The West Policy on Libya Vs Putin

The West Policy on Libya Vs Putin

Tukikusifia LEO kwamba una tabia nzuri, KESHO ukionyesha tabia mbaya unataka tuendelee kukusifia?
 
mwandishi ana mentality za Kisoviet. Lazima awe biased.

Mkuu, kumbuka kuwa yule mtoto wa kike wa Col. Gadaffi, Prof. Aisha al-Gadaffi alikuwa ni UN goodwill ambassador wa UNDP toka mwaka 2009. Pia Libya kama nchi ilikuwa ni member wa UN Human Rights Council...Wamekuwa suspended baada ya hizi vuruguvurugu...

Report ya UN kuisifia Libya juu ya Human Rights ni hii hapa chini...sasa hivi source ni New York Times (sio wakomonisti!):juggle:

http://www.nytimes.com/2011/03/06/weekinreview/06libya.html
 
Na kama kweli lengo la mataifa ya magharibi ni amani mbona wamekataa ombi la ghadafi kujadiliana?
 
Jamani hawa Wamarekani ni watu wa namna gani? Mbona hawana huruma na biaadamu wenzao? hivi wanaweza kuwa na Uchungu na Walibya kuliko Muamar Gadaf!

Ni wakati muafaka kwa Wafrika kuwa na Siasa za kupendana kwa kuwa kitu kimoja na kuacha binafsi unofanya Raia wanateseka.
 
Tukikusifia LEO kwamba una tabia nzuri, KESHO ukionyesha tabia mbaya unataka tuendelee kukusifia?

Mkuu, suala hapa sio kusifiwa au kujaa sifa...

Mpaka hivi sasa tunajadili hili suala kuna:

mgogoro wa Ivory Coast ambao ni wa muda mrefu kuliko huu wa Libya;

mgogoro wa Yemen watu wanakufa kila siku;

mgogoro wa Bahrain mfalme anaua waandamanaji mpaka madaktari na manesi;

mgogoro Saudia Mfalme ametangaza kuwa hataki kuona maandamano na mwenye kuandamana atakiona cha mtema kuni....

Kwanini suala la Libya limekuwa magnified kwa haraka sana kuna nini pale???

Watu wako tayari kutumia mamilioni ya dola kwa kila kombora wanalotupa Libya wakati huko kwao wametangaza budget za kufunga mkanda (mfano mzuri ni Cameron wa Uingereza)....
 
Jamani hawa Wamarekani ni watu wa namna gani? mbona hawana huruma na biaadamu wenzao? hivi wanaweza kuwa na Uchungu na Walibya kuliko Muamar Gadaf!
Ni wakati muafaka kwa Wafrika kuwa na Siasa za kupendana kwa kuwa kitu kimoja na kuacha binafsi unofanya Raia wanateseka.

Wamarekani au Waisrael?

Gaddafi aliingia mkenge mmwenyewe alipoachana na mpango wa kufuga nyukilia. Alipigwa changa la macho. Sasa wanamshughulikia kikamilifu kwa sababu wanajua yuko uchi.
 
Na kama kweli lengo la mataifa ya magharibi ni amani mbona wamekataa ombi la ghadafi kujadiliana?

Unaua watu makusudi, unaombwa ujadiliane na watu wako unagoma tena kwa matusi kedekede, hadi watu wanaamua kumwaga pesa zao kukuchapa, unazidiwa ndo unajifanya uko tayari kujadiliana!!! Viongozi wa Africa bana! Sasa asubiri tu afanyiwe kitu ile ya S. Huessein na watachota mafuta hadi wavimbiwe ndo wataondoka!
 
Hoja ya kuzingatia ni kwamba Libya ya Ghadaffi imeendelea kutoka giza la mambo ya chinichini na uachaji wa kuunga mkono harakati za siasa kali na ugaidi na kuelekea kwenye sera za uwazi ambazo zilianza kuiletea sifa.

Vidonda kwamba Ghadaffi alihusika na Lockerbie bombing na udikteta wa kukandamiza watu wake na hasa mahasimu wake wa kisiasa unahoji nia halisi ya jitihada za Ghadaffi.

Wimbi la kudai demokrasia limemshinda pale alipotangaza kwamba atasafisha nyumba hadi nyumba na tena kuanza kuwapiga mabomu na silaha kali wananchi waliodai demokrasia zaidi.

Hapa ndipo sura yake ya kweli ilipodhihirika kuvaa ngozi ya kondoo ilihsli ni mbwa mwitu. Ni kweli amefanya mengi mazuri pia lakini huwezi kuyatia hayo maanani ikwapo ataua kwa makusudi raia wanaotaka uhuru wa kutoa mawazo yao bila kupatilizwa.Hili ndilo changa moto kwa nchi za kiarabu ambazo kwa muda mrefu zimeendesha utawala wa kiimla.
 
Mkuu, suala hapa sio kusifiwa au kujaa sifa...

Mpaka hivi sasa tunajadili hili suala kuna:

mgogoro wa Ivory Coast ambao ni wa muda mrefu kuliko huu wa Libya;

mgogoro wa Yemen watu wanakufa kila siku;

mgogoro wa Bahrain mfalme anaua waandamanaji mpaka madaktari na manesi;

mgogoro Saudia Mfalme ametangaza kuwa hataki kuona maandamano na mwenye kuandamana atakiona cha mtema kuni....

Kwanini suala la Libya limekuwa magnified kwa haraka sana kuna nini pale???

Watu wako tayari kutumia mamilioni ya dola kwa kila kombora wanalotupa Libya wakati huko kwao wametangaza budget za kufunga mkanda (mfano mzuri ni Cameron wa Uingereza)....

Hapo penye red ndio pamejibu swali lako. Jibu lipo wazi na hakuna kuzunguka mbuyu. Ni Mafuta, narudia kusisitiza, "NI MAFUTA". Gadaffi analijua hilo na siku zote alikua analijua hilo na anazijua fika human rights kuwa ni mtego mkubwa kwake lakini ameachia mwanya kwa kuwashambulia watu wake. Wamemtega akategeka akaingia kwenye 18 zao. Haya matatizo yasingekuwepo kama kusingekua na uprising iliyoanzia Tunisia, then Misri. Tunisia na Misri majeshi yalikaa pembeni na kukataa kudhuru raia wanaowalinda, Ben Ali na Mubaraka wakaondoka kwa amani, yeye kajifanya mbabe kwamba yeye ndio pekee anayeweza kuiongoza Libya kwa mafanikio utadhani yeye ni wa kuishi milele akaanza kuwamiminia risasi na mabomu raia, na ndio sasa wababe wakapata pa kuanzia. Now the question remains, "shem on who??"
 
Tunisia na Misri majeshi yalikaa pembeni na kukataa kudhuru raia wanaowalinda, Ben Ali na Mubaraka wakaondoka kwa amani, yeye kajifanya mbabe kwamba yeye ndio pekee anayeweza kuiongoza Libya kwa mafanikio utadhani yeye ni wa kuishi milele akaanza kuwamiminia risasi na mabomu raia, na ndio sasa wababe wakapata pa kuanzia. Now the question remains, "shem on who??"

The whole coalition's mission is a big flop..we subiri uone mwisho wake, rebels wataachwa kwenye mataa!
 
The whole coalition's mission is a big flop..we subiri uone mwisho wake, rebels wataachwa kwenye mataa!

Umeshaambiwa sera ya US ni "Gadaffi must GO", do you think naye watamuacha hivihivi tu!

Nilikua nawachukia hawa jamaa kama wewe vile lakini nimekuja kutambua kuwa jamaa they do watever it takes to make sure their countries' and people's future well being is maintained at whatever the cost na they protect their citizens kuliko kitu kingine chochote. We mguse mmarekani yeyote popote ulimwenguni ukione cha moto. Hata watu wao wakiandamana they do watever it takes to calm them down hata iwe ni raisi kujiudhuru.

Sisi je? We do every thing we can to protect the outsiders and/or our own personal interest. We let our LOVE for Power overpass the power of love to our own fellow citizens. Ndio maana Gadaffi yupo tayari kuua even millions as the cost for him to stay in power.

Shem on who????
 
Wakuu,naomba tujadi.Je ni sahihi majeshi ya muungano kuishambulia Libya?Je Africa Unioni inafanya nini?Hebu tujaribu kujadili,kuna sehemu nyingi sana zina waasi Africa kwa nini wasipige siku zote?Naomba tujadili kwa hoja na sio ushabiki
 
Ni sahihi.......lakini ni sahihi kwa upande upi......wa mataifa ya magharibi
au mataifa ya affrika.
Mataifa ya magharibi na marekani ni sahihi sana kwakuwa lengo ni kupata
rasilimali kwa uchumi wao,ni kwasababu umeuliza kwa wabongo wenzako
lakini kama ungemwuliza mfaransa angejibu tena sahihi mno ni hii ni kwasa-
babu wananufaika na uvamizi ule.

Mataifa ya afrika si sahii kwa ule uvamizi kwa maana wanaokufa libya
ni waafrika wenzetu na kwa asilimia ndogo libya imechangia katika uchumi
wa afrika lakini ni nani atahoji juu ya uvamizi ule na ikiwa bajeti zetu kwa
asilimia kubwa tunategemea kwenye mataifa hayo.
 
Kabla ya haya mashambulizi dhidi ya Libya,ujerumani ndio walikuwa na share kubwa ya biashara ya mafuta na Libya...Labda wanaanza kuona hawapo upande wa ushindi kwenye hili sakata.
Lets wait and see.
 
Ni sahihi.......lakini ni sahihi kwa upande upi......wa mataifa ya magharibi
au mataifa ya affrika.
Mataifa ya magharibi na marekani ni sahihi sana kwakuwa lengo ni kupata
rasilimali kwa uchumi wao,ni kwasababu umeuliza kwa wabongo wenzako
lakini kama ungemwuliza mfaransa angejibu tena sahihi mno ni hii ni kwasa-
babu wananufaika na uvamizi ule.

Mataifa ya afrika si sahii kwa ule uvamizi kwa maana wanaokufa libya
ni waafrika wenzetu na kwa asilimia ndogo libya imechangia katika uchumi
wa afrika lakini ni nani atahoji juu ya uvamizi ule na ikiwa bajeti zetu kwa
asilimia kubwa tunategemea kwenye mataifa hayo.
Jibu kwa upande wako wewe unavyoona wewe binafsi bila kujali kama ni mwafrika ama mfaransa,yani kwa kutumia vigezo ambavyo ni universally accepted.
 
Sio sahihi hata kidogo wanavyofanya,yaani huu ni ukoloni mpya,waafrika tuungane kwa pamoja kupinga mashambulizi haya yanayofanywa na nchi za magharibi.
 
Wakuu,naomba tujadi.Je ni sahihi majeshi ya muungano kuishambulia Libya?Je Africa Unioni inafanya nini?Hebu tujaribu kujadili,kuna sehemu nyingi sana zina waasi Africa kwa nini wasipige siku zote?Naomba tujadili kwa hoja na sio ushabiki

naona ni sahihi kabisa.
 
Back
Top Bottom