Thanx to mobile tracker,found back my phone

Thanx to mobile tracker,found back my phone

Paul S.S

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2009
Posts
6,408
Reaction score
3,269
Wakuu juzi kati nilikuwa natoka kupata kilaji nikapata kaajali mitaa ya magomeni kama saa 5 usiku hivi, katika kurupushani ya ajali nikatoka nje ya gari kwa bahati mbaya nikasahau kulock milango wahuni wakajisevia LG yangu.

Kesho yake majira ya saa 2 usiku ikaingia sms kwa no yangu nyingine na kwa waifu, ina inasema simu ime no xxxxxx inatumiwa na simu no xxxxx, nikashtuka kuja kukumbuka kumbe niliset mobile tracker siku nyingi nilipo inunua kiasi kwamba nilisahau kabisa hiyo maneno.

Kwakuwa ilikuwa ni no ya voda nikatumia trick ya kujua jina lake kwa kumtumia MPESA kwa kuweka kiwango kikubwa ambacho simu yako haina, kisha ikaleta sms kuwa "huna pesa ya kutosha kumtumia xxxxxxx sh kadhaa", jina la kike

Bila kukawia nikaipiga ile no fasta,akapokea mdada, nikamwambia wewe ndio fulani, akasema yes nikamwambia hiyo simu imeibiwa na kwa usalama wake airudishe haraka, akakata simu na haikupatikana tena
kesho yake saa 4 asbh akaweka line ya tigo meseji ikaingia, nikampigia nikachimba biti akakata simu, siku nzima akawa hapoke simu nikawa natuma sms za mikwara, akazima simu.

Keshokutwa yake akaweka line ya airtel kitendo bila kuchelewa nikampigia, ilibidi awe mdogo tu na akanambia kweli simu kapewa na basha wake na akaomba suluhu nisimfikishe mbali ila hataki kuonana na mimi naweza kuwa na polisi hivyo tukakubaliana aipeleke baa fulani kaunta, akafanya hivyo, akaipeleka kwanza kisha akanipigia nikaenda nikaikuta kaunta.Ila biti nililomchimba lilikuwa sio la kitoto,

Chakusikitisha ni kuwa nilipo kwenda vodacom kuifunga no yangu ilikuwa na muda wa kutosha wa hewani mwizi wangu akajihamishia lakini Voda walishindwa kunisaidia kumtrace mwizi wangu wakanipa mlolongo mgumu na kunishauri bora kununua nyingine
 
mkuu maelezo yako yanamake sense kwani unaset vipi mobile tracker maana mimi nimeibiwa simu yangu hivi karibuni lkn sikuweza kuipata
msaada tafadhali
 
mkuu maelezo yako yanamake sense kwani unaset vipi mobile tracker maana mimi nimeibiwa simu yangu hivi karibuni lkn sikuweza kuipata
msaada tafadhali
Mkuu nadhani LG zote zinakuja na hii application toka kiwandani, Sio simu zote zinakuja na hii appl, inabidi kutafuta za kudownload lakini ni za kulipia, labda tusubiri wataalamu watudadafulie zaidi, maana hata mimi nakumbuka sikumoja wakati naipekua pejua simu yangu ndio nikakutana na hii kitu kwenye security. nikaweka tu bila kujua kama inaumuhimu kihivyo
 
Duh hii kali
je huo mkwara unaweza kutumwagia hapa labda na sisi tutauhitaji siku hiyo....
 
wakuu sim zote za samsung zina izo program ni nzuri sana.
 
mkuu maelezo yako yanamake sense kwani unaset vipi mobile tracker maana mimi nimeibiwa simu yangu hivi karibuni lkn sikuweza kuipata <br />
msaada tafadhali
Unaweza kudownload free NetQin ktk simu yako na ukapata huduma hiyo bureee! Mi nimeweka na iko poa. Ila usisahau kuleta matokeo na senkyu (hasa kwa PM) ukifanikiwa... Senkyu.
 
Duh hii kali
je huo mkwara unaweza kutumwagia hapa labda na sisi tutauhitaji siku hiyo....
Mkuu kwanza nili take advantage kwa yeye kutojua najuaje kila sim card anayoweka? nikamwambia hiyo ni simu maalumu kwa kazi za ofisini hivyo hata afanye nini nitajua killa anachofanya inamitambo maalumu.

nikamwambia kuwa nakwenda voda na kitu cha kwanza voda wanablock namba za watu wake wote wa karibu anaowasiliana nao na watakapo kwenda voda watashikiliwa hadi wakutaje, hivyo asishangae anakuja gugongewa mlango usiku mkali.

Pia nilimwambia hiyo simu iliibiwa na Milion kadhaa na laptop nk hivyo atakapo kamatwa asinilaumu kwani nampa muda uirudishe mwenyewe vinginevyo kesi itakuwa yake.

Mkuu mara ya mwisho alikuwa mdogo pengine alidhani mimi mchawi, aliniomba msamaha sana na kunisihi nisimripoti ndugu zake watapata usumbufu na kujua yeye mwizi na tapeli



 
Duh...but angekuwa ana knowledge na nizi tknoloji
ingekuwa ngumu naona...
 
Lukenza, hii sio advertisement ya LG?
FF umenifurahisha sana, is it sound like advertisement?
Simu nyingi sana zina hiyo maneno, huwezi amini baada ya tukio hilo nikaanza kukaguwa simu zangu zingine sijaziona nimekuja kuikuta hiyo appl ipo kwenye simu ya nyumbani vodafone 150 ingawa yenye unaingiza no moja tu.

By the way kama nitangazo basi mimi ni mbunifu mzuri teh teh teh
 
Duh...but angekuwa ana knowledge na nizi tknoloji
ingekuwa ngumu naona...
Sijajua bado kama ukiflash simu au kuifanyia hard reset kama inafuta hiyo maneno, ngoja nijaribu ku google.
Lakini kwa waTz tulio wengi akili yetu huwa ni kutoa line na kuweka nyingine na kisha anafuta phone book anajua kamaliza mchezo.

Lakini hebu nikuulize mkuu mfano ikatokea mtu kakuuzia simu na baada ya kuweka simcard yako unakutana na mkasa huu je utairudisha? kumbuka umesajili no yako, assume huwezi kumpata aliye kuuzia
 
sijajua bado kama ukiflash simu au kuifanyia hard reset kama inafuta hiyo maneno, ngoja nijaribu ku google.
Lakini kwa watz tulio wengi akili yetu huwa ni kutoa line na kuweka nyingine na kisha anafuta phone book anajua kamaliza mchezo.

Lakini hebu nikuulize mkuu mfano ikatokea mtu kakuuzia simu na baada ya kuweka simcard yako unakutana na mkasa huu je utairudisha? Kumbuka umesajili no yako, assume huwezi kumpata aliye kuuzia

kama nimeinunua kwa bei mbaya.nitaizima kwa muda kwanza
au kumuuzia mwingine.....lol
 
Wakuu juzi kati nilikuwa natoka kupata kilaji nikapata kaajali mitaa ya magomeni kama saa 5 usiku hivi, katika kurupushani ya ajali nikatoka nje ya gari kwa bahati mbaya nikasahau kulock milango wahuni wakajisevia LG yangu.

Kesho yake majira ya saa 2 usiku ikaingia sms kwa no yangu nyingine na kwa waifu, ina inasema simu ime no xxxxxx inatumiwa na simu no xxxxx, nikashtuka kuja kukumbuka kumbe niliset mobile tracker siku nyingi nilipo inunua kiasi kwamba nilisahau kabisa hiyo maneno.

Kwakuwa ilikuwa ni no ya voda nikatumia trick ya kujua jina lake kwa kumtumia MPESA kwa kuweka kiwango kikubwa ambacho simu yako haina, kisha ikaleta sms kuwa "huna pesa ya kutosha kumtumia xxxxxxx sh kadhaa", jina la kike

Bila kukawia nikaipiga ile no fasta,akapokea mdada, nikamwambia wewe ndio fulani, akasema yes nikamwambia hiyo simu imeibiwa na kwa usalama wake airudishe haraka, akakata simu na haikupatikana tena
kesho yake saa 4 asbh akaweka line ya tigo meseji ikaingia, nikampigia nikachimba biti akakata simu, siku nzima akawa hapoke simu nikawa natuma sms za mikwara, akazima simu.

Keshokutwa yake akaweka line ya airtel kitendo bila kuchelewa nikampigia, ilibidi awe mdogo tu na akanambia kweli simu kapewa na basha wake na akaomba suluhu nisimfikishe mbali ila hataki kuonana na mimi naweza kuwa na polisi hivyo tukakubaliana aipeleke baa fulani kaunta, akafanya hivyo, akaipeleka kwanza kisha akanipigia nikaenda nikaikuta kaunta.Ila biti nililomchimba lilikuwa sio la kitoto,

Chakusikitisha ni kuwa nilipo kwenda vodacom kuifunga no yangu ilikuwa na muda wa kutosha wa hewani mwizi wangu akajihamishia lakini Voda walishindwa kunisaidia kumtrace mwizi wangu wakanipa mlolongo mgumu na kunishauri bora kununua nyingine
mobile tracker ni kweli kabisa inafanya hivyo, sio story.. kwenye simu zingine kama Nokia, BlackBerry, Iphone na Android os userphones hizo applications unaweza kuziweka manually..mfano hiyo niliyoAttatch hapo chini ni ya symbian s60v3 & v5, ya BlackBerry inaitwa PHONEBAK2U Anti-Theft, Iphone ipo iLocalis Anti-theft, Anti-Theft + GPS Security alarm na AntiDroid Theft kwaajili ya Android..zinapatikana kwenye forums mbalimbali kwenye internet na pia Apps stores'..
 

Attachments

nilisha ona jamaa wanauza hiyo software ya kulinda simu, nikapuuza.
Nikiona tena na mimi ntainunua ili kuilinda Siemen yangu C25 Twanga Pepeta
 
Mkuu Paulss Asante sana kwa sredi yako. Kweli hapa tunajifunza vitu vingi sana ambavyo tulikua hatuvijui kabla. Sasa hivi na mimi naweka kwenye Nokia zangu E61i na E 7 .
Thank you!
 
Mkuu Paulss Asante sana kwa sredi yako. Kweli hapa tunajifunza vitu vingi sana ambavyo tulikua hatuvijui kabla. Sasa hivi na mimi naweka kwenye Nokia zangu E61i na E 7 .
Thank you!
Mkuu inasaidia sana wakati mwingine.
Lakini kinacho niudhi mimi ni kuwa hivi hawa service provider wetu Voda,Tigo, Airtel nk wanashindwaje kujiorganise na kublock simu zote zitakazo ibiwa kwa imei no?

Kama handset yenyewe inaweza kuripoti kuwa inatumiwa na no gani je itakuwa kwa hawa provider? inatakiwa ukiibiwa simu unakwenda kuripoti kisha provider wote wanaiblock hiyo imei na simu ina kuwa useless labda akaiuze nje ya nchi hii ingepunguza wizi wa simu.

Kingine ni mlolongo wa ugumu kutaka hata ku trace namba alizopiga au kujihamishia salio kabla hajatoa simcard yako, yaani yule mdada wa Voda alinipa mlolongo mgumu nikatamani kumnasa vibao, akaishia kunishauri eti bora ninunue nyingine.

Mimi naona issue ni rahisi kama wakijipanga wenzetu mbele huwezi iba simu ya mtu ukathubutu kuitumia kwa kuweka simcard yako watakupata dakika sifuri, wana deal na watuwako wa karibu unaowasiliana nao mara kwa mara, na hapa swala la usajili ndio umuhimu wake unapokuja
 
ngoja niiseti ktk simu yangu na ya waifu
 
ngoja niiseti ktk simu yangu, na add namba yangu na ya waifu.
Bravo Paulss
 
Back
Top Bottom