TCU wameua ndoto yangu

TCU wameua ndoto yangu

poppah

JF-Expert Member
Joined
Dec 19, 2014
Posts
630
Reaction score
548
Nakumbuka nilipokuwa mtoto watu wazima wakiniuliza,"ukiwa mkubwa unataka kuwa nani?" niliwajibu "nataka kuwa daktari kwani napenda nije kuwasaidia wagonjwa"

Wazazi wangu ni maskini lakini hawakutilia shaka na uamuzi wangu.Walijitahidi kwa hali na mali ili nifikie ndoto yangu.Walilipa karo zangu za shule na hata pesa kwa ajili ya tuition.

Nilipofika A level nilijitahidi sana kwenye masomo yangu ya mchepuo wa PCB.Wazazi wangu hawakuwa nyuma kunipa msaada wa kimawazo na pesa pale ilipohitajika kunilipia tuition na kununua mavitabu makubwa kama BS,Chand,Nelkon na mavitabu mengineyo ingawa hali yao kiuchumi haikuwa nzuri.

Picha lilianza pale NECTA walipobadilisha gia kwa kupandisha grades tukiwa kwenye hatua za mwisho za kumaliza kidato cha sita.Lakini hilo halikunishtua sana nilijitahidi sana bila kukata tamaa ingawa sikusoma shule bora sana.

Matokeo yalipotoka sio haba nilipata Div 2.11 yaani DDC, nikajipa moyo kwamba nitachaguliwa medical school.Part two ya picha ilikuja pale TCU ilipovifungia baadhi ya vyuo ambavyo vinatoa course za afya na kupunguza admission capacity kwenye vyuo vilivyobaki.

Nimepigwa danadana katika selections kutoka 1st round hadi 3rd round.Roho imeniuma pale nilipoona hata hii 3rd round haina vyuo za afya.

Nimebaki kushika tama, medical school ni jambo la kusikika tu kwangu.

Ndoto yangu tayari imeyeyuka.
 
hautakiwi kulalamika mdogo wangu,ushauri wangu fanya haraka uombe dip in clinical medicine kupitia nacte ni miaka 3 tu,ukimaliza unaweza ukaendelea na MD,ingawa ni njia ndefu itakulazimu uvumilie tu cz wenzako wengi waliotemwa wameamua kukimbilia huko.
Usikae makuanza kulalamika haitokusaidia chukua hatua
 
pitia diploma ..lakn umesema wazaz hawana hela ushakwama tayari ..poleeee sana Mdogo wangu.........
 
Nakumbuka nilipokuwa mtoto watu wazima wakiniuliza,"ukiwa mkubwa unataka kuwa nani?" niliwajibu "nataka kuwa daktari kwani napenda nije kuwasaidia wagonjwa"

Wazazi wangu ni maskini lakini hawakutilia shaka na uamuzi wangu.Walijitahidi kwa hali na mali ili nifikie ndoto yangu.Walilipa karo zangu za shule na hata pesa kwa ajili ya tuition.

Nilipofika A level nilijitahidi sana kwenye masomo yangu ya mchepuo wa PCB.Wazazi wangu hawakuwa nyuma kunipa msaada wa kimawazo na pesa pale ilipohitajika kunilipia tuition na kununua mavitabu makubwa kama BS,Chand,Nelkon na mavitabu mengineyo ingawa hali yao kiuchumi haikuwa nzuri.

Picha lilianza pale NECTA walipobadilisha gia kwa kupandisha grades tukiwa kwenye hatua za mwisho za kumaliza kidato cha sita.Lakini hilo halikunishtua sana nilijitahidi sana bila kukata tamaa ingawa sikusoma shule bora sana.

Matokeo yalipotoka sio haba nilipata Div 2.11 yaani DDC, nikajipa moyo kwamba nitachaguliwa medical school.Part two ya picha ilikuja pale TCU ilipovifungia baadhi ya vyuo ambavyo vinatoa course za afya na kupunguza admission capacity kwenye vyuo vilivyobaki.

Nimepigwa danadana katika selections kutoka 1st round hadi 3rd round.Roho imeniuma pale nilipoona hata hii 3rd round haina vyuo za afya.

Nimebaki kushika tama, medical school ni jambo la kusikika tu kwangu.

Ndoto yangu tayari imeyeyuka.
Uckate tamaa hii ndo serikali yetu ndugu
 
Polee sana.

Ungeanza Diploma ila kutokana na ada zake kuwa kubwa sana na wewe umesema wazazi wako hawana uwezo nakushauri uvumilie kukaa mwaka mmoja then mwakani uapply upya.
 
Najua ulifanya uchaguzi mbaya wa kozi na huenda vyuo vyenye ushindani mkubwa sana ndio uliviweka,next time wakati unaomba zingatia ushinda,usichgue tu Muhimbili na Udsm ,anza na vyuo kama AJUCO,St. Francis etc

You still have a chance
 
Dokta gani unakua mvivu wakufikiri.Kwani ni lazima upitie njia hiyo.

Nenda Diploma.
 
Kijana we are on the same boat picha yako na yangu ni sawa kabisaaa ko nadhan tukubali matokeo ili tusiwavunje moyo wazaz waliojitowa hata kwa maombi tukafika hapa tukawe maticha2 udactar mungu akipenda tutaangalia miaka ijayo!
 
Mh pole mpendwa. Vumilia tu mpaka mwakani
 
Back
Top Bottom