Terminal ya Clouds FM wanapiga kampeni michango ya Harusi.

Terminal ya Clouds FM wanapiga kampeni michango ya Harusi.

Wachaga hawawezi kukuelewa kwao kuchangia Sio swala la hiari ni la lazima utake usitake.Unakuta mwenyekiti anafoka kuwa kima Cha chini hiki hapa utatoa wapi utaiba au vipi lazima utoe
Mimi ni mchaga, kwanini mtu anisumbue wakati sio ndugu yangu?
 
Naunga mkono hoja... ukitaka kuoa jipange...

Michango ya watu siyo lazima...



Cc: mahondaw
 
Ungewapigia simu na kuwasilisha hoja yako kuwapinga
Halo JF.
Nipo hapa Nyumbani nasikiliza Terminal ya clouds FM radio ya jiji la karaha na raha la Dar.

Wanaonekana kupinga michango ya harusi wakidai sio lazima. Wote Haris Kapiga na Vivian Mwasha na mgeni mwalika wanasema eti nichango ya harusi sio lazima na inabidi ihusishe ndugu tu kama wafanyavyo wenzetu Rwanda na Kenya na pia Uganda.

Sasa najiuliza hivi Harris na Vivian siku wakioa au kuolewa hawakuchangiwa. Wameenda mbali kwa kusema Tanzania ni nchi ya kishamba mtu kusumbua michango hata kwa watu wasio nduguze.

Hiki ni kipindi cha hovyo kabisa clouds FM kwani kila nchi na utamaduni wake. Ikumbukwe pia ujamaa wa MWL Nyerere ulihimiza undugu na kushirikiana na pia kusaidiana kwa hali na Mali.

NB: Mods naomba mada isome wanapiga kampeni dhidi ya michango ya harusi.
 
Wachaga hawawezi kukuelewa kwao kuchangia Sio swala la hiari ni la lazima utake usitake.Unakuta mwenyekiti anafoka kuwa kima Cha chini hiki hapa utatoa wapi utaiba u utatoa wapi utajijua lazima utoe
Safi sana hii, kusaidiana hata kwenye mitaji hili hufanyika
 
Lkn sasa wa tz misiba wanatoa buku na mgonjwa wanaenda kumuona na chupa ya chai na maandazi ya jero lkn harusi kamati 100000,double 70000 na single 40000 mpaka kadi zinaisha.
Upuuzi mtupu
aaaaahhhhhaaaaaaaahhh
 
Watanzania wakiambiwa wachange pesa ya kuwasaidia hao maharusi kuanzia maisha na sio kwenda kunywa na kula hawawezi kukubali.
 
Kuna wakati kuna jamaa yangu alikuwa anafatilia michango kufanikisha harusi yake. Kuna boss mmoja alimsumbua sana. Boss katoa ahadi lakini jamaa kila akienda anakula kalenda. Siku moja akamuita na akaanza kumpa wosia mrefuu kama wote vile halafu akamkabidhi jamaa elfu 10 km mchango wake. Jamaa yngu kila ukikutana nae anasema hajawahi kumsahau yule bwana ktk maisha yake.
 
Kuna wakati kuna jamaa yangu alikuwa anafatilia michango kufanikisha harusi yake. Kuna boss mmoja alimsumbua sana. Boss katoa ahadi lakini jamaa kila akienda anakula kalenda. Siku moja akamuita na akaanza kumpa wosia mrefuu kama wote vile halafu akamkabidhi jamaa elfu 10 km mchango wake. Jamaa yngu kila ukikutana nae anasema hajawahi kumsahau yule bwana ktk maisha yake.
Hajamsahau kwa mchango mdogo au wosia?
 
Nisicho kipenda mm kwenye michango hii ni kuwekewa kiwango alafu unakuta hakishuki 50k kwa single & 80k kwa double
 
Kweli kuchangia harusi ya mtu ambaye sio wa karibu kabisa ni ushamba. Unachangia laki unapata kinywaji kimoja maana gharama nyingi za ziada (kukodisha magari ya ajabu ajabu, farasi, n.k.) zinapunguza bajeti za vyakula na vinywaji. Tena mara nyingi "wenyeviti wa idara" (k.m. chakula, upambaji n.k.) wanapata "cha juu" kwa kumleta mhusika anayetoza gharama kubwa kuliko inavyostahili. Nimewahi kuona harusi ambazo kamati ya maandalizi imeweka "sherehe ya kujipongeza" kwa sababu michango ilibaki. Yaani badala ya kuwapa maharusi hiyo baki iwasaidie kwenye kodi ya pango au kwenye ujenzi kama tayari wana kiwanja, kamati inazila hizo fedha. Halafu mwisho wa siku baada ya harusi ya kifahari sa-a-na ndoa inavunjika (wakati mwingine hata mwaka haujaisha). Napendekeza muoaji aite tu marafiki wa karibu, wajomba, mashangazi, na wazazi na ndugu upande wa mume na mke. Jumla ya watu isizidi 50. Na gharama isizidi milioni nne. Mradi picha na video ziwepo basi. Kama gharama ni ndogo hapatakuwepo haja ya kuomba michango mingi. Siku hizi unaweza kujikuta una kadi nne au tano zinataka michango kila mwezi. Na ukimchangia mtu elfu 20 anakudharau. Si afadhali kuacha kuchangia kuliko kutoa pesa kibao kila mwezi kuchangia harusi? Mwisho kabisa:- Kwenye mila za makabila mengi ni watu wa ukoo tu ndio walikuwa wanachanga, na kwenye makabila mengi michango ilikuwa ni vitu vya kusaidia maharusi katika maisha yao yajayo (yaani fenicha na vyombo vya ndani) na sio pesa za kwenda kula na kunywa.
Mkuu mimi nikienda harusini /send off either directly nimechangia 70k au cost sharing( kuchangia 35k watu wawili), nahakikisha
Napiga supu
Napiga wine( full chupa nzima mezani)
Karanga zile
Napiga msosi wa maana( highly selective- items)
Ikifika kwa zawad... natoa mkono au naondoka kabla.
 
Halo JF.
Nipo hapa Nyumbani nasikiliza Terminal ya clouds FM radio ya jiji la karaha na raha la Dar.

Wanaonekana kupinga michango ya harusi wakidai sio lazima. Wote Haris Kapiga na Lilian Mwasha na mgeni mwalika wanasema eti nichango ya harusi sio lazima na inabidi ihusishe ndugu tu kama wafanyavyo wenzetu Rwanda na Kenya na pia Uganda.

Sasa najiuliza hivi Harris na Lilian siku wakioa au kuolewa hawakuchangiwa. Wameenda mbali kwa kusema Tanzania ni nchi ya kishamba mtu kusumbua michango hata kwa watu wasio nduguze.

Hiki ni kipindi cha hovyo kabisa clouds FM kwani kila nchi na utamaduni wake. Ikumbukwe pia ujamaa wa MWL Nyerere ulihimiza undugu na kushirikiana na pia kusaidiana kwa hali na Mali.

NB: Mods naomba mada isome wanapiga kampeni dhidi ya michango ya harusi.
Hata mimi naunga mkono, sijawahi kuchangia mtu harusi na sitakaa nichangie. Siku ya harusi yangu napanga budget ya watu 150 tuu basi bila kuchangisha. Hizo zama za michango zilishapitwa na wakati tubasilike.
 
Halo JF.
Nipo hapa Nyumbani nasikiliza Terminal ya clouds FM radio ya jiji la karaha na raha la Dar.

Wanaonekana kupinga michango ya harusi wakidai sio lazima. Wote Haris Kapiga na Lilian Mwasha na mgeni mwalika wanasema eti nichango ya harusi sio lazima na inabidi ihusishe ndugu tu kama wafanyavyo wenzetu Rwanda na Kenya na pia Uganda.

Sasa najiuliza hivi Harris na Lilian siku wakioa au kuolewa hawakuchangiwa. Wameenda mbali kwa kusema Tanzania ni nchi ya kishamba mtu kusumbua michango hata kwa watu wasio nduguze.

Hiki ni kipindi cha hovyo kabisa clouds FM kwani kila nchi na utamaduni wake. Ikumbukwe pia ujamaa wa MWL Nyerere ulihimiza undugu na kushirikiana na pia kusaidiana kwa hali na Mali.

NB: Mods naomba mada isome wanapiga kampeni dhidi ya michango ya harusi.
Kuchangishana harusi ninkuendekeza umasikini . Mwalimu Nyerere hakufundisha kuchangia bia na kusaza ila kuchangia maendeleo.

Nawaunga mkono terminal tufikie mahami tuchangie elimu afya na mitaji na si harusi ni aibu kufanya sherehe kwa mifuko ya watu. Kama huna ishi within your means.
 
Kwann uoe Kwa michango ya wengine ?? Hii tabia mbovu ipo Tanzania Tu,
 
Chinua Achebe alisema ...Ukiona mtu anatoka kwake anaungana na wenzake kwenye mbalamwezi usiku..sio kwamba kwake huo mbalamwezi haumuliki lkn ni kwa sababu ni vizuri watu kukaa pamoja na kujumuika, huu ndo utaratibu wa kiafrika...mila zetu zimetujenga hivyo...
Hivyo hata michango ya harusi...ni kitu chema watu kujumuika...pili michango sio lazima, hakuna mtu atakae kupeleka polisi au mahakamani sababu hujamchangia harusi...Cha msingi jipime tu..uwezo wako.....
Kama huna hela kausha tu.....lkn ujue sherehe ni watu, watu ndo sherehe....na ndo maisha hayo....Furahi na wanaofurahi, lia na wanaolia.....kusaidiana kupo tu......

Mtu anaesema et atawaalika ndugu, wajomba etc..hivi ni kweli kwenye maisha ndugu tu ndo wanatushika mikono au kutuma connections etc......???Tafuta watu wa karibu marafiki, ndugu etc..washirikishe...sherehe ipendeze...Mwisho wa yote haya ni Futi Sita....
 
Back
Top Bottom