This is very interesting story of my life

King Kong III

JF-Expert Member
Oct 15, 2010
51,637
68,566
"THIS IS VERY INTERESTING STORY OF MY LIFE"
......baada ya kulog in facebook inbox yangu ilikua inaonyesha kwamba una msg 2 moja ilikua inatoka kwa mdogo wangu akiwa ananijulia hali, msg ya pili ilinishtua kidogo maana ilikua inatoka kwa mtu ambaye si mfahamu na ilikua ina ujumbe wa kuvutia sana na kunifanya nijione kama mtu mwenye bahati ya kipekee, msg yenyewe hii hapa.........

"Hi King ! we have some mutual friends on FB and i so your page and some of your photoes- so i decided to write and ask you are you in the fasion/Beauty business in TZ? if so pls. contact me.. On fashionblacks@yahoo.co or call +1285234466 "
Hii msg ilinipa matumaini makubwa sana, japokua sikuwahi kufanya fashion show yoyote wala sijawahi kufikiria kufanya kitu kama hicho maishani mwangu, ilibidi niwashirikishe marafiki zangu, kwa kuwaomba ushauri wakanipa go ahead na baada ya mda mfupi nkamjibu kwa njia ya e-mail, nikamdanganya kwamba "Yeah i got your msg and i was so happy with it, its true that i have been in the fashion beauty for 2 years now but i didn't have any support to move foward...

"Jamaa tuliendelea kuchat akaniambia nimtumie Cv pamoja na picha zangu zisizopungua 5 nikiwa katika mavazi na pozi tofauti na baada ya kufanya hivyo alinikubali na kunisifia sana na alinieleza yakwamba kutakua na new york fashion week ambayo inategemea kufanyika very soon na alihitaji sana uwepo wangu katika hiyo show, niliendelea kua na furaha ya ajabu na matumaini makubwa, sikuamini kilichokua kinanitokea na niligundua kwamba Mungu anatenda sana miujiza.

Jamaa alinitumia invitation latter ikaenda moja kwa moja Ubalozi wa Marekani kwakua naishi Arusha ilibi nifunge safari mpaka Dar es Salaam ili kufuatilia hiyo invitation, visa pamoja na ticket nilivyokua Dar nikiwa nafuatilia hivyo vitu nilifikia nyumbani kwa rafiki yangu Tony Yayo, kwakua alikua ni rafikiyangu wa sikunyingi na ni rafiki tulieshibana japokua ni wapinzani wa jadi kama Simba na Yanga lol.
Kwakua nilikua na invitation latter niligongewa visa bila shida yoyote after there nkafuatilia ticket na mpaka mida ya jioni nlikua na kilakitu na furaha yangu ndipo ilipozidi kupita maelezo, sikutaka kuwaambia nduguzangu kilichokua kikiendelea kwakua nlitaka kuwafanyia suprise.

Usiku wa kuamkia siku ya safari ukawajia, tulikula sana bata na rafikiyangu Tony Yayo ili angalau masaa yaende ila wapi saa moja kwangu lilikua kama masaa matano, me na Tony tuliendelea kula bata na utani wetu uliendelea kama kawaida furaha ya kupitiliza ilitawala moyoni mwangu kwani kwani kila nikifikiria kwenda New york nilihisi furaha ya ajabu, kila mara nlikua nikicheka mwenyewe na mda wote nilionekana nikitabasamu kama vile naenda mbinguni lol.

Siku ya safari ikafika flait ilikua inaondoka saa 10pm, mida ya saa 2pm me na TonyYayo tukawa tumeanza safari ya kuelekea airport tulifika pale nkapekuliwa kilakitu tukawa tumekaa kwenye waiting place nikisubiria kuingia kwenye KLM, me na Tony Yayo utani uliendelea kama kawaida huku Tony aliendelea kuniita we dogo (japokua me ni mkubwa kake lol) angalia usije ukafika Marekani halafu ukagoma kurudi maana wewe nakujua vizuri :), kadri mda wa kukwea pipa ulivyokua ukizidi kukaribia furaha ilizidi kutanda moyoni mwangu nikiwa kama bado siamini amini vile, mara nkasikia tangazo kwamba tunatakiwa tuingie ndani ya ndege tayari kwa safari! furaha ilizidi mpaka mapigo ya moyo wangu yakaanza kwenda mbio nlikua na shauku kubwa sana ya kutua mji wa new york.... Nilisimama huku tukiagana na Tony Yayo kwa furaha na hugs za ukweli then nkaanza kuelekea kwenye KLM huku Tony Yayo akiwa kama haamini vile kwamba King anaelekea pande za Obama na kumuacha bongo akiendelea kunywa safari lol, nilivyopanda ngazi ya pili nikielekea kwenye pipa huku nikiwa nimeshikilia simuyangu mkononi nikiwa najiandaa kupost status FACEBOOK kwamba "I'm on my way to New York City"... mara nkasikia.............. Alarm ya simu yangu inalia! "Treeeeeeeee......
Treeeeeeeee......

Nkashtuka kumbe nipo kitandani na ni alarm ya kuniamsha saa 12 asubuhi niende JOB... LoL

"THIS IS THE BEST DREAM I EVER HAD SINCE I WAS BORN"
......thanks all for taking your time and read this story have a nice day.......
 
Sasa mkuu ndoto za hivyo sometyms si nzuri as well !
Mfano hapo ulipokua waiting lounge ungejisikia kwenda lon call or o/wise !
Nina imani ingekua sad story ujue!
 
watu8, Judgement Mtambuzi naombeni msaada wenu wa summary ndefu hiyo imenichosha kusoma

Huyu Mhe. Story yote hiyo ni dreamz tu!
Ila haelezi yote yaliojiri ndotoni ! Mengine anayafunikafunika !
Ndy tunamwambie afunguke yote! We kuanzia hom hadi Airport ambapo internalional Airline , reportin tym ni 2 hrs before departure! Mda wote huo hata short call usipate ?
 
Last edited by a moderator:
watu8, Judgement Mtambuzi naombeni msaada wenu wa summary ndefu hiyo imenichosha kusoma

Huyu Mhe. Story yote hiyo ni dreamz tu!
Ila haelezi yote yaliojiri ndotoni ! Mengine anayafunikafunika !
Ndy tunamwambie afunguke yote! We kuanzia hom hadi Airport ambapo internalional Airline , reportin tym ni 2 hrs before departure! Mda wote huo hata short call usipate ?
 
Last edited by a moderator:
Ooh pole mkuu kingkong. Hiyo ndoto imekukatili sana kwa kukatika mapema! Angalau ingesubiri hadi utue new york bhana
 
Last edited by a moderator:
Huyu Mhe. Story yote hiyo ni dreamz tu!
Ila haelezi yote yaliojiri ndotoni ! Mengine anayafunikafunika !
Ndy tunamwambie afunguke yote! We kuanzia hom hadi Airport ambapo internalional Airline , reportin tym ni 2 hrs before departure! Mda wote huo hata short call usipate ?


Asante kama ni ndoto ngoja nisepe....... Judgement thanks
 
Last edited by a moderator:
watu8, Judgement Mtambuzi naombeni msaada wenu wa summary ndefu hiyo imenichosha kusoma

Huyu ndugu yetu kaota amepata deal la umodel(wa kiume) huko US akafanye mi cat walk kwenye ile New York fashion week, hilo deal kalipata kupitia unknown friend wa FB...ikaemda hadi amefikia kupanda ndege hapo JKNIA ndio anakurupuka kitandani na kugundua the whole thing was a vapour(dream)
 
Last edited by a moderator:
Huyu ndugu yetu kaota amepata deal la umodel(wa kiume) huko US akafanye mi cat walk kwenye ile New York fashion week, hilo deal kalipata kupitia unknown friend wa FB...ikaemda hadi amefikia kupanda ndege hapo JKNIA ndio anakurupuka kitandani na kugundua the whole thing was a vapour(dream)


Ok thanks dear Watu*
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom