Tecno User Vs Samsung and iphone user

Tecno User Vs Samsung and iphone user

Mi nilikuwa natumia Galaxy s2 mwaka 2013 hiyo, akaja dada mmoja akataka nimbadulishie anipe tecno m5 na laki mbili juu. Nikampa.

Ile tecno nilitumia mwezi tayari kioo kishachakaa na kustack.

Akaja jamaa enzi hizo chuon wenye smartphones chuon wanahesabika nikamkamata bei.

Toka siku hiyo tecno sitaki hata kuishikaa.
Asa M5 uliingia kichaka
 
Ngoja waje mpambane ila kiukweli Tecno niliwahi tumia na ikanizingua upande wa Network yaani ukiwa mjini ndio unapatikana nikirudi home ni kama nina kopo tu.

Toka hapo sijawahi tumia tena Tecno aiseee na sitatumia tena. Ilikuwa Tecno C9 hiyo.
Samsung nimetumia nayo ilikuwa inazingua sana net, Iphone ndo nilisema sintoitumia tena, maana kipindi kile wasap tunalipia $0.99 kwa mwaka ilikuwa Iphone huwezi kudownload kwenye appstore hadi uilipie kwanza na hivyo hivyo kwa apps zingine za trail wao wanataka ulipie kwanza.
 
Ngoja waje mpambane ila kiukweli Tecno niliwahi tumia na ikanizingua upande wa Network yaani ukiwa mjini ndio unapatikana nikirudi home ni kama nina kopo tu.

Toka hapo sijawahi tumia tena Tecno aiseee na sitatumia tena. Ilikuwa Tecno C9 hiyo.
Sasa hivi unatumia nini?

Mi Tecno ilinishinda kwa visa vyake. Bombardier ikipita juu yenyewe inajichaji automatikale. Ukienda hospitalini nesi akishika sindano yenyewe ina vibrate. Ukienda nayo msalani inapoteza network afu inaanza kuimba taarab...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom