Brother Mwanakijiji, usiumize kichwa bure! FELESHI KAMWE HAWEZI KUMSHITAKI CHENGE, ANALIPA FADHILA! Hata akilazimishwa yuko tayari kujiuzulu alimradi mzee wake hasimamishwi kizimbani!
Eliezer Feleshi amevunja rekodi kuwa DPP wa kwanza, si Tanzania tu bali Afrika ya Mashariki, kushika wadhifa huo mkubwa akiwa na umri mdogo chini ya miaka 40 na akiwa na uzoefu mdogo katika uongozi na katika taaluma ya sheria. Uteuzi wake uliacha vinywa wazi miongoni mwa wanasheria wote nchini maana Feleshi hana sifa ya pekee kuweza kuwaruka mawakili waandamizi lukuki walio katika wizara ya sheria. Aliyewezesha yote haya kufanyika si mwingine ni Andrew Chenge. Alijua alichokuwa anafanya: alikuwa anawekeza kwa kijana mdogo, Msukuma mwenzake na ndugu yake kiukoo akijua kuwa siku moja atasimama kidete kulipa fadhila kwake! Sasa yanaonekana: faili la Chenge litazungushwa wee mpaka Waswahili msahau kuhusu majambo ya mzee wa vijisenti.
Ndiyo maana nasema, Mzee Mwanakijiji achana na hoja nzito unazotaka kuingiza kwenye suala hili: hapa hakuna jurisprudence ni WIZI MTUPU!!!