Anthony Kabeho
Member
- Apr 12, 2018
- 71
- 33
He was a hero
ICC ilianzishwa kwa lengo la kuwahukumu viongozi wa Africa & Uarabuni mkuu.Sakozy alishiriki kumuua Gadafi ili tu akwepe deni la mil.40.dola alizokopeshwa.unajiuliza Mtu kama Sakozy bado yuko huru anadunda ICC haijawahi kumkamata.
Maelfu ya Watu.wamekufa Libya kila uchao nchi ile imeparaganyika vibaya sana ni Somalia nyingine.waliofanya hayo wapo wabakula bata akina Obama walishiriki wako tu mtaani.
Ni upuuzi mkubwa
Ni kweli mkuu. Jamaa Libya ilimshinda..Naona wenye Libya yao wanaimudu vizuri .. Iko vizuri leo, kuliko jana..Heshima kwenu wanajamvi,
Colonel Muammar al-Gaddafi ni mtawala wa Libya tangu mwaka 1969,ametawala Libya kwa zaidi miaka arobaini haonyeshi dalili za kuachia madaraka ana mwandaa mwanae Sayf al-Islam kutawala nchi baada ya yeye kuanza kuchoka hiyo ndiyo demokrasia ya nchi nyingi za kiaarabu.
Colonel Muammar al-Gaddafi ni aina ya watawala wanaodhani utawala ni kwaajili ya wao na familia zao pekee wananchi wengine kazi yao kubwa ni kutawaliwa tu na si vinginevyo.Hosni Mubarak alimwandaa mwanae Gamal Mubarak kutawala Misri haikuwa kitu cha ajabu au kushangaza kwa wanaofuatilia siasa za waarabu.Pengine Colonel Gaddafi alitaka kuiga mfano wa rais wa Syria Hafez al-Assad aliyemwandaa mtoto wake Bashir al-Assad kutawala baada ya kufariki.
Wananchi wa nchi za kiaarabu wameamuka sasa hawataki ujinga wa watawala wa kujilimbikizia mali na kurisisha utawala kwa watoto na familia zao.Nguvu ya umma ni kubwa kuzidi vifaru na bunduki hakuna wa kuzuia mabadiliko sana sana wataweza kuchelewesha kidogo tu.Hakuna mtu angeweza kuamini Colonel Gaddaf mtawala aliyewatisha hata mataifa makubwa kwa kufadhili vikundi vya kigaidi yuko katika hatihati ya kuondolewa na wananchi wake waliomchoka.Inashangaza zaidi Colonel Gaddaf alikuwa na tamaa ya kutaka kutawala Afrika [United State of Africa]wakati nchi ndogo ya Libya yenye ukubwa wa sq km 1.77 million na idadi ya watu milion 6.5 ilishamshinda siku nyingi.
Muda...Umeongea na kuamuaDoctoz,akissumo na wewe Mringo mimi nawaelewa SANA na siegemei mambo ya Imani lakini nilichotaka kusema ni kuwa walibya wanayo haki ya kuamua nani kiongozi Bora na nani mbaya wao hivyo wamuondoe.
Nakubali kunaweza kuwa na influence toka nje lakini Kama nguvu ya umma iko upande wake wasingeweza kumuondoa lakini kulikuwa na GAP ambalo ndiyo udhaifu Wa Gaddafi
Tusijenge kichwani mwetu kuwa kila sehemu kunapotokea matatizo basi woote wanasema kuna mkono Wa Marekani si kila kitu Marekani tatizo kubwa ni viongozi wetu si wazelendo wanasababisha hata maanguko yao.
Kinachonishangaza mpaka sasa hivi ni kuwa Libya wananchi wanamuona Gaddafi Kama dikteta lakini sisi tuliokuwa tunapokea Misaada yake tunamuona kama Shujaa Wa Afrika tumefikia hata kubadirisha Historia ya Vita vya Kagere ambapo Gaddafi ameondolewa kama mshirika mkubwa aliyetoa Ndege(Tupolev),Askari na Silaha ili kumsaidia Idd Amin kuivamia nchi yetu
Hivi misaada ya Gaddafi ndiyo imetufanya tubadili historia na tumwite shujaa?????
Osama kwao anaonekana Kama Gaidi sisi huku tukimwita Shujaa ita-sound vipi????????
Huu uzi umenifundisha mengi sana juu ya tabia za watanzania. Tupo tayari kukaa upande wowote ule ili mradi unufaishe tunachotaka.
Mwisho tunaona watu wanavyoanza kuwalaani NATO na washirika wake juu ya Qaddafi, lakini hao hao watu hawakulaani wakati magharibi ikichochea haya. Pengine tukaenda mbali kumlaani Mugabe kwa kutoa mawazo yake.
Sad, very Sad indeed.
Kwa ufupi ni kwamba ICC ipo kuwasaidia USA & washirika wakeICC ilianzishwa kwa lengo la kuwahukumu viongozi wa Africa & Uarabuni mkuu.
Kwa ufupi ni kwamba ICC ipo kuwasaidia USA & washirika wake
Hapana mkuu, ICC + USA & WASIRIKA WAO ipo kwa ajili ya kuwaondoa viongozi ambao ni wabishi kufuata maagizo/matakwa yao pasi na kujali km waliwaweka wenyewe ama lah!.Sasa si ndio wanawaweka madarakani, lazima wawe na chombo chao cha kuwawajibisha wakienda kinyume na makubaliano yao.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ishakombolewa mkuu ,waweza kwenda sasa .
John Pombe MagufuliKuna mwafrika(mwarabumwafrika) mwingine atakaekuwa na msimamo na mtendaji kama Gaddafi?
Bofya http://a2.sphotos.ak.fbcdn.net/hpho...77416200950_714010949_9508348_729709553_n.jpg
Was very intelligent person Kwanza alikuwa na idea ya kuunganisha bara la Afrika iwe na rais mmoja na bank ya AfrikaSemeni yooote lakini LIBYA WAS THE ONLY COUNTRY isiyokuwa na madeni mpaka Gaddafi anavyong'olewa. Hakuna nchi nyingine diniani!!!!
ukipata jibu,,uni tagHivi hii furaha baada ya kifo cha Gadaff bado ipo huko Libya?