TFF hii inaiimarisha Yanga kwa uonevu

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,315
12,614
Mashabiki wa Simba wamempiga shabiki wa Yanga uwanjani lakini TFF haikutoa adhabu kwa Simba badala yake imewatafuta waliompiga TU na kuwapa adhabu hao tu. Kwa timu nyingine TFF haitafuti mashibiki wao waliokosea uwanjani badala yake wanatoa adhabu kwa timu nzima kwa makosa ya mashabiki wao wawili waliorudha chupa za maji uwanjani, double standard. Je, itaendelea na zoezi la kuwatafuta na kuwaadhibu mashabiki wa timu wanaokosea badala ya kuziadhibu timu kwa makosa ya mashabiki wao?

Angalia adhabu iliyopewa Simba kwa wachezaji kuchelewesha kuanza kwa mechi na matangazo ya mdhammi kwa kuchelewa kufika uwanjani kwa wakati ni sh. 1m TU, lakini Yanga kupitia mlango mwingine ni 5mil. Nani kafanya kosa kubwa kati ya Simba aliyechelewesha mchezo kuanza na matangazo ya mdhammi na Yanga aliyepitia mlango mwingine kuingia na kufika uwanjani kwa wakati?. Nani kasababisha hasara na usumbufu mkubwa kati ya hawa wawili? Nani alistahili adhabu kubwa kuliko mwingine?

Adhabu ya Halid Aucho ya kumfungia mechi 3 bila kumuadhibu Ajib kama vile hawakuona alichomfanyia Aucho ni dalili ya TFF kuikataa Yanga uwanjani. Kumfungia mechi tatu!!!!

Mungu Yuko pamoja na kila anaeonewa na kudhulumiwa, wanaipaka mafuta Yanga izidi kupaa kimataifa, inakomazwa na TFF kwaajili ya mashindano ya ndani na nje ya nchi. Hata mama anaemnyanyasa house girl na kumpendelea mwanawe ajue anampaka mafuta yule house girl na kumpaka mavi usoni mwanawe. TFF inawapaka mavi usoni Simba, coastal Union na Ibrahim Ajib badala ya kuwasaidia kukua.

Oneni aibu.
 
Mashabiki wa Simba wamempiga shabiki wa Yanga uwanjani lakini TFF haikutoa adhabu kwa Simba badala yake imewatafuta waliompiga TU na kuwapa adhabu hao tu. Kwa timu nyingine TFF haitafuti mashibiki wao waliokosea uwanjani badala yake wanatoa adhabu kwa timu nzima kwa makosa ya mashabiki wao wawili waliorudha chupa za maji avi usoni mwanawe. TFF inawapaka mavi usoni Simba, coastal Union na Ibrahim Ajib badala ya kuwasaidia kukua.

Oneni aibu.
Usimuingize Mungu hapo cha msingi yanga wako njema bado wapambane ili wanaowahujumu waumbuke.
 
Usimuingize Mungu hapo cha msingi yanga wako njema bado wapambane ili wanaowahujumu waumbuke.
Hakuna mafanikio yasiyokuwa na mkono wa Mungu, Wacha upagani. Yanga pamoja na kuwa na vipaji vingi uwanjani lakini haiachi kumpendeza Mungu wao pia. Ndio maana hawaachi kutoa sadaka na kusaidia watu wenye uhitaji kila wakati. Hii ndio Ngao ya kuwakinga na wote wenye Nia mbaya na timu yao
 
Hakuna mafanikio yasiyokuwa na mkono wa Mungu, Wacha upagani. Yanga pamoja na kuwa na vipaji vingi uwanjani lakini haiachi kumpendeza Mungu wao pia. Ndio maana hawaachi kutoa sadaka na kusaidia watu wenye uhitaji kila wakati. Hii ndio Ngao ya kuwakinga na wote wenye Nia mbaya na timu yao
Sawa mshika dini
 
Nguvu ya Yanga tunaiona Sasa, big up Kwa kuweka Uzi mwingine, Hawa TFF chini ya Mr Karai ni wapumbavu sana , lazima tupaze sauti kukemea double standards zao ambazo bila wao kujua zitaiimarisha zaidi Yanga,

Tumeshajua adhabu wanazoipa Yanga kiuonevu lengo lao TFF ni kumpunguza Kasi Eng Hersi ambae Sasa anakaa mezani na kina Motsepe na Rais wa Fifa akiwasalimia Kwa 5G na sio matopeni karume!

Yanga ikate rufaa BMT , CCM, Kwa Waziri wa Michezo , Fifa , Kwa Mwananchi Kikwete na Mama Samia maana kiukweli Aucho ndie roho ya Yanga katikati na ameonewa mbona wachezaji wengine wakiadhibiwa na refa imetosha TFF wanatulia kwanini Aucho tu ndo aongezewe adhabu? Kama ni hivyo Kila Mchezaji aliepewa kadi aongezewe adhabu na TFF, Ally Kamwe usikubali TFF wanakuharibia kikosi chako Cha ushindi! Nakujua we na Priva ni vijana wenye akili na ni wabishi msiwaachie wale Makolo waliovaa koti la TFF kujinafasi Kwa kumtoa kafara Aucho! Mabango ya 5G yanawauma sana TFF

Yanga tusikubali kuonewa TFF watazoea na siku ingine watafungia timu nzima itacheza Yanga B au Yanga Princess!!

Mpango wao eti Simba mbovu ichukue kombe la ligi na tayari umebuma pengo la points linakua na timu ndogo kama Namungo zimekaza Simba haitotoboa tuko paleeee!!

Refa aliechezesha kihalali mechi Simba vs Namungo atapewa shavu Afcon sio wengine marefa kama Singapore Big Stars vs Simba marefa wajinga wanaibeba Simba mbovu na CAF haina shida nao!
 
Usimuingize Mungu hapo cha msingi yanga wako njema bado wapambane ili wanaowahujumu waumbuke.
Kbsaaaa asiingizee mambo yake mungu kwa kuwa timu inatumia na kuamini ushirikina. Alfu ajabu eti wawapo uwanjanj unawaona wakipinga magoti Tena kumlilia na kumuomba mungu ..mm huwa sielewi kbsaa mambo ya kishirikina wkt huo huo Bado mnaenda kumuomba mungu awafushe


Kwa kifupi Sana kuwa hao wachezaji wache tabia za kilozi
 
Kbsaaaa asiingizee mambo yake mungu kwa kuwa timu inatumia na kuamini ushirikina. Alfu ajabu eti wawapo uwanjanj unawaona wakipinga magoti Tena kumlilia na kumuomba mungu ..mm huwa sielewi kbsaa mambo ya kishirikina wkt huo huo Bado mnaenda kumuomba mungu awafushe


Kwa kifupi Sana kuwa hao wachezaji wache tabia za kilozi
Hahaha watakuja wakuambie hata mchawi humuomba mungu 😂😂😂
 
Kbsaaaa asiingizee mambo yake mungu kwa kuwa timu inatumia na kuamini ushirikina. Alfu ajabu eti wawapo uwanjanj unawaona wakipinga magoti Tena kumlilia na kumuomba mungu ..mm huwa sielewi kbsaa mambo ya kishirikina wkt huo huo Bado mnaenda kumuomba mungu awafushe


Kwa kifupi Sana kuwa hao wachezaji wache tabia za kilozi
Yanga haijawahi kuwasha moto uwanjani na Wala kupulizia dawa watu vyumbani. Kama timu inaweza kuwasha moto katikati ya uwanja wa nchi ya nje je, kwenye uwanja wa nyumbani, kwaMkapa inafanya nini? Na je, itakuwaje kama ikimiliki uwanja wake yenyewe kama vile Azam? Uwanja huo utanuka tunguli kila mahali.
 
Mnapenda kulalamika, ngoja nikukumbushe.
Kuna mashabiki wa Simba walivamiwa na kupigwa na washabiki wa yanga morogoro hao washabiki walipewa adhabu gani?
Yanga imeshaadhibiwa Mara ngapi kwa kosa la kupita mlango usiotakiwa, je wamejirekebisha?
Msimu uliopita Aziz K na Chama waliofungiwa mechi tatu na kutozwa faini kwa kosa la kutetea kuingia uwanjani lakini Mdathir na Feitoto wamefanya kosa lilelile kwanini hawakupewa adhabu waliyopewa Aziz K na Chama au kwa sababu wakijua angekosa mechi ya Simba na yanga. Nyinyi ndio mnasababisha hizi timu ziendelee kutumia ushirikina badala ya kukemea mnaziunga mkono.
 
Nguvu ya Yanga tunaiona Sasa, big up Kwa kuweka Uzi mwingine, Hawa TFF chini ya Mr Karai ni wapumbavu sana , lazima tupaze sauti kukemea double standards zao ambazo bila wao kujua zitaiimarisha zaidi Yanga,

Tumeshajua adhabu wanazoipa Yanga kiuonevu lengo lao TFF ni kumpunguza Kasi Eng Hersi ambae Sasa anakaa mezani na kina Motsepe na Rais wa Fifa akiwasalimia Kwa 5G na sio matopeni karume!

Yanga ikate rufaa BMT , CCM, Kwa Waziri wa Michezo , Fifa , Kwa Mwananchi Kikwete na Mama Samia maana kiukweli Aucho ndie roho ya Yanga katikati na ameonewa mbona wachezaji wengine wakiadhibiwa na refa imetosha TFF wanatulia kwanini Aucho tu ndo aongezewe adhabu? Kama ni hivyo Kila Mchezaji aliepewa kadi aongezewe adhabu na TFF, Ally Kamwe usikubali TFF wanakuharibia kikosi chako Cha ushindi! Nakujua we na Priva ni vijana wenye akili na ni wabishi msiwaachie wale Makolo waliovaa koti la TFF kujinafasi Kwa kumtoa kafara Aucho! Mabango ya 5G yanawauma sana TFF

Yanga tusikubali kuonewa TFF watazoea na siku ingine watafungia timu nzima itacheza Yanga B au Yanga Princess!!

Mpango wao eti Simba mbovu ichukue kombe la ligi na tayari umebuma pengo la points linakua na timu ndogo kama Namungo zimekaza Simba haitotoboa tuko paleeee!!

Refa aliechezesha kihalali mechi Simba vs Namungo atapewa shavu Afcon sio wengine marefa kama Singapore Big Stars vs Simba marefa wajinga wanaibeba Simba mbovu na CAF haina shida nao!
Daah!! Nyerere alisema maadui watatu nchi hii ni ujinga, maradhi na umaskini! Kwa maandishi yako haya,wewe ni mjinga na ni masikini, nina uhakika wa asilimia tisini.
Huna maisha ya maana na pia huna elimu ya maana pole sana.
 
Mnapenda kulalamika, ngoja nikukumbushe.
Kuna mashabiki wa Simba walivamiwa na kupigwa na washabiki wa yanga morogoro hao washabiki walipewa adhabu gani?
Yanga imeshaadhibiwa Mara ngapi kwa kosa la kupita mlango usiotakiwa, je wamejirekebisha?
Msimu uliopita Aziz K na Chama waliofungiwa mechi tatu na kutozwa faini kwa kosa la kutetea kuingia uwanjani lakini Mdathir na Feitoto wamefanya kosa lilelile kwanini hawakupewa adhabu waliyopewa Aziz K na Chama au kwa sababu wakijua angekosa mechi ya Simba na yanga. Nyinyi ndio mnasababisha hizi timu ziendelee kutumia ushirikina badala ya kukemea mnaziunga mkono.
Hivi wewe na TFF bado mnaamini ushirikina kwenye mpira wa miguu? Yanga ya sasa wameshavuka huko ndio maana inasogea kwa kasi kuliko Ile Yanga ya akina Tabu Mangala.
 
Hivi wewe na TFF bado mnaamini ushirikina kwenye mpira wa miguu? Yanga ya sasa wameshavuka huko ndio maana inasogea kwa kasi kuliko Ile Yanga ya akina Tabu Mangala.
Sababu gani walipitia mlango usio rasmi. Ndio maana wanasema huko wenye akili ni wawili.
 
Sababu gani walipitia mlango usio rasmi. Ndio maana wanasema huko wenye akili ni wawili.
Ni psychological war (vita ya kisaikolojia TU) brother, nothing more, Yanga imesajili vizuri, Ina bench la ufundi safi na uongozi Bora, nothing more nothing less. Uchawi hauna nafasi, na TFF wataukuza kama watakuwa wanautaja kila wakati. Simba waliwasha moto uwanjani na kufungwa mechi pia. Kama uchawi ingekuwa unasaidia basi Nigeria ingekuwa bingwa wa dunia. Tiwache kuukuza uchawi bali tupambane na madawa ya kulevya, kusisimua misuli na Yale yanayolegeza misuli ya wachezaji wa timu pinzani yasitumiwe. Mbona hawawakatazi wale mashabiki wanaoingia na vikapu, njiwa, mchele na vItochi uwanjani?
 
Back
Top Bottom