THE GODFATHER:
Mwanzoni mwa miaka ya 60 alikuwapo mwandishi mashuhuri aitwae MARIO PUZZO aliandika kitabu wakati huo kikiitwa THE GODFATHER..ndani yake kulikuwa na main character akiitwa VITO ANDOLIN CORLEONE.."THE GODFATHER"
Mwandishi huyo alijaribu kuandika mahusiano yaliyokuwepo baina ya Serikali na Organised Criminal Gangs "the family" na kuonyesha nguvu ambayo the family inayo katika maamuzi ya Serikali na Taasisi kubwa Duniani, kwa kutumia nguvu ya PESA ama kwa jina halisi RUSHWA, ambayo kwa rushwa waliwakamata wanasiasa, wanasheria na watendaji wakubwa katika Serikali.
Mwandishi akaonesha nguvu ya those powerful organised criminal gangs alipoodhihirisha walivyojipenyeza katika THE MOST POWERFUL AND SECURE INSTITUTION IN THE WORLD-the so called ROMAN CATHOLIC CHURCH kiasi cha kufanya ASSASSINATION ya POPE.
Hii ni nguvu ya Ajabu,.,kwa wale ambao wanaelewa nguvu ya Kanisa wanaelewa ninachokimaanisha.
Nirudi katika Uhalisia wa maisha yetu ya KBONGO.,nitaanza kwa mifano hai..
Katika Moja ya Vikao vya Halmashauri Kuu ya CCM(kikao kikubwa cha maamuzi ndani ya chama kinachoongoza Serikali) Mjumbe mmoja aitwae KILUMBE NG'ENDA - Ambaye alikuwa ni Katibu wa Mkoa wa Dar es salam wa CCM.,aliwahi kutamka jina la GODFATHER kwenye kikao hicho., akimtuhumu kwa yafuatayo:-
@ Kuwa "GODFATHER" sio mwanaCCM kwa maana hana kadi ya Chama hicho.
b) Godfather anakihujumu Chama kupitia TV yake, Radio na Magazeti.
c) Akatoa nyaraka na meseji zenye kuthibitisha kuwa GODFATHER anafadhili CHASO na midahalo na makongamano ya CDM.
d) Ng'enda akataka Chama kimshughulikie GODFATHER kwani anakidhohofisha na kukipa taswira hasi kwa watanzania.
MATOKEO YAKE..,
Baada ya Mwaka mmoja, Kilumbe Ng'enda alivuliwa GAMBA, akanyang'anywa nafasi yake ya Ukatibu wa Mkoa na kushushwa Cheo, mpaka hivi tunavyojadiliana KILUMBE na miongoni mwa watumishi wa CCM wasiojulikana ofisi yao, hadhi yao, cheo chao wala idara (yupo yupo tu)
Na leo MKOA wa Dar ndio ngome ya Upinzani., Kila uchao nguvu ya CCM inapwaya na Upinzani unapata nguvu ktk Jiji hili, lakini CCM ilikubali ifikwe na hayo kuliko kushughulika na THE GODFATHER.
NAIZUNGUZA CCM AMBACHO NDICHO CHAMA TAWALA TANGU UHURU - THE MOST POWERFUL INSTITUTION HAPA NCHINI...wanaoijua nafasi ya CCM katika maisha ya Watanzania nadhan wananielewa.
Lakini kama Kumbukumbu zetu ziko sahihi kidogo, mtakumbuka kila WAZIRI wa Serikali hii ambae kwa namna yeyote alijaribu kugusa interest ya Godfather aliishia pabaya hasa kwa kuipoteza nafasi yake na kusahaulika kabisa katika siasa za nchi hii.
NDUGU ZANGU..,tunaiishi Tanzania ambayo Criminals wananguvu isiyomithilika na isiyozuilika.
Miaka kadhaa nyuma tulimsikia mmoja ya WAZALENDO HALISI wa nchi hii akitamka kwa ujasiri kuwa atashughulika na wauza dawa za kulevya, mtakuwa mashahidi kuwa HAKUDUMU na hatunae tena..
Miezi michache tu alitokea kidume mwingine aliyekuwa akikamata Nyara za Serikali kila asubuhi na jioni..,MAJANGILI wakakosa kupumua na wakahisi kubughudhiwa..kama hamjasahu Huyo KIDUME sasa hivi sio Waziri tena na taarifa nilizonazo ni kuwa hivi sasa MAJANGILI HAWAUI WANYAMA bali wanawasafirisha wazima wazima tena kwa kutumia NDEGE za SERIKALI.
MUHONGO nae alifikiri kwa kuwa amefika nafasi ya uwaziri bila kupiga magoti ya kuomba hela ya kampen kwa MAGODFATHER wala hawategemei kwa lolote akadhani anaweza kufanya jambo la sawasawa..,Nadhan mnashuhudia kinachomkuta.
HII NDIO TISA (TANZANIA ILIVYO SASA)
Wanyonge, masikini wa nchi hii wanayashuhudia haya kuwa kila anayejitahidi kuwahurumia na kujaribu kuwapunguzia maumivu yao na hadha za maisha magumu anaishia kupotea..
Masikini hawa ni wanyonge, ni masikini hawana nguvu wanaishia kulalamika (tena kimya kimya) lakini nafikiri wanakoelekea sasa wataanza kupaza sauti zao..MIMI NITAUNGANA NAO siku wakipata UJASIRI HUO.
Kwa maoni yako kuna mambo ambayo sijaelewaz intention yake hasa kwa public.
Huyo Godfather unayedanganya uma siyo sahihi. Yeye amekuwa mwiba kwa wezi kwa kujaribu kufungua wananchi macho. Kwa mtu kama wewe ambaye ni mnufaika wa syndicates za Wizi, ufisadi (Mapapa), madawa ya kulevya (Nzowa issue), watapanya mali zaumma ikiwemo ardhi, na wasiotaka jamii ielewe mambo viongozi washenzi wa CCM wanaifanyia nchi mko sahihi kumuana ni adui wenu. Vyombo vya habari vya huyu unayemhadaa kwa umma vimesaidia sana kuleta uelewa wa mbambo yaliyofichika ikiwemo midahalo huru, taarifa za pande mbili kueleweka vizuri. amefichua maovu mengi na kusababisha CCM kuaibika na kutafuta mbinu nyingi chafu za kudhuru vyombo hivi vya habari. Uzuri huyu ndugu awe na tabia gani ila Kupitia kwa vyombo vyake vya habari taifa limekomboa raslimali nyingi, limejengea wazalendo uzalendo wa kweli na kuimarisha confidence ya wananchi.
KUPITIA VYOMBO HIVI VYA HABARI HUYU NDUGU MBALI NA KUTENDA HAKI NA KUAJIRI WENGI, amesaidia sana kukuwa kwa uhuru wa vyombo vya habari, kuamsha ari ya wanahabari kutngeneza habari sanifu, za kimaendeleo, makala constructive na ripoti mbalimbali maalumu ambazo ni matukio ya kweli wananchi wanafanyiwa na hakuna uwajibikaji kuwaadhibu wahusika. mfano migogoro ya ardhi.
Naona wanaosupport mawazo yako mufilisi ni wezi wenzako ambao walitaka wakishaiba waitwe heros kama Chenge (Mwaandaaji wa katiba ya CCM) ambao hawataki kabisa kuwajibika. Kiburi cha Muhongo, majidai, mbwembwe, dharau, dhihaka, uongo na kujiona anajua kila kitu ndo kilimuondoa kwenye uwaziri. fedha kama hazikukwapuliwa, kwa nini ajiuzulu?? Viongozi wenu CCM wezi na walafi ndio wanaosababisha maisha ya wananchi yanakuwa magumu na wanaichukia chama chenye serikali kwakuwa kimekosa kutoa sera zenye tija zaidi ya kujikita kwenye wizi, ufisadi, kuuwa aldino , na kuuza nchi kwa mafungu na rasilimali zake kwa wawekezaji wezi.
Kwa taarifa yako inaonesha una bifu binafsi ila jamii inaelewa fika muuaji wa Chama chenu cha wizi ni viongozi wachafu ikianzia kwa mwenyekiti mpaka kwa watendaji wadogo katika chama. mha husda mna hadaa na mnafanana kabisa na ibilisi mwaribifu. mfsno ni njia CCM inazotomua kuwadhuru waaduilifu wa chama na kuwainua waovu. Kuna waliolishwa sumu na wengine kuuawa au kudhuriwa kwa kusababishiwa ajali. mfano mzuri tu ni recent incidence ya Mgimwa na Dr. Mvungi. Jamii inaelewa fika unyama CCM inaoufanya kwa raia wema kupitia polisi na vyombo vya usalama. wapinzani wanajua uchungu wa kuwepo CCM kwa jinsi walivyotumia fedha na madaraka kukandamiza wapinzani mpaka kuanzisha hujuma ya kudhuru raia wakisingizia wapinzani. mfano ni Mwigulu nchemba na wengine.
Tumeshuudia rafu za chaguzi mbalimbali zikifanywa na CCM ba sio ripot za TV, tumeona rafu ndani ya chama, tumeona hujuma kwenye elimu, viongozi wasio na weledi wakipewa nafasi nyeti, maisha kuzidi kuwa magumu huku kina masaburi na viwanda vya ARV faki wakizidi kuneemeka, mahospitalini dawa shida na huduma mbovu, elimu ndio changa la macho, vyuo vikuu mikopo inatolewa kama dawa, sasa utamlaumu Godfather ndio kasababisha haya?????? Ufisadi, Wizi, tafakari na chukua hatua, muuanyi wa CCM ni UFISADI KIKWETE na Syndicate iliyomuweka madarakani. Udhaifu,hadaa, fedha, umasikini, visasi na umimi ndio vinaiharibu CCM.
God father anafanya ligal businesses ila CCM wanafanya illegal business kuanzaia madawa ya kulevia, pembe za ndovu, madini, warumwa (wanapelekwa uarabuni kiagent wakilaghaiwa kazi nzuri) na ndio in ayoharibu nchi.
Tutafakari pamoja.