Chris!, mbona huna utalivu wa akili!..inaonyesha wewe unashabikia kupigwa na kuteswa wananchi wa Mtwara kwa kosa la kuhoji juu ya hatima ya rasilimali zao?. Waonee huruma watanzania wenzako, hii serikali unayoishabikia inatarajiwa ku ekspaya hivi karibuni lakini wa wananchi wa mtwara waataendelea kuwepo juu ya ardhi yenye hizo rasilimali.
Chris!...nilipo kufahamu mwanzo ulifanana na kijana msomi na mzalendo anayependa mabadiliko chanya kwa nchi yake, nakumbuka ulikuwa ukivaa magwanda ya khaki na hata michango yako ilikuwa chanya kama msomi.
Chris!....toka umejiunga na chama chako hiki kipya, umekuwa kama vile umeondolewa ubongo na kubaki na fuvu tupu!......inasikitisha sana. Hivi kwani ukiwa katika chama chako hicho kipya, ni lazima ufanane na mwigulu?
mkuu hakuna raslimali ya mtwara,popote pale zilipo raslimali za nchi hii ni za watanzani hakuna kuwaonea huruma wahuni,watu wanachoma mpaka nyumba na kuvunja madaraja halafu unasema wahurumiwe kwa kipi.