Umezungumza mambo mengi lakini nasikitika kukwambia kwamba kiufundi/kiteknilojia hayana mantiki,simu karibu zote zinatumia hardware zinazo fanana kuanzia processor na chipsets mpaka Operating Systems save Iphone na Black Berry ambazo OS zake ni tofauti lakini hardware ni zile zile.
Naona maoni yako yamekaa kaa kishabeki zaidi kuliko kiuhalisia,lengo lako ni kutaka kuonyesha kwamba Watanzania wanao tumia simu za TECHNO ni washamba au masikini vile wakati wewe katika maoni yako unaonekana wazi wazi uelewi vizuri jinsi mobile phones zinavyo undwa/ fanya kazi,kuanzia: hardware,firmware,software:OS na apps zake, ndio maana unatujia na madai eti TECHNO inasumbua kwenye google!! nani kakwambia kwamba kampuni ya TECHNO inahusika katika masuala ya ku-code search engines za mitandaoni??? Mara eti speaker za Techno zinakorofisha baada ya mwaka mmoja kupita, nani kakwambia kampuni ya Techno inaweka timer ya ku-degrade quality za speaker baada ya mwaka mmoja kupita? mara, sijui IPhone haiwezi kuwa hacked kuna ukweli gani katika madai yako. Bottom line is: msitake kukatisha tamaa Watanzania wenzenu, wana akili timamu za kuchagua wanacho kipenda kutegemea na mifuko/mahitaji yao.