The earth is flat and is not rotating

Duh, kumbe zile assumptions za kwenye physics zilinisaidia,
naona kuna watu hawana vivid imaginations kabisa ndo maana wanaongea kama wako 2000BC, inabidi warudie form 1/2 kabisaaaa
 
Habarini,

Katika pitapita zangu za kujua vitu nikakuta hii kitu kuhusiana na dunia kutokuwa ni duara na ni tambarale pia haizunguki katika muhimili wake kama tulivofundishwa huko shule za awali.

Kuna baadhi ya ushahid unaotokana na mazingira jinsi yalivo pamoja na udini kidogo...

1. kwa mazingira jinsi yalivyo:

Kwanza kuhusu "earth is not rotating" .... kawaida dunia inazunguka jua kwa muda siku 365 na hujizungusha katika muhimil wake kwa muda wa masaa 24 kumaliza mzunguko wake, na ndipo tunapata usiku na mchana.... (hivi ndivo navojua mm na wewe)

lakini kuna maelezo yanayo onyesha kuwa dunia haijizungushi bali jua na vilivo juu vinaizunguka dunia. proof wanaosema kwamba dunia haizunguki ni hii ya usafiri wa ndege.

Tuanze kwa kusema kwamba dunia inajizungusha katika muhimili wake kwa speed ya 6070 km/hr kutokea magharibi kwenda mashariki, ndio maana tunapata kuona jua linachomoza kutokea mashariki na kuzama magharibi.

Sasa tuchuke mfano ndege inatokea marekani (Washington DC) kwenda uingereza (London). Hivyo ndege inatoka magharibi kwenda mashariki. Umbali kutoka marekani mpaka uingereza ni 5934.6 km na inachukua masaa 7 na dakika 39, hivyo ndege husafiri katika umbali huo kwa 775.76 km/hr. Hivyo kama dunia inakuwa katika speed yake ya 1675 km/hr basi huu umbali ungeongezeka zaid maana dunia ingekuwa inazidi kwenda mbele kutoka magharibi kwenda mashariki na ndege hiyo kwa speed hiyo ya 775.76 km/hr. [lets assume kwamba umbali huo unatokana na speed ya dunia na speed ya ndege kutoka magharib kwenda mashariki]

JE, KAMA NDEGE INATOKA UINGEREZA KWENDA MAREKANI UMBALI UTAKAO KUWA COVERED NA NDEGE UTAKUWA SAWA NA WA MWANZO (5934.6 KM) KAMA DUNIA INAJIZUNGUSHA KUTOKA MAGHARIBI KWENDA MASHARIKI?

JIBU NI HAPANA, MAANA KAMA NDEGE INATOKA MASHARIKI KWENDA MAGHARIBI NA DUNIA INAZUNGUKA KUTOKA MAGHARIBI KWENDA MASHARIKI BASI UMBALI UTAPUNGUA MAANA DUNIA NA JUA ZITAKUWA OPPOSITE DIRECTION.

View attachment 216726

Lakini kiuhalisia umbali utakuwa ni huohuo na masaa ya kusafiri yatakuwa ni hayohayo... HIVYO HII INAONESHA KUWA DUNIA HAIZUNGUKI.

Pili kuhusu "the earth is flat and not round".... bado kuna debate zinaendelea kuelezea kivipi dunia ni flat na sio duara kama tunavojua. Ila katika hili kuna maswali mengi sana, maana kuna issues za horizon, light, space and sky ceiling, land curvature ambazo mm mwenyewe binafsi naendelea kuzifatilia ila kwa sasa sina clue ambazo zitani support kuelezea kivip dunia ni tambarale.

Ila inasemekana dunia ina umbo la flat disk kama hii.

View attachment 216727

Hii ni bendera ya United Nations na ramani yake ya dunia iko tofauti na ramani ambazo tunazozijua. Hivyo inasemekana kuna siri katika shape ya dunia. flat earth society wanaamini kuwa dunia iko hivyo ila kwa pande nne sio round kama inavoonekana kwenye hiyo picha juu.

Pia kuhusu maji ya bahari kuna kuta za barafu zinashilia hayo maji. Hii inawezekana baada ya ile mada ya kuto kuwepo kwa south pole kule Antarctica.

Kunasemekana Antarctica ni kubwa kuliko tunavoiona katika ramani, pia ndiko kunakoaminika kuwa ni kitovu kitakocho onyesha kuwa dunia sio duara bali ni tambarale.

Maana hakuna ndege inayoruhusiwa kipita katika anga la Antarctica. Jiulize, Kina "NASA" wanadai wameenda mwezini, wametuma vifaa vya kisasa huko sayari mars na vyengine mbali zaid lakini wameshindwa kupita juu ya Antarctica kisa ni baridi kali... JIULIZE!!!!!!

2. Udini:

Katka udini nitazungumzia katika upande wa imani ya kikristo.

1. katika agano la kale yoshua alisimamisha jua. Yoshua 10: 12-13 "12 Ndipo Yoshua akanena na Bwana katika siku hiyo ambayo Bwana aliwatoa Waamori mbele ya wana wa Israeli; akasema mbele ya macho ya Israeli, Wewe Jua, simama kimya juu ya Gibeoni;

Na wewe Mwezi, simama katika bonde la Aiyaloni.
13 Ndipo jua likasimama, na mwezi ukatulia, Hata hilo taifa lilipokuwa limekwisha jipatiliza juu ya adui zao."

hii inaonyesha kuwa Jua ndilo linalozunguka dunia na sio dunia linazunguka Jua, Hivyo dunia haizunguki na iko stationary


2. katika agano jipya shetani alimchukua Yesu mpaka mahali pa juu na kumuonyesha ulimwengu wote:
Luka 4 : 5 -8

5 Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,


6 Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza. 7 Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu."
http://biblehub.com/luke/4-8.htm
8 Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake."

kama dunia ingekuwa duara basi ingekuwa haiwezekani kwa falme zote za ulimwengu kuonekana kwa mara moja.


3. malaika wanne katika kona za nchi:

Ufunuo 7 : 1

"1 Baada ya hayo nikaona malaika wanne wamesimama katika pembe nne za nchi, wakizizuia pepo nne za nchi, upepo usivume juu ya nchi, wala juu ya bahari, wala juu ya mti wo wote."


hii inaonesha kuwa dunia pia sio duara, maana kama ni round hizo pembe nne za nchi zitapatikanaje?. Hivyo dunia might be square or rectangle.


TUJADILI ZAID NI HAYA NILIYOYAKUTA KATIKA KUJUA ZAID...... THANKS
Bado sana,don't be fool please.Vipi kuhusu TIMEZONES,ECLIPSES,na pia four seasons of the year?
Pia naomba uniambie kuna uhusiano gani kati ya 360 degrees za duara na 365 days of the year.
 
Ina maana nikichukua ndege nikaanza safari ya kuelekea mashariki, ina maana itafika siku nitatokelezea magharibi au?

Nawaza tu......
 
Simlaumu mleta mada, kazaliwa bongo ambapo hata astronomy museums hakuna, na kuna uwezekano hajasoma chuo au kama kasoma basi sio sayansi na hawajahi fanya publication yoyote ile so anafikiri wanaweza tumia sayansi kutudanganya.

Mtu aliyefanya publication anajua vizuri inavyokaguliwa na kuombwa ku~prove kile anacho~claim, akishindwa inatupiliwa mbali. Kusema Earth is flat karne hii ni plain stupidity hakuna kingine. Wengine hizo article wanapublish kupiga tu hela maana zina wasomaji wengi sana wanaopenda ujinga, its human nature kushindana. Mleta mada kaombe kazi shirika la usafirishaji kupitia baharini ushangae unaenda east unatokea west na kurudi palepale. Kama ni square huko chini sijui ulipitaje.
 
Dunia ni round, hilo hata halihitaji ubishi, picha zipo nyingi zinapigwa kila siku kutoka angani.

Kila kitu kilichomo ndani ya atmosphere, binadamu na ndege vyote wakati dunia inazunguka, inazunguka navyo pia kwa hiyo usidhani ndege itaruka afu umbali upungue, ingekua hivo basi hata chini hapa tungekua tukiruka tunatua kwingine.. For as long as kitu kimo ndani ya atmosphere basi dunia inavozunguka na chenyewe kinazunguka vilevile kwa speed ileile...

Afu angalia satellites zilizoko angani, kuna satellite zinaitwa geostationery ambazo zenyewe hua zinaonekana kama zimesimama, zile satellite kwa kua ziko nje kiasi kwamba haziwezi kuzungushwa na dunia, hua zinapewa speed sawa na speed ya dunia, sasa kiukweli ni kama zinaanguka vile sema zinaonekana stationery sababu zinaenda kwa speed sawa na speed ya mzunguko wa dunia..

kama dunia ingekua flat hivi inategemea jua lingeonekana kama linazama kwenda chini?? si lingeonekana linapita tu kutoka kulia kwenda kushoto, sio kuonekana linatoka chini linakuja juu afu linaenda chini tena...

Afu watu NASA mnawaona kama mashetani, wanaofanya kazi pale ni watu ka wewe na mimi, yaweza kua ndugu yako au rafiki, sio watu walioletwa kutoka kuzimu wale kusema wanazuia ndege kupita Antarctica, mbona watu wanaenda kule kila mwaka, we aliyekwambia wanazuia ni akina nani?? hakuna evidence yoyote kule kua dunia haizunguki wala si duara..

Jamani nunueni hata telescope basi za bei nafuu mtumie kuangalia mwezi au sayari nyingine za karibu muone kua ni duara na hivi vitu vipo kweli sio kwamba vinaandikwa tu.. huwezi danganya science ambayo ndo leo hii inakusaidia wewe unatumia jamiiforums
Unajua n kwamba haujawasoma elite races vizuri uzi kama huu ulishawahi kuwekwa na mkuu

moudytunechi

Na akaweka ushahidi mkubwa 2 ila inavyoonekana haujauelewa dunia ni ...tambarare
 
Same speed!!! Vitu vyote vilivyoko duniani na kwenye atmosphere yake vina move at the same speed same momentum. Vituo vya anga vya utafiti ni moving station viko fixed kwenye orbit na vinazunguka kwa speed sawa na ya dunia. Na ndio maana unaviona kama viko stationary
parking orbit ee .wacha muchezo ww hii yote concpiracy 2
 
Simlaumu mleta mada, kazaliwa bongo ambapo hata astronomy museums hakuna, na kuna uwezekano hajasoma chuo au kama kasoma basi sio sayansi na hawajahi fanya publication yoyote ile so anafikiri wanaweza tumia sayansi kutudanganya.

Mtu aliyefanya publication anajua vizuri inavyokaguliwa na kuombwa ku~prove kile anacho~claim, akishindwa inatupiliwa mbali. Kusema Earth is flat karne hii ni plain stupidity hakuna kingine. Wengine hizo article wanapublish kupiga tu hela maana zina wasomaji wengi sana wanaopenda ujinga, its human nature kushindana. Mleta mada kaombe kazi shirika la usafirishaji kupitia baharini ushangae unaenda east unatokea west na kurudi palepale. Kama ni square huko chini sijui ulipitaje.
Mkuu mleta Mada ana point...ww cjui kwa nn unamshambulia...yeye kaleta mpaka ushahd wa ku support hoja zake...

Is better if u think twice...labda nam nifkrishe hakir hiv ndege inaporuka inakua within kwenye speed ya Dunia wakat tayar imeshaiacha surface ya Dunia...

Japo n cku nying nmeyasoma haya kwenye advanced level...hiv escape velocity ilimanisha nn.vs speed ya Dunia...?

Tukumbuke Dunia Ina tembea Katka different speed.. Yaan Katka mhil wake as Ina undergo rotation, na Katka revolution pia Ina speed yake....

Je ndege inapokua angan vp gravitional force...? Unataka kuniambia central fugal force na central petal force havko applied hapa.....! Nafkr mnaosoma physics na kufanya research tunaomba msaada...
 
labda tumuongezee tu kuhusu dunia kuzunguka na vitu vyote vilivyomo ndani.
mfano mzur ni pale nzi anapokuwa anafly ndani ya basi lililo kwenye mwendo, kwa idea ya mleta mada ilibidi nzi asiende sawa na basi na hvyo angejigonga kwenye kioo cha nyuma cha basi. but kama tunavyoshuhudiaga ni kuwa nzi nae huenda sawa na basi bila ya kujigonga.
Axha uongo ww
 
Hizi mada huwa zinapotea afu zinarudi tena na hoja zile zile.. Na mtu anakubali mpira unaorushwa live kwenye tv kwa kutumia technology ya satellite ila anakataa picha za satellites hizohizo zinazoonyesha picha ya dunia.. Technology yote hii iliyopo saiz bado unadhani kuna watu wangekubali kudanganywa na propaganda kama hizi..
 
Same speed!!! Vitu vyote vilivyoko duniani na kwenye atmosphere yake vina move at the same speed same momentum. Vituo vya anga vya utafiti ni moving station viko fixed kwenye orbit na vinazunguka kwa speed sawa na ya dunia. Na ndio maana unaviona kama viko stationary
Mkuu unachanganya vitu, kuna vituo vya anga viko low orbit ivi haviwezi kwenda same speed na dunia, Sattelite au station pekee zinazokuwa matched na speed ya dunia ni ziko Ktk Geostationary orbit kiasi cha 36000Km kutoka apa dunia, Chini ya huo umbali huwezi ku set sat ime match na speed ya dunia na ikakaa kwenye orbit yani below apo lazima speed ipungue ili kuepusha hio satellite kuvutwa na Gravity, kuna calculation zake kutegemea na umbali na Gravitational
 
Hivi hizo setelite ziko spinned katika orbit au zinatumia locomotive engenes kama jet engine katika kuvispeed up viendane sawa na speed ya dunia katika kulizunguka jua n at the same time katika kujizungusha yenyewe katika mhimili wake? Nataka kujua tafadhali
Sattelite zina Vitu vya kuiongezea spewd na kuipunguza nafikiri watu wa Mechanical hapa watadadavua in details what is this ila mimi nakupa General concept, Rocket ndio zinapeleka Sattelite katika orbit Ikifikisha katika orbit basi Sattelite inapaswa kupewa initial speed na rocket after there rocket huiachia hio Sattelite ikiwa na speed fulani, Sattelite haihitaji Engine kuendelea kurotate inazunguka kupitia nguvu ya uvutano yani gravitational force ila incase Sattelite imepungua speed au imezidi basi walioko ground station wata either switch on Means ya ku increase au kuipunguza speed ime match na calculation zao kulingana na orbit, Ukiwa kwenye ndege Ukarusha kitu chini mfano Mzigo hautahitaji Engine ili huo mzigo udondoke ardhini ila kani ya uvutano ndio ita act na kuupa speed fulani sasa unaweza kuweka engine huo mzigo ili kucontrol namna utakavyodondoka unaweza kufanya upungue speed au uongezeke kwa kutumia hio engine ila main speed italetwa na Gravitational force
 
Bado mtoa mada ana hoja za kufanyia kazi. ndege inaporuka inakua imeacha uso wa dunia hivyo ni kweli kama inaelekea mashariki basi umbali ungeongezeka na kama ingeelekea magharibi umbali ungepungua.
Ni rocket pekee ndio zinaweza kutoka nje ya Uso wa dunia yani atmosphere kumbuka Engine ya ndege inahitaji oxygen kuendelea kuburn fuel ivo ndege za kawaida ziko ndani ya atmosphere, Rocket kuna means wanaweka yani oxygen na combustion chamber viko enclosed, Pia kutoka kwenye uso wa dunia sio kitu cha mchezo mchezo ili Utoke unahitaji uwe na speed kuanzia 11000M/S, Hio ndio Escape velocity ya kuchomoka ktk Dunia
 
Wakuu dunia ni Sphere yani hio iko proved na mambo mengi sana Kuna Sattelite kibao zinaonyesha picha za dunia Tena kama international space station wako live youtube muda wote
 
Habarini,

Katika pitapita zangu za kujua vitu nikakuta hii kitu kuhusiana na dunia kutokuwa ni duara na ni tambarale pia haizunguki katika muhimili wake kama tulivofundishwa huko shule za awali.

Kuna baadhi ya ushahid unaotokana na mazingira jinsi yalivo pamoja na udini kidogo...

1. kwa mazingira jinsi yalivyo:

Kwanza kuhusu "earth is not rotating" .... kawaida dunia inazunguka jua kwa muda siku 365 na hujizungusha katika muhimil wake kwa muda wa masaa 24 kumaliza mzunguko wake, na ndipo tunapata usiku na mchana.... (hivi ndivo navojua mm na wewe)

lakini kuna maelezo yanayo onyesha kuwa dunia haijizungushi bali jua na vilivo juu vinaizunguka dunia. proof wanaosema kwamba dunia haizunguki ni hii ya usafiri wa ndege.

Tuanze kwa kusema kwamba dunia inajizungusha katika muhimili wake kwa speed ya 6070 km/hr kutokea magharibi kwenda mashariki, ndio maana tunapata kuona jua linachomoza kutokea mashariki na kuzama magharibi.

Sasa tuchuke mfano ndege inatokea marekani (Washington DC) kwenda uingereza (London). Hivyo ndege inatoka magharibi kwenda mashariki. Umbali kutoka marekani mpaka uingereza ni 5934.6 km na inachukua masaa 7 na dakika 39, hivyo ndege husafiri katika umbali huo kwa 775.76 km/hr. Hivyo kama dunia inakuwa katika speed yake ya 1675 km/hr basi huu umbali ungeongezeka zaid maana dunia ingekuwa inazidi kwenda mbele kutoka magharibi kwenda mashariki na ndege hiyo kwa speed hiyo ya 775.76 km/hr. [lets assume kwamba umbali huo unatokana na speed ya dunia na speed ya ndege kutoka magharib kwenda mashariki]

JE, KAMA NDEGE INATOKA UINGEREZA KWENDA MAREKANI UMBALI UTAKAO KUWA COVERED NA NDEGE UTAKUWA SAWA NA WA MWANZO (5934.6 KM) KAMA DUNIA INAJIZUNGUSHA KUTOKA MAGHARIBI KWENDA MASHARIKI?

JIBU NI HAPANA, MAANA KAMA NDEGE INATOKA MASHARIKI KWENDA MAGHARIBI NA DUNIA INAZUNGUKA KUTOKA MAGHARIBI KWENDA MASHARIKI BASI UMBALI UTAPUNGUA MAANA DUNIA NA JUA ZITAKUWA OPPOSITE DIRECTION.

View attachment 216726

Lakini kiuhalisia umbali utakuwa ni huohuo na masaa ya kusafiri yatakuwa ni hayohayo... HIVYO HII INAONESHA KUWA DUNIA HAIZUNGUKI.

Pili kuhusu "the earth is flat and not round".... bado kuna debate zinaendelea kuelezea kivipi dunia ni flat na sio duara kama tunavojua. Ila katika hili kuna maswali mengi sana, maana kuna issues za horizon, light, space and sky ceiling, land curvature ambazo mm mwenyewe binafsi naendelea kuzifatilia ila kwa sasa sina clue ambazo zitani support kuelezea kivip dunia ni tambarale.

Ila inasemekana dunia ina umbo la flat disk kama hii.

View attachment 216727

Hii ni bendera ya United Nations na ramani yake ya dunia iko tofauti na ramani ambazo tunazozijua. Hivyo inasemekana kuna siri katika shape ya dunia. flat earth society wanaamini kuwa dunia iko hivyo ila kwa pande nne sio round kama inavoonekana kwenye hiyo picha juu.

Pia kuhusu maji ya bahari kuna kuta za barafu zinashilia hayo maji. Hii inawezekana baada ya ile mada ya kuto kuwepo kwa south pole kule Antarctica.

Kunasemekana Antarctica ni kubwa kuliko tunavoiona katika ramani, pia ndiko kunakoaminika kuwa ni kitovu kitakocho onyesha kuwa dunia sio duara bali ni tambarale.

Maana hakuna ndege inayoruhusiwa kipita katika anga la Antarctica. Jiulize, Kina "NASA" wanadai wameenda mwezini, wametuma vifaa vya kisasa huko sayari mars na vyengine mbali zaid lakini wameshindwa kupita juu ya Antarctica kisa ni baridi kali... JIULIZE!!!!!!

2. Udini:

Katka udini nitazungumzia katika upande wa imani ya kikristo.

1. katika agano la kale yoshua alisimamisha jua. Yoshua 10: 12-13 "12 Ndipo Yoshua akanena na Bwana katika siku hiyo ambayo Bwana aliwatoa Waamori mbele ya wana wa Israeli; akasema mbele ya macho ya Israeli, Wewe Jua, simama kimya juu ya Gibeoni;

Na wewe Mwezi, simama katika bonde la Aiyaloni.
13 Ndipo jua likasimama, na mwezi ukatulia, Hata hilo taifa lilipokuwa limekwisha jipatiliza juu ya adui zao."

hii inaonyesha kuwa Jua ndilo linalozunguka dunia na sio dunia linazunguka Jua, Hivyo dunia haizunguki na iko stationary

2. katika agano jipya shetani alimchukua Yesu mpaka mahali pa juu na kumuonyesha ulimwengu wote:
Luka 4 : 5 -8

5 Kisha Ibilisi akamchukua hadi mahali pa juu, akamwonyesha kwa mara moja falme zote za ulimwengu. Huyo Shetani akamwambia,

6 Nitakupa uwezo juu ya falme zote hizi na fahari zake, kwa maana nimepewa hivi vyote; nikitaka kumpa mtu ninaweza. 7 Hivi vyote vitakuwa mali yako wewe, kama ukiniabudu."

8
Yesu akamjibu, "Imeandikwa: Utamwabudu Bwana Mungu wako, na utamtumikia yeye peke yake."

kama dunia ingekuwa duara basi ingekuwa haiwezekani kwa falme zote za ulimwengu kuonekana kwa mara moja.


3. malaika wanne katika kona za nchi:

Ufunuo 7 : 1

"1 Baada ya hayo nikaona malaika wanne wamesimama katika pembe nne za nchi, wakizizuia pepo nne za nchi, upepo usivume juu ya nchi, wala juu ya bahari, wala juu ya mti wo wote."

hii inaonesha kuwa dunia pia sio duara, maana kama ni round hizo pembe nne za nchi zitapatikanaje?. Hivyo dunia might be square or rectangle.


TUJADILI ZAID NI HAYA NILIYOYAKUTA KATIKA KUJUA ZAID...... THANKS
The earth is a flattened sphere...
Nilishafaulu kwa hivyo hivyo buanaaaa
 
Back
Top Bottom