Tecno User Vs Samsung and iphone user

Tecno User Vs Samsung and iphone user

Hivi thread imenikumbusha msemo wa umoja ni nguvu, naona Team Techno imekataa kunyanyaswa na muda si mrefu wataondoka na ushindi, refa kanyanganywa filimbi, baadhi ya wachezaji timu pinzani wanalazimishwa kupiga mipira kuelekea golini kwako.
 
Tecno baada ya miez 6 inastack
Hii ni guarantee, haijaalishi unatumia tecno ipi, yaani ikifika miezi sita tu kuanzia apo simu itaganda. Unaweza kufuta na kui restore upya ukafikiri itarudi perfomance yake lakini bado itaendelea kuganda.

Ninayo K8, simu imebakia 480MB free storage, eti sms haiwezi kuingia, inakuja notification inanambia kuna sms imeshindwa kuingia kwa sababu ya storage ndogo. yaani sms ya 13kb haiwezi kuingia, lakini ukipiga picha inakubali. Sijui ni Tecno au ni Android tu!
 
Usiwe mpole hivyo Dada yangu

Mwamba ngoma huvutia upande wake.

Nasubiri kamba ikatikie katikati mambo yaishe
😂😂😂😂 nimewaachia team tecno mserereke nayo maana naona mnajitahidi kuhalalisha ukweli ambao kiuhalisia uko tofauti kabisaaaaaa.

Maana mie kama mie zingekuwa tecno zina haya mnayoyasema nisingethubutu kuhamia kungine. Hongereni mmeshinda kwa maandishi. 😂😂😂😂😂
 
Mi ni tecno user na siyo kwamba sijawahi kumiliki samsung hapana ila ilinichosha kutokana na kutaka kunigeuza kuwa teja wa kwenye soketi ya umeme.

Toka nimeanza kutumia tecno hizo changamoto kwangu ni no japo hazidumu sana sometime na mapicha picha yake lakini Tecno is the best kwangu.

---inakaa na chaji 24+ hours kama sina mambo ya kufanya online.

__Camera yake iko vizuri .

__Kioo kikubwa

__Rahisi kuitumia haina mambo mengi.

__Space ya kutosha tu 16GB siyo haba kwa matumizi yangu binafsi.

__bei yake ni kawaida tu kwa mimi mjasiriamali au ata mkulima kuweza kuimudu.

__Upande wa data ni 4G+ na hazina ugumu kwenye upande wa Network setting.


Mnaotuponda watumia Tecno mkuje hapa mtupe Utofauti wa simu zenu.


Mi niko hapa natumiaTecno na hii post mnayoina nimeandika kwa kutumia tecno bila shaka mmeiona haina tofauti na atakaekuja kuandika kwa kutumia Samsung au I phone.
Tecno ni jina la kampuni ya simu, unatumia tecno ya aina gani kwani ndugu maana nimehisi kama vile unaogopa kuitaja, sitaki kuamini kama umesahau kuitaja licha y maelezo toshelezi juu ya tecno.
 
nimewaachia team tecno mserereke nayo maana naona mnajitahidi kuhalalisha ukweli ambao kiuhalisia uko tofauti kabisaaaaaa.

Maana mie kama mie zingekuwa tecno zina haya mnayoyasema nisingethubutu kuhamia kungine. Hongereni mmeshinda kwa maandishi.
Usikimbie bhana tuambie uzuri wa simu yako
 
Hii ni guarantee, haijaalishi unatumia tecno ipi, yaani ikifika miezi sita tu kuanzia apo simu itaganda. Unaweza kufuta na kui restore upya ukafikiri itarudi perfomance yake lakini bado itaendelea kuganda.

Ninayo K8, simu imebakia 480MB free storage, eti sms haiwezi kuingia, inakuja notification inanambia kuna sms imeshindwa kuingia kwa sababu ya storage ndogo. yaani sms ya 13kb haiwezi kuingia, lakini ukipiga picha inakubali. Sijui ni Tecno au ni Android tu!
Yaani unatumia simu mpaka inafikia 480 mb alafu bado unalalamika ikiwa inastack ?

Simu unaigeuza laptop mkuu?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom