Habibu B. Anga
JF-Expert Member
- May 7, 2013
- 6,557
- 25,748
- Thread starter
- #681
*THE OTHER HALF*
*SEASON 1 - THE LEGEND OF ANABELLE*
EPISODE 47
Si lazima kuwa Nabii ili kuweza kuona nyakati zijazo na wala si lazima kuwa mtume ili kuwa wakala wa habari njema. Kuna jambo au kitu au kiumbe kilicho juu ya sisi wote, si Mungu kwa kuwa Mungu ni mkuu zaidi. Lakini kiko kiumbe ambacho kilipata kuwepo kabla hata ya mito, maziwa, bahari na hata jua kupata kuwepo. Mwenye werevu wa kujua siri zote kuu juu ya ardhi. Mwenye uhai usiokoma kwa maelfu na maelfu ya miaka. Mwenye kujidhihirisha katikati yetu kama binadamu mara kadhaa katika umbo la uanadamu. Mwanzilishi wa starehe, anasa tangu mwanzo wa ustaarabu wa dunia.
Pengine ndiye ambaye alijidhihirisha akiwa katika hali ya ubinadamu kupitia mashujaa wa historia kama Mfalme Alexander, au shujaa wa vita kama Archilles. Pengine alijidhihirisha tena katila sura ya wanataaluma kama Leonardo Da Vinci au mwanamapinduzi wa kimuziki kama Morzart.
Hakuna anayejua, lakini kiko kiumbe cha hali ya juu zaidi yetu. Kiumbe ambacho kina uhai usio koma. Kiumbe ambacho kimewahi kukutana ana kwa ana na Zeus, Mungu wa Kigiriki. Kiumbe ambacho kimewahi kufanya jaribio la kumuoa Hera, Mungu mkuu wa miungu yote ya kike ya kale. Kiumbe ambacho kimewahi kukabiliana na kutunishiana misuli na Hades, mungu wa vita na mungu wa ulimwengu wa giza.
Hakuna kitabu cha imani ambacho kimethubutu kumzungumzia kiumbe huyu na vitabu vya kihistoria ni vile vitabu vya siri pekee ambavyo vimethubutu kutia mkono kumdhihirisha.
Mara ya mwisho alijidhihirisha katika karne ya 16 akiishi katikati yetu. Kwa zaidi ya karne tano hakuna mwanahistoria ya giza ambaye amefanikiwa kunasa walau dalili ya uwepo wake katikati yetu. Lakini ni tukio moja tu, tukio ambalo limetokea mwaka 2038 ndilo ambalo liliamsha uwepo wake kutoka chini kabisa ya vilindi vya bahari na hatimaye kwa mara ya kwanza kuonekana dalili ya uwepo wake katikati yetu. Tukio la kufunguliwa kwa chupa kutoka katika sanduku la Pandora.
Kalamu hii ikawe ushuhuda wa yale ambayo yametokea, yanatokea na yatakuja kutokea siku chache za usoni.
******
Mawimbi ya bahari yalikuwa yanapiga kwa nguvu kiasi na kuwasukuma akina Mzee Caleb na wenzake ambao walikuwa wamelala pembezoni mwa bahari mchangani bila kujitambua.
Kadiri ambavyo mawimbi yalivyokuwa yanapiga na kuwasukuma ndivyo ambavyo yalikuwa kama yanawatikisa ili kuwaamsha warudi katika ufahamu.
"Koh koh koh koh..!!"
Walker ndiye alikuwa wa kwanza kuamka kabla ya wenzake wote. Alijitahidi kusimama japo bado alikuwa anatapika na kichwani ana kizungu zungu.
Pale mchangani walikuwa wamelala wenzake wengine makomando sita pamoja na Mzee Caleb.
"Mzee mzee mzee! Mzee Caleb.!"
Walker alimkimbilia kwanza mzee Caleb ambaye alikuwa amelala pembeni yake huku akiwa hajitambui.
Alitumia karibia dakika nzima kumtikisa mpaka Mzee Caleb alipoamka na kupata ufahamu.
"Koh koh… tuko wapi.!?" Mzee Caleb alimka huku anahema kwa nguvu na kukohoa mfululizo.
Kabla Walker hajajibu, makomando wenzake nao walikuwa wameamka tayari. Silaha ambazo walikuwa nazo awali walipokuwa wanaingia msitu wa Ox kule Maryland hawakuwa nazo tena. Wala yale mabegi ya mgongoni ya kijeshi hawakuwa nayo tena.
"Nini kimetokea?" Mmoja wa wale vijana makomando akauliza.
Walisimama pale kwenye pwani wakiangaza macho huku na huko. Mara ya mwisho walipokuwa na fahamu zao walikuwa ndani ya msitu wa Ox na wakikuwa wanakaribia kushambuliwa na kuraruriwa vipande vipande na binadamu wa ajabu ambaye alikuwa anawafuatilia.
Sent using Jamii Forums mobile app
*SEASON 1 - THE LEGEND OF ANABELLE*
EPISODE 47
Si lazima kuwa Nabii ili kuweza kuona nyakati zijazo na wala si lazima kuwa mtume ili kuwa wakala wa habari njema. Kuna jambo au kitu au kiumbe kilicho juu ya sisi wote, si Mungu kwa kuwa Mungu ni mkuu zaidi. Lakini kiko kiumbe ambacho kilipata kuwepo kabla hata ya mito, maziwa, bahari na hata jua kupata kuwepo. Mwenye werevu wa kujua siri zote kuu juu ya ardhi. Mwenye uhai usiokoma kwa maelfu na maelfu ya miaka. Mwenye kujidhihirisha katikati yetu kama binadamu mara kadhaa katika umbo la uanadamu. Mwanzilishi wa starehe, anasa tangu mwanzo wa ustaarabu wa dunia.
Pengine ndiye ambaye alijidhihirisha akiwa katika hali ya ubinadamu kupitia mashujaa wa historia kama Mfalme Alexander, au shujaa wa vita kama Archilles. Pengine alijidhihirisha tena katila sura ya wanataaluma kama Leonardo Da Vinci au mwanamapinduzi wa kimuziki kama Morzart.
Hakuna anayejua, lakini kiko kiumbe cha hali ya juu zaidi yetu. Kiumbe ambacho kina uhai usio koma. Kiumbe ambacho kimewahi kukutana ana kwa ana na Zeus, Mungu wa Kigiriki. Kiumbe ambacho kimewahi kufanya jaribio la kumuoa Hera, Mungu mkuu wa miungu yote ya kike ya kale. Kiumbe ambacho kimewahi kukabiliana na kutunishiana misuli na Hades, mungu wa vita na mungu wa ulimwengu wa giza.
Hakuna kitabu cha imani ambacho kimethubutu kumzungumzia kiumbe huyu na vitabu vya kihistoria ni vile vitabu vya siri pekee ambavyo vimethubutu kutia mkono kumdhihirisha.
Mara ya mwisho alijidhihirisha katika karne ya 16 akiishi katikati yetu. Kwa zaidi ya karne tano hakuna mwanahistoria ya giza ambaye amefanikiwa kunasa walau dalili ya uwepo wake katikati yetu. Lakini ni tukio moja tu, tukio ambalo limetokea mwaka 2038 ndilo ambalo liliamsha uwepo wake kutoka chini kabisa ya vilindi vya bahari na hatimaye kwa mara ya kwanza kuonekana dalili ya uwepo wake katikati yetu. Tukio la kufunguliwa kwa chupa kutoka katika sanduku la Pandora.
Kalamu hii ikawe ushuhuda wa yale ambayo yametokea, yanatokea na yatakuja kutokea siku chache za usoni.
******
Mawimbi ya bahari yalikuwa yanapiga kwa nguvu kiasi na kuwasukuma akina Mzee Caleb na wenzake ambao walikuwa wamelala pembezoni mwa bahari mchangani bila kujitambua.
Kadiri ambavyo mawimbi yalivyokuwa yanapiga na kuwasukuma ndivyo ambavyo yalikuwa kama yanawatikisa ili kuwaamsha warudi katika ufahamu.
"Koh koh koh koh..!!"
Walker ndiye alikuwa wa kwanza kuamka kabla ya wenzake wote. Alijitahidi kusimama japo bado alikuwa anatapika na kichwani ana kizungu zungu.
Pale mchangani walikuwa wamelala wenzake wengine makomando sita pamoja na Mzee Caleb.
"Mzee mzee mzee! Mzee Caleb.!"
Walker alimkimbilia kwanza mzee Caleb ambaye alikuwa amelala pembeni yake huku akiwa hajitambui.
Alitumia karibia dakika nzima kumtikisa mpaka Mzee Caleb alipoamka na kupata ufahamu.
"Koh koh… tuko wapi.!?" Mzee Caleb alimka huku anahema kwa nguvu na kukohoa mfululizo.
Kabla Walker hajajibu, makomando wenzake nao walikuwa wameamka tayari. Silaha ambazo walikuwa nazo awali walipokuwa wanaingia msitu wa Ox kule Maryland hawakuwa nazo tena. Wala yale mabegi ya mgongoni ya kijeshi hawakuwa nayo tena.
"Nini kimetokea?" Mmoja wa wale vijana makomando akauliza.
Walisimama pale kwenye pwani wakiangaza macho huku na huko. Mara ya mwisho walipokuwa na fahamu zao walikuwa ndani ya msitu wa Ox na wakikuwa wanakaribia kushambuliwa na kuraruriwa vipande vipande na binadamu wa ajabu ambaye alikuwa anawafuatilia.
Sent using Jamii Forums mobile app
(search) andika chaguo lako, mfano " The other half Episode 21"... Kisha search..