VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
John Billy Tendwa,Msajili wa Vyama vya Siasa nchini,amegeuka mwanasiasa wa chama cha Mapinduzi. Tendwa,mhitimu wa Shahada ya Kwanza ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,hatumii vyema uanasheria wake. Tendwa,aliyepata Uwakili tarehe 13/6/2008 na kuwa na nambari ya Uwakili 1018,hatumii weredi wake wa kisheria ipasavyo.Anajipendekeza kwa CCM na Serikali yake.
Zipo taarifa kuwa John Billy Tendwa anajiandaa kuwania Ubunge 2015 kwenye jimbo mojawapo mkoani Kilimanjaro. Ana matumaini kuwa atateuliwa na chama hiki cha kijani anachojipendekeza kwacho.Chama cha Mapinduzi hakijengwi wala kulindwa na Tendwa. Kilishajengwa na kulindwa na sasa kinateketea.Tendwa si msaada tena.
Kauli zake za kisiasa za kutishatisha vuguvugu la mbadiliko hazina nguvu.Hazina nafasi. Kwanza,hana mamlaka anayoyasema kwa namna anayojitambia. Chama maarufu kama CHADEMA hakifutwi hivihivi tu. Kama ni mpira wa miguu,basi refarii aumalize mpira huu akiwa tayari amejitafutia njia ya kukimbilia. Lakini,ipo siku atagundua kuwa CCM si chama cha siasa ili ni genge la waropokaji na wachumia tumbo. Watamtenda tu...
Zipo taarifa kuwa John Billy Tendwa anajiandaa kuwania Ubunge 2015 kwenye jimbo mojawapo mkoani Kilimanjaro. Ana matumaini kuwa atateuliwa na chama hiki cha kijani anachojipendekeza kwacho.Chama cha Mapinduzi hakijengwi wala kulindwa na Tendwa. Kilishajengwa na kulindwa na sasa kinateketea.Tendwa si msaada tena.
Kauli zake za kisiasa za kutishatisha vuguvugu la mbadiliko hazina nguvu.Hazina nafasi. Kwanza,hana mamlaka anayoyasema kwa namna anayojitambia. Chama maarufu kama CHADEMA hakifutwi hivihivi tu. Kama ni mpira wa miguu,basi refarii aumalize mpira huu akiwa tayari amejitafutia njia ya kukimbilia. Lakini,ipo siku atagundua kuwa CCM si chama cha siasa ili ni genge la waropokaji na wachumia tumbo. Watamtenda tu...