Mbowe Aisahihisha Historia ya Lowasa katika Mazishi huko Monduli

Umkonto

JF-Expert Member
Dec 27, 2018
2,102
3,615
Kwenu wataalamu wa mambo ya siasa, je ilikuwa sahihi kamati ya mazishi ambayo inaongozwa na PM kuandaa historia ya hayati Lowasa bila kuhusisha kuhamia upinzani?

Mama alipokuja kuhutubia yeye binafsi hakutaja neno Chadema ila alihusisha historia ya Lowasa na upinzani kwa namna fulani ambapo alisema "Lowasa alihamia upande mwingine".

Pia, mama alikuwa anasoma hotuba yake. Sasa sijui alibadilisha upepo baada ya hotuba ya Mboye au alikuwa amedhamiria kuhusisha historia ya Lowasa kuhamia upinzani, anajua yeye!.

HABARI KAMILI

Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema hauwezi kuiandika historia ya waziri mkuu mstaafu, Edward Lowasa, na ukaliacha neno CHADEMA.

Ameyasema hayo akitoa salamu baada ya maziko ya Lowasa yaliyofanyika leo tarehe 17-02-2024, kijijini Ngarashi wilayani Monduli mkoani Arusha.

"Rais nashindwa kujua niseme nini kuhusu Lowasa lakini niombe kwa sababu ya rekodi niweke kumbukumbu sahihi"

"Huwezi kuiandika historia ya Lowasa ukaliacha neno CHADEMA. Huwezi ni kujidanganya tu na kujaribu kuiua historia ambayo huwezi kuiua" Amesema Mboye.

Mbowe amesema ameisikiliza na kusoma historia ya Lowasa kama ilivyowasilishwa na kuongeza;

"Binafsi ni mtu mkweli na nimesikitika kwa sababu amefanya mambo makubwa ndani ya serikali, ndani ya CCM na vyama vya upinzani na katika taifa letu na taifa hili ni letu sote.

"Unawezaje kuandika historia ya Lowasa ukasahau utumishi wake wa miaka minne kama mjumbe wa kamati kuu ya CHADEMA, mgombe wa urais wa mwaka 2015 ambaye alijenga demokrasia kwa viwango ambavyo haijawahi kufikiwa na mgombea yoyote wa upinzani katika taifa letu hili" Amesema Mboye.

"Wenzangu mtatambua Lowasa alianza safari ya matumaini ndani ya CCM baada ya hapo mimi siyazungumzi, na baadaye akahamia safari ya mabadiliko ndani ya CHADEMA. Huyu alileta kasi ya mabadiliko ya demokrasia ndani ya ncgi yetu" Amesema Mbowe.

Mbowe amesema pia "Lowasa alilifanya bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa na wabunge 115 kutoka vyama vinne vya upinzani. Hili linapaswa kuzungumzwa kwa sababu ni hatua ya ujenzi wa demokrasia katika katika taifa letu"

"Huyu kiongozi aliongoza uchaguzi na kuwezesha vyama vya upinzani kupata madiwani 2000 karibu nusu ya madiwani wa nchi"

"Vyama vingine tofauti na CCM vikaongoza jiji la Dar es Salaam, Arusha, Tanga, Moshi, Mtwara, Iringa na Mbeya. Hampaswi kupuuza historia hii viongozi wangu. Tunatakiwa wakati wote tumuenzi Lowasa kwa sababu ni katika ujenzi wa demokrasia na ujenzi wa taifa letu zote" Amesema.

"Lowasa ni muathirika wa mifuno yetu ya uchaguzi lakini alikuwa mgombea wa upinzani kupata kura zaidi ya milioni sita. Halikuwa jambo dogo, ni kwa sababu ya karama yake" Ameongeza Mboye.

Chanzo: Mwananchi
 
Ndiyo, alipewa nafasi ya kuongea ndiyo akaweka kumbukumbu sawa za historia ya marehemu!
 
Ahaa! Kumbe tusipende kuamini sana historia kwa sababu kuna kupindishwa wakati mwingine!
Mfano baba Yako Mzazi kafa Kwa kupigwa rungu baada ya kufumaniwa au Nduguyo kafa Kwa Kwa Ukimwi kwenye historia ya Marehemu utaandika hivyo?

Mfano alikufa Kwa shinikizo la damu ndugu wakaibuka wakasema shinikizo la damu alilipata baada ya kuwekewa sumu na Chadema utajibu Nini? Historia ya Marehemu ni pamoja na Historia ya ugonjwa wake

Lowasa akiwa CCM alikuwa mzima wa Afya alipoenda Chadema akiwa kule Hali yake akiwa kule ndipo ilianza kuharibika akiwa hata akiwa jukwaani anapoteza kumbukumbu hawezi hata simamia dakika Tano kuhutubia

Ndugu kutoweka historia akiwa kule kule Chadema msiwaone wajinga nyie

Lowasa Hali mbaya kiafya ilimuanza akiwa Chadema hilo mbona Mbowe hakusema.Historia ya Lowasa ni pamoja na Historia ya ugonjwa wake
 
" Pilato akaandika Yesu Mnazeleti mfalme wa Wayahudi, wakamuuliza Kwa nini umeandika hivyo? Pilato akajibu nilichoandika nimekwishaandika"

Tafakari ya hayo maneno ni kwamba mtu mkubwa anaposema na kutenda historia umeandika na kutenda alichoandika hivyo basi Alichosema Rais Samia ndio kimeandikwa katika historia ya Lowassa na hiyo ndio historia itakayokuja kusomwa vizazi vyote
 
Yale yale kuhusu harakati za kuupata uhuru wetu, history imepindishwa kwa makusudi ili tuone was a man alone aliyeleta uhuru wa Tanganyika, mpaka kukatungwa kitabu eti kama mtu yule asingeacha kazi ya ualimu, Tanganyika ingekua wapi!,nachelewa kuingia kwenye vitindi vyangu vya ulanzi, naanza kuwa na mori, nisije kula ban kwa mara ya kwanza
 
Mfano baba Yako Mzazi kafa Kwa kupigwa rungu baada ya kufumaniwa au Nduguyo kafa Kwa Kwa Ukimwi kwenye historia ya Marehemu utaandika hivyo?

Mfano alikufa Kwa shinikizo la damu ndugu wakaibuka wakasema shinikizo la damu alilipata baada ya kuwekewa sumu na Chadema utajibu Nini? Historia ya Marehemu ni pamoja na Historia ya ugonjwa wake

Lowasa akiwa CCM alikuwa mzima wa Afya alipoenda Chadema akiwa kule Hali yake akiwa kule ndipo ilianza kuharibika akiwa hata akiwa jukwaani anapoteza kumbukumbu hawezi hata simamia dakika Tano kuhutubia

Ndugu kutoweka historia akiwa kule kule Chadema msiwaone wajinga nyie

Lowasa Hali mbaya kiafya ilimuanza akiwa Chadema hilo mbona Mbowe hakusema.Historia ya Lowasa ni pamoja na Historia ya ugonjwa wake
kuwa mkweli acha upotoshaji. Lowassa hali yake kiafya iliyumba zaidi baada ya kufanyiwa figisu na chama chake pendwa. Mzee wa watu akabadilika, ameenda chadema akigombea urais huku afya yake ikiwa si nzuri
 
Sasa hiyo ndiyo historia gani ya kupindishwa kwa makusudi. Huko ni kuficha aibu walizomfanyia mzee wa watu
 
kuwa mkweli acha upotoshaji. Lowassa hali yake kiafya iliyumba zaidi baada ya kufanyiwa figisu na chama chake pendwa. Mzee wa watu akabadilika, ameenda chadema akigombea urais huku afya yake ikiwa si nzuri
Sio kweli mbona Hadi mikutano ya Mwanzo akiwa Chadema mbona alikuwa na nguvu zake imara hasa

Mbowe alichofanya pale sio sahihi ashukuru walimuweka Mwisho msiba ungechafuka sababu ingekuwa sehemu ya majibizano ya nani hasa kahusika na Afya mbaya ya Lowasa ilianzia Chadema Wala sio Siri

Kule ndiko tatizo la Afya lilianza kuonekana
 
Sio kweli mbona Hadi mikutano ya Mwanzo akiwa Chadema mbona alikuwa na nguvu zake imara hasa

Mbowe alichofanya pale sio sahihi ashukuru walimuweka Mwisho msiba ungechafuka sababu ingekuwa sehemu ya majibizano ya nani hasa kahusika na Afya mbaya ya Lowasa ilianzia Chadema Wala sio Siri

Kule ndiko tatizo la Afya lilianza kuonekana
acha ubishi, Lowassa alienda chadema tayari yuko hoi amedhoofika, ongea yake tu ilikuwa ya shida si kama alipokuwa anatangaza nia kutaka ateuliwe na chama chake pale arusha. Mzee wa watu alipokatwa alinyong'onyea afya yake ikaanza kudorora. Alianza kufanya kampeni zake akiwa chadema yuko hoi hawezi kuongea kwa nguvu kiasi cha wapiga kura wake kutofurahia kampeni zake kwa kushindwa kuongea kwa nguvu
 
acha ubishi, Lowassa alienda chadema tayari yuko hoi amedhoofika, ongea yake tu ilikuwa ya shida si kama alipokuwa anatangaza nia kutaka ateuliwe na chama chake pale arusha. Mzee wa watu alipokatwa alinyong'onyea afya yake ikaanza kudorora. Alianza kufanya kampeni zake akiwa chadema yuko hoi hawezi kuongea kwa nguvu kiasi cha wapiga kura wake kutofurahia kampeni zake kwa kushindwa kuongea kwa nguvu
Kifupi Mbowe Pale hapakuwa mahali pake pa kuongea yale
Hata aliyemkaribisha kuongea yule MC alimkaribisha kuwa Sasa tunamkaribusha Mbowe ndugu wa karibu aongee

Ule ukaribisho tu kwa mtu mwenye akili timamu alitakiwa kutiririka eneo Hilo kuwa Mimi kama ndugu wa Karibu nilimfahamu Lowasa hivi na hivi yeye na familia yetu tuko pamoja hata mwanangu alipoumwa mama Lowasa alisaidia matibabu nk

Lakini ule unati naona ulimlevya.Msibani mtu ukipewa kuongea akili inatakiwa kutulia

Yule MC yuko vizuri ni kama alimpa heading kuwa ongelea upande huu wa kama ndugu wa Karibu akashindwa kuzingatia alivyo wa ajabu

MC yuko fit sana na alimwambia ajikite kule .Asivyo na hekima akaenda mazima upande mwingine .

Misibani sikiliza Vizuri MC yeye maskio sijui aliweka wapi
 
Historia ya Marehemu ndugu ndio Huwa na maamuzi ya mwisho isomekeje sio awaye yeyote
Nimetonywa kuwa state burial ni tofauti kidogo na family burial, kwenye state burial kunafanywa screening ya maana kabla ya historia ya marehemu kusomwa hadharani, state inaweza kuamua nini kisomwe na kipi kiachwe.
 
Yule ni mwenyekiti wa chadema taifa, sasa kama aliona historia imepindiswa na amepewa nafasi adimu why asiitumie vema on the spot kurekebisha mambo? Hata kama asingepewa nafasi tayari wachunguzi wa mambo walisha sense kuna kupindishwa kwa historia
 
Nimetonywa kuwa state burial ni tofauti kidogo na family burial, kwenye state burial kunafanywa screening ya maana kabla ya historia ya marehemu kusomwa hadharani, state inaweza kuamua nini kisomwe na kipi kiachwe.
Familia Huwa na nguvu sana pia
Huwa hawataki mitafaruku kwenye state burial ndio maana hata mkuu wa msiba waziri mkuu alisema yote yaliyofanyika yalihusisha wote familia,Serikali , Viongozi wa dini na kimila ambao Lowasa alikuwa ndio bosi wao kama Laigwani

Ina maana hata hiyo Risala ya historia ilikubaliwa na makundi yote hayo manne sababu iligusa maisha yake ya kifamilia,kidini, kiserikali na kimila
 
Yule ni mwenyekiti wa chadema taifa, sasa kama aliona historia imepindiswa na amepewa nafasi adimu why asiitumie vema on the spot kurekebisha mambo? Hata kama asingepewa nafasi tayari wachunguzi wa mambo walisha sense kuna kupindishwa kwa historia
Familia ingeona umuhimu wake ingemtafuta Mbowe kuwa weka paragraph Yako hapa ya huko Chadema alikokuwa walimpuuza
Pale analaumu nani alaumu familia wenye msiba wao kama Raisi Samia alivyosema huu ni msiba mkubwa sana Kwa familia japo wote ni wetu lakini Kwa familia ndio mkubwa mno
 
Mfano baba Yako Mzazi kafa Kwa kupigwa rungu baada ya kufumaniwa au Nduguyo kafa Kwa Kwa Ukimwi kwenye historia ya Marehemu utaandika hivyo?

Mfano alikufa Kwa shinikizo la damu ndugu wakaibuka wakasema shinikizo la damu alilipata baada ya kuwekewa sumu na Chadema utajibu Nini? Historia ya Marehemu ni pamoja na Historia ya ugonjwa wake

Lowasa akiwa CCM alikuwa mzima wa Afya alipoenda Chadema akiwa kule Hali yake akiwa kule ndipo ilianza kuharibika akiwa hata akiwa jukwaani anapoteza kumbukumbu hawezi hata simamia dakika Tano kuhutubia

Ndugu kutoweka historia akiwa kule kule Chadema msiwaone wajinga nyie

Lowasa Hali mbaya kiafya ilimuanza akiwa Chadema hilo mbona Mbowe hakusema.Historia ya Lowasa ni pamoja na Historia ya ugonjwa wake

Na sio lazima kusoma history ya marehem

Inaweza isisomwe pia
 
Back
Top Bottom