babukijana
JF-Expert Member
- Jul 21, 2009
- 13,071
- 15,928
Bw.Tito Onesmo Machibya, mkazi wa Arusha maeneo ya Sombe, ametinga jijini Dar es Salaam na kujitangazia kuwa nabii aliyetumwa na mungu kuukomboa ulimwengu.
Machibya alinaswa na kamera yetu maeneo ya Posta Mpya jijini Dar es Salaam akijitangazia unabii wake ambapo mada yake kuu anasistiza kuwa; kunywa pombe si dhambi na kila mwanaume anatakiwa kuoa wanawake kuanzia saba.
Nabii huyo amekumbwa na upinzani mkali kutoka kwa baadhi ya wakazi wa jiji wanaomshutumu kuwa anafanya kufuru na kuupotosha ulimwengu.
Licha ya kupata upinzani mkali kutoka kwa wakazi wa jiji, Nabii huyo amewaambia wakazi hao kuwa bia ya Serengeti ndio kiburudisho muruuuwa… kinachompendeza Mungu na ni kinga ya mwili.
source:global publishers