- Thread starter
- #41
:A S crown-2:
Hapa umeniacha mkuu!
:A S crown-2:
Mungu akupe nguvu kaka na naamini utampata mwanamke bora
Nimekutwa na HIV mwezi wa 11, 2014. Yawezekana nimepata maambukizi katika kipindi kinachoanzia mwezi wa 8, 2014. Nimeogopa na kujitahidi kulinda afya yangu siku zote lakini imeshakuwa hivi.
Sijui imekuwaje nawaza sikustahili hali hii lakini ndio imekuwa. Sijafikiria kuwaambia ndugu au rafiki wa karibu kwa kuogopa kuwaumiza kimawazo zaidi yangu. Kwa sasa nahitaji kukamilisha sehemu ya maisha yangu, kwa kupata mwenza.
Mwenye sifa zifuatazo:
- Muislamu au awe tayari kuwa muislamu.
- Asiwe mtoto, na asiwe anakaribia miaka 40.
- Awe na afya njema , na haijalishi kama ameanza kutumia dawa.
- Awe tayari kuolewa (akinipenda) na kupata watoto.
- Awe anajituma na asiwe na tabia ya uvivu iliyokithiri.
Baadhi ya wasifu wangu:
- Sina mtoto na sijawahi kuoa.
- Ninakazi na elimu ni shahada.
- Ninajitegemea katika maisha ya kawaida, ni msaada kwa baadhi ya ndugu zangu na, ni mchapa kazi na mpenda maendeleo.
- Nina miaka 35, lakini watu huniona nina umri mdogo zaidi.
- Umbo la wastani, urefu ni kama sentimeta 165 (5'5"), rangi ni nyeusi kiasi.
Je ulikuwa kwenye mahusiano wakati unapima --just curious if you cared to hint your x? and kitu gani kilifanya upime , uliugua au routine checkup?
Mkuu siku hizi na madawa na vyakula unaweza kuishi miaka mingi sana 20+ so take it as a small challenge ila ukiwa mentally free u will win this battle. Hongera kwa uwazi.
Hongera sana kwa research yako unayoifanya.
Mkuu kwanza nakupongeza sana kwa ujasiri wako. Kwa kipindi hiki cha maendeleo ya tiba kupata HIV sio kufa you can live up to your maximum life span.Ninachokushauri ulichofanya hapa ukifanye kwa watu walio karibu nawe na pia ofisini kwako, hiyo itakujengea hali ya kujiamini hasa unaposikia watu wakinong'ona mambo yao na wewe ukadhani wanakuteta. Pia ofisni watakuelewa na kukupunguzia majukumu na mambo yanayoweza kukuletea stress. Pia kwa mjibu wa sheria ya HIV ya mwaka 2008 kuna malipo ambayo waathirika wote wa HIV hupewa ili kuwasaidia lishe.Nakutakia maisha marefu ya heri , uhuru na mafanikio.
Umenikumbusha jamani kuna mtu mmoja nlimsave soul mate!
Mbona sioni watu wakiomba PM jamani huu ni ugonjwa kama Malaria tuu,BTW bora amejitolea kuwalinda watu kuliko angeamua kuusambaza ovyo tu
Usikate tamaa kijana ebu fikiria kuna watu wenye cancer wanatamani ata wangekuwa na HIV waondokane na maumivu makali yanayowapata.
Vile vile jitahidi najua ni ngumu lakini jitahidi usiwe na huzuni kila wakati kwasababu huzuni itakufanya macho na maskio na fikra kutafanya kazi kwa ufanishi.
Wishing you all the best
Pole saana! Njoo kanisani hapa kuna watu wanapona HIV mkuu.
Unaweza kushinda hili. Trust me sir.
Regards,
Humble african.
Mkuu kwanza nakupongeza sana kwa ujasiri wako. Kwa kipindi hiki cha maendeleo ya tiba kupata HIV sio kufa you can live up to your maximum life span.Ninachokushauri ulichofanya hapa ukifanye kwa watu walio karibu nawe na pia ofisini kwako, hiyo itakujengea hali ya kujiamini hasa unaposikia watu wakinong'ona mambo yao na wewe ukadhani wanakuteta. Pia ofisni watakuelewa na kukupunguzia majukumu na mambo yanayoweza kukuletea stress. Pia kwa mjibu wa sheria ya HIV ya mwaka 2008 kuna malipo ambayo waathirika wote wa HIV hupewa ili kuwasaidia lishe.Nakutakia maisha marefu ya heri , uhuru na mafanikio.
Asante mkuu. Najua umetumia utani kidogo kuniwekea mambo sawa, lakini naamini watu wanaelewa kuwa malaria ni ugonjwa na hivi ni virusi vinavyoharibu kinga mwilini. Kwa hiyo hili ni tatizo la kipekee na kwangu mimi nafasi ya kumpata ambaye hajaathirika ni kama hakuna. Labda tuwashauri wengine wakapime haraka ili waamue vizuri ikitokea wako +ve au -ve.
Mkuu dhambi ya kuambukiza mtu siiwezi. Kwa bahati mbaya kuna mtu ameanza kuwa karibu yangu kwa kasi and she is okay, inanipa machungu maana najiuliza alikuwa wapi siku zote!!? Namtafutia dawa ya kumkimbia (wisely) awe salama hata kiakili. Nataka kunasihi kuwa tuwe na tahadhari sana, maana sio kila muathirika anaweza kuhurumia wasioathirika. Wengine huweza kutojali na kuambukiza wengine kutokana na maumivu alopata yeye, mwishowe utu wote unamuondoka na kuwa ni kawaida yake kueneza. Nahitaji kuishi maisha ya furaha na kutimiza ndoto zangu; hali hiyo haiwezi kufikiwa kwa kutojali wengine.
Mimi naomba iwe siri yako jamii yetu wote tunaifahamu ukweli ndio huo, ukiwaambia watakusema tu na hata kukutenga kiaina bora iwe siri yako na close family members
Nimekutwa na HIV mwezi wa 11, 2014. Yawezekana nimepata maambukizi katika kipindi kinachoanzia mwezi wa 8, 2014. Nimeogopa na kujitahidi kulinda afya yangu siku zote lakini imeshakuwa hivi.
Sijui imekuwaje nawaza sikustahili hali hii lakini ndio imekuwa. Sijafikiria kuwaambia ndugu au rafiki wa karibu kwa kuogopa kuwaumiza kimawazo zaidi yangu. Kwa sasa nahitaji kukamilisha sehemu ya maisha yangu, kwa kupata mwenza.
Mwenye sifa zifuatazo:
- Muislamu au awe tayari kuwa muislamu.
- Asiwe mtoto, na asiwe anakaribia miaka 40.
- Awe na afya njema , na haijalishi kama ameanza kutumia dawa.
- Awe tayari kuolewa (akinipenda) na kupata watoto.
- Awe anajituma na asiwe na tabia ya uvivu iliyokithiri.
Baadhi ya wasifu wangu:
- Sina mtoto na sijawahi kuoa.
- Ninakazi na elimu ni shahada.
- Ninajitegemea katika maisha ya kawaida, ni msaada kwa baadhi ya ndugu zangu na, ni mchapa kazi na mpenda maendeleo.
- Nina miaka 35, lakini watu huniona nina umri mdogo zaidi.
- Umbo la wastani, urefu ni kama sentimeta 165 (55), rangi ni nyeusi kiasi.
Mkuu haujaeleza jinsi ulivyopata,maana umesema kati ya mwezi wa nane na wa 12,je ulitembea na mtu yeyote hapo kati ya mwezi wa nane na 12?
Kwani njia za kujipatia ukimwi huzijui??