Ningejifunza haya kabla ya kufika 30

Ningejifunza haya kabla ya kufika 30

Dr leader

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2016
Posts
1,080
Reaction score
1,448
MAMBO 6 NINGEJIFUNZA KABLA YA KUFIKA MIAKA 30

NAMBA 1

Mwanamke anayekupenda kwa dhati, huwa tayari kubadilika kwa ajili yako.
Atarekebisha tabia yake, sauti yake, mienendo yake na kila kitu kinachoweza kuhatarisha kukupoteza.
Mapenzi ya kweli huambatana na jitihada za kulinda uhusiano.

NAMBA 2

Kama mwanaume, epuka kujionyesha.
Jifanye huna pesa hata kama mifuko yako imejaa fedha.
Watu wengi hubadilika wanapoona mafanikio yako, na si kila anayekusogelea ana nia njema.
Unyenyekevu hukulinda zaidi kuliko kujionyesha.

NAMBA 3

Katika kizazi hiki, wanaume wenye nia safi hupitia changamoto kubwa sana.

Ukweli, uaminifu na moyo wa dhati mara nyingi havithaminiwi kama zamani.

Lakini usibadili utu wako kwa sababu ya dunia iliyobadilika.

NAMBA 4

Wewe ni mwanaume.

Asilimia kubwa ya mawazo yako inapaswa kuelekezwa kwenye:

Kutafuta pesa

Kuinua maisha yako

Kujenga future yako

Kutengeneza heshima yako

Sio kutumia muda mwingi kuwaza nani hakukusalimii au nani haongei na wewe.

Mwanaume mwenye malengo makubwa huwa bize kujijenga.

NAMBA 5

Usiwe mchoyo unapowekeza kwenye maisha yako mwenyewe.

Vaa nguo zenye ubora

Fanya mazoezi

Soma vitabu bora

Jifunze kwa watu sahihi

Kula chakula bora

Uwekezaji wa bei rahisi mara nyingi huleta matokeo ya bei rahisi.
Maisha bora yanahitaji kiwango bora.

NAMBA 6

Kata mahusiano na mtu yeyote anayekudanganya, anayekudharau, anayekutumia au anayekufanyia mzaha wa kukuumiza.

Hata kama ni rafiki wa karibu au ndugu.

Amani yako ya akili ni muhimu kuliko kulazimisha mahusiano yasiyo na heshima.

Maisha humfundisha mwanaume kupitia maumivu, makosa na experience.

Lakini mwanaume mwenye hekima hujifunza mapema kabla maisha hayajamlazimisha kwa nguvu.

Abuuabdillah ✍️
0744 883 353
 
Unaona una watu kumbe watu wanaona pesa zako furia ujue hilo, unampenda mtu tu vizuri ye tena ana ona kama vile huna pa kwenda eboo, Chali ntemee ati!!!!!, unawekeza sana Kwa watu mpaka kununua suruali mpya inakushinda, kisa unahudumia sijui demu, rafiki, ndugu aaah big noooo, chapa kulee
 
Inategemea na economic status ya Huyo mwenye 30
Huwezi kupata utariji kwenye 20' then ukifika 30' Ndo uanze kuboronga Lisa Huo umri
 
Sio bahati mbaya teenager ana behave kama teenager, under 30 ana behave kama under 30,40s anabehave kama 40s. Ni nature.
 
Tatizo halipo Kwa binadamu mwingine, tatizo lipo kwako. Badili mfumo wa maisha yako, usiweze ku attract scenario hizo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom