Kizazi cha magazeti na taarifa za habari kinatoweka

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,634
697,916
Je, ni mashirika mangapi ya habari Tanzania yana maono kama ya BBC? Maana BBC baada ya kuona mapinduzi makubwa kwenye mawanda ya upashanaji habari na hatari iliyopo mbeleni ya kukosa wasomaji na wasikilizaji wakaja na uamuzi mzito wa kufunga ofisi zao nyingi za kikanda hali iliyopelekea punguzo kubwa la wafanyakazi

Mashirika mengi ya habari kwasasa yanabadilika na kuwekeza mitandaoni zaidi.. Na hili limewafanya wapunguze gharama za uendeshaji na kufikia watu wengi zaidi!

Kwa Tanganyika yetu zile enzi za kuwahisha magazeti mikoani zinakufa..zile enzi za kujikusanya saa 12 jioni ili kupata habari za dunia zinamalizia kukata roho! Zile enzi za kujikusanya saa mbili usiku ili kupata yaliyojiri siku nzima ni kama hazipo tena! Maendeleo makubwa ya teknolojia yameua hayo yote! Sasa hivi hakuna haja ya kusubiri saa saba mchana, saa 12 jioni ama saa mbili usiku kujua kilichojiri nchini na duniani

Sasa hivi huna haja ya kwenda kununua gazeti kuweza kujua yaliyojiri kitaifa na kimataifa! Kila kitu kiko kiganjani kwako kupitia simu janja.. Kwa kifurushi chako cha elfu moja tuu unaweza kujua yaliyojiri duniani kote ndani ya dakika chache kupitia magazeti mitandaoni, habari picha, habari video na makala mbalimbali.. Tena nyingine unazipata kupitia live coverage!

Maendeleo haya yamevuka vikwazo vingi vya mamlaka zinazo control media nyingi kwenye upashanaji habari.. Kupangiwa cha kuandika, kupangiwa cha kuripoti nknk.. Japo kuna shida kidogo kwenye habari za mitandaoni kwakuwa karibu kila mtu ni mwandishi sometimes kuna upotoshaji, uongo, uzushi na hata kutoa habari zisizohaririwa, sanifiwa na kukosa viwango bora vys uandishi

Kuna baadhi waliofanikiwa kuwa waandishi wa mitandaoni kwa kusanifu kazi zao, kutoa habari za uhakika na za kuaminika, kutoa habari kupitia live coverage hawa wana maisha ya mafanikio makubwa mbeleni

Juzi kanisani kwangu niliona kitu kilichonifikirisha mno! Waumini kuuziwa magazeti ya kanisa baada ya ibada.. Zamani yaliwekwa nje na muuzaji na baada ya ibada watu walinunua kwa hiari yao! Siku hizi kwa mtindo huo hayauziki tena!

Haya magazeti yanatoka maramoja kwa wiki.. Imagine kwa ulimwengu wa leo matukio ya Jumapili hii Kanisani ama nje ya kanisa yaje yaripotiwe Jumapili inayofuata kanisani

Natambua dhima ya taasisi za kidini kujaribu kwenda na wakati, nyingi zina vyombo vya habari lakini kwenye ishu ya magazeti (hasa RC na Lutheran) wanafeli pakubwa.. Magazeti yanauzwa kwa lazima na kuna wakati mengi hubaki na kuingiza hasara kwenye taasisi husika. Ni rai yangu wawe na maono makubwa kwenye hili haraka!

Miradi ya uchapishaji magazeti sio miradi yenye tija tena! Miradi ya taarifa za habari kwenye tv na radio nayo inachechemea.. BBC wameona mbali wamegutuka mapema! Vipi wengine?
 
Kuna swali moja; teknologia imeongeza au imepunguza nafasi za ajira? Kila mtu ana majibu kwa context yake!

Hili ni swali gumu na Pana sana linalotakiwa kufanyiwa kazi na taasisinza elimu, waajiriwa watarajiwa na wale ambao ndio wameingia kwenye ajira. Sie ambao jua linazama hatuwezi kufukuzana na nyakati, enzi zinabadilika Kwa Kasi sana, ujuzi, utaalam, mahitaji ya soko la ajira Kwa Sasa yamebadilika na yataendelea kubadilika sana, lakini daima, wale watakaokua wamejiandaa, hawatakosa ajira.

Nimegusia taasisi za elimu kuhakikisha mitaala Yao inaendana na mabadiliko yanayoendelea ili kuhakikisha wanazalisha watu wenye uwezo wa kufanya kazi kwenye haya mazingira.

Tukirudi kwenye swali lako, wakati baadhi ya ajira zinafariki, fursa nyingine mpya zinaibuka Kwa wale walio tayari kubadilika kulingana na enzi tulizonazo.
 
Mambo hubadilika kwa Kasi, Posta wao soko la barua limekufa sasa wamejikita zaidi ktk usafirishaji!

Magazeti muda si muda wataacha kuyakimbiza mikoani usiku kucha coz wasomaji hakuna.. wateja ni wachache ambao wamesogea umri ..

Japo sina umri mkubwa sana ila sikumbuki mara ya mwisho kununua magazeti ilikuwa mwaka gani, sijui hata bei zake kwa sasa
 
Unaweza kuandika jibu ukifika mwisho ukasoma upya unajikuta unafuta na kuanza upya kuandika jibu.

Uko sahihi linahitaji utulivu wa Hali ya juu sana napo haina guarantee kwamba utaibuka na jibu sahihi la wakati wote.

Uko salama Mkuu?
Hahahahaha hilo swali ukiliangalia kwa haraka unaeza jibu ki rahisi tu ila ndio km unavyosema, utaandika then utafuta

Nipo Mkuu
 
Mambo hubadilika kwa Kasi, Posta wao soko la barua limekufa sasa wamejikita zaidi ktk usafirishaji!

Magazeti muda si muda wataacha kuyakimbiza mikoani usiku kucha coz wasomaji hakuna.. wateja ni wachache ambao wamesogea umri ..

Japo sina umri mkubwa sana ila sikumbuki mara ya mwisho kununua magazeti ilikuwa mwaka gani, sijui hata bei zake kwa sasa
Kizazi cha mikanda ya deck
Kizazi cha mikanda ya cassete
Kizazi cha walkman
Kizazi cha CD/radio za CD changer
Kizazi cha DVD
Kizazi cha flash
Kizazi cha memory card....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli Kabisa ulicho andika...ila hao kwetu imecchochiwa oia na Siasa chafu zaMagufuli.Ilifika wakati taarifa ya habari ni Magufuli,magazeti yoye yote yanamuimba,Radio ..Sasa hapo Wenye akili tukaona ya Nini.
Hata hivyo Hatari.iliyopo,ni kuwa kw nchi za Dunia ya Tatu ,hali hii inaenda na kuonhezeka.wajinga!
Kuna watu hata hiyo mitandaonya kijamii hawaihjui na bado magzeti hawasomi,Redioni wanasilikioza miluziki,akwenye TV wanaangalia Tamthlia hii ni Hatari kubwa !
Kuna Mkoa fulani majuzi takribani miezi mitatu hakukuwa na Magazeti 🇹🇿😁!Baadaye ya muuza Magazeti pekee kufariki!
Na hapo Makao.Makuu ya Mkoa Kuna muuzaji mmoja tu Magazeti ukikosa hapo basi Uñaenda kusoma vichwavya habari myandaoni!
 
Na magazeti yanayonunuliwa kwa sasa ni udaku na michezo. Ukata nao umepunguza wanunuzi. Watu hujikusanya kwa muuza magazeti kuchungulia vichwa vya habari.
Gazeti linauzwa buku na habari zake ziko very limited.. Buku hiyohiyo napata kifurushi cha MB 400 hivi.. Hiki kitaniwezesha kusoma magazeti yote mtandaoni na kuperuzi mambo mengine! Wangejua wangeshusha bei ya magazeti yao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah thanks mkuu kumbe ulikuwepo

Sent using Jamii Forums mobile app

Aaah wapi, nilikuwepo kidijitali Mkuu. Naona shindano kinazidi kuboresha Kila mwaka.

Nafurahi pia Maxence Melo na JF Kwa ujumla kupiga hatua kwenye eneo la kupashana habari Kwa kutumia zaidi mitandao na wanazidi kuboresha kadri ya maendeleo yanavyozidi kuibuka kwenye Hilo eneo.
Ukiptia JF unaona kujua japo Kwa uchache Nini kinaendelea nchini na hata duniani Kwa ujumla.

Magazeti na vitabu Kuna watu wanapenda wasome kitabu kabisa au gazeti la karatasi, Bado hao watu tunao hiyo itachukua muda kufutika kabisa. Ni ukweli usiopingika kutokana na uhitaji kupungua, utafika mahali gharama za uzalishaji hazitahimilika kutokana na uhafifu wa wateja/ mauzo. Ni mchakato.
 
Ni kweli Kabisa ulicho andika...ila hao kwetu imecchochiwa oia na Siasa chafu zaMagufuli.Ilifika wakati taarifa ya habari ni Magufuli,magazeti yoye yote yanamuimba,Radio ..Sasa hapo Wenye akili tukaona ya Nini.
Hata hivyo Hatari.iliyopo,ni kuwa kw nchi za Dunia ya Tatu ,hali hii inaenda na kuonhezeka.wajinga!
Kuna watu hata hiyo mitandaonya kijamii hawaihjui na bado magzeti hawasomi,Redioni wanasilikioza miluziki,akwenye TV wanaangalia Tamthlia hii ni Hatari kubwa !
Kuna Mkoa fulani majuzi takribani miezi mitatu hakukuwa na Magazeti !Baadaye ya muuza Magazeti pekee kufariki!
Na hapo Makao.Makuu ya Mkoa Kuna muuzaji mmoja tu Magazeti ukikosa hapo basi Uñaenda kusoma vichwavya habari myandaoni!
Kuna Mkoa fulani majuzi takribani miezi mitatu hakukuwa na Magazeti !Baadaye ya muuza Magazeti pekee kufariki!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aaah wapi, nilikuwepo kidijitali Mkuu. Naona shindano kinazidi kuboresha Kila mwaka.

Nafurahi pia Maxence Melo na JF Kwa ujumla kupiga hatua kwenye eneo la kupashana habari Kwa kutumia zaidi mitandao na wanazidi kuboresha kadri ya maendeleo yanavyozidi kuibuka kwenye Hilo eneo.
Ukiptia JF unaona kujua japo Kwa uchache Nini kinaendelea nchini na hata duniani Kwa ujumla.

Magazeti na vitabu Kuna watu wanapenda wasome kitabu kabisa au gazeti la karatasi, Bado hao watu tunao hiyo itachukua muda kufutika kabisa. Ni ukweli usiopingika kutokana na uhitaji kupungua, utafika mahali gharama za uzalishaji hazitahimilika kutokana na uhafifu wa wateja/ mauzo. Ni mchakato.
JF imewin mno kwenye hiki kipengele na zaidi sasa inangaazia kwenye usahihi wa habari..Maana kwenye usalama tayari kuko njema
Jamii check ni project iliyoletwa kwa wakati sahihi mno na ambayo imepongezwa na serikali kupitia msemaji wake mpya!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom