Terminal ya Clouds FM wanapiga kampeni michango ya Harusi.

Terminal ya Clouds FM wanapiga kampeni michango ya Harusi.

Nimepitia posts zote! Takribani 95% ya walioandika comments wanapinga michango! Nyuzi nyingi ninazokutana nazo kuhusu michango ya harusi, nakuta wachangiaji wengi wanapinga michango! Cha ajabu, michango bado inaendelea kuombwa kila leo!! Sasa hawa wanaopinga michango wanatoka jamii ipi na hawa wanaoendelea kutoa michango wanatoka jamii ip? Au ndo ule unafiki wa Kibongo?! Kwamba mtu akikujia live, unaona noma kumpa makavu kwamba hayo mambo yenu ya kingesengese huko huko, lakini aikitoka, unatafuta uzi kuhusu michango ili ndipo ueleze hisia zako!!
 
Halo JF.
Nipo hapa Nyumbani nasikiliza Terminal ya clouds FM radio ya jiji la karaha na raha la Dar.

Wanaonekana kupinga michango ya harusi wakidai sio lazima. Wote Haris Kapiga na Lilian Mwasha na mgeni mwalika wanasema eti nichango ya harusi sio lazima na inabidi ihusishe ndugu tu kama wafanyavyo wenzetu Rwanda na Kenya na pia Uganda.

Sasa najiuliza hivi Harris na Lilian siku wakioa au kuolewa hawakuchangiwa. Wameenda mbali kwa kusema Tanzania ni nchi ya kishamba mtu kusumbua michango hata kwa watu wasio nduguze.

Hiki ni kipindi cha hovyo kabisa clouds FM kwani kila nchi na utamaduni wake. Ikumbukwe pia ujamaa wa MWL Nyerere ulihimiza undugu na kushirikiana na pia kusaidiana kwa hali na Mali.

NB: Mods naomba mada isome wanapiga kampeni dhidi ya michango ya harusi.
Watanzania jamani, ni wapi tulikosea? Where are our priorities? Kama kuna utamaduni nahisi umepitwa na wakati ni hii michango ya harusi. Naona how simple harusi za watu wa magharibi zilivyo. Attendance watu 20 mpaka 40ndugu and close friends tosha. chakula just snacks and drinks. Why do we complicate life? If you can afford it, well and good do it but if you can't, please live within your means.
 
Kwa kweli hii mambo yakuchangisha watu kwa ajili ya harusi yako inakereketa mnoo. Wewe una million moja unataka harusi ya million ishirini hii ni ujinga Sana, unaanza kusumbua watu weee mchongo mchongo Tena unawawekea watu na viwango vya lazima eti laki single chini ya laki hupewi kadi, I see hii kitu inaudhi Sana Sasa toa hata hiyo laki ushangae unachokikuta uko harusini ni ujinga mtupu vinywaji vi Tatu, na miwali Yao njegere na mi watermelon yakumwaga baada ya hapo mtacheza ule wimbo hakuna Mungu kama wewee, then kila mtu kwaoo! Jipange muoaji/muolewaji andaa harusi yako invite watu unaowataka wa maana kama Mia wa nguvu waje na zawadi basi tosha yaani mtu unajikuta una mi kadi ya harusi ofisini, nyumbani, kwenye gari yaani yametapakaa ukipiga hesabu ni Ada ya mwanao ya shule miaka miwili dah!
 
Back
Top Bottom