The Other Half (Simulizi)

The Other Half (Simulizi)

THE OTHER HALF



EPISODE 7


"Wengi wanaamini binadamu aliumbwa na Mungu au kiumbe kingine chenye nguvu na uwezo zaidi. Wengine wanaamini kwamba binadamu ni zao la mabadiliko ya viumbe vya kale na dunia. Vyovyote, kama tuliumbwa au tilitokea tu, kitu kikubwa zaidi ambacho kiliwekwa ndani yetu ni uhuru wa kuamua, free will.! Uwezo wako wewe binafsi kuamua kufanya utakacho na kuamua muelekeo wa maisha yako. Zawadi hii tuliyopewa licha ya kuwa adhimu, lakini pia inabeba mzigo wa jukumu linalowatesa binadamu tangu kuwepo kwa ulimwengu. Uhuru wetu wa kufanya maamuzi unaweza kutupeleka katika kuikuza mbari ya binadamu au kuipoteza kabisa. Mzigo huu pia wa jukumu unagusa mtu mmoja mmoja. Ni mara ngapi ambapo nafsini mwako, uamuzi unaotaka kufanya ni kukimbia hali iliyopo lakini moyoni unafahamu inatakiwa ubaki na kupambana? Ni mara ngapi ambapo nafsini mwako uamuzi unaotaka kufanya ni kuishi katika mstari mnyoofu lakini moyoni mwako unajua kabisa unapaswa kuvunja kanuni ili upate unachokitaka??

Uhuru wa kufanya uamuzi, free will ni Zawadi kubwa zaidi iliyowekwa ndani mwetu lakini ni mzigo mkubwa zaidi wa uwajibikaji binafsi ndani yetu na mara nyingi umekuwa ni kikwazo pale tunapotaka kusonga mbele au kupambana kutetea tunachokiamini. Mbaya zaidi ni pale tunapopambana na viumbe walio tofauti na sisi, viumbe ambao hawana hisia zetu.…. Binadamu tunajivunia ubora wa hisia, hii ni moja ya vitu ambavyo vinafanya haijalishi kutakuwa na maendeleo kiasi gani ya teknolojia, lakini kamwe roboti hawezi kufafanana na binadamu. Kwa sababu huwezi kutengeneza hisia. Hisia ni kitu tunazaliwa nacho, hakifundishwi. Hisia zote, mbaya na nzuri, hisia zote kuanzia urafiki, huruma mpaka ukatili. Ni binadamu pekee anazaliwa nazo. Lakini hisia nayo ni Zawadi na papo hapo ni kikwazo kwetu kufika tunapotaka.

Sasa je, itakuwaje pale ambapo binadamu atatakiwa kupambana na kiumbe chenye ubora kama walionao binadamu, lakini wenyewe ni bora zaidi kwa kuwa hawana hisia. Hisia pekee waliyonayo ndani yao ni Kiu ya kutaka kuishi, yaani survival.!

Binadamu, anawezaje kushinda vita pale anapotakiwa kushindana na viumbe wa ajabu, watotot wa Anabelle 1 (Maldives), waliozaliwa mwaka 1936.? Binadamu anawezaje kutetea haki yake ya kuendelea kuishi juu ya uso wa Dunia??







NDANI YA ANABELLE 27 (ULIPOKUWA MJI WA DAR ES SALAAM)

Dr. Cindy Wheaton alikuwa amemaliza kumchuna ngozi yule kiumbe pale chini na sasa alikuwa amesimama anawaangalia wenzake huku mkononi ameshikilia ngozi ya binadamu yenye manyoya mengi kama paka.

"Hii ngozi ya nini?" Kanali akauliza kwa mshangao.

"No no! Kabla hajajibu hii ngozi ya nini ni vyema kwanza atuambie anajuaje mambo mengi hivi kuhusu Anabelle na vilivyomo ndani yake?" Salim akadakia kabla Cindy hajajibu swali la Kanali.

"Salim! Huo sio muda sahihi wa kuanza kupeana mihadhara, mimi ni mtaalamu wa akiolojia kwahiyo si ajabu kujua vitu vingi." Cindy akajibu akiwa anaikunja ile ngozi bila kumuangalia Salim.

"Sikiliza Cindy… mke wangu na mtoto wangu wako humu ndani na watu wengine zaidi ya milioni nne... Mpaka sasa sijui ninachokifanya humu na nahitaji kujua unafahamu vipi taarifa zote hizi kuhusu Anabelle.?" Salim akauliza kwa hasira safari hii.

Cindy akavuta pumzi kubwa ndani na kuishusha.

"OK! Mnafahamu hili jina la Anabelle limetokea wapi?" Cindy akawauliza huku anawaangalia wenzake mmoja mmoja.

Wote wakaangaliana huku wanatikisa vichwa.

"Nadhani ndivyo zinavyoitwa… ndivyo ambavyo imezoeleka na kuripotiwa hivyo kwenye vyombo vya habari kwamba " mji fulani umegeuzwa kuwa Anabelle " Magdalena akjibu.

"Nadhani mmewahi kusikia simulizi kuhusu Pandora, si ndivyo?" Cindy akawauliza.

Wote wakaangaliana na kisha kutingisha vichwa.

Cindy akaanza kuwasimulia simulizi kuhusu Pandora kama ambavyo Mzee Caleb aliwasimulia makamu wa Rais wa Marekani David Logan na timu yake kwenye situation room. Akawaeleza kila kitu kuhusu namna ambavyo mungu wa kigiriki, Zeus alivyomuumba mwanamke wa kwanza Pandora na kumpa sanduku lenye chupa zilizojazwa udhalimu wa ulimwengu na kumpa sharti la kutofungua sanduku hilo.

Lakini hakuwaeleza chochote kuhusu mchoro wa George Washington kuhusika na sanduku hilo kwa kuwa hata yeye Cindy alikuwa haijui siri hiyo.

"Sasa! Hii simulizi ya kale inatuambia kuwa mwanamke huyu wa kwanza Pandora aliwekwa kwenye mji wa kale unaoitwa Anabelle zaidi ya miaka elfu kumi iliyopita… ndipo hapa baada ya haya matukio ya miji kutwaliwa kuanza na tulipong'amua matukio haya kuhusiana na chupa za kwenye sanduku la Pandora… tukaibatiza jina la Anabelle miji hii inayotwaliwa.!"

Cindy akanyamaza kidogo kumeza mate. Kisha akaendelea.

"Sasa huu mji wa kufikirika wa Anabelle ambao Pandora aliwekwa na Mungu Zeus, ulikuwa na visa vinavyofanana kabisa na haya yanayotokea sasa duniani… watu kupotea, wanawake kuzalishwa viumbe vya ajabu na kadhalika… kwa hiyo baada ya kutafiti sana kinachoendelea duniani kwa sasa… najaribu kuoanisha na kilichotokea kwenye Anabelle halisi ambayo Pandora aliwekwa na Mungu Zeus… na ninachoamini ni kwamba hawa viumbe wanataka kuibadili dunia nzima kuwa kama mji wa dhahania wa Anabelle ambao Mungu Zeus alimuweka Pandora baada ya kumuumba…. kwa hiyo kujibu swali lako Salim, hivyo ndivyo namna gani najua yote haya.!"

Cindy akamaliza kujieleza. Wote walikuwa wako kimya wanamuangalia tu.

Giza bado lilikuwa kama ndio linazidi kuongezeka pale walipo. Bado kwenye madirisha ndani ya nyumba kulikuwa kuna mwanga mkali kana kwamba chemli au moto umewashwa ndani. Lakini ajabu ni kwamba vile vivuli vya watu madirishani havikuwepo tena.

Cindy alikuwa amemaliza kuikunja ile ngozi ya yule kiumbe waliyemuua. Alikuwa ameikunja ngozi kama nguo na kumpa kanali aishike. Kisha akachukua ile chupa kutoka kwa Magdalena.

"Tuna Masaa machache sana mbele yetu tunatakiwa tufike katikati ya mji.!" Cindy akaongea huku anaanza kutembea kuondoka pale waliposimama.

"Tunaenda kufanya nini katikati ya mji?" Akauliza Salim.

Cindy hakujibu papo hapo. Akanyamaza kama anatafakari jambo fulani hivi namna gani amjibu Salim.

"Umemuona huyo kiumbe tuliyemuua?" Cindy akamuuliza Salim huku wanatembea kuelekea mbele.

Walikuwa wanatembea taratibu sana kwa tahadhari kubwa huku Cindy ameshikilia chupa mkononi na kuiweka mbele kama ameshika tochi.

"Nimemuona!" Salim akajibu kwa kukereka na swali hili. Kwanini amuulize kama amemuona wakati walikuwa wote tukio likiwa linatokea.

"Kama angekuwa binadamu wa kawaida unamkadiria angekuwa na miaka mingapi?" Cindy akamuuliza.

"Kwenye 28 hadi 30 hivi" Salim akajibu.

"Unakumbuka nimewaambia kuwa hawa ni watoto waliozaliwa nchini Maldives, kabla haijageuzwa kuwa Anabelle.?"

"Ongea point yako Cindy, tunakumbuka yote hayo!" Salim akang'aka huku akijitahidi sauti yake isitoke kwa nguvu.

"Nadhani kuna jambo la msingi hamlioni hapa… mnakumbuka hawa watoto walizaliwa mwaka gani kule Maldives?" Cindy akawauliza kwa msisitizo mkubwa akiata waone kile anachokitaka.

"Mungu wangu!!!" Magdalena akadakia, "walizaliwa mwaka 2036, kwa hiyo mpaka sasa walitakiwa kuwa na miaka miwili tu!" Magdalena akaongea kwa mshangao na hofu.

"Miaka miwili???" Shafii ambaye alikuwa kimya muda wote akahamaki "haya madude yanaonekana mababa mazima mnasema yana miaka miwili??"

Ikabidi wenzake watoe kicheko cha chini chini baada ya shafii kuhamaki kuwa vile viumbe ni "mababa mazima"!

" kuna jambo la muhimu sana ambalo nataka mlifahamu kuhusu Anabelle!" Cindy akaongea serious baada ya vicheko kuisha.
"Muda ndani ya Anabelle haufuati kanuni kama muda nje kwenye ulimwengu!"

"Una maanisha nini?" Kanali akauliza.

"Nadhani anamaanisha muda ndani ya Anabelle unaenda kwa kasi zaidi tofauti na muda nje huko ulomwenguni.!" Salim akajibu akiwa serious pia.

"Uko sahihi kabisa" Cindy akaongea, "muda ndani ya Anabelle unaenda kasi zaidi tofauti na ulimwenguni… ndio maana unaona hawa viumbe wana miaka miwili pekee lakini wanaonekana ni watu wazima kabisa wa miaka 30!! Na hii ndio sababu kwanini mji ukishatwaliwa unaonekana umechakaa kana kwamba haujawahi kukaliwa na watu kwa karne kadhaa.. Yote hii ni athari ya muda... Unakuwa unaenda kasi zaidi ndani ya Anabelle tofauti na duniani.!"

Cindy aliongea huku amegeuka kuwatazama wenzake. Wote walikuwa wamesimama wanamuangalia.

"Kwa hiyo basi... Unataka kusema kwamba huu muda ambao tumekaa humu ambao nakadiria ni kama masaa mawili pekee inawezekana kabisa tumekuwa humu kwa muda zaidi ya huo?" Kanali akauliza.

"Kabisa… hilo sio swali… hiyo ndiyo hali halisi… sisi tunahisi timekuwa humu kwa muda mchache lakini labda mwasaa mawili… lakini uhalisia ni kwamba… muda humu upo kasi zaidi kwahiyo inawezekana pengine tuko humu kwa wiki kadhaa tayari.!" Cindy aliongea huku ametoa tabasamu la huzuni.

"Umesema kwamba ni muhimu tufahamu hili? Unaweza kuwa mahususi zaidi kutueleza kwanini tunapaswa kuzingatia tofauti ya kasi ya muda tukiwa humu ndani?" Salim akaukiza.

"Nadhani anamaanisha kuwa tutazeeka haraka!" Shafii akatoa jibu la kijinga tena.

Kutokana na msongo waliokuwa nao kutokana na taarifa hii hata vicheko havikuwatoka.

"Ni bora hata tungekuwa tunazeeka haraka pekee.. Lakini ubaya ni kwamba ubongo wetu unaweza kuchanganyikiwa katika kung'amua uhalisia wa muda kiasi kwamba unaweza kupata shinikizo na kitu kibaya zaidi kikatokea.!" Cindy akajibu huku anageuka na kuanza kutembea.

Na wenzake nao wakamfuata.

"Kitu kibaya?? Kama kipi?" Kanali akauliza.

Magdalena akadakia na kujibu.

"Kanali, nadhani wote tunafahamu kuwa muda ni tofauti, yaani interval baina ya matukio mawili… na ubongo wetu una uwezo wa kuhisi hii interval na pia hii inaathiri fiziolojia ya mwili na mfumo… kwa kuwa tumezaliwa kwenye Dunia ya kawaida ubongo wetu tayari umeweka namna ambayo unahisi interval hizi na kuoanisha na fiziolljia na mabadilikk ya mfumo wa mwili… kwahiyo tukiwa humu kwa kuwa muda unaenda kasi zaidi maana yake pia kutakuwa na mabadiliko ya kimwili ya kasi zaidi, mfano kuzeeka… lakini ubongo wetu haujawahi kuhisi interval za humu kwa kuwa hatunazaliwa humu… hii unaweza kusababisha ubongo kupata msongo na shinikizo kwa kutumia oksojeni nyingi zaidi na glucose nyingi zaidi ili kuhimili hali hii mpya ya intervals na mabadiliko ya fiziolojia… sasa hii ndio itatuletea balaaa… ubongo unaweza kufeli muda wowote.!"

Magdalena akaawaeleza wenzake kitaalamu kabisa na kwa umahiri wa hali ya juu. Cindy akaitikia kwa kutikisa kichwa kuashiria kukubali maelezo aliyoyatoa.



“kwa hiyo tunatakiwa tufanye tulichokuja kukifanya haraka sana.” Cindy akaongea huku anazidi kutembea kwa haraka wenzake wakimfuata.



“na haujatuambia mpaka sasa ni nini hasa tunatakiwa kukifanya humu?” Salim akauliza.



“kitu cha kwanza kabisa tunatakiwa kutafuta mlango wa kikundi cha cha watu wanaojiita The 46.!” Cindy akaongea kwa kifupi.



“ndio kina nani hao?” Salim akauliza kwa shauku.





INAENDELEA POST INAYOFUATA…
 
THE OTHER HALF



SEASON 1 - LEGEND OF ANABELLE


"…wazo! Yaani 'idea', ndio kirusi kibaya zaidi kuwahi kutokea tangu kuumbwa kwa ulimwengu. Ubongo unapopata wazo, na wazo hilo likichipua ndani yako kamwe huwezi kulitoa akilini. Wazo lolote baya au zuri likipata nafasi ya kuchipua kwenye ubongo, wazo hilo litakutesa na hautapata raha mpaka pale siku utakapolitimiliza.

Ukitaka kumjenga binadamu, mpe wazo… kisha lichochee hili wazo lichipue ndani yake. Wazo dogo kiasi cha punje ya mchanga Lina uwezo wa kukua na kubadili ulimwengu. Ni wazo dogo lililochipua ndilo lilisababisha mwanafizikia Newton kuvumbua nguvu za uvutano na hivyo kuwa mwanzo wa msingi wa sayansi ya fizikia. Ni wazo dogo lililochipua, ndilo lililo mfanya Steve Jobs kuleta mapinduzi katika ulimwengu wa teknohama.
Unahitaji wazo dogo tu, kisha unalichochea lichipue, kisha unaweza kabisa kuubadili ulimwengu.


Pia ukitaka kumuangamiza binadamu, mpandikizie wazo hasi. Kisha lichochee likue. Wazo hili likimea, linakuwa baya kama kirusi ambacho hawezi kulitoa akilini mwake. Huitaji bunduki wala upanga, kitu pekee unachohitaji kumuangamiza binadamu na ulimwengu, ni wazo dogo tu lililo hasi.!





EPISODE 8

Book Of Codes



MAHALI FULANI PA SIRI JIMBONI VIRGINIA, MAREKANI

Makamu wa Rais David Logan alikuwa anasikia sauti kwa mbali zikimuita kumuamsha. Alikuwa hajafahamu bado yuko wapi au alikuwa amepoteza fahamu kwa muda gani. Kitu pekee ambacho alikuwa anakikumbuka ulikuwa mlipuko baada ya kuingia kwenye gari alipotoka chuo Kikuu cha Stanford.

"Mr. Vice President! Mheshimiwa… mheshimiwa unanisikia??"

Logan alisikia kwa mbali hii sauti inamuita na kumuuliza kwa kurudia rudia. Pia aligundua kuwa mtu huyu alikuwa ameshika kijitochi kidogo cha kidaktari mkononi mwake anamfunua macho na kumuangalia kwa kummulika na tochi.

"Mr. Vice President… mheshimiwa? Unanisikia mheshimiwa?" Ile sauti ikaendelea kumuita.

"Niko wapi hapa?" Makamu wa Rais David Logan akajibu kwa sauti ya chini huku akiugulia maumivu aliyokuwa anayasikia mgongoni.

Kitu pekee ambacho alikuwa anakikumbuka ulikuwa ni mlipuko mkubwa baada ya kupanda kwenye gari na msafara kuanza kuondoka. Baada ya hapo alikuwa hakumbuki tena ni nini kilitokea.

"Niko wapi hapa?" Logan akauliza tena.

"Mr. Vice President upo site namba SQ1204 Virginia!" Yule mtu aliyekuwa anamuamsha akaongea.

"Kuna maana gani kunileta hapa?" Logan akajibu huku anaamka kutoka kwenye kitanda alichokuwa amelazwa.

Site namba SQ1204 ni moja kati ya maeneo ya siri 41 ambayo Rais wa Marekani anaweza kufichwa endapo kuna tishio kubwa juu ya maisha yake.
Kitendo cha yeye kuletwa mahali hapa ilimaanisha kwamba kulikuwa na hali ya hatari hasa juu ya maisha ya Makamu wa Rais.

"Mr. Vice President… tumekuleta hapa kwa kuwa nadhani umefahamu shambulio lililotokea wakati tunatoka Chuo Kikuu cha Stanford. Kutokana na udharura wa hali iliyopo hatiwezi kukurudisha Ikulu sasa hivi… tunaamini sehemu salama zaidi ya wewe kuwepo ni hapa!" Yule mtu ambaye baada ya Logan kuinuka akagundua kuwa alikuwa ni afisa wa Secret Service.

Alikuwa amelazwa kwenye chumba fulani hivi chenye milango ya vioo na chumba kilikuwa na muonekano kama chumba cha hospitali.
Alipoangalia ng'ambo ya chumba hiki, kulikuwa na chumba kingine ambacho kinafanana kabisa na hiki na kwenye chumba hicho kingine alikuwa amelazwa Mzee Caleb.

Logan akashituka kidogo na kuanza kusimama huku anavaa vizuri koti lake la suti.

"Mheshimiwa nadhani ungendelea kupumzika kidogo!" Yule ofisa wa Secret Service akaongea huku anajaribu kumlaza tena Logan kitandani.

"Kijana… nashukuru kwa kujali, lakini niko sawa na nina nchi inayohitaji niiongoze… kwahiyo tafadhali sana siwezi kulala" Logan akaongea kwa kujiamini huku anavaa vyema koti lake la suti na kuanza kutoka kwenye kile chumba.

Akatoka huku yule afisa wa Secret Service pamoja na wengine waliokuwa wamesimama mlangoni nao wakimfuata.

"Wengine wako wapi? Rupert na Naomi?" Logan akauliza.

"Wako salama mheshimiwa… wako chumba cha kupumzika masuala wanaongea na maafisa wengine wa usalama.!" Afisa wa Secret service akajibu.

"Nahitaji kuungana nao!" Logan akaamuru.

Maafisa wa Secret Service wakamuongoza moja kwa moja mpaka kwenye chumba fulani kama sebule hivi ambapo aliwakuta Mwanamama Naomi Cole mshauri wa Rais kuhusi Usalama na James Ruppert Mkurugenzi wa CIA wakiwa wamezungukwa na maafisa wengine wa usalama wakiwa wanajadili suala fulani hivi.

Baada ya Makamu wa Rais Logan Kuingia wote wakasimama na baada ya yeye kuketi wote nao wakaketi.

Naomi na Ruppert walikuwa pamoja na Logan kipindi shambulio linatokea Stanford lakini walikuwa kwenye gari tofauti.
Yaani Logan na Naomi walipanda gari moja na Ruppert na Mzee Caleb walipanda gari lingine kwenye msafara.

Kwa hiyo kitendo cha Logan na Mzee Caleb kuumia mpaka kupoteza fahamu hii ilimaanisha kuwa magari yote hayo mawili kwenye msafara yalishambuliwa. Lakini ajabu ni kwamba, Naomi na Ruppert hawakuwa na majeraha yoyote na walionekana wako salama salimini.

"Nini kinaendelea?" Logan akauliza kwa uso wa kuchanganyikiwa mara baada ya kuketi.

"Tumeshambuliwa mkuu.. Mara tu baada ya kutoka Stanford!" Ruppert akaanza kueleza.

"Mmefahamu kwa nini tumeshambuliwa au ni nani ametekeleza hili shambulizi?"

"Hatujafahamu hasa ni nani amefanya hili shambulizi lakini dalili inaonyesha kwamba waliofanya shambulizi walikuwa wanamlenga Mzee Caleb!" Naomi akaongezea.

"Kwa nini mnaamini kuwa alilengwa Mzee Caleb?" Logan akauliza kwa mshituko.

"Mr. Vice President… taarifa tulizozipata mpaka sasa kutoka FBI inaonyesha kwamba kombora lilirushwa kutoka ghorofa ya kirani na msafara ulipokuwa na Kombora hili lililengwa kwenda kwenye gari ambalo nilipanda mimi Mzee Caleb… gari ambayo mlipanda wewe na Naomi lilipinduka kutokana na nguvu ya mlipuko tu lakini silo ambalo lililengwa.!" Ruppert akaeleza.

"Na kwa nini uhisi walimlenga Caleb na sio wewe Mkurugenzi wa CIA?" Logan akauliza.

"Mheshimiwa ni kwasababu baada ya mlipuko kutokea na mambo kuvurugika kulitokea jaribio la watu wasiojulikana kumteka Mzee Caleb… Bahati nzuri maafisa wa Secret Service waliwahi kuwadhibiti na kumuua mmoja na mwingine alitoroka japo alijeruhiwa.!" Ruppert akafafanua zaidi.

"Na maiti ya huyo mmoja aliyeuwawa tuko nayo hapo nadhani ni vyema ukiiona!" Naomi akaongezea.

Baada ya Naomi kusema hayo wote wakainuka na kuelekea upande ule ambao kulikuwa na vile vyumba vya milango ya vioo vyenye mandhari ya hospitali.
Hapa kulikuwa na vyumba vitano, chumba kimoja ndicho kile ambacho alilazwa Makamu wa Rais Logan, chumba kinachofuata alikuwa amelazwa Mzee Caleb na vyumba viwili vilivyofuatia vilikuwa tupu na chumba cha mwisho cha tano ndicho ulilazwa mwili wa huyo mtu aliyeuwawa na Secret Service.

Mwana usalama mmoja akafungua mlango baada ya kufika nje ya mlango, kisha wakaingia ndani ya chumba.

Juu ya kitanda pale chumbani ulikuwa umelazwa mwili wa mwanaume mwenye kuonekana kama mwenye miaka kati kati ya thelathini hivi.
Mwili wake ulikuwa umejengeka hasa kimazoezi na alionekana alikuwa mkakamavu hasa. Alikuwa na majeraha mawili ya risasi kifuani.

"Mr. Vice President kuna kitu nataka ukione!" Ruppert akaongea huku anazunguka upande wa pili wa ile maiti.

Ruppert akanyoosha mkono wake na kuipindua shingo ya yule maiti ili kuonyesha sehemu ya nyuma ya shingo yake.

Alikuwa na tatoo kubwa imeandikwa,

'SANCTA CEDES'



"Ni nini hii?" Makamu wa Rais David Logan akauliza.

"Hatujajua hasa ni nani huyu mtu na mwenzake aliyekimbia. Lakini tunachokifahamu ni kwamba lengo lao la kushambulia msafara ilikuwa ni ili waweze kumteka Mzee Caleb.!" Ruppert akajibu.

Kabala hawajaongea zaidi, kupitia ile milango ya vioo wakamuona kuna afisa wa Secret Service alikuwa anakuja mbio kuja kwenye chumba walichopo.

"Mzee Caleb ameamka!" Yule afisa aliyekuwa anakuja huku anakimbia aliongea baada ya kufika kwenye chumba walichopo Logan na Wenzake.

Wote kwa pamoja wakatoka nje ya chumba kwa haraka kuelekea kile chumba cha pili ambacho alikuwa amelazwa Mzee Caleb.

Walipoingia walikuta kuna daktari ambaye pia ni afisa usalama alikuwa anampa maelezo Mzee Caleb Kuhusu nini kimetokea na wako mahali gani hapo.

"Unajisikiaje Mzee?" Logan akamsalimu mara tu daktari aliposogea pembeni.

"Kizungu zungu tu bado kwa mbali!" Mzee Caleb akaongea huku akakaa vizuri kitandani kwa kuninginiza miguu.

"Daktari amekueleza kama shambulio lilikuwa linakulenga wewe?" Ruppert akamuuliza.

"Mimi?" Mzee Caleb akaongea kwa mshtuko mkubwa hasa.

"Ndio, wewe Mzee! Shambulio zima lilipangwa ili waweze kukudhuru au kukuteka wewe!" Ruppert akaongezea.

"Ni akina nani hao?" Mzee Caleb akauliza.

"Tumefanikiwa kumuua mmoja wao, mwingine au wengine maana hatujui wako wangapi walifanikiwa kukimbia!" Ruppert akaeleza tena.

Mzee Caleb hakusema chochote akabaki amejiinamia tu kama kuna kitu fulani anatafakari.

"Unaweza kufahamu kwa nini walikulenga wewe Mzee?" Logan akauliza.

"Hapana… sijui hata hao watu ni akina nani!" Mzee Caleb akajibu huku bado amejiinamia.

"Mmoja tuliyemuua shingoni ana tatoo imeandikwa 'Sancta Sedes'! Unaweza kujua lolote kuhusu hilo?" Naomi ambaye alikuwa amekaa kimya muda wote huu akaongea hatimaye.

Mzee Caleb akainua kichwa ghafla kwa haraka baada ya Naomi kutaja 'Sancta Cedes'.

"Umesema tatoo imeandikwaje?" Mzee Caleb akauliza tena kwa mshangao mkubwa zaidi.

"Sancta Cedes" Naomi akajibu.

"Mungu wangu!" Mzee Caleb akajiinamia kwa woga.

Wote wakatazamana kwa pamoja kisha wakamuangalia Mzee Caleb.

"Nini Mzee! Unafahamu nini kuhusu Sancta Cedes?" Logan akamuuliza.

"The Holy Chair" Mzee Caleb akajibu kwa sauti ya chini huku bado amejiinamia.

"Umesemaje Mzee?" Ruppert akauliza kana kwamba hakusikia.

"Sancta Cedes! Ni The Holy Chair!" Akaongea huku anainua uso.

"The holy chair?? Una maana gani?" Makamu wa Rais Logan akauliza kwa mshangao.

"Vatican!" Naomi akadakia na kujibu kwa kifupi.

"Ati nini?" Logan akauliza kwa mshangao mkubwa.

"Makazi ya Papa wa Kanisa au kwa maneno mengine mamlaka aliyonayo, yaani Vatican… ndiye pia inaitwa 'The Holy Chair'." Naomi akafafanua zaidi.

"Vatican??" Logan akashikwa na bumbuwazi alishindwa afikiri vipi kitafsiri maana ya hii anachokisikia au aoanishe vipi na matukio yanayoendelea duniani.
"Vatican wanahusika vipi na hawa watekaji?" Hatimaye Makamu wa Rais akajikuta anauliza.

"Unauliza swali ambalo sio sahihi Mr. Vice President! Swali sio Vatican wanahusika vipi na hawa watu… swali la msingi zaidi ni namna gani hawa wapiganaji wa kuzimu wameweza kurudi juu ya uso wa dunia?" Mzee Caleb akaongea huku anainuka kutoka kitandani.

"Una maana gani kuwa wapiganaji wa kuzimu?" Safari hii ni Ruppert akauliza swali.

"Kikundi cha Sancta Cedes, mara ya mwisho kuwepo duniani ilikuwa ni mwaka 1490… baada ya hapo wapiganaji wake wote waliteketezwa kwa amri ya Papa kutoka Vatican ingawa ni Vatican hiyo hiyo ililiunda karibia miaka 150 nyuma kabla ya siku hii UA kukiteketeza"

Mzee Caleb aliongea huku anavaa koti kana kwamba anataka kuondoka.

"Wanataka nini hasa?" Naomi akamuuliza Mzee Caleb.

"Sifahamu… hata mimi niko gizani kama wewe lakini nina kila sababu ya kuamini kuna mahusiano fulani na matukio ya miji kutwaliwa na kugeuzwa Anabelle!" Mzee Caleb akajibu.

"Tunafanyaje kukabiliana nao kama wako wengi wengine?" Naomi akauliza tena.

"Sina jibu la hilo pia! Lakini nadhani naweza kujua tuanzie wapi!"

"Wapi?"

"Book of Codes" Mzee Caleb akajibu kwa ufupi.

"Ni kitu gani?" Logan akadakia na kuuliza swali.

"Nahitaji kwenda Maryland sasa hivi" Mzee Caleb hakujibu swali badala yake akatoa amri.

"Mzee huwezi kuondoka hapa… tuko eneo la siri ambalo linatumika kumuhifadhi Rais na Makamu wa Rais wakati wa hatari kubwa dhidi ya maisha yake… hatuwezi kutoka humu mpaka tupewe taarifa ya tathimini huko nje kwamba hali mi shwari!" Ruppert akaeleza.

"Sio lazima Mr. Vice President au nyinyi mfuatane nami… naweza kwenda mwenyewe.!" Mzee Caleb akaongea huku anaaza kuondoka.

"Huwezi kwenda mwenyewe Mzee muda mchache uliopita wamejaribu kukuteka! Hauko salama tena huko nje" Naomi akamuonya Mzee Caleb.

"Mpeni ulinzi!" Logan akaongea kwa kukereka haswa.

"Mr. Vice President, hawa watu waliotuvamia ni wahuni… naomba ruhusa yako nimpe ulonzi wa 'wahuni' Mzee Caleb ili wakakabiline wahuni kwa wahuni kama wakijaribu tena kumteka Caleb." Ruppert akaongea kwa hasira akimuangalia Makamu wa Rais Logan.

"OK! Nimeruhusu!" Logan akajibu kwa kifupi huku akienda kukaa kwenye kiti pembeni ya kitanda mule ndani.

Ruppert akatoa simu na kubofya bofya namba na kisha akapiga simu makao makuu ya CIA, Langley Idara maalumu ya SAD (Special Activities Division).

"Namuomba Ethan na kikosi chake mara moja!" Ruppert akaongea mara baada ya simu kupokelewa.



ITAENDELEA IJUMAA..
 
EPISODE 7 & 8


Nifah Divine... glory to yhwh BansenBurner Alisen Papushikashi Magazine Fire miss chagga SANCTUS ANACLETUS mngony Excel Mussolin5 Jimena Inferiority Complex gwijimimi wambura marwa Hoshea shareef conscious wambeke The Boss Deejay nasmile gkileo Juma chief Mangi flani hivi Ngongo makaveli10 KENZY kadada wa pili Root aretasludovick jonnie_vincy Clkey KAFA.cOm mbewe makedonia Afande Nyati peterchoka Leonard Robert Nchi Kavu STUNTER Chrizo jully Van persie Khalidoun Tetramelyz punje haradari Mazigazi @Alybaba babu na mjukuu platozoom jimmyfoxxgongo Nicodemas Tambo Mwikozi Ls man Heaven Sent sifongo Infantry Soldier haa mym 20acres MTS MarkHilary compos Tembo2 Erick the future nancy1983 Bulah binsaad Fazzaly the wolf everhurt Melvine Mgibeon kijana wa leo samsun Coolant Jagood pacesetter apologize payton George Betram kisengeli Kiranga Jiwe Linaloishi Madame B jay john Guasa Amboni Dinazarde Analyse Diva Beyonce snowhite Mmanu Expected Value onechromosome Missy rose Innocenthezron Immortal_MH Ficus sunola Robot la Matope mamaafacebook II JEKI likikima Compact scorpio me G'taxi YNWA adna yuzo ntamaholo Otorong'ong'o naan ngik-kundie kandukamo1 AFRICA101 mwalidebe Kobe Blaki Womani kalendi savius The Great Emanuel r2ga Ntaluke.N. Transcend Msemachochote Mchumiajuone mwampepec MTOTO WA KUKU Fukara proto cute kawombe zinginary MLALUKO JR Vupu barafu BlackPanther Ntuzu Matola impongo ntamaholo Mkoroshokigoli Deadbody KING easy mahoza Msolo kkenzki deborah1 KIDUDU buffalo44 winlicious riziki Allys MUHUNZI Moses2015 nacktary Liuumi dochivele Renzo @barbers hmjamii mbere TATIANA famicho LUCKDUBE mwanadome Straton memphis ghazar Graph Theory Honey Faith Shunie Slave ddcmanesto zinginary pacesetter Nkanaga KOMUGISHA mikatabafeki johnsonmgaya lee empire wigo MJINI CHAI Asprin mtzmweusi Erasto kalinga Chrizo kichakaa man LULU bike FORTALEZA poleni shibumi ZE DONE umande Edger Sr sir joshua sammoo Roram Password Bavaria hambiliki mwanangu Asili100 Evarist Massawe nice1 Jumong S Rogie 1babake nasreen uberito baest dustless Kilemachocho Tumosa mtembea kwa miguu Debbs Joe scorpnose musacha shibumi seeker of knowledge Simuchi Veni Vidi Vici TUJITEGEMEE abuu garcia Hon Nkundwe Festo Festo marion09 mike2k The dream bro kay vandelintz kirikou1 POINT LOAD lusaka city Dirham Rodcones bato MANCNOO multiphill90 GEORGE Dalali mwanamalundi90 MwaFreeca Roram Ta-kibombo troublemaker mambo KOMUGISHA calabocatz Papaa Azonto Msemachochote Mdomo bakuli tizo1 option dikembe iL Buono fakalava ABDUL KAREEM @Gobe Justine Marack Goodluck Mchika MR UNINFORMED darcity nkasoukumu nG'aMBu thatonegAl kabanga MPARE KIBOGOYO Edward Sambai Rassa mnonje srinavas last king of uscoch proto cute Kennedy krava Rais2020 kbosho Mzee wa BsN sam2000 fuma 999 Bableee dawa yenu The Certified DON SINYORI mij adden
bwii ONTARIO Kobe The Vein Mondray jaxonjaxon successor mzee wa liver sawariya Sitaki ukuda Domhome Mpatanishi MKANDAHARI mtugani wa wapi huyo wealthier cluecell Toyota escudo mgumu2 troublemaker Linamo shedede kamtu33 SteveMollel ngushi Donald stewart Mshuza2 Glycel mnonje Ochuanilove SingleFather Santi DEOD 360 ngushi anatory antony ukhuty chris van chicha
 
Daah! Nikama vile nangalia movie yenye kuogofya.. Bado unanipa tafakari kichwani ni wazo gani lilikuingia kichwani mpaka ukaja na story kama hii..!? Naweza sema wewe nikati ya watunzi bora kabisa wazama hizi niliye wahi kuona kazi zake ongera sana mkuu @The_bold ila tafadhali mkuu niongeze kwenye list ya unao watag
 
Daah! Nikama vile nangalia movie yenye kuogofya.. Bado unanipa tafakari kichwani ni wazo gani lilikuingia kichwani mpaka ukaja na story kama hii..!? Naweza sema wewe nikati ya watunzi bora kabisa wazama hizi niliye wahi kuona kazi zake ongera sana mkuu @Thebold ila tafadhali mkuu niongeze kwenye list ya unao watag
 
Daah! Nikama vile nangalia movie yenye kuogofya.. Bado unanipa tafakari kichwani ni wazo gani lilikuingia kichwani mpaka ukaja na story kama hii..!? Naweza sema wewe nikati ya watunzi bora kabisa wazama hizi niliye wahi kuona kazi zake ongera sana mkuu @The_bold ila tafadhali mkuu niongeze kwenye list ya unao watag
Shukrani sana Mkuu kwa pongezi..
Ubarikiwe!

Nimekuongeza kwenye taglist tayari..
 
Back
Top Bottom