Wanasiasa ni watu wanafiki sana na ndio wanaosababisha nchi zetu za kiafrika zinaendelea kuwa masikini licha ya kuwa na rasilimali nyingi za kutosha.Wanasiasa wakati mwingine wanashindwa kufanya maamuzi sahihi kwa kuangalia upepo wa kisiasa.Kujiuzulu kwa Prof. Muhongo kumedhihirisha jinsi gani baadhi ya wanasiasa wetu wasivyo na nia njema na nchi yetu.Tumepoteza mtendaji anaejiamini sana, mtendaji ambaye alikuwa anakijua anachokifanya, Mtu ambae naamini kupitia kwake nadhani mafuta na gesi yangetunufaisha zaidi.Namuona Prof. Muhongo anaenda kutumiwa na nchi zingine licha ya kwamba alikuwa na uzalendo.
Unaweza kujiuliza kwa nini Jiji la Dar es salaambado lina shida kubwa ya maji wakati sehemu kubwa ya Temeke ina maji mengi yaliyo aridhini, tatizo ni wanasiasa kutowaruhusu wataalamu kufanya kazi kwa masilahi yao binafsi.Mikataba mingi ya madini Tanzania iliyosainiwa hapo kabla haitunufaishi, Hebu jiulize leo kapatikana mtaalaam wa kutunufaisha kwa kuziba mianya ya wazawa feki basi anaonekana hafai.
Jiulize: Huyo mzawa Mengi ulishawahi kusikia akitoa misaada sumbawanga, kigoma, lindi, makete, etc. Yeye anatoa misaada kwa wachaga wenzake.
Mzawa mwingine Bakhresa ulishawahi kusikia akitoa misaada kwa wakiristo zaidi mara nyingi ni kwa waislamu, tena na ajira anatoa kwa upendeleo kwa waislamu wenzake, ukiwa mkiristo kama unataka kazi nzuri basi ukubali kuslimu.Hii ni mifano ya baadhi ya wazawa ambao unadhani watatunufaisha kumbe watajinufaisha wenyewe na kikundi kidogo tu.
mkuu nikusahihishe, tatizo la Muhongo sio Mengi, tatizo la muhongo ni uwendawazimu wa kisomi, akjiamini yeye ni mtaalamu na msomi kuliko wengine...na nitakupa facts juu ya fikra zake kupotoka...
1. Hakuna nchi yeyote inayoendelea au itakayoendelea kwa kutumia umeme wa gas, geothermal au diesel/HFO;
why? Generation cost kwa hiyo mitambo semwa hapo juu ni ghali sana, initial investment ni ndogo sawa, but kurun, maintaining na operational cost ni ghali mnooo, pia durability ni ndogo...i tell u umeme tanzania ungefika tsh 500 per unit very soon.
2. nchi zote dunian ambazo zipo serious na power, back borne yao ya grid is either Hydro au Nuclear...lakini nyingi ni hydro, na hiyo ndio njia rahisi sana ya kutengeneza umeme, na ndio njia nzuri ya kukupa umeme rahisi, initial investment ni kubwa lakin operational ni ndogo sana...maintenance pia ni ndogo...u can even run a plant which is automatic by only 4 people.
vyanzo vya maji tunavyo tele tena na feasibility study zilishafanyika some areas we can generate up to 4000 MW.
sasa swali kwako, Muhongo tangu aingie madarakan uliwah msikia akiongelea Hydro powers? (forget about sijui mambo ya kina cha maji kimepungua maana ile ilikuwaga ni upigaji ili IPTL auze umeme tanesco)
narudia kilichomponza Muhongo zaidi ni kiburi chake cha kisomi...kujiona yeye ni kila kitu, lakini sie tunaojua mambo ya umeme we tell u it was about time tu kwa bomu haswaa la matatizo ya umeme na bei juu ya umeme kulipuka...
yeye kama alikuwa anajua mambo ya miamba na madini its fine, umeme angeomba tu ushauri...na sio kutuletea umeme ghali zaidi...