Mi naona hapa kuna mawili:
1. Watu wengi wanaozisifia simu kama tecno, ni watu ambao wana matumizi madogo sana ya simu.. yaani kupiga, kutuma msg, na ku browse internet na mitandao ya kijamii. Mtu akishaona simu aliyo nayo inaweza kufanya mambo hayo pamoja na labda ku play mziki na kupiga picha (regardless ya quality), ana conclude kwamba hiyo ni simu nzuri sana na haina tatizo lolote. Kitu ambacho kwa level yake ni kweli.. Ikumbukwe kwamba hayo niliyotaja ni mambo basic sana ambayo low- end smartphone yoyote hata ya kichina inaweza kufanya! Kwahiyo mi siwalaumu hawa watu. Huo ndio ukweli wa upeo wao kwenye simu. Mtu wa aina hii hahitaji Galaxy Note 3. Tecno inamfaa kabisa..
2. Kwa upande mwingine nawalaumu sana wauzaji wa simu. Siku hizi ukitembelea maduka mengi ya simu huwezi kukuta low-end smartphones za samsung, htc, motorola n.k.. Simu zote utakazokuta zenye majina makubwa ni zile za bei ghali tuu.. Lakini ukweli ni kwamba kuna simu nzuri tu za samsung, nokia, HTC, Sony n.k ambazo ni za bei ya chini karibu sawa tu na hizo tecno, ila zina ubora wa hali ya juu! Simu hizi hazipo madukani hivyo kuwalazimu watu kuchagua kati ya tecno au Galaxy s5. Kwa uchumi wetu, haishangazi kuona wengi wakiangukia kwenye tecno.