Ule ugonjwa wa kupukutika meno yote mdomoni unautwaje? Nasikia ati huyu babu hahitaji tena mswaki, ya kwake huwa anayasafisha "in vitro" (wameniambia madaktari kuwa hii inamaanisha "nje ya mwili") kwenye beseni lenye JIK. Ingawa nakusudia sentensi iliyotangulia iwe utani, ung'ang'anizi wa babu Kingunge kwenye siasa za bongo ni mfano mbaya sana na ni jambo la kukemewa kabisa, hasa ushirika wake na mafisadi siku hizi.