The Godfather

The Godfather

Mkuu the horse

Tena huyu Godfather wetu hapa anasaidiwa na SOLOZO
 
Mkuu sana,

Tanzania imejengwa kwa msingi imara wa umoja na mshikamano kwa faida ya wananchi wote.
Hata hivyo, msingi huo unamomonyoka kidogo kidogo kwa wachache kutetea uovu, wizi, ubadhirifu kwa misingi ya urafiki, ukabila, ukanda, vyama n.k.
Maendeleo ya kweli yatapatikana pale tu wananchi kwa pamoja watakuwa wakweli na siyo kumtetea mtu au kumtuhumu mwingine bila kuthibitisha kwa vielelezo.
Hizi hadithi zinaweza kuzidi kuwagawa watanzania, vinginevyo ulete vielelezo kama ifuatavyo;
1. Kwamba GODFATHER ana nguvu kuliko serikali na ana uwezo wa kuiyumbisha anavyotaka.
2. Kwamba hao wote aliowashinda walikuwa wanatetea maslahi ya taifa na wala siyo maslahi binafsi au ya vikundi vinavyowanyonya wananchi.
3. Kwamba GODFATHER hana hoja za msingi ila hao walioshindwa ndio wenye hoja.

Kama unaweza pia naomba ujibu swali hili la kizushi;
Je kuna tofauti kati ya maslahi ya taifa na maslahi ya vyama? Kama jibu ni ndiyo, tunatofautishaje?
 
Call him godfather or mother the true has been reveal and the ccm party has come to the end, they will soon be a opposition party in this country you will see it. The only one big problem that facing CCM followers, they never accept the true.

Mkuu si ungeandika Kiswahili tu, mbona ungeeleweka tu.
 
Hii ndio tanzania yetu mtu hata awe mzuri vipi mradi ni mzalendo badala ya kumkweza kwa mazuri afanyayo mnamdidimiza tuache wivu tufanye kazi tusonge mbele majungu yanadumaza maendeleo
 
Nianze na huu msemo, "We need strong Institutes not strong people". Mnaotoa madai kuwa Prof. Muhongo ameondoka kwa shinikizo la Bw. Mengi mtakuwa na safari ndefu sana ya kujifunza. Mfumo wa utawala/serikali umeoza 100%. Unanuka rushwa za kila aina na ombwe kubwa la uongozi. Kuanzia ofisi kuu ya nchini (iKulu) hadi ofisi za vijiji. Ni rushwa, rushwa, rushwa, kiburi cha madaraka na uozo mwingine mwingi sana. Hata kama uwe msafi vipi, strong vipi lakini kama taasisi ni dhaifu na chafu lazima utaanguka tu.

Inawezekana ni kweli Bw. Mengi ana visasi binafsi na Prof. Muhongo. Lakini hili halibadilishi ukweli kuwa sakata la ESROW ni la kweli na kuna watu lazima wawajibike (Rejea maelezo ya Mh. Raisi Kikwete; kuna kodi ilipaswa kulipwa haikulipwa na taratibu nyingine nyingi zilikiukwa). Katika mlolongo wa watu na taasisi zinaolazimika kuwajibika huwezi kuikosa Wizara ya Nishati na Madini hivyo "automatically" waziri Mhongo ataguswa tu. Sikutarajia kwa sakata hili la ESCROW Prof. Muhongo apone hata kama angekuwa msafi vipi; tayari yupo kwenye nyumba chafu, lazima naye atanuka. Hapa Bw. Mengi kama ametumia nafasi ya swala la ESROW kumnyuka mpinzani wake haitakua jambo jipya. Iwe kampuni au watu binafsi hutumia makosa ya mpinzani kujinufaisha.

Lakini suala la msingi hapa ni maslahi ya taifa. Hata kama Mengi ametumia nafasi hii kumdhibiti Prof. Muhungo wananchi wa kawaida tutaangalia ni kwa jinsi gani maslahi ya taifa yamezingatiwa. Katika suala la Tegeta Escrow Account nchi ilipoteza mabilioni kwa uzembe (hapa nasemea kodi tu ambayo raisi Kikwete anakiri haikulipwa). Lazima tuone waliohusika wanawajibika kwa kadiri ya ushiriki wao kwa kujua au kwa bahati mbaya au hata kwa shinikizo. Suala la Mengi na Muhungo halina maslahi kwa taifa.
 
Tujiulize:

Pamoja na yoote hayo, vyombo vya habari vya huyu Godfather unayemsema vinajitahidi walau kutuonyesha sura ya upande wa pili wa hao waliopewa dhamana ya uongozi kupitia chama tawala.

Wewe ulitaka vifanye kazi ya kuwasifia na kuwapamba watu wanaohujumu na kulidhoofisha taifa hili? Kama ilivyo TBC ambayo haionyeshi uhalisia wa masuala ya nchini mwetu?


Ni kweli nashangaa mtu anakaa na kuandika mada ambayo yeye mwenyewe ukimuuliza umeandika kwa maslahi ya nani?. Hajui kama ni maslahi binafsi au ya chama chake au jamii kwa ujumla. Tuongeze nguvu tuikomboe Tanzania mikononi pa mafisadi.
 
Ni kweli nashangaa mtu anakaa na kuandika mada ambayo yeye mwenyewe ukimuuliza umeandika kwa maslahi ya nani?. Hajui kama ni maslahi binafsi au ya chama chake au jamii kwa ujumla. Tuongeze nguvu tuikomboe Tanzania mikononi pa mafisadi.

Una akili? Za kawaida tu.??
 
Back
Top Bottom