Tetesi za kuachwa loemba na siasa za Mo

Tetesi za kuachwa loemba na siasa za Mo

rodrick alexander

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2012
Posts
18,070
Reaction score
25,745
Baada ya usajili wa dirisha dogo miongoni mwa watu waliosifiwa ni Jayrutu hasa kwa kumsajili Inno Loemba. Sifa hizi zilimfanya hadi mwenyekiti wa bodi ya Simba Magori kutoka na kuongea na waandishi wa habari, kuwaambia yule mchezaji kasajiliwa na Simba.

Wakati huo tajiri anayependa kususa timu ikifanya vibaya akarudi kwa kasi baada ya kuona mwelekeo wa timu umebadilika, akatoa picha anamsainisha mkataba Mpanzu na juzijuzi katembelea timu na kuwaahiidi bilioni 1 wakitwaa ubingwa.

Pia dada yake naye ameonekana akienda kuitembelea timu wakati timu inafanya vibaya walikuwa wamejitenga. Sasa hivi kuna wachambuzi na watu wanaolipwa mtandaoni wameanza kutengeneza propaganda kuhusu ubora wa Inno Loemba makusudi aachwe ili mradi mo hapendi mtu mwingine apate sifa zaidi yake.

Timu ikifanya vizuri sifa ziende kwake ila timu ikifanya vibaya alaumiwe Mangungu na sasa hivi Jayruty alikuwa anasifiwa usajili wa dirisha dogo kitu ambacho kinamuuma.
 
Loemba kuachwa Simba ni yeye mwenyewe na miguu yake ndiyo ataamua na wala sio kiongozi au mtu mwingine yoyote yule. Loemba ni bonge la mchezaji na hilo amelithibitsha yeye mwenyewe na miguu yake mara tu alipofika Simba. Mechi za mwanzo za ligi ya nyumbani na hata za kimataifa kacheza vizuri sana kama "play maker" pale katikati lakini sijui ni ushamba au kulewa sifa mpira mkubwa wote aliouonyeshwa mwanzo umeyeyuka. Baada tu yakupewa zawadi ya gari basi akarudi kuwa mchezaji wa kawaida sana. Kama ligi ingekuwa inaisha leo nina hakika kabisa wanachama na mashabiki wa Simba wakiambiwa Loemba anaachwa wala wasingeshtuka.

Kikubwa mtu aliye karibu amshtue kuwa mechi zilizobaki ni chache sana na yeye mpira anajua sana tu na hilo halina shaka kwa mtu yoyote aliyemuona mwanzoni; basi aache tu masihara na "show off" uwanjani badala yake arudi afanye kazi kama mwanzoni alivyofika. Pia akinyang'anywa mpira katikati ya uwanja aache kukaba kwa macho na kusimama badala yake awe anamkimbiza adui kumkaba au kumpa presha. Akijirekebisha akarudi vizuri nina hakika hata mashabiki wa Simba wakisikia anaachwa basi watakufa na viongozi na wala hakuna kiongozi atakayejaribu kufanya hivyo.

Ni mtizamo tu.
 
Loemba kuachwa Simba ni yeye mwenyewe na miguu yake ndiyo ataamua na wala sio kiongozi au mtu mwingine yoyote yule. Loemba ni bonge la mchezaji na hilo amelithibitsha yeye mwenyewe na miguu yake mara tu alipofika Simba. Mechi za mwanzo za ligi ya nyumbani na hata za kimataifa kacheza vizuri sana kama "play maker" pale katikati lakini sijui ni ushamba au kulewa sifa mpira mkubwa wote aliouonyeshwa mwanzo umeyeyuka. Baada tu yakupewa zawadi ya gari basi akarudi kuwa mchezaji wa kawaida sana. Kama ligi ingekuwa inaisha leo nina hakika kabisa wanachama na mashabiki wa Simba wakiambiwa Loemba anaachwa wala wasingeshtuka.

Kikubwa mtu aliye karibu amshtue kuwa mechi zilizobaki ni chache sana na yeye mpira anajua sana tu na hilo halina shaka kwa mtu yoyote aliyemuona mwanzoni; basi aache tu masihara na "show off" uwanjani badala yake arudi afanye kazi kama mwanzoni alivyofika. Pia akinyang'anywa mpira katikati ya uwanja aache kukaba kwa macho na kusimama badala yake awe anamkimbiza adui kumkaba au kumpa presha. Akijirekebisha akarudi vizuri nina hakika hata mashabiki wa Simba wakisikia anaachwa basi watakufa na viongozi na wala hakuna kiongozi atakayejaribu kufanya hivyo.

Ni mtizamo tu.
Upo sahihi mkuu...Jamaa ni bonge moja la player.Ana nguvu na pumzi,anakaba,anakokota na ana uwezo wa kusambaza mipira.

Shida:Maamuzi mabovu ya mwisho, kucheza na Jukwaa na kulalamika sana.

Sitashangaa kweli akiachwa maana Mo naye ana utoto sometimes.
 
Upo sahihi mkuu...Jamaa ni bonge moja la player.Ana nguvu na pumzi,anakaba,anakokota na ana uwezo wa kusambaza mipira.

Shida:Maamuzi mabovu ya mwisho, kucheza na Jukwaa na kulalamika sana.

Sitashangaa kweli akiachwa maana Mo naye ana utoto sometimes.
Ni kweli shida ya baadhi ya wachezaji wakisikia mashabiki wanakaanga chipsi jukwaani mabega yanapanda na kifua kinatanuka lakini kiukweli hakuna mashabiki wa hovyo kama wakibongo leo wanakusifia kesho wanaandama kwa viongozi utimuliwe.
 
Baada ya usajili wa dirisha dogo miongoni mwa watu waliosifiwa ni Jayrutu hasa kwa kumsajili Inno Loemba. Sifa hizi zilimfanya hadi mwenyekiti wa bodi ya Simba Magori kutoka na kuongea na waandishi wa habari, kuwaambia yule mchezaji kasajiliwa na Simba.

Wakati huo tajiri anayependa kususa timu ikifanya vibaya akarudi kwa kasi baada ya kuona mwelekeo wa timu umebadilika, akatoa picha anamsainisha mkataba Mpanzu na juzijuzi katembelea timu na kuwaahiidi bilioni 1 wakitwaa ubingwa.

Pia dada yake naye ameonekana akienda kuitembelea timu wakati timu inafanya vibaya walikuwa wamejitenga. Sasa hivi kuna wachambuzi na watu wanaolipwa mtandaoni wameanza kutengeneza propaganda kuhusu ubora wa Inno Loemba makusudi aachwe ili mradi mo hapendi mtu mwingine apate sifa zaidi yake.

Timu ikifanya vizuri sifa ziende kwake ila timu ikifanya vibaya alaumiwe Mangungu na sasa hivi Jayruty alikuwa anasifiwa usajili wa dirisha dogo kitu ambacho kinamuuma.
Kwani wewe unamuonaje Loemba
 
Ningekuwa na maamuzi pale simba wachezaji wa kwanza kuwapa thanks pale simba ni
1. Yule mkongomani winga, anajua mpira sana ila shida yake ni selfshness
2. Yule beki tatu mfupi mtanzania zile back pass mkaa zake zingekutana na waarabu sijui na habadiliki
 
Loemba kwa upande wangu aende tuu. Hata Mpanzu mwenyewe km habadiliki Atupishee.
Aaah.
 
Loemba, Maema na Kante jamaa ni wakawaida sana
 
Mchezaji katoa ya moyoni, hawa vuongozi Simba wanajiona Mungu watu ngoja ligi iishe tupambane.
 
Loemba, Maema na Kante jamaa ni wakawaida sana
Mwingine aliyeharibika ni huyo Kante. Jamaa alipokuja alikuwa akipata mpira anageukia mbele halafu anapiga pasi rula zinavunja safu mbili mpaka tatu za timu pinzani na zinafika kwa usahihi kwa washambuliaji wa Simba. Sasa hivi sijui nani kamloga. Sasa hivi jamaa kawa kituko kila akipata mpira anarudisha "back pass" kwa mabeki wake wakati wakati yeye ni kiungo anatakiwa aendeshe timu iende mbele. Kawa mzito balaa hata kugeuka kwa haraka hawezi tena na akipiga pasi 10 lazima 7 ziwe mkaa. Jamaa anawachomesha sana Simba pale kati sema tu wale mabeki wa kati ndio huwa wanaua soo. Mwanzoni alipofika alikuwa anapokonya mipira kwa akili sana kwa kutumumia lile umbo lake vizuri lakini siku hizi anachojua ni kupokonya mipira kwa rafu tena za kijinga kabisa. Na wakati mwingine huwa hata simuelwi kabisa kwani huwa anatafuta kadi kwa matukio ya ajabu ajabu ambaya hayana hata faida kwa timu.
 
Mwingine aliyeharibika ni huyo Kante. Jamaa alipokuja alikuwa akipata mpira anageukia mbele halafu anapiga pasi rula zinavunja safu mbili mpaka tatu za timu pinzani na zinafika kwa usahihi kwa washambuliaji wa Simba. Sasa hivi sijui nani kamloga. Sasa hivi jamaa kawa kituko kila akipata mpira anarudisha "back pass" kwa mabeki wake wakati wakati yeye ni kiungo anatakiwa aendeshe timu iende mbele. Kawa mzito balaa hata kugeuka kwa haraka hawezi tena na akipiga pasi 10 lazima 7 ziwe mkaa. Jamaa anawachomesha sana Simba pale kati sema tu wale mabeki wa kati ndio huwa wanaua soo. Mwanzoni alipofika alikuwa anapokonya mipira kwa akili sana kwa kutumumia lile umbo lake vizuri lakini siku hizi anachojua ni kupokonya mipira kwa rafu tena za kijinga kabisa. Na wakati mwingine huwa hata simuelwi kabisa kwani huwa anatafuta kadi kwa matukio ya ajabu ajabu ambaya hayana hata faida kwa timu.
Kuna tatizo Simba wanapenda sana kupiga back pass na hili nimeliona hata kwa timu za waafrika world cup, inawezekana ni mafunzo wanayopewa makosa lakini hili limechangia Simba kutolewa mashindano ya Afrika na aliyesababisha ni huyohuyo Kante, Kibabage naye alitaka kuchomesha na kagoma anataka awe wa kwanza kupasiwa lakini option yake ni kurudisha nyuma Duchu naye hivyohivyo. Unakuta timu imevuka katikati ya uwanja wanarudisha pasi nyuma tatizo linaanzia kwenye benchi la ufundi.
 
Back
Top Bottom