Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Nionavyo mimi afya za viongozi wengi hapa nchini zina mushkeli mkubwa na matokeo yake mabwanyenye hawa hukimbizwa nje ya nchi badala ya kutibiwa hapa nchini. Gharama za kutibu viongozi hawa sasa ni mzigo mkubwa kwa taifa na sioni dalili ya kupungua bali kuongezeka. Sehemu kubwa ya matumizi haya wala hayana kibali cha bunge. pendekezo langu ni kuwa kuna uhaja wa kuwashinikiza wabunge kufuta kabisa kasma ya matibabu nje na yeyote anayetaka kutibiwa nje atoe pesa mfukoni kwake. Hii pia itaongeza kasi kwa watunga sera kuimarisha huduma za afya hapa nchini badala ya kuimarisha mfuko wa kuwapeleka nje kwa matibabu..............
Viongozi wengi magonjwa yao hayana tiba lakini kwa sababu ya ubinafsi wao hawako tayari kukubali ya kuwa safari zao hapa duniani zimefikia ukingoni na hivyo kuendelea kutubebesha mzigo wa kuwahudumia nje ya nchi. Mimi huwasifu Cuba ya kuwa pamoja na umasikini wao ni marufuku kwa serikali kugharimia matibabu ya kiongozi au raia yoyote nje ya nchi matokeo yake Cuba ina huduma bora za tiba hapa duniani ambazo hazina ubaguzi wowote huhusani wa kipato au cheo............
Viongozi wengi magonjwa yao hayana tiba lakini kwa sababu ya ubinafsi wao hawako tayari kukubali ya kuwa safari zao hapa duniani zimefikia ukingoni na hivyo kuendelea kutubebesha mzigo wa kuwahudumia nje ya nchi. Mimi huwasifu Cuba ya kuwa pamoja na umasikini wao ni marufuku kwa serikali kugharimia matibabu ya kiongozi au raia yoyote nje ya nchi matokeo yake Cuba ina huduma bora za tiba hapa duniani ambazo hazina ubaguzi wowote huhusani wa kipato au cheo............