The rise and fall of Colonel Muamar Gadaffi

Sakozy alishiriki kumuua Gadafi ili tu akwepe deni la mil.40.dola alizokopeshwa.unajiuliza Mtu kama Sakozy bado yuko huru anadunda ICC haijawahi kumkamata.

Maelfu ya Watu.wamekufa Libya kila uchao nchi ile imeparaganyika vibaya sana ni Somalia nyingine.waliofanya hayo wapo wabakula bata akina Obama walishiriki wako tu mtaani.

Ni upuuzi mkubwa
ICC ilianzishwa kwa lengo la kuwahukumu viongozi wa Africa & Uarabuni mkuu.
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Colonel Muammar al-Gaddafi ni mtawala wa Libya tangu mwaka 1969,ametawala Libya kwa zaidi miaka arobaini haonyeshi dalili za kuachia madaraka ana mwandaa mwanae Sayf al-Islam kutawala nchi baada ya yeye kuanza kuchoka hiyo ndiyo demokrasia ya nchi nyingi za kiaarabu.

Colonel Muammar al-Gaddafi ni aina ya watawala wanaodhani utawala ni kwaajili ya wao na familia zao pekee wananchi wengine kazi yao kubwa ni kutawaliwa tu na si vinginevyo.Hosni Mubarak alimwandaa mwanae Gamal Mubarak kutawala Misri haikuwa kitu cha ajabu au kushangaza kwa wanaofuatilia siasa za waarabu.Pengine Colonel Gaddafi alitaka kuiga mfano wa rais wa Syria Hafez al-Assad aliyemwandaa mtoto wake Bashir al-Assad kutawala baada ya kufariki.

Wananchi wa nchi za kiaarabu wameamuka sasa hawataki ujinga wa watawala wa kujilimbikizia mali na kurisisha utawala kwa watoto na familia zao.Nguvu ya umma ni kubwa kuzidi vifaru na bunduki hakuna wa kuzuia mabadiliko sana sana wataweza kuchelewesha kidogo tu.Hakuna mtu angeweza kuamini Colonel Gaddaf mtawala aliyewatisha hata mataifa makubwa kwa kufadhili vikundi vya kigaidi yuko katika hatihati ya kuondolewa na wananchi wake waliomchoka.Inashangaza zaidi Colonel Gaddaf alikuwa na tamaa ya kutaka kutawala Afrika [United State of Africa]wakati nchi ndogo ya Libya yenye ukubwa wa sq km 1.77 million na idadi ya watu milion 6.5 ilishamshinda siku nyingi.
Ni kweli mkuu. Jamaa Libya ilimshinda..Naona wenye Libya yao wanaimudu vizuri .. Iko vizuri leo, kuliko jana..

Pumzika kwa Amani Gaddafi.
Mengine atahukumu Mungu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Doctoz,akissumo na wewe Mringo mimi nawaelewa SANA na siegemei mambo ya Imani lakini nilichotaka kusema ni kuwa walibya wanayo haki ya kuamua nani kiongozi Bora na nani mbaya wao hivyo wamuondoe.
Nakubali kunaweza kuwa na influence toka nje lakini Kama nguvu ya umma iko upande wake wasingeweza kumuondoa lakini kulikuwa na GAP ambalo ndiyo udhaifu Wa Gaddafi
Tusijenge kichwani mwetu kuwa kila sehemu kunapotokea matatizo basi woote wanasema kuna mkono Wa Marekani si kila kitu Marekani tatizo kubwa ni viongozi wetu si wazelendo wanasababisha hata maanguko yao.
Kinachonishangaza mpaka sasa hivi ni kuwa Libya wananchi wanamuona Gaddafi Kama dikteta lakini sisi tuliokuwa tunapokea Misaada yake tunamuona kama Shujaa Wa Afrika tumefikia hata kubadirisha Historia ya Vita vya Kagere ambapo Gaddafi ameondolewa kama mshirika mkubwa aliyetoa Ndege(Tupolev),Askari na Silaha ili kumsaidia Idd Amin kuivamia nchi yetu
Hivi misaada ya Gaddafi ndiyo imetufanya tubadili historia na tumwite shujaa?????
Osama kwao anaonekana Kama Gaidi sisi huku tukimwita Shujaa ita-sound vipi????????
Muda...Umeongea na kuamua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huu uzi umenifundisha mengi sana juu ya tabia za watanzania. Tupo tayari kukaa upande wowote ule ili mradi unufaishe tunachotaka.

Mwisho tunaona watu wanavyoanza kuwalaani NATO na washirika wake juu ya Qaddafi, lakini hao hao watu hawakulaani wakati magharibi ikichochea haya. Pengine tukaenda mbali kumlaani Mugabe kwa kutoa mawazo yake.

Sad, very Sad indeed.
 
Watu wanaangalia majina tu, tangu lini Kina Idd wakawa wakosaji dhidi ya kina Jukius ?

Hata Gadaff wakati analeta majeshi yake kuwaua wadanganyika hakukosea, mbna ni mtu wetu hatumi wala hatusikii
 
Huu uzi umenifundisha mengi sana juu ya tabia za watanzania. Tupo tayari kukaa upande wowote ule ili mradi unufaishe tunachotaka.

Mwisho tunaona watu wanavyoanza kuwalaani NATO na washirika wake juu ya Qaddafi, lakini hao hao watu hawakulaani wakati magharibi ikichochea haya. Pengine tukaenda mbali kumlaani Mugabe kwa kutoa mawazo yake.

Sad, very Sad indeed.

..mimi sijawahi kumuunga mkono Gaddafi tangu ashirikiane na Iddi Amini ktk vita vya Kagera.

..na ilikuwa almanusra tushindwe vita vile kutokana na Gaddafi kuingilia akitumia silaha kali ambazo vijana wetu walikuwa na wakati mgumu kuzimudu.

..ilibidi wapiganishaji vita wa Jwtz wabadilishe makamanda waliokuwa mstari wa mbele, pamoja na mbinu za kimapigano, ili kuokoa jahazi maana Walibya na Waganda walianza kutuelemea ktk uwanja wa vita.
 
Ndio maana Hitler alisema Mwili wake uchomwe moto na uteketezwe wote kwa sababu aliogopa fedheha na hukumu ya Wananchi,wananchi wana hukumu mbaya sana Gaddafi alichomwa Singe makalioni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom