TCU yafungua dirisha la udahili awamu ya nne

ushahd

Senior Member
Jul 30, 2019
180
101
Habari za jion wadau samahn mm nimeomba chuo round ya kwanza mpaka ya tatu sijapata chuo nimesoma Cbg na ufaulu wangu two ya 12 je nauliza kuna uwezekano wa kufungua dirisha kwa awamu ya nne kwa mwaka huu mwenye uzoefu tafadhali

=====================================

Tume ya vyuo Vikuu Tanzania(TCU), imefungua dirisha la udahili kwa awamu ya nne utakaoanza Oktoba mosi hadi 4, mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Septemba 25, Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Charles Kihampa amesema lengo ni kutoa fursa kwa wananchi ambao hawakuweza kuahiliwa katika awamu tatu kupata nafasi hiyo.

Amesema tume imepokea maombi pia kutoka kwa vyuo ambavyo bado vina nafasi kuhitaji kuongezwa muda wa udahili.

“Tume imeongeza muda wa udahili kwa kufungua dirisha la udahili kwa awamu ya nne utakaoanza Oktoba mosi hadi 4,mwaka huu,” amesema profesa Kihampa.

Amevitaka vyuo vyote vya elimu ya juu kubainisha proramu zenye nafasi ili kuwawezesha waombaji kufanya maamuzi sahihi wakati wa kutuma maombi ya udahili.
Amewakumbusha waombaji wote kuwa masuala ya yanayohusiana na udahiliama kuthibitisha yawasilishwe moja kwa moja katika vyuo husika na si TCU.
 
mkuu usiwe unaomba udsm na udom tu jaribu na vyuo vingine la si hivyo awamu nyingine ikiwepo utakosa tena
Ooh sawa sasa mbali na udsm na udom chuo kipi cha serikali chenye course inayonifaa mm niliyesoma cbg
 
sasa hizo huoni kama zina ushindani mkubwa yaani kwa vyuo hivyo wanachukua wale wenye division one wengi kama una two hiyo hasa UDSM pale huwezi kupata
 
sasa hizo huoni kama zina ushindani mkubwa yaani kwa vyuo hivyo wanachukua wale wenye division one wengi kama una two hiyo hasa UDSM pale huwezi kupata
Kumbe daah ngoja tusubili wakitoa round ya nne nitabadili course
 
SUA na Ardhi wanazo pia Environmental Science
Pia hivi kwa matokeo yake system inaweza ikamtema, cha kufanya apitie TCU guide book angalie vyuo vingine vinavyotoa hizo programs.

nb, Tanzania vyuo vinatofautiana majina na majengo tu, ila vngine vyote sawa tu.
 
Pia hivi kwa matokeo yake system inaweza ikamtema, cha kufanya apitie TCU guide book angalie vyuo vingine vinavyotoa hizo programs.

nb, Tanzania vyuo vinatofautiana majina na majengo tu, ila vngine vyote sawa tu.
Kwan Kuna uwezekan wa round ya nne kuwepo
 
Achana na majina ya vyuo vikubwa utasubili sana, chagua vyuo vya vingine, ukiona huna div 1 neno udsm,mhimbili na udom kata kabisa kichwani tofaut na apo uwe mtu wa bahati na connection kwenye selection.

NB. Mwajili hangalii jina la chuo kwenye cheti anangalia una cheti husika na competence
 
Achana na majina ya vyuo vikubwa utasubili sana, chagua vyuo vya vingine, ukiona huna div 1 neno udsm,mhimbili na udom kata kabisa kichwani tofaut na apo uwe mtu wa bahati na connection kwenye selection.

NB. Mwajili hangalii jina la chuo kwenye cheti anangalia una cheti husika na competence
Ouky thanks mr
 
Sua wanasema wait round three
Screenshot_20190924-120239.jpeg
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom