Wako. Kila siku watu 6 huzunguka Dunia mara kadhaa. Wako kilomita 400 juu ya uso wa ardhi wakikaa kwenye ISS (Kituo cha Anga cha Kimataifa). Kituo hiki kipo pale juu tangu mwaka 2000 yaani karibu miaka 20. Inazunguka Dunia mara 15 kila siku. Mara nyingi naweza kuiona kwenye anga la usiku inapoonekana kama nyota angavu inayopita haraka. Tangu mwaka 2000 watu 240 wamekaa pale juu, kwa kawaida kwa miezi kadhaa, wakati mwingine kwa muda mfupi zaidi. Wanaanga 6 wanaweza kukaa pale pamoja. Hadi sasa walifika 151 kutoka Marekani, 47 kutoka Urusi, 9 kutoka Japani, 8 kutoka Kanada, 5 kutoka Italia, 4 kutoka Ufaransa, 3 kutoka Ujerumani na 1-2 kutoka Belgium, Brazil, Denmark, Kazakhstan, Malaysia, Uholanzi, Afrika Kusini, Korea Kusini, Hispania, Sweden, Falme za Kiarabu (UAE), na Uingereza.
Waliopo sasa hivi ni "Expedition 61" ni wafuatao:
Luca Parmitano, Italia anaruka mara ya 2 , ndiye rubani kiongozi
Aleksandr Skvortsov, Urusi anaruka mara ya 3
Andrew Morgan, Marekani anaruka mara ya 1
Christina Koch, Marekani anaruka mara ya 1
Oleg Skripochka, Urusi anaruka mara ya 3
Jessica Meir, Marekani anaruka mara ya 1
Wote hao wanatazama umbo laDunia kuwa tufe, wakiangalia kwenye dirisha la kituo.