The Legacy of Kingunge Ngombare Mwiru

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Najiuliza hivi historia ya Tanzania itaandika nini kuhusu mchango wa Kingunge katika Taifa letu ukiondoa jina hilo la "Kingunge" ambalo limebakia kuwa alama ya mtu ambaye ni kigogo na kiongozi mkubwa? Ni nini hasa mchango wa Kingunge katika siasa, uchumi, na maisha ya Tanzania? Ni kitu gani tunaweza kusema kuwa kisingefanyika kama Kingunge asingekuwepo? Je historia itaandika nini juu ya Kingunge au atabakia na alama ya nyota tu katika footnote ya historia?
 
Alikuwa Mbepari wa ukomunisti wa kijamaa, basically opportunistic glutton aliyewashikia watu akili.
 
alikuwa mhubiri mzuri, aliyekuwa anahubiri na kusisitiza watu wanywe maji, wakati yeye akinywa divai
 
Alisimama kidete kuhakikisha JK anakuwa rahisi, what a hero????????????
 
Kiongozi anayeshikilia nafasi ya juu kabisa kwa unafiki tangu enzi ya mwalimu; hakuna msimamo wowote anayaliowahi kuisimamia. Yeye kwenye kila jambo anaangalia upepo unakoendelea na yeye huko ndiko aendako.

Nathani japo kwa Jijini Dar "Kinje" atakuwa na legacy yake kuliko huyu mzee. Kwani legacy lazima iwe positive..!!!
 
hakuna alichofanya zaidi ya kuandika volumes ya vitu visivyotelezeka, hakuwa mjamaa au bapari, bali aliyechanganyikiwa, hadi akamwasi Mungu, akajiweka mahali pa juu sana, kiasi ambacho akadiriki kupuuza misahafu mikuu iliyopo kwa zaidi ya miaka milioni moja.

hana mchango wowote katika taifa hili ambao ni chanya

mchango mkuu aliofanya ni kulea mafisadi na kuwalinda kwa nguvu zote, pia kuiondoa ccm kwen ye dira aliyonayo julius
 
Ukiona watu hawawezi kueleza achievements zake mara moja, ujue kuna walakini.

Hata mimi kichwani, hakuna linalonijia la maana kuhusu huyu mzee.


Sana sana ni mtu anayeamini na kutuhubiria juu ya party(political) supremacy (chama kushika hatamu).
 
..Kingunge aliwahi ku-serve kama mkuu wa mkoa kwa miaka kadhaa.

..kila mkoa aliofanya kazi alianzisha vijiji vya ujamaa vya mfano. vijiji hivyo vilikuwa hata vikivuma sana ktk kipindi cha mbiu ya mikoa.

..nyakati zile za Ujamaa huyu Mzee alihubiri na kuutekeleza ujamaa kwa VITENDO.

..Mwalimu alimtumia sana Kingunge kwa ushauri wa kisiasa na kiitikadi. naweza ku-speculate kwamba mahusiano yao yalikuwa ni kama yale ya Papa Paulo na Kardinali Josef Ratzinger.

..Kingunge aliongoza idara ya Uhamasishaji na Ushirikishwaji umma[political propaganda and mass mobilization] wakati wa chama kushika hatamu. hayo hayakuwa madaraka yanayoshikwa na political light weights.

..Kingunge na wenzake ndiyo waliokuwa wakiuandaa umma wa Tanzania "kimapokeo" katika zama zile za Ujamaa. Watanzania mpaka leo tunaupenda na kuulilia Ujamaa.

..hata siku moja siwezi kumlaumu Kingunge kwa kuwa Ujamaa umefeli Tanzania. nina imani kabisa kwamba alihubiri na kuishi kama mjamaa.

NB:

..Siasa za Tanzania zilikuwa za kumtukuza na kumkweza kiongozi mkuu. kuna michango ya watanzania wengi tu imefichwa na itapotea kutokana na dhana hiyo.
 
He will be remembered for being an opportunistic,self imposed,mentally corrupt,communist and good for nothing old fella!
 
JK, naomba tutajie angalau jina la kijiji kimoja cha mfano kilichoanzishwa na Kingunge na kikapata sifa kama ulivyosema.
 
..Kingunge aliwahi ku-serve kama mkuu wa mkoa kwa miaka kadhaa.

..kila mkoa aliofanya kazi alianzisha vijiji vya ujamaa vya mfano. vijiji hivyo vilikuwa hata vikivuma sana ktk kipindi cha mbiu ya mikoa.

..nyakati zile za Ujamaa huyu Mzee alihubiri na kuutekeleza ujamaa kwa VITENDO.

..Mwalimu alimtumia sana Kingunge kwa ushauri wa kisiasa na kiitikadi. naweza ku-speculate kwamba mahusiano yao yalikuwa ni kama yale ya Papa Paulo na Kardinali Josef Ratzinger.

..Kingunge aliongoza idara ya Uhamasishaji na Ushirikishwaji umma[political propaganda and mass mobilization] wakati wa chama kushika hatamu. hayo hayakuwa madaraka yanayoshikwa na political light weights.

..Kingunge na wenzake ndiyo waliokuwa wakiuandaa umma wa Tanzania "kimapokeo" katika zama zile za Ujamaa. Watanzania mpaka leo tunaupenda na kuulilia Ujamaa.

..hata siku moja siwezi kumlaumu Kingunge kwa kuwa Ujamaa umefeli Tanzania. nina imani kabisa kwamba alihubiri na kuishi kama mjamaa.


Interesting
Baada ya ujamaa kutiwa kapuni, Kingunge ameendelea kuwa political heavy weight. Kwa itikadi ipi hasa? Ujamaa ule ule?
 
[/U][/B]

Interesting
Baada ya ujamaa kutiwa kapuni, Kingunge ameendelea kuwa political heavy weight. Kwa itikadi ipi hasa? Ujamaa ule ule?

He must have studied in Russia no wonder why he is a conservative old craphead!He doesnt wanna accept changes.He is static and rigid and thus believing that CCM will rule forever!
 
Invicible said:
Interesting
Baada ya ujamaa kutiwa kapuni, Kingunge ameendelea kuwa political heavy weight. Kwa itikadi ipi hasa? Ujamaa ule ule?

..for better or worse he was good at what he was tasked to do.

..huyu Mzee ame-serve Maraisi wote wa Tanzania. do not underestimate his abilities.

..ni kosa kubwa sana kutokumsoma, na zaidi kumu-underestimate, mpinzani wako ktk harakati zozote zile.

NB:

..waliobadilika na kuwa Mabepari ni viongozi wa Tanzania.

..wananchi bado wanaamini na kuulilia Ujamaa.

..kazi ya Kingunge na Wajamaa wenzake wa kweli wa zama hizo!!
 
Mwanakijiji said:
JK, naomba tutajie angalau jina la kijiji kimoja cha mfano kilichoanzishwa na Kingunge na kikapata sifa kama ulivyosema.

Mwanakijiji,

..sikumbuki kwa jina lakini najua kuna kijiji kilianzishwa Tanga wakati Kingunge ama ni mkuu wa mkoa au katibu wa chama. wapenzi wa kipindi cha mbiu ya mikoa wanaweza kunisaidia hapa.

..Watanzania walio wengi mpaka leo bado wanautamani Ujamaa. naamini kabisa hayo ni matokeo ya jitihada za uhamasishaji za makada wa CCM kama Kingunge Ngombale Mwiru.

..tunaweza tusikubaliane na Kingunge kutokana na mitizamo yake ya sasa hivi, lakini hiyo isitukwaze kuona pale ambapo alifanya "vizuri" tulipokuwa tukifuata siasa za Ujamaa.
 
Najiuliza hivi historia ya Tanzania itaandika nini kuhusu mchango wa Kingunge katika Taifa letu ukiondoa jina hilo la "Kingunge" ambalo limebakia kuwa alama ya mtu ambaye ni kigogo na kiongozi mkubwa? Ni nini hasa mchango wa Kingunge katika siasa, uchumi, na maisha ya Tanzania? Ni kitu gani tunaweza kusema kuwa kisingefanyika kama Kingunge asingekuwepo? Je historia itaandika nini juu ya Kingunge au atabakia na alama ya nyota tu katika footnote ya historia?

Mimi namkumbuka miaka ya '80's wakati akiwa mkuu wa mkoa Mbeya, alikuwa ni kiongozi pekee (au mmoja wao) aliyetekeleza "Operesheni Maduka" wilayani Kyela. Tulipata shida sana .... maduka yote ya wahindi na watu wengine binafsi yalifungwa .... yakafunguliwa "maduka ya ujamaa/ushirika" ... management ikawa mbovu; bidhaa zikakosekana .... kwa kweli tulikiona cha moto. Nilikuwa bado kijana mdogo lakini I still remember this. Kilichonisikisha zaidi ni kutufanya watu wa Kyela "guinea pigs", bila kuwa na mikakati inayoeleweka .... tulifanywa watu wa kufanyiwa "majaribio" ya sera zao bila kuweka mazingira ya mafanikio.
 
Haya mambo yakujadili watu mimi nadhani yamepitwa nawakati.

mimi nafikiri tujadili jinsi gani kila mmoja kujaribu kuweza kutuwezesha sisi watanzania tujiajiri.
Mambo yakuhoji fulani kafanya nini, mimi nafikiri jibu lake linakua rahisi sana kwa yule anayehoji yeye kwanza atuambie Jamii ya Kitanzania ameifanyia nini? na hatimaye wantanzania tupate mkumbuka ama atuambie ni kitongoji gani kafanikisha kuwepo ?na ndipo hapo atapata mwanya murua wa kumhoji mwenzako.
 
..Kingunge aliwahi ku-serve kama mkuu wa mkoa kwa miaka kadhaa.

..kila mkoa aliofanya kazi alianzisha vijiji vya ujamaa vya mfano. vijiji hivyo vilikuwa hata vikivuma sana ktk kipindi cha mbiu ya mikoa.

..nyakati zile za Ujamaa huyu Mzee alihubiri na kuutekeleza ujamaa kwa VITENDO.

..Mwalimu alimtumia sana Kingunge kwa ushauri wa kisiasa na kiitikadi. naweza ku-speculate kwamba mahusiano yao yalikuwa ni kama yale ya Papa Paulo na Kardinali Josef Ratzinger...Kingunge aliongoza idara ya Uhamasishaji na Ushirikishwaji umma[political propaganda and mass mobilization] wakati wa chama kushika hatamu. hayo hayakuwa madaraka yanayoshikwa na political light weights.

..Kingunge na wenzake ndiyo waliokuwa wakiuandaa umma wa Tanzania "kimapokeo" katika zama zile za Ujamaa. Watanzania mpaka leo tunaupenda na kuulilia Ujamaa.

..hata siku moja siwezi kumlaumu Kingunge kwa kuwa Ujamaa umefeli Tanzania. nina imani kabisa kwamba alihubiri na kuishi kama mjamaa.

NB:

..Siasa za Tanzania zilikuwa za kumtukuza na kumkweza kiongozi mkuu. kuna michango ya watanzania wengi tu imefichwa na itapotea kutokana na dhana hiyo.


Mkuu Jokaa kuu,

Tafadhali usimfananishe na mtu yeyote mwenye dini.mkuu next time utatutaka radhi. kwi kwi kwi.
 
Haya mambo yakujadili watu mimi nadhani yamepitwa nawakati.

mimi nafikiri tujadili jinsi gani kila mmoja kujaribu kuweza kutuwezesha sisi watanzania tujiajiri.
Mambo yakuhoji fulani kafanya nini, mimi nafikiri jibu lake linakua rahisi sana kwa yule anayehoji yeye kwanza atuambie Jamii ya Kitanzania ameifanyia nini? na hatimaye wantanzania tupate mkumbuka ama atuambie ni kitongoji gani kafanikisha kuwepo ?na ndipo hapo atapata mwanya murua wa kumhoji mwenzako.

katika mazingira ambayo wewe hutaki kujadili watu, unachotakiwa kufanya ni kwenda thread nyingine. Kwani kwa maneno yako mwenyewe unataka kujadili watu. Anayejadiliwa ni kiongozi wa umma hao wengine wakiwa viongozi wa umma una uhuru wa kutaka kujua wamefanya nini kama legacy yao.

Vinginevyo itabidi tuishie kujadili miti!
 
Kingunge ametoa mchango mkubwa katika swala zima la mfumuko wa idadi ya MAFISADI nchini kwa;

a. kuwazaa vimafisadi
b. kuwalea tumafisadi
c. kuwatetea mafisadi vingunge
d. kuimarisha mianya ya ufisadi kwa kushiriki katika kupitisha sera za kifisadi
f. kuweka maslahi ya MAFISADI mbele ya maslahi ya wananchi na hivyo kufanikiwa kuididimiza Tanzania.

Kwamba yote haya ameweza kuyafanya Kingunge kwa uadilifu mkubwa na bila kuchoka hata katika umri wake mkubwa wa sasa, ni jambo litakaloacha historia ya pekee Tanzanaia.
 
Back
Top Bottom