TCU 'wazishukia' shahada za heshima!

TCU 'wazishukia' shahada za heshima!

SMU

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2008
Posts
9,613
Reaction score
7,902
Yaonya watanzania kuwa makini:
- Nyingi zinatolewa na vyuo visivyotambulika wakiwalenga zaidi watu maarufu wakiwamo marais wa nchi za kiafrika
- Mara nyingi zinatolewa kwa manufaa ya vyuo husika
- Nyingine zinapatikana kwa kubadilishana na fedha
 

Attachments

Wasipewe tuu Maraisi, hata wajasiria mali walioweza kumilika makampuni na kutoa ajira za kutosha kwa Watanzania wangetunikiwa PHD za Uchumi bila kuja mitaji yao waliipata kihalali, kuwapora raia wenzao au kwa kuifisadi Serikali
 
Wanasiasa wetu wengi "mazuzu". Hata wakipewa vichupa wanadhani ni almasi!
 
Wanasiasa wetu wengi "mazuzu". Hata wakipewa vichupa wanadhani ni almasi!

Wengine wasio na aibu hata huwaita Dr Dr Dr hawajui kama wanawadhalilisha wanaowaita hivyo. Mimi napendekeza hata mgambo au askari wa jiji tuwe tunawaita General au Major, itakuwa ni sawa tu.
 
kila mtu anaweza kuzipata kwa KUGONGA HAPA kwa dola 180 tu. Unajichagulia hadi chuo. 80% ya wakenya wengi walioajiriwa hapa tz wamegraduate kwa style hii.
 
ila ni fedheha sana kutumia degree ya kupewa kwenye utambulisho wako..kwa Dr Jakaya..haina maana yoyote kwani hadhi ya uraisi ni kubwa kuliko hiyoo fake degree..

Ghana raisi wao ni Prof ila hajitambulishi kwa cheo hichoo..media zetu nazishangaa sanaa kumpamba muungwana kwa hiyoo degree ya kupewaa...
 
Wazitumia majukwaani tu kama alivyokuwa Dr Remmy........wasiombee kazi wala kura
 
Wazitumia majukwaani tu kama alivyokuwa Dr Remmy........wasiombee kazi wala kura

Naona kuna wengine zinawaongezea waumini! Au labda ni mchanganyiko na siasa. Lakini kwa vyovyote vile, zinadhalilisha sana taaluma!
 
ila ni fedheha sana kutumia degree ya kupewa kwenye utambulisho wako..kwa Dr Jakaya..haina maana yoyote kwani hadhi ya uraisi ni kubwa kuliko hiyoo fake degree..

Ghana raisi wao ni Prof ila hajitambulishi kwa cheo hichoo..media zetu nazishangaa sanaa kumpamba muungwana kwa hiyoo degree ya kupewaa...

...kama yule Reinfred Masako wa ITV...anapenda sana hii Dr Jakaya Mrisho Kiwete...sijui angombea ubunge na yeye
 
cjui mantiki yake ni nini, kwa nini isitambulishwe wazi kua ni ya heshima kwani inavyotamkwa ktk majukwaa neutral inaonekana kana kwamba ame i earn wakati ame i chukua tu! kuna tofauti kati ya ku earn na ku take! inadhalilisha taaluma sana tu! kua dr maana ou have some sort of philosophic thinking in your head, sasa wengi ya hawa wanaopewa ni majuha tupu, system tu ndo imewaweka apo walipo, idea ya kuwapa ii degree wajasiriamali ambao wameanza from the scratch wakaanzisha makampuni makubwa yanayotoa ajira kwa wengi ni nzuri!
 
...kama yule Reinfred Masako wa ITV...anapenda sana hii Dr Jakaya Mrisho Kiwete...sijui angombea ubunge na yeye

Umemsahau yule mmwaga upupu wa Clouds -Kibonde, naye humwita Dr. mheshi kama vile kuna kitu anaomba au anajikomba. kuliko wenye Dr zao za shule.
 
ila ni fedheha sana kutumia degree ya kupewa kwenye utambulisho wako..kwa Dr Jakaya..haina maana yoyote kwani hadhi ya uraisi ni kubwa kuliko hiyoo fake degree..

Ghana raisi wao ni Prof ila hajitambulishi kwa cheo hichoo..media zetu nazishangaa sanaa kumpamba muungwana kwa hiyoo degree ya kupewaa...
Hawa ndugu zetu wao wanaona sifa kuitwa DR.....
 
It is so sad wengine hawana hata first degree lakini wana Phd ya heshima.

Tutawatofautishaje na Dr. Remmy, Dr. Maji marefu, Dr Matuja, ..............
 
Naona kuna wengine zinawaongezea waumini! Au labda ni mchanganyiko na siasa. Lakini kwa vyovyote vile, zinadhalilisha sana taaluma!

mimi kuna kipindi nilalamika kuwa iweje raisi wa nchi akubali tu kupewa degree (honorary degree), inabidi tumcheck IQ yake, halafu nikalalamikia media kuanza kuwaita sijui Dr. Kikwete, sijui Dr. Karume, nikasema huku ni kudhalilisha taaluma ambayo wengine wameisotea for 9yrs, kuna lecturer mmoja amewahi kunifundisha pale UDSM alipata doctorate yake after 9yrs, so how come someone acquiring it through cheap words, cheap piecemouth, haiwezekani. Nafikiri Prof. Nkunya is right, hizi honorary drgree kwanza zinapunguza heshima, personally siwezi kuaaccept degree kama hiyo, lakini naona mkuu wa Kaya yeye anachekelea tu-------------inampunguzia heshima ile mbaya
 
Kwani kuna tatizo gani? itungwe sheria kuzuia vihiyo kuitwa vyeo vya kitaaluma. Kama wanapewa vyeo hivyo wakae navyo vyumbani mwao ila wasiitwe hivyo hadharani.
 
TCU sasa nao ni vigeu-geu wakati Msemakweli akipambana na uhuni huu walimshambulia lakini sasa nao wanacheza ngoma ya mSemakweli inabidi tuwe makini sasa kuangalia feki feki hizi.

Kwa nini wasitumie TAKUKURU style. Inabidi kila mtu asubmit vigezo vilivyotumika na pia ripoti iliyo katka chuo husika kuhusu degree yake.
 
Hakuna kitu kibaya kama mtu kuamua kutomia kichwa chake kufikiri.Hujawahi kwenda soma upewe Phd, leave alone hiyo masters..huo Dr unatokea wapi? Wa uganga wa kienyeji? Hizi sifa nyingine bwana
 
Huyu profesa wa TCU asiishie kuandika hizo press releases tu; huu ni wakati wa taasisi yake wakishirikiana na Tume ya uchaguzi kufanya due diligence ya elimu ya wananchi wote walioomba kuteuliwa kugombea ubunge/urais toka vyama vyote. Si sahihi kwa wao kukaa kimya wakati jamii inalalama kuhusu kuzagaa kwa viongozi waliotumia vyeti feki kupata ajira!!
 
Back
Top Bottom