Amani Dimile
JF-Expert Member
- Jul 27, 2022
- 243
- 395
Ikiwa ndio najua sekunde zangu za mwisho za kuishi duniani, halafu nikaambiwa nikupe ushauri madhubuti sana kabla sijafa ambao utakusaidia maishani, basi ningekushauri hivi vitu kumi;
1. Muda unaweza ukakusaiadia au kukuangamiza yote inatokana na jinsi unavyoutumia. Kuwa makini na muda kwani mara zote huwa haurudi nyuma.
2. Elewa utofauti kati ya ku enjoy maisha na kuharibu future. Kuna maisha baada ya anasa/starehe.
3. Njia fupi au za mkato mara nyingi zimejaa uharamu. Hakuna mafanikio ya kirahisi yasiyohitaji juhudi vinginevyo ni udhalimu, dhambi na kufuru kwa Mungu.
4. Jitahidi kuwa na heshima, utu na uaminifu, na kamwe usipoteze hata kimoja sababu ukipoteza kimoja utakosa vyote. Siku zote heshima, utu na uaminifu ni vitu vinavyoenda sambamba.
5. Msaada sio haki yako ukinyimwa usilalamike. Usiwe mwepesi kuwachukia watu waliokataa kukusaidia hata kama uwezo walikuwa nao. Huwezi kumchukia mtu aliyeshindwa kufanya kitu ambacho wewe mwenyewe kilikushinda kufanya.
6. Usifurahie anguko la mtu, usiwe chanzo cha kumkwamisha mtu fulani kimaendeleo. Usichukie mafanikio ya watu, sababu kufanikiwa kwao hakuwezi kukuzuia wewe usifanikiwe. Anga ni pana na inatosha kwa kila ndege kupaa kivyake.
7. Ishi na watu kwa moyo wa huruma na upendo, wasaidie watu hadi ambao unajua hawawezi kukusaidia wewe. Mara zote binadamu huwahi kusahau wema, ila Mungu kamwe hawezi sahau.
8. Nyuma ya kila mtu unaemjua kuna mtu usiemjua. Hivyo usijiaminishe kwamba unamjua sana mtu fulani, hapana humjui ila unajua yale aliyokuruhusu uyajue tu. Kuwa makini.
9. Mpambanie mtu anaekupenda ila kamwe usithubutu kumpambania mtu ili akupende. Utaumia.
10. Usiwachukie watu sababu ya maneno ya kuambiwa wala usithubutu kuwaamini watu kutokana na maneno yao. Mara nyingi binadamu hudanganya na asipodanganya basi hunena bila kufikiri.
Baada ya hapo nitakuwa huru kufa !!
"The author is dead"
Amani Dimile aliandika
#amanidimile #fikrazadimile #misemoyahekima #hekimayadimile #tusomevitabu #swahilicaption
1. Muda unaweza ukakusaiadia au kukuangamiza yote inatokana na jinsi unavyoutumia. Kuwa makini na muda kwani mara zote huwa haurudi nyuma.
2. Elewa utofauti kati ya ku enjoy maisha na kuharibu future. Kuna maisha baada ya anasa/starehe.
3. Njia fupi au za mkato mara nyingi zimejaa uharamu. Hakuna mafanikio ya kirahisi yasiyohitaji juhudi vinginevyo ni udhalimu, dhambi na kufuru kwa Mungu.
4. Jitahidi kuwa na heshima, utu na uaminifu, na kamwe usipoteze hata kimoja sababu ukipoteza kimoja utakosa vyote. Siku zote heshima, utu na uaminifu ni vitu vinavyoenda sambamba.
5. Msaada sio haki yako ukinyimwa usilalamike. Usiwe mwepesi kuwachukia watu waliokataa kukusaidia hata kama uwezo walikuwa nao. Huwezi kumchukia mtu aliyeshindwa kufanya kitu ambacho wewe mwenyewe kilikushinda kufanya.
6. Usifurahie anguko la mtu, usiwe chanzo cha kumkwamisha mtu fulani kimaendeleo. Usichukie mafanikio ya watu, sababu kufanikiwa kwao hakuwezi kukuzuia wewe usifanikiwe. Anga ni pana na inatosha kwa kila ndege kupaa kivyake.
7. Ishi na watu kwa moyo wa huruma na upendo, wasaidie watu hadi ambao unajua hawawezi kukusaidia wewe. Mara zote binadamu huwahi kusahau wema, ila Mungu kamwe hawezi sahau.
8. Nyuma ya kila mtu unaemjua kuna mtu usiemjua. Hivyo usijiaminishe kwamba unamjua sana mtu fulani, hapana humjui ila unajua yale aliyokuruhusu uyajue tu. Kuwa makini.
9. Mpambanie mtu anaekupenda ila kamwe usithubutu kumpambania mtu ili akupende. Utaumia.
10. Usiwachukie watu sababu ya maneno ya kuambiwa wala usithubutu kuwaamini watu kutokana na maneno yao. Mara nyingi binadamu hudanganya na asipodanganya basi hunena bila kufikiri.
Baada ya hapo nitakuwa huru kufa !!
"The author is dead"
Amani Dimile aliandika
#amanidimile #fikrazadimile #misemoyahekima #hekimayadimile #tusomevitabu #swahilicaption