Thomas Nyimbo, ajitoa CHADEMA!

WOWOWO nimekuelewa vizuri sana ,huyu mzee ni mtu asiyeshaurika ,akiamua jambo hata kama halipo sawa yeye huling,ang,ania,ni rahisi sana kumtetea ukiwa nje y aina ya siasa zake lkn ukisha ingia ndani ukamjua huwezi kufanya naye siasa nakuambia labda uwe mtu wa ndiyo mzee,baadhi ya majimbo yaliyopo ktk mkoa huu wa njombe na mbeya baada ya kujua aina ya siasa zake yalianza kumukwepa kumtegemea yeye na kuendeleza harakati za kukijenga chama bila yeye ndo maana kuna watu leo hii wameshangilia kujitoa kwake kwenye chama,suala la kutumioa pesa zake kuendesha cdm jimboni kwake ni kweli lkn asilimia kubwa ilisababishwa na yeye mwenyewe kupenda kutukuzwa ndo maana makao makuu walipowaagiza viongozi wa majimbo kufungua account za majimbo ili angalau ruzuku kidogo iwe inafika kwa ajili ya kupunguza matatizo madogo madogo yeye aliwakatalia viongozi wajimbo lake kutii agizo hili na kutusurutisha na sisi tusifanye hivyo,tulipoamua kumupuuza tuligombana naye sana .hoja yake ni kuwaonyesha viongozi wa taifa kuwa yeye yupo anaweza kukisaidia chama peke yake,pili sisi wote tuna toa pesa za kukijenga chama lkn ifike wakati kuheshimu vingozi wako wa chama iwepo na si kuwa dharau kwa vile unatoa hela zako,je kila anayetoa fedha akitaka kufanya anlotaka chama kitaenda kweli ?mzee ni mbabe mno na kuwezana naye yataka uwe na roho ya mtoto mchanga
 
Sikufuatilia saana uzi huu, niliuona jana kwa ufupi, ila kama analysis ya lole gwankaja ni kweli, viongoz cdm wanapotoka
 

Tusitazame upande mmoja tu, kama Mbowe ratiba haikumruhusu na tunajua vema pilikapilika walizokuwa nazo kipindi hiki kwa nini Nyimbo mwenyewe hakuenda kumjulia Mbowe alikokuwa? Dalili zi wazi anapenda kuabudiwa na kwa vile ana madafu ndiyio anayojivunia. Arudi kwa wanaoona pesa ni jambo la msingi kuliko uwajibikaji. Lakini amepima na kuona upepo unavyomwendea hapokeleki kote kote ndio maana anahitimishwa kwa kusema anageukiwa kuwa mgombea binafsi kama katiba mpya itamruhudu. Zaidi kuna kitu ambacho hajakigusa, kwani wengine wanafikiria kujiunga na vyama vya upinzani watahemekewa na kupewa vyeo kienyeji bila taratibu stahiki.
 
Sikufuatilia saana uzi huu, niliuona jana kwa ufupi, ila kama analysis ya lole gwankaja ni kweli, viongoz cdm wanapotoka

Walichopotoka ni kutokwenda kumjulia hali Nyimbo au kitu kingine? Kesho Mbowe akifika kwenye kitongoji chako asipofika kukujulia khali ni nongwa? Tunakutana ofisini na kazini kwani haya ya kwenye vipenyo majumbani ni urafiki mwingine si kikazi.
 
Mob Politics; viongozi wakuu Mbowe na Slaa kujinufaisha binafsi si kauli za kufumbia macho bado tunasubiri habari zaidi

Chama
Gongo la mboto DSM
 
 
Mkuu Lole Gwakisa, nadhani humfahamu Thomas Nyimbo, amasivyo usingepoteza muda kutoa maelezo marefu haya. Nyimbo hafai kuwa kiongozi hata kidogo, aliingia CHADEMA baada ya kuwekewa zengwe na CCM na kwa ujinga wake alidhani angepata ubunge kupitia CDM, hakuingia huko kwa mapenzi mema. Nyimbo ni mlafi, mbinafsi na mwenye hila, anapenda kunyenyekewa na kuabudiwa kama nini! aliwahi kuwatisha watu walioonesha nia ya kugombea ubunge katika jimbo alilodhani ni miliki yake. Bora ameondoka mapema kwani naamini angebaki angewanyanyasa sana watu ambao angedhani ni wapinzani wake. Kumbuka akiwa CCM aliwahi adhibiwa kwa utovu wa nidhamu. Hafai mtu huyu.
 
Alisema siasa za namna hiyo ni hatari kwa taifa kwa kuwa baada ya kuungwa mkono kwa kiwango cha juu na kundi la vijana kwa imani ya kukombolewa pale watakapofanikiwa kuingia madarakani na kushindwa kuwatimizia kutazua vurugu.
“Nimeachana na Chadema baada ya kubaini kuwa siasa za vyama havina tija kwa wananchi na taifa kwa ujumla na ni wakati huu sasa wa kuachana na dhana ya vyama vya siasa vituandalie sera na tunahitaji sasa itungwe sera ya kitaifa ambayo mgombe inabidi atueleze tukimchagua ataitekeleza vipi” alisema Nyimbo.


Haya ameyesema mambo ya maana sana.......mengine tunayaona sasa..chanzo cha vurugu za sasa ni ugumu wa maisha ambao hatukuutegemea....licha ya ahadi."maisha bora kwa kila mtanzania"...watakuja wengine na ahadi zao..tutawapigia makofi....tutawapa ofisi..tutawalipa...hawatatutekelezea...wataondoka....watakuja wengine.. na wengine...hadi tutakapoiaga dunia...
Cha msingi kuwa na sera ya taifa kama Ndugu yetu Nyimbo alivyoona....watueleze jinsi watakavyoitekeleza kwa rasilimali tulizo nazo... na si kwa ahadi za maneno matamu pekeee.
Pia kiundwe chombo cha kitaifa cha kuweza kudhibiti utekelezaji huo na kama rais akishindwa basi aondolewe madarakani hii itasaidia pia kuwepo kwa dhana ya uwajibikaji..kuliko sasa ambavyo kuna kulindana kwa hali ya juu.
Hongera Mheshimiwa mstaafu..karibu kundini
 
Ukiona manyoya,ujue kaliwa!.CCM wameshampa dau la kutosha.CHADEMA tusonge mbele,hamna kurudi nyuma.
 
Hivi nyie CDM mnaona ubaya wa nyimbo baada ya kujitoa. Jamani sifa zake mpeni, kama katoka why mseme mabaya yake leo siku zote mlikuwa wapi? Huu unafiki ndio unaowamaliza. Mi simo na siasa zenu za majitaka!!
 
Anaposema ishu si kuiondoa ccm na kuiweka cdm ana maana gani? Anataka ccm iendelee kuwepo hapo na itajirekebisha ikiwa madarakani. Kwa nini awaamulie vijana kuwa cdm sio suluhu? Hana nyimbo huyo!
 
Kama mambo ndiyo haya, kwa mtu aliyekuja CDM kutoka CCM makmruzuku hadi cheo cha Mlezi wa Chama kwa mikoa kadhaa, Leo amejitoa mnaona kama alikuja kutafuta ubunge, hafai kuwa kiongozi hata kidogo, ni mlafi na kadhalika. Kauli hizi zinasadifu 100% yale aliyosema Nyimbo mwenyewe kuwa CDM hakuna siasa bali kunyenyekewa na ndiyo ameamua kuondoka.
Siasa za namna hii ni hatari kwa ukuaji wa demkrasia nchini maana kuna watu wataamua kuendelea kubaki CDM kisa wakiondoka wataitwa hawafai, matapeli, walafi nk. Tulisikia mengi kuhusu SHIBUDA, MILLYA JAMES alipokuwa CCM aliitwa Fisadi leo anaitwa KAMANDA! Naogopa kuona kundi kubwa la vijana wanenda CHADEMA huku wanaona kabisa wakishaingia huko kutoka hata mazingira yatakaporuhusu watakuwa hawawezi kisa wataitwa majina mabaya. Kama vijana wa Tanzania tuna nia njema na maisha yetu na ustawi wa taifa letu, basi kama CCM imetushinda ni afadhali kukaa bila chama cha siasa maana CDM ni janga. Na kila siku njia kuelekea machafuko wao wanaita mabadiliko inatengenezwa na ufadhili mkubwa uko Marekani na Ujerumani, kumbuka hawa wanatengeneza Silaha, hakuna kwa kuzijaribisha maana hakuna Vita baridi tena.
CDM iogopwe kama ugonjwa hatari hasa linapokuja suala la kujenga chuki miongoni mwa watanzania hasa wasioko CDM!
 
Unajuwa principle ama unaropoka tu.Aliyebanwa ni nani?Asiyekuwa na mfano ama mwenye kutoa reference ya mchangiaji kipuuzi?Mifano ipo mingi,nipe mmoja tu.
 
80% ya wanachama wa Chadema ni Wachaga! Hii ina leta maana ya kua chama hiki ni cha kikabila,binafsi nimefanya research maofsini kati ya wachaga 10 utakuta 8 ni Chadema! ni kweli mtu ana haki ya kujiunga na chama chochote lakini kwa hawa wenzetu wanaonekana wana agenda ya kikabila zaidi na chadema yao!
 
Na mimi ni mlezi wa CDM huku Simiyu nimeamua kujivua gwanda! Nyooo! Thubutu! Huyo atakuwa amenusa harufu ya kijana msomi anayenyemelea hilo jimbo 2015! Anajidai kuwa huru kesho utamsikia kala matapishi yake. Chejea njaa wewe!
 
hebu tuambie sasa amejiunga na kambi ipi ya ccm ccm ya mafisadi, ccm ya waasi au ccm mkemwenza(cuf)
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…