengu'. Vile vile kinachohuishwa katika ulimwengu huchukua sura yake kwa daraja la 'Nia' na 'Pumzi ya Uzima' kwa jinsi ya 'Ulimwengu Hai'. Ulimwengu wote uliodhahirika ni 'Neno linaloishi'. Binadamu amefanyika kwa mfano wa 'Neno Linaloishi' lakini kwa funguo ya 'Nia' anao utashi wa kuamua kuzitambua siri za 'uzima wa milele' ama kusadiki 'mwili wa mauti' na kughafilika na adha zake zote. Siri ya maumbile na 'uzima' inashikiliwa na 'Utangamano uliofichika' uliyo pia ni muktadha wa 'Nia'.

Nyoka kujiviringishia katika Yai ni ishara ya 'Nia' na 'Uwezo' unaofanyikia ndani ya Yai--haya katika kutoa kielelezo cha 'Uzima wa Ulimwengu'. Kwa kuwa nyoka ni kadri ya unyoofu wa mantiki na utumikivu katika 'visomo' vyenye kutanabahi 'viasi'; na hivi ndivyo imekuwa nyoka ni kielelezo cha werevu. Mviringisho ni sifa ya kike ya uumbaji 'inayosiganisha' unyoofu na hivyo nyoka huwa ni alama kwa vyote viwili—akili yenye kumaizi mwelekeo na ile yenye kumaizi 'hadhi' ya mwelekeo. Ni hivi viwili vinavyozaa utambuzi wa 'wakati' katika mtu. Katika maisha, uwezekano wa wakati kutokea ni kwa sababu tu ya uwepo wa 'jinsi ya kiume' na 'jinsi ya kike'. Viwili hivi vikiwa katika 'Ndoa kamili'; hakuna 'wakati' na ni 'Uzima Kamili'. Lakini katika maumbile yaliyohuishwa 'Ndoa' ya 'jinsi ya Kiume' na 'jinsi ya kike' huja kwa utangamano maalum. Katika kila kile cha kiume kuna sehemu ya ukike na katika kila kile cha kike kuna sehemu ya ukiume... hii huleta 'mvutano' kati ya 'jinsi ya kiume' na ile 'jinsi ya kike'. Yin na Yang ni kielelezo cha 'Jinsi ya Kike' na 'Jinsi ya Kiume'.

Katika jinsi ya mfumo ndani ya mfumo, 'Nia' ndiyo hufanya 'Mwana'--hadhi ya chembe yenye mwelekeo na kutafuta 'kudhahirika'--ilivyo mbegu. Uzima ni 'uambukizaji uhai' na hivyo katika viumbe hai vyote vyenye kufanya jinsi ya 'uzazi' ; mazao yake hustahimilishwa na 'Uzima wa Vyote' na ulioko kote. Katika maungano ya kimaumbile ‘nia ya msingi’ ni habari/neno la jinsi ya chini, lakini 'Nia kuu’ huja kwa nafsi-roho na hasa katika kumzungumzia mwanadamu. Hata hivyo nia zote huneemeshwa na 'Uzima wa Milele' na huku zenyewe zikiakisi 'marefu' ya uhai. Marefu ya uhai ni neno liliandikwa katika jinsi ya msokoto wa chembe za kimwili. Pumzi ijazapo 'nguvu' neno hili, lenyewe huhaisha mienendo ya kimaada kukirimu hadhi ya kuwa ni kiumbe hai mpaka pale mwili huo utavyokosa 'kusharabu' pumzi kwa uadilifu wake.

Yai hujakutotoa vifaranga kwa mchakato unahusisha 'maada za ndani' yake na nguvu zisizotokana na maada yenyewe moja kwa moja. 'Namna' ya nuru na pumzi huhaisha kiumbe kipya katika yai na kusuka mwili wake katika mazingira fulani. Hili haliko katika yai tu, seli zote za uhai zinadumishwa nguvu kwa 'jinsi ya nuru' na 'jinsi ya pumzi' isiyoonekana kwa vipimo. Jinsi hii ya hivi viwili kudakwa na 'pete' ya uhai inayojulikana katika uwanja wa sayansi kama DNA. Umbo la 'pete' ni umbo lenye uwezo usiowakawaida wa 'mpitisho' wa 'wakati' na 'habari/neno' lisilo na umahala.

Inafahamika katika sayansi kuwa katikati ya seli yenye uhai kuna kiini chenye kuongoza mienendo yote ya mabadiliko ya uhai wa seli husika na humo ndani yake hukutwa 'jinsi ya misokoto pacha' inayopachikwa jina la 'utepe wa DNA'. Utepe huu huwa hasa ni 'pete' ya misokoto ya 'nyuzi' mbili ambazo hujizungusha kujisokota kulingana na kiasi cha ukali wa 'tindikali' iliyomo katika mfumo wake na hivi kusema kadri ijisokotavyo ndivyo 'maji maji' husukumwa nje na mnyongoroto kuwa mkali zaidi (B DNA, muundo wa uonekanao katika seli za kawaida za wanyama). Maji ni chombo shikilivu muhimu katika muonekano wa DNA kwa wakati. 'Maneno manne' yanayofanya DNA ni adenaini A—adenine, sitosaini C—cytosine, guanaini G—guanine na Thaimaini T—Thymine. Haya ndiyo hujirudia rudia katika msuko wote wa DNA katika 'kuchora' picha yake ya muundiko. Hizi hufanyika kwa maada zenye mfanyiko wa kuunda mienendo hai ya seli na uwepo wake katika vimimika vya kwenye seli hurahisisha msuko zaidi wa DNA pale seli inapoelekea kugawanyika na hivyo kuhitaji 'DNA pacha' ya kuendeleza 'Habari' za ususi wa seli na shughuli zake nyingine zote.

Uchunguzi wa DNA katika ugani wa fizikia umepata kufunua mawezekano yasiyo ya kawaida yatokanayo na hiyo. Gariaev kutoka Urusi, mwaka 1985 aligundua 'Athari Kizuka'--Fanthom Effect, alipokuwa wakifanyia kazi 'upipichumwa'-upigaji picha za kiuchunguzi mwanga—spectroscopy, kwa 'ribosamu' na 'kolagini'; katika taasisi ya fizikia, Urusi. Matokeo ya utafiti wake kamili alikuja kuchapisha mwaka 1991 na baadaye kutoa kitabu kulingana na kikundi chake cha kisomo maalum kilichopendekeza humo kitabuni shauri la natharia ya 'Jinomi yenye Msingi wa Mawimbi'--Wave Based Genome. 'Athari Kizuka' huonesha wazi machoni jinsi ya ugani mpya yenye kuvutia udadisi katika kuzungumzia vijinafasi vidogo vidogo vya muundiko 'ndani' ya ombwe—vacuum substructure; kwa kumulikia hiyo sehemu yenye 'Athari Kizuka' kwa Biru(jinsi ya mwanga isiyo ni mseto wa mawimbi mbalimbali ila namna ya namna ya mkusanyiko wa mawimbi mengi ya jinsi ya wimbi moja lenye nguvu na mwelekeo bayana, Laser) pamoja na namna ya mwanga wa kawaida. Na kama ilivyo ada, japo itifaki za jaribio ni zenye kubana ugumu, jaribio liliweza kurudiwa Moscow na huko Starnford na hivi ni 'ukweli' wenye kuthibitika.

Mawaidha ndani ya shauri la Jinomi yenye Msingi wa Mawimbi ni yenye kudadavua ukweli wa kwamba palipo na DNA pana sifakazi kama ngamuzi/kompyuta ya uhai ambapo ‘jinsi ya mawimbi’ huchimbuka--yenye sifa kuu tatu za kimsingi (1) kama 'vijineno' vilivyo katika muktadha wa lugha ya mwanadamu (2) Kromosamu, ambamo ndani yake huwepo DNA, ina hadhi ya kuweza kufanikisha sifakazi mbili--kurusha na kupokea mawimbi yachukuayo 'vijineno' na vile vile kung'amua maana wakati wa kupokea; kufungashia maana wakati wa marusho na (3) Kromosamu hufanya kazi kama 'chanja' za utengenezaji hologramu(holografia).

Holografia ni neno lenye kuwakilisha ufundi wa 'kupiga picha' wenye kuleta taswira ya mwonekano wa vina vya pembe zote tatu za uono yaani '3D'. Ufundi huu huja kwa kugonganisha 'miale' miwili toka katika 'chanzo cha mwanga' kulengwa kuishia kwenye uso wa 'kihifadhi picha'. Mmoja kutoka katika chanzo ni wenyekuja kuakisika toka kwenye 'kipigwacho picha' hadi kwenye uso wa 'kihifadhi picha'; na mwingine moja kwa moja toka kwenye chanzo kile kile, na kwa wakati mmoja--kwa jinsi tu iliyogawanyika njia; kwenda hadi kwenye uso wa 'kihifadhi picha'. Miale hiyo ili kufanya hologramu ['holo'-kamili, 'grafe'-andiko/mchoro/picha; kigiriki] yapasakuwa na 'unyoofu' na 'ukali' sawa wa jinsi ya mawimbi yake. Hili hufanikishwa kwa kutumia 'jinsi ya chanja' ya mpenyesho mwanga iliyo na mwachano sawa kwa 'nyufa' zake ndogo ndogo sana kadri ya 'urefu wa wimbi' la kuchujwa kupenyezea mbele. Vile vile hili linawezekana kwa kutumia biru, namna ya nuru yenye 'rangi moja' isiyo na asili ya 'mchangamano' ili kudhahirisha kadiri ya zile rangi za sekondari... Haya yote katika mpangilio maalum huwezesha upigaji picha yenye 'taswira ya ujazo' ilivyokutokea kama kile kitu kilichopigwa kilivyonekana kabla ya kupigwa picha ya holografia. Hii inamaana mara baada ya kupiga picha ya holografia, kile kitu kilichopigwa picha kikiondolewa lakini mwanga wa 'miale rangi moja nyoofu' kumulika pale pale palipopata kuwa na kitu na hapo hapo kumulika 'kihifadhi picha' basi kile kitu 'kitajitokeza' kuonekana kama vile kimewekwa tena mahala pale pale na kwa ujazo wake...

Hivyo ndivyo mfano pia 'Athari Kizuka' inavyokuwevyo kwa 'kuzuka' katika sehemu na hali kilichoasili ya kweli hakipo tena.

Jinsi hii ya shughuli itendekayo ndani ya seli za uhai inafunua ufunguo muhimu sana wa maarifa. Penye DNA pana 'kalamu' za kuandika/kuchora maumbo ya uhai na nyenendo zake za tabia katika miili ya viumbe hai. 'Sura ya umbo' katika fumbo lake, haiko popote pa umahala na ndivyo kuwa sayansi ya baiyolojia inayokubalika katika taasisi nzima; hudhanifu 'habari' yote ya msuko wa mwili huifadhiwa katika DNA. Lakini kumbe DNA hiyo hiyo ikianza kuhusishwa na vitu kama 'Mwanga' ama 'Sauti' huanza kuonesha dalili zisizokuwa za kawaida! Yumkini kusema sura ya viumbe hai ni 'kizuka' kitokanacho picha iliyoko 'mahala' pasikoonekanika. Hili katika kisomo cha uchunguzi ndani ya ugani wa baiyolojia, kimeleta nadharia ya 'Baiyoholografia ya Kikwantumu'--Quantum Bioholography.

Sauti nayo kwa jinsi ile ile ya 'kuchanjisha' mawimbi yaweza kuleta namna ya 'holografia ya kisauti' ambayo nayo hutumika katika kukadirisha chanzo cha sauti inayopimwa kule inakotokea.

'Mawimbi' na mfanyiko wa 'Unyoofu' kurahisisha mdhahiriko wa sura ya jinsi ya 'umbo hai' ndiyo ile alama ya Asclepius; Nyoka anayejivingirishia katika jiti.

Asclepius, mganga na tabibu wa kiyunani anayekuja kuwakilishwa katika ngano za kiyunani kama yule mtu aliyetupwa nyotani na kuwa 'ukanda nyota' wa Ophiuchus—'Mbeba Nyoka'. Huo upo katikati ya sekta ya Nge na Mshale; na hivi baadhi ya wanajimu wasiofuatisha mtindo wa mgawanyo wa nyuzi 30 za Zodiaki, huita Ophiuchus kama alama ya 13. Kusemwa kwamba alama 12 hujumuisha Dunia, Jua, Mwezi na Sayari lakini kuhusisha alama ya 13 ni kupenya zaidi kwenye kutambua mwenendo mzima wa mfumo wa Jua katika mfumo mwingine mpana wa 'mafungu unyota' ambako mfumo wetu wa Jua nao huzingusha dhidi ya ukati wake.

Husemwa Asclepius alijifunza siri za 'kughairisha' mauti baada ya kutia machoni nyoka wawili 'wakipeana' mzizi wa uponyaji, na hivi Ziusi, Mungu mkuu wa wayunani, ili kuepusha binadamu wasiwe 'watokufa' alimuua yeye kwa nguvu za radi na kutupia taswira yake nyotani.

Kisa hiki kizuri ni fumbo tu linalozungumzia 'udadisi' na 'hamasa ya kuingiliana kimwili'; kwa kuwa kupeana mzizi ni mbadala wa tendo la kupandikiza upya 'uhai' ambayo ndiyo hutawala 'sindano' ya Nge—nayo hutawaliwa kwa hayo; na nguvu za radi ni alama ya Mshale—alama ya yule mtu mwenye kasi na kulenga kufika katika mbingu; ambayo ni kama vile Asclesius alisulubiwa kwa kupigwa nao.

Nyoka kupeana mzizi pia huwa na kielelezo mbadala cha Nyoka Ouroboros pale 'wakati' unapogusiwa.

Ouroboros ni ile alama ya nyoka anayefukuzia kuungata mkia wake mwenyewe na hivi kutengeneza mduara kamili wa kujikunja. Ni alama ya fumbo la 'milele' ya wakati. Katika Pentauki, vile vitabu vitano vya Musa kutoka jamii ile ya watu kutoka mashariki ya kati, Israeli, huwa kina kisa cha nyoka 'amgongae' mwanadamu kisigino na mwanadamu yule 'aliyeandikwa shurti' la kumgonga huyo nyoka kichwa popote atakapompata. Lugha hizi za vielelezi ni mafumbo ya mfanyiko wa 'uzima' na madhahirisho yote katika wakati wote. Huitwa ni kama simulizi la 'Mwanzo' lakini hii ni kwa kuwa mwanzo wa vyote ni suala lenye kuvuta udadisi wa wanadamu wote katika kutafuta asili ya mambo yote na wakati wote.

Ukweli wa simulizi lenyewe ni kitendo kisicho cha jana wala kesho ila kutegemea tu na 'busara' ya yule aliyekusudiwa kukirimika kwa 'hekima' ya jinsi ya rohoni. Binadamu anayegongwa na nyoka ni ishara ya mauti isiyoepukwa na tena ijayo kwa mtu kwa kuviziwa—pale mtu alipojisahau kabisa kwa nyuma yaani kisiginoni. Vile pia kufanana na kile kisa cha 'Achelis' wa vita vya Troyi katika uyunani ya kale—aliyekuwa shujaa wa mapigano lakini udhaifu wake ulikuwa kisiginoni na ndivyo alikuja kuuliwa kwa kugongwa mshale katika kisigino na siyo kungineko kote katika mwili wake.

Hatua za mwanadamu ni msongo wa vizazi na mwendo wa safari yake ya ubinadamu. Vizazi vya mwandamu havikamiliki ila kwa kuandamwa na mauti. Na hivi shauri kuu la mwanadamu katika kuishi kwake ni kutafuta ile siri ya 'kutokufa'. Jinsi moja wapo ni kuendeleza hatua za uzazi wake; lakini hiyo siyo suluhu hasa. Yeye inampasa kumtafuta yule 'nyoka' mviziaji na 'kumuua' kabisa kwa kumponda si kwingineko kungine ila kichwani. Uadui wa nyoka na mwanadamu ni fumbo la wakati na kutupia kwake mkono dhamira ya kuishi kwa mwanadamu kusivyo na hakika ya kudumu. Sehemu ya ukweli wa maisha ambao husabisha mtu kufa daima utamchochea mwanadamu kutafuta maarifa na ukweli wa shauri lake la kuwa hai.

Na binadamu hawezi kuwa na amani mpaka afumbue fumbo la 'wakati' na 'uzima'. Uvumbuzi wa tendo la kujamiiana katika mwanadamu unaleta na adha ya 'kutambua' hakika ya mauti. Kwa kuwa uzazi ni ncha moja; na mauti ni ile ingine katika fimbo ya wakati—hakika ya kwamba 'hakuna refu lisilo na ncha'; kila chenye mwanzo hakikosi mwisho. Maisha na vitimbi vyote vya mwandamu kujisokotea katika 'wakati'.
***
Hmmm
More Article about time you got out there??
 
More Article about time you got out there??
Right,

And it prepares those are meant to be; to get in touch with symbolic meanings and extended cognitive faculties onto reality.

Only if you are predisposed towards gnosticism -- you stand the chance to be the one.

However one and one can be enticed into mysticism, gnostic disposition, if her/his individuality is willing to be transformed through love, and the love for wisdom...

You have got to outlive the old ways, transcend the fallacy of separativeness of life -- learn to discern and drop associative prejudice prescribing one and one's outer cultures, limits and bondage.

Halafu uje kuwa ni 'mtu mpya' -- 'mtu myunivasali'... Mtu mtamaduni... Makuu ya jamii zote ni urithi wako kadri vile madhaifu ya jamii zote katika mapana ya nyakati ni yako pia -- kadri vile upendo huitika kutumikia... Mtu uliye ni nuru na chumvi kwa dunia.

Ufahamu juu ya mambo ya nyakati na wakati ni kiini cha 'maajabu na miujiza' ilivyo ni maisha na kuishi...

Kama ilivyo kwa dini, ni starehe ya juu kwa mwenye kuishi katika 'hali ya neema', mtu wa busara, mtu myunivasali adumuye katika upendo na miditisha... Twaaishi kukirimika kuyajua hata yale yanayokataliwa na watu kwa kuwa wengi huonekana ni mafumbo, kufuru ama batili... Lakini ni nani aijuaye kweli?

Je, utamtambuaje yeye mwenye neema na rehema ya kweli?

Yakupasa uwe ni Pendo, na mwenye Kupendwa.

Mauwlana wa kuugusa moyo wako -- atakusaidia kile ambacho mtu mmoja wa kuitwa 'Paulo' -- kutoka kwenye vitabu vya mapokeo -- alizungumza kuhusu 'mapana, marefu na kina' cha 'Pendo'...

Pendo Kristu.

Pendo hili linafanyikaje kuwa Maumbo na Uzima kwa yote yanayonekana na yasiyonekana? Hilo nukuu ulilolileta linaoneshea njia kwa nia ya utambuzi...



Are you getting 'the message'?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom