Tecno mobile Mega Thread

Tecno mobile Mega Thread

Hivi karibuni zimeanzishwa thread nyingi hapa JF za watu wakisifia na wengine kukandia simu za TECNO. Lakini hebu tujiulize, ni kwanini watu wengi wanaangukia kwenye simu hizi ambazo zinaonekana kama ni za ubora wa hali ya chini huku wengine wakizisifia kwamba zina ubora wa hali ya juu?

Kwa maoni yangu mi naona hapa kuna mawili:
1. Watu wengi wanaozisifia simu kama tecno, ni watu ambao wana matumizi madogo sana ya simu.. yaani kupiga, kutuma msg, na ku browse internet na mitandao ya kijamii. Mtu akishaona simu aliyo nayo inaweza kufanya mambo hayo pamoja na labda ku play mziki na kupiga picha (regardless ya quality), ana conclude kwamba hiyo ni simu nzuri sana na haina tatizo lolote. Kitu ambacho kwa level yake ni kweli.. Ikumbukwe kwamba hayo niliyotaja ni mambo basic sana ambayo low- end smartphone yoyote hata ya kichina inaweza kufanya! Kwahiyo mi siwalaumu hawa watu. Huo ndio ukweli wa upeo wao kwenye simu. Mtu wa aina hii hahitaji Galaxy Note 3. Tecno inamtosha kabisa na wala huwezi kumlaumu akiisifia..

2. Kwa upande mwingine nawalaumu sana wauzaji wa simu. Siku hizi ukitembelea maduka mengi ya simu huwezi kukuta low-end smartphones za Samsung, HTC, Motorola n.k.. Simu zote utakazokuta zenye majina makubwa ni zile za bei ghali tuu.. Lakini ukweli ni kwamba kuna simu nzuri tu za samsung, nokia, HTC, Sony n.k ambazo ni za bei ya chini karibu sawa tu na hizo tecno, ila zina ubora wa hali ya juu! Tatizo simu hizi hazipo madukani hivyo kuwalazimu watu kuchagua kati ya tecno au Galaxy s5. Kwa uchumi wetu, haishangazi kuona wengi wakiangukia kwenye tecno. Hebu chukulia mfano wa simu hizi mbili:
TECNO F7 PHANTOM A: Internal Memory 4Gb, RAM 1Gb, Processor 1Ghz, Display 5inch (293ppi) Bei ~ 450,000/=
SAMSUNG GALAXY NOTE 1: Internal memory 16Gb, RAM 1Gb, Processor 1.4Ghz, Display 5.3inch (285ppi) Bei ~ 450,000/=
Tecno-F7-Phantom-A-Plus-214x300.jpg
tmobile-samsung-galaxy-note.jpg

Tatizo sasa.. Ukitembelea madukani utazikuta TECNO phantom zimejaa tele lakini Note 1 unaweza kumaliza maduka yote bila kuipata..! Nina uhakika ukimuwekea mtu simu hizo mbili side by side ukamuambia achague, matokeo yanaweza kuwa tofauti sana na hali ilivyo sasa.
 
wengi wanatumia smartphone kwa matumizi basic tu, mtu wa hivyo hahitaji high end smartphone, hata nokia asha inamtosha, wala haina haja ya kumcheka mtu anatumia tecno.
hapo kwenye namba mbili, hivi maduka ya samsung hawaweki simuza nyuma, mbona vi galaxy pocket vipo?
wengine wagonjwa wa iOS, nikipoteza iPhone yangu natumia kisimu cha tochi siku mbili nanunua nyingine.
 
Hata hizo online multimedia streaming wanazodai ni SLOW sana ukilinganisha na simu original kama Nokia.
 
Kuna miongozo ambayo uwa naifata kabla sijanunua simu au kifaa chochote cha electronic,
je kitakidhi mahitaji yangu? Durable? Naweza kupata technical support mtandaoni kiurahisi, bei yake inafit bajeti yangu,

kitakachofata ntaingia google ntatafuta nnachotaka pia nikipata ntaangalia shortcomings zake ntaweza kuzivumilia

tunapokuja kwenye swala tecno, watanzania wengi kipato chetu si cha kutosha kununua high end simu japo matumizi yetu wengi uwa machache hata 50% ya features hazitumiki,

tunapenda tuonekane tunaenda na wakati icho kinatufanya tuishie kuchukua alternative, kama ambavyo mtu mmoja alisema ist na hummer zote gari ilimradi tufike

kwa upande wa wauzaji siwalaumu saana, wao hawajali mteja wao wanajali nini kinauzika, nashangaa mtu hasa anaetembelea jukwaa hili ambae hawezi kusoma makala za chifu mkwawa kuhusu simu za bei nafuu, ambae hawezi kugoogle aone ajionee duniani kuna simu za aina gani zaidi ya tecno, siku izi unaweza nunua simu online tena kwa gharama ndooogo kuliko hata madukani huku bongo,

conclusion: hatuwezi kulazimisha watu wote wawe na vitu orijino, wengine wanapenda mchina kutoka damuni, so kila mtu atasema yake ila muamuzi wa mwisho ni mnunuaji
 
Okay mmesema mengi sana kuhusu matumizi basics sijui ya techno or whatever sasa orodhesheni basi hayo matumizi yasiyo basic ya hizo simu zingine...via situmii techno...tuone matumizi yasiyo ya kawaida i.e samsung galaxy or whatever....!!
 
Ndo matokeo ya vya bei rahsi..

Wakala wa Tecno tawi la JF,bwana shiny c njoo utoe ufumbuz wa hili tatzo kwa wateja wenu..
 
Last edited by a moderator:
Okay mmesema mengi sana kuhusu matumizi basics sijui ya techno or whatever sasa orodhesheni basi hayo matumizi yasiyo basic ya hizo simu zingine...via situmii techno...tuone matumizi yasiyo ya kawaida i.e samsung galaxy or whatever....!!

Live streaming,mfano nmeshndwa kuangalia kombe la dunia kwa TECNO P9,ila nmeweza kwa Blackberry Q5..

hyo tecno ilkua haziishi sekunde 10 imekwama..
 
Huo mlio ni baada ya simu 2 kupokelewa na baada ya kukata hauwezi toka lbd uediti system build prop ambyo ndo inafanya simu inavibrate ( inatoa huo mlio ) baada y kupokea simu

Nawezaje ku edit hiyo system build ,nisaidie namna ya kufanya
 
Okay mmesema mengi sana kuhusu matumizi basics sijui ya techno or whatever sasa orodhesheni basi hayo matumizi yasiyo basic ya hizo simu zingine...via situmii techno...tuone matumizi yasiyo ya kawaida i.e samsung galaxy or whatever....!!

Umeongea point ya msingi sana, wangetaja na hayo matumizi yaxiada tuyajue nasisi wenye vitochi tujipange.
 
Umeongea point ya msingi sana, wangetaja na hayo matumizi yaxiada tuyajue nasisi wenye vitochi tujipange.

Okay mmesema mengi sana kuhusu matumizi basics sijui ya techno or whatever sasa orodhesheni basi hayo matumizi yasiyo basic ya hizo simu zingine...via situmii techno...tuone matumizi yasiyo ya kawaida i.e samsung galaxy or whatever....!!

Tecno ni simu nzuri kwa matumizi ya kawaida, mfano wa matumizi ya simu yangu.
1. Server Manager android application
2. cPanel/WHM android application
3. Client Management Custom android application
4. Pingdom web tools

Kwa matumizi haya tu nahitaji processing power kubwa na simu iwe na uwezo ili kuweza run vyote kwa mpigo pasipo shida. Kwa kutumia ya chini ya 450000TSH (Phantom) huwezi fanya yote kwa ufasaha.


Live streaming,mfano nmeshndwa kuangalia kombe la dunia kwa TECNO P9,ila nmeweza kwa Blackberry Q5..

hyo tecno ilkua haziishi sekunde 10 imekwama..

Live Streaming mkuu nadhani ulitakiwa kuangalia net yako. Nimewahitumia Tecno P5 kuangalia mechi nzima.
 
vipi nokia tochi nayo ni low end au high end???
 
Hiyo galaxy note1 haiuzwa laki 450 labda used lkn mpya si chini ya laki 6 kwenye maduka ya samsung zipo kibao
 
Hiyo galaxy note1 haiuzwa laki 450 labda used lkn mpya si chini ya laki 6 kwenye maduka ya samsung zipo kibao

kaka note 1 ilitoka 2011 sawa na s2 sasa hv unlocked kkoo hadi laki 3 unazipata. Ukiona mtu anauza laki 6 ujue ana stock ya zamani anataka akulalie. Even s3 ambayo ni bora kwa note 1 haiuzw laki 6 siku hizi
 
Tecno na wachina wengine wanatumia pia android concern inakuja kwenye hardware na sio software.

unajua why simu za kichina haziendi marekani na ulaya? Kule kila simu inapimwa kabla haijaingia wanaangalia issue za radiation na madhara mengine, zingekua safe zingeuzwa kibao. Hapa tz hata SAR simu hazipimwi.

ni rahisi kusema simu yangu naangalia movie lakini ubora wa kioo chako upoje? Kioo kama cha tecno ni horible kina kijivu blue effects hata details hazipo clear mwisho wa siku tunabishana hapa same ukija kwenye camera, processor, mic, updates, after sale support, gpu, optimazion ya software na mengine mengi
 
kaka note 1 ilitoka 2011 sawa na s2 sasa hv unlocked kkoo hadi laki 3 unazipata. Ukiona mtu anauza laki 6 ujue ana stock ya zamani anataka akulalie. Even s3 ambayo ni bora kwa note 1 haiuzw laki 6 siku hizi

Nakwambia maduka ya samsung unaniambia unlocked? Hakuna note 1 ya laki 450 brand new labda used au kanyanga
 
Hata bila ya kufanya uchunguzi unaweza ng'amua kwamba asilimia kubwa ya Watanzania wanaotumia smartphone wanatumia Tecno. Wengi wa Watanzania hawa ni watu wa "kawaida" kabisa. Matumizi yao makubwa ni kupiga/kupokea simu, kutuma msg, alarm, kuhifadhi media zao (nyimbo na picha) na wachache ku-browse. Kwa mantiki hiyo, hata zile features za techno hawatumii hata robo yake...yaani uwezo wa tecno tayari ni zaidi ya mahitaji yao. Unadhani mtu huyu atanunua simu nyingine yenye hata tofauti ya elfu tano?
Na Wachina kama kawaida yao, wanajua sana wanamtarget nani. Wanachunguza soko na uwezo wa wateja walengwa, hawaji kichwa kichwa. Wana standards zote kwa watu wote (Ulaya na America kuna bidhaa nyingi sana tu China). Kwa upande mmoja wamesaidia sana wanyonge kuwa sehemu ya ulimwengu wa technolojia. Kama kusingekuwa na watengenezaji wa simu za bei nafuu, hiyo galaxy usingeipata kwa bei iliyopo sasa. Ni haka kaushindani ka watengenezaji wengine kama techno kanaowafanya samsung and the likes kuweka mipaka ya bei.

Na jambo muhimu zaidi katika maisha ni "satisfaction". Kama wewe sio mtu wa kuridhika, hata uwe na galaxy 5s, kesho wakiibadilisha jina (features zote zibaki vilevile) lakini waiite 6s utainunua, tena bila kujali gharama. Watanzania wengi tunatumia "vitu" kuonyesha uwezo na wengine show-off tu sio kwa msingi wa mahitaji/matumizi!!!
 
Hata bila ya kufanya uchunguzi unaweza ng'amua kwamba asilimia kubwa ya Watanzania wanaotumia smartphone wanatumia Tecno. Wengi wa Watanzania hawa ni watu wa "kawaida" kabisa. Matumizi yao makubwa ni kupiga/kupokea simu, kutuma msg, alarm, kuhifadhi media zao (nyimbo na picha) na wachache ku-browse. Kwa mantiki hiyo, hata zile features za techno hawatumii hata robo yake...yaani uwezo wa tecno tayari ni zaidi ya mahitaji yao. Unadhani mtu huyu atanunua simu nyingine yenye hata tofauti ya elfu tano?
Na Wachina kama kawaida yao, wanajua sana wanamtarget nani. Wanachunguza soko na uwezo wa wateja walengwa, hawaji kichwa kichwa. Wana standards zote kwa watu wote (Ulaya na America kuna bidhaa nyingi sana tu China). Kwa upande mmoja wamesaidia sana wanyonge kuwa sehemu ya ulimwengu wa technolojia. Kama kusingekuwa na watengenezaji wa simu za bei nafuu, hiyo galaxy usingeipata kwa bei iliyopo sasa. Ni haka kaushindani ka watengenezaji wengine kama techno kanaowafanya samsung and the likes kuweka mipaka ya bei.

Na jambo muhimu zaidi katika maisha ni "satisfaction". Kama wewe sio mtu wa kuridhika, hata uwe na galaxy 5s, kesho wakiibadilisha jina (features zote zibaki vilevile) lakini waiite 6s utainunua, tena bila kujali gharama. Watanzania wengi tunatumia "vitu" kuonyesha uwezo na wengine show-off tu sio kwa msingi wa mahitaji/matumizi!!!

Nimekukubali sana mkuu wewe ni mchambuzi mzuri sana
 
Back
Top Bottom