Hili jukwaa la "Tech,gadgets and science forum" lilitakiwa kuwa na sub-forums ndani yake.
inaweza kuwa idea nzuri lakini mbona zamani haikuwa hivi ?
au moderation za siku hizi na kipindi kile ni tofauti ?
I miss old days za hili jukwaa ,, hili jukwaa lilikiwa kina hadhi yake ya kipekee na kiubunifu, kulikuwa na e2themiza mzee wa internet tricks, chief mkwawa yupo kitambo mtaalam wa simu mpaka sasa, good guy, njunwa, mwl rct hata muanzisha thread,,, I really miss those days jukwaa katika ubora wake
Umewataja woote lakini hujamtendea haki Chief Mkwawa huyu jamaa japokuwa na changamoto zote hizo bado yupo na amebaki na ataaendelea kuwa msaada mkubwa WA jukwaa Hili.
nipo huko pia but all i do there ni kuangalia comparisons ya best tech thingys,best tech stuffs reviews in general,tech solutions etc etc.I feel very lost kule,sehemu kama hizi za nyumba zakujidai ndo upuuzi mtu!I spend most of my time on Quora na stackoverflow, ila mostly on Quora, its more social na i get to learn a lot from there japo wabongo nshawahi kukutana na mmoja tu kule.
Tatizo kila mtu sahivi akishajua kuroot simu then he thinks yeye ndo one Techie guy anayejua kila kitu!,na badala ya kuchangia mada kwa ujuzi,wengi wanachangia mada kwa "Majibu ya Google" bila hata kujua nini anapost!kwa style hii,ni vigumu sana Logic people kuendelea kuexit Kwenye hii Forum!Hili suala ni sahihi kabisa mkuu na tena limeniface sana binafsi, sio siri sometimes yataka moyo sana, i've been mistreated alot tena mtu from nowhere anakuletea mambo ambayo yako wazi kabisa kuwa ni chuki zisizo na msingi wowote, just because they sometimes don know a thing alike you.
Kabisa mkuu, kuna watu wakaanza kuwekea wenzao vinyongo na vivu huku, watu kama Njunwamavoko, MLMRct wakaanza kususa., dstv ya bure nk.sitamsahau Paje maishani hasa kwenye net ya 0/= bila kusahau uchakachuaji Wa software kama IDM nk.
Hizi kero za vifurushi vinavyobadiriswha bila taarifa tusingekuwa tunapata shida sana.
I sure miss the old Tech group indeed!! Alot of challenges zilikuwepo indeed!! But its not all gone, kuna msimu wa hawa watu na naamini utapita! This place will rise from the ashes !! :ranger:
Hata mimi nimepotea kitambo sana na huwa napitia kwa mwezi mara 1 au 2 katika Jukwaa ila naona maada zote hazina mvuto hata kukupa hamu ya kuchangia au kusaida na yote ni kohofia kutusiwa maana ilifikia hawa new commers kututusi hadi niliomba uwongozi wa JF wafute thread zangu zote na comments zangu zote za thread za watu wengine, unajuwa wengi hawaelewi reputation za watu sasa unapoanza kumwagia matusi mtu katika mitandao unaharibu reputation zao, na wengine wanashindwa kutambua kuwa wengi huwa tunatumia majina yetu ya ukweli na unapoanza kututusi mitandao inasomwa na wengi, wiki 1 iliyopita nilibahatika kwa mara ya kwanza maishani kuonana na Mshumaa Morogoro (huyu jamaa ni legend humu ndani kwa thread zake za misaada na kufundisha watu hadi kufunga satelite dish kama mtamkumbuka alikuwa na thread ambayo ilikuwa inaongoza kwa viewers na wachangiaji) tulipiga story zaidi ya masaa mawili na tulijadiliana sana kuhusu kurudi kuchangia JF jukwaa letu hili ila mambo mengi yanaturudisha nyuma hadi kukosa imani. Ila bado tupo na tutaendelea kuwepo ila wengi tumekuwa tukitoa misaada kwa njia nyengine, mimi natoa kwa njia ya sms, simu, mtandao wa fb na web Munjy1.com Bingwa wa Ving'amuzi but niko limited sana sababu ya muda na majukumu mengi niliyonayo.ni kweli aisee nikikumbuka hata mm kabla sijajiunga rasmi jf nishakuwa naperuzi huku zaidi ya 3yrs ndio baadae nikaamua kujiunga na jukwaa ambalo nilikuwa naperuzi ni hili.
aisee kweli Paje kapotea mazima namkumbuka.sana kipindi cha internet ya guru.
tatizo letu humu wengi hatujui kitu lakini wataalamu wanapojitolea kuweka mambo kuna wengi wanatokea na kuanza kupinga tena kwa kashfa na matuzi na zarau kubwa wakati watu wanakesha na kuumiza kichwa ni vipi wanaokoa jahazi la wana jf wengi wataalam wakakata tamaa mkuu kama @munjy 1 sasa hivi baada ya kutusiwa sana na kutukanwa juu ya vile visumbusi kaamua kuliendeleza upande mwingine kimya kimya.
tatizo wengi kujua kwingi mwisho wa siku wenye uelewa wametuacha wakiwa