The Chanzo: Tanzania yauza Afrika Mashariki kuliko inavyonunua

The Chanzo: Tanzania yauza Afrika Mashariki kuliko inavyonunua

Stuxnet

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2011
Posts
17,562
Reaction score
27,633
20260114_065330.jpg


Tanzania ina trade surplus dhidi ya nchi jirani — hii inamaanisha inapata fedha zaidi kutoka mauzo ya nje kuliko inavyotumia kwa uagizaji kutoka nchi hizo.

Nchi zinazotoa surplus kubwa zaidi ni DRC, Rwanda, Uganda na Burundi. Hii inaonyesha Tanzania imekuwa muuzaji mkuu wa bidhaa (hasa bidhaa za viwanda, chakula kama mahindi/unga wa mahindi, saruji, n.k.) katika eneo la maziwa makuu na kusini.

Kenya pekee ndiyo kama haina surplus kubwa, hii inaonyesha ushindani mkali lakini Tanzania inazidi kuimarika.

Kwa ujumla, data hii inaonyesha mafanikio makubwa ya sera za kuongeza mauzo ya nje na kuimarisha viwanda vya ndani katika kipindi cha 2024/25. Hii inasaidia uchumi wa Tanzania kukua, kuongeza mapato ya serikali, na kuimarisha nafasi yake kama kitovu cha biashara katika Afrika Mashariki na Kusini mwa Jangwa la Sahara.
 
View attachment 3529629

Tanzania ina trade surplus dhidi ya nchi jirani — hii inamaanisha inapata fedha zaidi kutoka mauzo ya nje kuliko inavyotumia kwa uagizaji kutoka nchi hizo.

Nchi zinazotoa surplus kubwa zaidi ni DRC, Rwanda, Uganda na Burundi. Hii inaonyesha Tanzania imekuwa muuzaji mkuu wa bidhaa (hasa bidhaa za viwanda, chakula kama mahindi/unga wa mahindi, saruji, n.k.) katika eneo la maziwa makuu na kusini.

Kenya pekee ndiyo kama haina surplus kubwa, hii inaonyesha ushindani mkali lakini Tanzania inazidi kuimarika.

Kwa ujumla, data hii inaonyesha mafanikio makubwa ya sera za kuongeza mauzo ya nje na kuimarisha viwanda vya ndani katika kipindi cha 2024/25. Hii inasaidia uchumi wa Tanzania kukua, kuongeza mapato ya serikali, na kuimarisha nafasi yake kama kitovu cha biashara katika Afrika Mashariki na Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Nazani kama serikali ingewekeza kwenye bidhaa za kilimo hasa zao la mchele tungeuza zaidi maradufu,maana mfano hizo inchi unazozizungumzia wanategemea mchele kutoka inche
 
Hizo ni bidhaa tunauza kwa kuzalisha kweli au nyingine tunasafirisha baada ya kununua. Thamani yote inayosomeka hapo haijaingia kwetu.

Mfano nikinunua nguo shilingi 600 kutoka China nikaiweka dukani Kariakoo na kuuza kwa bei ya jumla kwa shilingi 990 kwa mteja wa Burundi, inaonekana nchi imeingiza 990 wakati kati ya hiyo 600 ilikwishatumwa China kwa mtengenezaji.
Kwahiyo net ya nchi hapo unakuta ni ndogo.

Najua wabobezi wa uchumi wa terms za kuelezea contradiction hii.
 
Kenya haina faida.Tujikite DRC, Rwanda, Burundi, Zambia, na nchi nyingine zenye faida.Pongezi Kwa RAIS wetu John pombe magufuli Kwa kuboresha bandari za kalemie na karema iliyochochea biashara Drc na Tz
Biashara DRC na tz kubwa kitambo tu,siyo kwa 'juhudi' za dikteta wa chato
 
Hizo ni bidhaa tunauza kwa kuzalisha kweli au nyingine tunasafirisha baada ya kununua. Thamani yote inayosomeka hapo haijaingia kwetu.

Mfano nikinunua nguo shilingi 600 kutoka China nikaiweka dukani Kariakoo na kuuza kwa bei ya jumla kwa shilingi 990 kwa mteja wa Burundi, inaonekana nchi imeingiza 990 wakati kati ya hiyo 600 ilikwishatumwa China kwa mtengenezaji.
Kwahiyo net ya nchi hapo unakuta ni ndogo.

Najua wabobezi wa uchumi wa terms za kuelezea contradiction hii.
Mradi tusiwe na positive balance of trade,huko nyuma kwa mfumo huuhuu tulikua na negative trade balance na kenya,kenya tunawalisha kwa 40+%,tunawauzia bidhaa za ujenzi pia,pongeza kwa hilo
 
Nazani kama serikali ingewekeza kwenye bidhaa za kilimo hasa zao la mchele tungeuza zaidi maradufu,maana mfano hizo inchi unazozizungumzia wanategemea mchele kutoka inche
Morogoro na Mbeya zinaweza kuibeba nchi kwenye zao hili la mpunga (siyo mchele)
 
Hizo ni bidhaa tunauza kwa kuzalisha kweli au nyingine tunasafirisha baada ya kununua. Thamani yote inayosomeka hapo haijaingia kwetu.

Mfano nikinunua nguo shilingi 600 kutoka China nikaiweka dukani Kariakoo na kuuza kwa bei ya jumla kwa shilingi 990 kwa mteja wa Burundi, inaonekana nchi imeingiza 990 wakati kati ya hiyo 600 ilikwishatumwa China kwa mtengenezaji.
Kwahiyo net ya nchi hapo unakuta ni ndogo.

Najua wabobezi wa uchumi wa terms za kuelezea contradiction hii.
Ni kweli hoja yako iko kitaalamu mno. Inabidi kuangalia incremental figure ndiyo tuirekodi. Lakini wachumi kwenye estimation wanapopima GDP wameamua kuchukua thamani yote hivyo hivyo. Kwa hiyo kuna onekana kama kuna double counting
 
Kenya haina faida.Tujikite DRC, Rwanda, Burundi, Zambia, na nchi nyingine zenye faida.Pongezi Kwa RAIS wetu John pombe magufuli Kwa kuboresha bandari za kalemie na karema iliyochochea biashara Drc na Tz
Trade surplus au favourable balance of payment siyo faida, bali ni uwiano kati ya nchi ilichopeleka nje dhidi ya nchi ilichoagiza kutoka nje.

Hatuwezi kuacha kufanya biashara na Kenya kwa kuwa ndiyo soko letu kubwa la bidhaa za kilimo kama mahindi, mchele, maharage, mbogamboga nk. Majirani zetu hawana ardhi ya kutosha kwa mazao ya chakula, hivyo basi sisi tuna competitive advantage kwenye hili.

Nadharia Comparative Advantage (David Rucardo) au Production Probability Advantage (Adam Smith) inaelekeza kuwa, nchi izalishe zao ambalo yenyewe inazalisha kwa nafuu kuliko nchi nyingine.

Kwa ku trade na Kenya tunatengeneza ajira, tunakusanya kodi, na mwisho tunajenga jamii stable kijamii na kisiasa
 
Nazani kama serikali ingewekeza kwenye bidhaa za kilimo hasa zao la mchele tungeuza zaidi maradufu,maana mfano hizo inchi unazozizungumzia wanategemea mchele kutoka inche
Yaaan umenena. Tanzania kama tungeboresha sera zetu vzr, hasa kupunguza makodi na gharama za kuendesha makampub ya kizawa yanayouza nje. Mazao kama mahindi, mpunga na maharagwe tunaweza zalisha na kuzilisha nchi majiran vizuri kabisa kama tutaboresha miundombinu na sera za kilimo.

Mfano huko bonde la usangu, wanalima mpunga sana ila sehemu kubwa wanategemea misimu ya mvua, kuna mabwawa yanasemekana kujengwa ila hayatumiki na yalichakachuliwa.

Taasisi zijikite kwenye mbinu za kuboresha na sio kuwabana wazalishaj na wakulima.
 
ningependa kujua kinachouzwa nje, isije kuwa mahindi na mpunga mchafu wenye mawe, pia chanzo cha hiyo habari …
 
View attachment 3529629

Tanzania ina trade surplus dhidi ya nchi jirani — hii inamaanisha inapata fedha zaidi kutoka mauzo ya nje kuliko inavyotumia kwa uagizaji kutoka nchi hizo.

Nchi zinazotoa surplus kubwa zaidi ni DRC, Rwanda, Uganda na Burundi. Hii inaonyesha Tanzania imekuwa muuzaji mkuu wa bidhaa (hasa bidhaa za viwanda, chakula kama mahindi/unga wa mahindi, saruji, n.k.) katika eneo la maziwa makuu na kusini.

Kenya pekee ndiyo kama haina surplus kubwa, hii inaonyesha ushindani mkali lakini Tanzania inazidi kuimarika.

Kwa ujumla, data hii inaonyesha mafanikio makubwa ya sera za kuongeza mauzo ya nje na kuimarisha viwanda vya ndani katika kipindi cha 2024/25. Hii inasaidia uchumi wa Tanzania kukua, kuongeza mapato ya serikali, na kuimarisha nafasi yake kama kitovu cha biashara katika Afrika Mashariki na Kusini mwa Jangwa la Sahara.
Hayo ni manambari tu ya kwenye makaratasi ukweli tunauona huku mitaani kwani vyuma vilikaza mpaka vikakazuka , mikanda tumeikaza mpaka hamna sehemu nyengine ya ya kukazia . Au ndio haya magari manenne na mishahara minono ya wabunge na viongozi
 
Yaaan umenena. Tanzania kama tungeboresha sera zetu vzr, hasa kupunguza makodi na gharama za kuendesha makampub ya kizawa yanayouza nje. Mazao kama mahindi, mpunga na maharagwe tunaweza zalisha na kuzilisha nchi majiran vizuri kabisa kama tutaboresha miundombinu na sera za kilimo.

Mfano huko bonde la usangu, wanalima mpunga sana ila sehemu kubwa wanategemea misimu ya mvua, kuna mabwawa yanasemekana kujengwa ila hayatumiki na yalichakachuliwa.

Taasisi zijikite kwenye mbinu za kuboresha na sio kuwabana wazalishaj na wakulima.
Ni kweli Mkuu !! Wakati wa JKN kulikuwa na mashirika mawil; Mbarali rice farms chini ya NAFCO na Kapunga rice project.

Yote yaliuzwa mwishoni mwa 1990s baada ya Watanzania kushindwa kuyaendesha. Ila kuna big potential
 
Back
Top Bottom