Tweetylicious
Member
- Apr 10, 2012
- 17
- 11
Kutokana na kuwa thread nyingi zimekuwa zikifunguliwa na nyingi zikizungumzia yaleyale, nimeonelea kuziunganisha ili kupata thread moja yenye kila kitu kuhusu simu za tecno
wakuu naomba msaada mwenye kuilewa hii simu ya Tecno phantom.nasikia ina specifications kama za samsung galaxy S3. price is good but is it worth buying kwa mwenye nayo au anayeitumia i would appreciate the review and comments on ys good or bad features.thanks in advance.
wadau hebu tuwekane sawa maana sisi timu tecno tunapigwa majungu sana na hawa wa upande wa pili, NI KITU GANI HASA AMBACHO SIMU ZAO SIJUI GALAXY SIJUI HTC SIJUI IPHONE NGAP NGAP HUKO SIJUI LUMIA NGAP NGAP HUKO ZINA FANYA AMBACHO TECNO ZETU HAZIFANYI????
mnatupigia kelele weee wakat unachokifanya kwako na mim nafanya vile vile
Kuweni wapole, kubalin mmepoteza hela tu, ubora n ule ule, uwezo n ule ule, tofaut n makampun tu na gharama
Mungu mbariki mchina aendelee ku produce hii bidhaa, hehehe Simu inayozalishwa na samsung yenye thaman ya lak 6 kendelea n= Tecno ya lak na nusu, Tuambizane n nini mnafanya kwenye cm zenu sisi familia ya Tecno hatuwez
Nina tecno 3 zimenifia. Mbaya zaidi haujaisha hata mwaka.. nina s5 imekufa touch na mic, p5 imekufa lcd na m3 imepasuka lcd na touch. Kwa hiyo nina majanga ya tecno.
Tecno smartphones ni miongoni mwa simu zinazokosesha raha makampuni makubwa kama samsung hapa bongo, hili kampuni limefanikiwa kupenyeza kiakili bidhaa zake kwenye soko, hakika hutajutia pesa yako maanaenjoy sana, vijana wengi unakuta life limemchapa ila mfukoni ana simu ya milioni huu ndo nauita ujinga, ya nini ununue kitu cha milioni wakati kuna smartphone za bei rahisi tena original, hizi ndo sababu za kununua tecno:
1.Unapata bidhaa kwa bei rahisi , watu wote wa juu na chini wanauwezo wa kuinunua bei ikianzia laki hadi laki nne kulingana na sifa za simu
2.Ubora na Ugumu ni wa hali ya juu huyu ni mchina original sio wale kina -tide wale wanaosema hazidumu naona wanafki, watu wanadumu nazo miaka na miaka
3.Unaweza kuichaji popote hata kwenye basi maana unapewa kifaa kinaitwa power bank ambacho hutunza nguvu za kuchajia simu, hivyo hata safari za vijijin itafaa uende na hii simu
4.Zina Mapungufu madogo sana ukilinganisha na zile za makampuni makubwa kama HTC ambazo huuzwa kwa bei ghali sana kwenye mamilioni , mwisho wa siku unakuta vitu ni vidogo sana vilivyoizidi tecno mfano labda kuna simu zinakunjika ila tecno haiwez na kuna simu nyingine waweza tumia kwenye maji ila simu nyingi kama tecno haziwezi, na mapungufu mengine madogo sana
5.Ni simu iliyokaa kimawasiliano sana maana inapiga simu hata kwa njia ya internet na pia ina application kama whatsapp na facebook bila kusahau hii simu imeongezewa sehemu ya kuweka laini ya pili.