Wakuu juzi kati nilikuwa natoka kupata kilaji nikapata kaajali mitaa ya magomeni kama saa 5 usiku hivi, katika kurupushani ya ajali nikatoka nje ya gari kwa bahati mbaya nikasahau kulock milango wahuni wakajisevia LG yangu.
Kesho yake majira ya saa 2 usiku ikaingia sms kwa no yangu nyingine na kwa waifu, ina inasema simu ime no xxxxxx inatumiwa na simu no xxxxx, nikashtuka kuja kukumbuka kumbe niliset mobile tracker siku nyingi nilipo inunua kiasi kwamba nilisahau kabisa hiyo maneno.
Kwakuwa ilikuwa ni no ya voda nikatumia trick ya kujua jina lake kwa kumtumia MPESA kwa kuweka kiwango kikubwa ambacho simu yako haina, kisha ikaleta sms kuwa "huna pesa ya kutosha kumtumia xxxxxxx sh kadhaa", jina la kike
Bila kukawia nikaipiga ile no fasta,akapokea mdada, nikamwambia wewe ndio fulani, akasema yes nikamwambia hiyo simu imeibiwa na kwa usalama wake airudishe haraka, akakata simu na haikupatikana tena
kesho yake saa 4 asbh akaweka line ya tigo meseji ikaingia, nikampigia nikachimba biti akakata simu, siku nzima akawa hapoke simu nikawa natuma sms za mikwara, akazima simu.
Keshokutwa yake akaweka line ya airtel kitendo bila kuchelewa nikampigia, ilibidi awe mdogo tu na akanambia kweli simu kapewa na basha wake na akaomba suluhu nisimfikishe mbali ila hataki kuonana na mimi naweza kuwa na polisi hivyo tukakubaliana aipeleke baa fulani kaunta, akafanya hivyo, akaipeleka kwanza kisha akanipigia nikaenda nikaikuta kaunta.Ila biti nililomchimba lilikuwa sio la kitoto,
Chakusikitisha ni kuwa nilipo kwenda vodacom kuifunga no yangu ilikuwa na muda wa kutosha wa hewani mwizi wangu akajihamishia lakini Voda walishindwa kunisaidia kumtrace mwizi wangu wakanipa mlolongo mgumu na kunishauri bora kununua nyingine
Kesho yake majira ya saa 2 usiku ikaingia sms kwa no yangu nyingine na kwa waifu, ina inasema simu ime no xxxxxx inatumiwa na simu no xxxxx, nikashtuka kuja kukumbuka kumbe niliset mobile tracker siku nyingi nilipo inunua kiasi kwamba nilisahau kabisa hiyo maneno.
Kwakuwa ilikuwa ni no ya voda nikatumia trick ya kujua jina lake kwa kumtumia MPESA kwa kuweka kiwango kikubwa ambacho simu yako haina, kisha ikaleta sms kuwa "huna pesa ya kutosha kumtumia xxxxxxx sh kadhaa", jina la kike
Bila kukawia nikaipiga ile no fasta,akapokea mdada, nikamwambia wewe ndio fulani, akasema yes nikamwambia hiyo simu imeibiwa na kwa usalama wake airudishe haraka, akakata simu na haikupatikana tena
kesho yake saa 4 asbh akaweka line ya tigo meseji ikaingia, nikampigia nikachimba biti akakata simu, siku nzima akawa hapoke simu nikawa natuma sms za mikwara, akazima simu.
Keshokutwa yake akaweka line ya airtel kitendo bila kuchelewa nikampigia, ilibidi awe mdogo tu na akanambia kweli simu kapewa na basha wake na akaomba suluhu nisimfikishe mbali ila hataki kuonana na mimi naweza kuwa na polisi hivyo tukakubaliana aipeleke baa fulani kaunta, akafanya hivyo, akaipeleka kwanza kisha akanipigia nikaenda nikaikuta kaunta.Ila biti nililomchimba lilikuwa sio la kitoto,
Chakusikitisha ni kuwa nilipo kwenda vodacom kuifunga no yangu ilikuwa na muda wa kutosha wa hewani mwizi wangu akajihamishia lakini Voda walishindwa kunisaidia kumtrace mwizi wangu wakanipa mlolongo mgumu na kunishauri bora kununua nyingine