The difference between Toyota VVTI and D4 Engines


Soma reply yangu hapo juu
 
D4 Engines?
Hiyo literature yako TUPA KULE. D4 kwa ninavyojua mimi inahusiana na maswala ya transmission. Yani gearbox has hasa ya auto. Kuna gearbox zenye gear tatu pamoja na gear ya nne ya ziada ambayo inaitwa overdrive. in total making it four gears.

But gari ambazo ni D4 ina maana zina gearbox zenye gear nne ambazo ni maini na gia ya nyongeza ambayo inaitwa overdrive making it with a total of five gers. Unapozungumzia suala la VVT hapo sasa ndio unazungumzia suala la kwenye engine. Go and re check your study...
 

Watu wengine bana wanajua kuvamia thread, si uende kwenye udaku kule utaeleweka? Kaa pembeni bwana waache wataalamu na wenye magari wazungumze... Au we ni mmojawapo wa wanaogonga nyundo gereji zetu zile? Nenda shule hata VETA sikuhizi wanafundisha

Unachoongea hakina uhusiano wowote na D4 engenes D4 na sasa VVTi ni system inayosaidia kuongeza ufanisi wa matumizi ya mafuta, upunguzaji wa hewa ukaa au CO2 na gari kuwa na nguvu kwa wakati mmoja. Ili hili kiweze kufanyika kawa ufanisi ni lazima mafuta yawe na ubora unaotakiwa, na hivyo uwepo wa sensor kwenye oil, injectors na hata gearbox ni muhimu, mawili mafuta au lubricants hazina viwango, au sensor zenyewe zimekufa, kuingia uchafu.

 

Mkuu next time kama hujui kitu kaa kimya !! Silence has, and will always be the better option if you don't know the right answer!!!!
Kwa kukusaidia tu, nembo zinazobandikwa kwenye magari, mara nyingi huwa zinazungumzia zaidi engine iliyomo kwenye gari hilo , kwa kiasi kidogo differential system na , ni adimu sana kuzungumzia gearbox! hii inatokana na ukweli aina ya engine ,(ujazo, ulaji wa mafuta, na aina ya mafuta) ,huwa ina influence gharama za uendeshaji moja kwa moja ikiwa , pamoja na uwezo wa kuhimili safari ndefu, n.k., kwa maana hiyo watengenezaji wa magari wamekuwa wakiboresha zaidi engine , kuliko eneo lolote lile..

D4 (direct injection four stroke) , D4D (direct injection four stroke diesel) ni mfumo wa kuingiza na kuunguza mafuta katika engine, Gari za D4 ziko. za manual na automatic , watu wengi wameijua D4 kupitia magari madogo, kama preimio, Rav 4, ambazo nyingi ni auto, wakahitimisha kuwa Gari ya d4 ni lazima iwe auto, lakini kuna magari ya petrol manual transmitted ,kama land cruiser , hilux na hiace yana engine za D4 ( simaanishi D4D).

Baadhi ya magari ya d4 yamekuja na gearbox za CVT , watu wamekuwa wakininua bila kujua kama ni cvt transsmission, , a complex automatic box ambayo ni very efficient , but very sensitive, ukisikia mtu kabadilisha tramsission fluid , halafu gari ikaanza kuleta matatizo, most likely, jua lina CVT autobox. na sababu huwa ni kutofuata masharti ya mtengenezaji, na sio kuwa gari ni bovu, bali umeriharibu kwa kutokujua kwako
 
Mkuu hao mafundi uliowasema hapo juu bei zao ziko poa kinoma. Watafute jumamosi na jumapili kwenye gereji zao kitaa ndo utajua nnalolisema. Mjini akili. Kijijini nguvu

Hapo bold, kumbe ndio siri ya mafanikio? Ila sasa, ni kitaa wapi?
 
Inategemea unazungumzia gari ya wapi! Ahaa, kumbe nyie mmezoe hizi asante Mjapani eeh? Wengine tunatumia western vehicles, unakuta ka gari kadogoo kama Vitz lakini kana engine cc 2500! Si unajua magari ya Mmarekani huwa hatanii kwenye engine eeh? Kule 'kwetu' Amerika hakunaga hivi vigari vya sisii buku!
Thankx for correction by the way...
 

Thanx for correction. At least you have improved your topic. In the previous ulifanya copy and paste ndio maana tukapata wasiwasi na literature yako. But now umekuja na kitu genuine. Hata kama ni uongo, just because you came with your own words, I treat u like a prophet and the only option is to believe you...
 
U must be out of ua mind. ....mtoa mada msamehe bure mtu huyu!
Nafikiri wewe ndio upo "in your mind" mimi sihitaji msamaha ila tu kama nitakuwa nimekosa, kumbuka mtaaluma yeyote hawezi ku quote bila kusema na hapa tunajiita GT sasa lazima kama umefanya quote useme, pitia posts kibao hapa utagundua mtu anatoa mada na source..
Motherfantass watu tunaelimika we unasema kacopy na kupaste haya tuelimishe wewe genius kutoka kichwani mwako. Si wote wanaoweza kusearch vitu ka hivo wengi wanaelimika kupitia JF.watch out!!!
Issue hapa sio kusearch wala u-genius ila ni kuweka wazi chanzo cha taarifa, kama wewe unafikiri ni mjanja zaidi kwa kufaidi kupitia jf kwa vyanzo visivyojulikana basi siku moja utaishia kwenye tango pori.
 

Mafundi wengi wa bongo ni kama dengue tu. Washanitesa hadi nikagundua tatizo mie nwenyewe through forums wao sijui Kwa nn hawapendi kujiupdate kabisa hawa
 

Mkuu,
Can the 2 technologies be applied on one engine? If no, then why is it that I own a Toyota premio with D4 Engine which hav VVTI and also coupled with CVT?

To me the FSI and VVTI might differ but D4 can only be improved with VVTI or COMMONRAIL technology. Sina uhakika kama kuna jukwaa la Automotives nadhani tungepata nafasi ya kupeana ufahamu zaidi kwenye maeneo haya.
 

Nimeipenda hii.. !!!! hujaona maandishi ya timing belt kwa kuwa D4 zinatumia timing chain ambayo ina lifespan ya km 300,000 , by then inakadiriwa gari liwe written off, system nzima ya vvti ni complex sana watengenzaji wengi waliona kuwa ingekuwa vigumu kutumia belt kwenye system hiyo , wakaamua ku deal na 'old school' -timming chain.

Timing chain ilikuwa ikitumika kwenye magari miaka ya nyuma , baadaye walibadilisha na kuweka timming belt ili kupunguza kelele, belt ilikuwa ina limitations za kuwa rubricated , na kwa kuwa ilikuwa inapita na kuzungusha vyuma , ni lazima ibadilishwe baada ya kipindi fulan...
 

nimejifunza kitu hapa. nilikuwa sijui hili.
 

Mkuu nakubaliana nawe kuwa kila engine ina code name, lakini si kweli kuwa vvti ina code ya 1g au 1jz pekee.

Vvti ni valve mechanism tu , hauhusiani hata kidogo na majina ya engine, kinachonishangaza mafundi wengi hawaelewi hili, mafano mdogo tu, hiyo engine ya 1g ipo toka miaka ya themanini, by then ilikuwa inatumia carburetor , na ilikuwa na valve mbili kwa kila cylinder na ilikuja kwenye mark two box za mwanzo kabisa, baadaye ilipokuwa updated the same 1g ikawa electronic fuel injected( 1g -Fe), baadaye ikawa updated na kutumia 24valve, leo hii the same 1g ni d4 vvti

Vvti ni mfumo tu, na uko kwenye engine nyingi za petrol mfano 1nz 1sz, 3s, 1g, 1jz, 1uz . Kwa wale wanaofuatilia vizuri watakubalian nami kuwa kuna engine toyota ametoka nazo mbali sana mfano 1g , S series, na R series.
 

Mkuu D4 mara nyingi huwa na Vvti, lakini si kila Vvti ni D4, put it simply D4 ni mfumo wa jinsi mafuta yanavyoingia kwenye cylinder (direct injected) , Vvti , however, ni jinsi hewa inavyoingia kwenye cylinder. The two systems ni updates ili kuboresha fuel efficiency...
CVT ni gear box za automatic zilizoboreshwa , kuna uwezekano mkubwa sana gari zenye engine za D4 , kuja na gearbox hii ,ingawaje sio zote.
Unfortunaltely common rail inahusiana na engine za diesel, (D4D)
 

mkuu naungana na ww mm nifundi umeme wa magari na katika engine amabazo nazipenda toka moyoni ni hizi za D4 sababu mafundi wengi wanazishambulia kuwa ni mbovu basi wabishi wachache huwatunapiga sana pesa.

nikweli watu wengi bado hawajui tofauti kati ya mfumo wa D4 na mfumo wa VVTI kiukweli hivyo nivitu viwili tofauti sana.
vvti huu mfumo huwa unahusika na valve kwaupande wangu naweza fananisha mfumo huu kuwa umeboreshwa kutoka kwenye mfumo wa distributer.huu mfumo huwa unahusika na kufanya advance ya valve na huwa unafanya kazi kwamsaada wa oil.

D4 huu ni mfumo unaohusisha uingizwaji wa mafuta kwenye combustion chamber.hapa ni kwamba mafuta huwa yanakwenda moja kwa moja kwenye combustion chamber.
kiukweli watu tunaogopa na kuilaum tu hii technologia lkn kiukweli ndio ratest technologia ya mzungu kwa sasa ww huoni sasa hivi magari yote mpaka ya disel yanatoka na mfumo huu??
faida za mfumo huu
1 unatumia mafuta machache
2 nirafiki wa mazingira /hakuna uchafuzi hapo no moshimoshi
3 engine /gari huwa na nguvu kubwa
hizo ni faida 3 kubwa.

tatizo kubwa la mfumo huu wa D4 nikwenye systerm ya mafuta tuu kwakuwa engine yake niyakisasa zaidi kwahiyo ina sensor nyingi sana .hapo ukiweka mafuta machafu yakuchakachua kamwe huto acha kulalamika na kuilaani aina hii ya engine.
na zilivyokuwa active kama ulikuwa unakalibia kabisa kuishiwa mafuta ukaenda sheli nakujaza mafuta hapohapo sheli gari lazima iibuke na miss ya ajabu tena kunazingine huwa zinakataa kabisa kuwaka.

mbona kwa nchi yetu ilivyokuwa yakimagumashi haya magari yenye engine ya D4 tutayalaani milele.

mwenye D4 yake inayomzingua tutafutane kubadilisha engine na kukimbilia kuwekaq ya 3S FE sio sawa kabisa gari itakuwa inatembea ila kuna mambo flani utaya miss kama speed usitegemee kbs.some times unatoa engine yenye cc kubwa unaweka engine yenye cc ndogo kuna zingine huwa zinatolewa engine ya 4wd na kuwekwa ya 2wd .

kingine gari kuwa na cc kubwa sio ndio itakuwa inakula sana mafuta sio kweli some times huwa inategemeana na technologia iliyotumika kutengenezea engine husika like D4 maana kuna wengi utasikia wanalalama sitaki kbs engine za 6cyrinder sababu zinakula sana mafuta kumbe kuna engine za 4 cyrindel zinabugia mafuta zaidi ya engine za 6cyrinder
 

nikweli mkuu inahitaji nguvu ya ziada sana kumueleza mtu ili aelewe tatizo wengi wetu tunakrem tuu juu kwa juu.

mm naona ili wanajamv wapate kuelewa ilibidi watofautishe kati ya D4 na VVTI wengi wanafikili ni kitu kimoja kumbe ni vitu 2 tofauti kabisaa
mwingine ni mfumo wa mafuta na mwingine ni mfumo wa uingizwaji wa hewa labda hapa ili tueleweshane vizuri yatubidi tuanzie kwenye D4 nakurudi nyuma na kutafuta ilikotokea mpaka kufika hapa je mwanzo kabisa mfumo wa mafuta kuingia kwenye combustion chember ulikuwaje mpaka kufikia hapa kwenye d4
hali kadhalika na mfumo wa vvti nao pia.
bado sikumbuki ni aina gani ya engine yenye mfumo wa D4 haina mfumo wa vvti.

ila ni engine nyingi sana zenye mfumo wa vvti peke yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ